Monday, February 26, 2007

Sinema ya 'Maangamizi' itaonyeshwa Toronto, Canada March 9th


Mimi na-acti katika hiyo sinema kama Nurse Malika. Karibuni Kwa habari zaidi kuhusu sinema ya Maangamizi: the Ancient One, bonyeza hapa. http://www.grisgrisfilms.com

***********************************************************************************

Friends of Alternative and Complementary Therapies presents a special screening of Maangamizi: The Ancient One on Friday March 9th, 2007.


This multi-award-winning film about healing trauma from a traditionalAfrican perspective is a Tanzanian-U.S. co-production (2001), co-directed by Martin Mhando and Ron Mulvihill and executive produced by Jonathan Demme.According to American author Alice Walker, "MAANGAMIZI - The AncientOne...is more than a movie. It is a look at how we've been torn at our roots; severed from nourishment at the source...Those of us who can remember and honor who we have been over eons of time, will be able to inspire the whole world to greater heights of compassion."


This powerful film about the role ancestor spirits play in healing will be followed by a panel discussion , moderated by Cameron Bailey, film critic and programmer of Planet Africa for the Toronto International Film Festival.


Panel members include: Ainajugoh Taylor is a traditional African healer from Sierra Leone who is currently helping the government of her home country draft legislation to formally recognize and register traditional healers there according to WHO criteria. She is also a recipient of the Michael Clemons Community Leadership Award for such activities as introducing live African music to Toronto and establishing the health-care team that lobbied the College of Physicians and Surgeons to acknowledge the credentials of foreign graduates in medicine and nursing.


Rebecca Rogerson, born in Toronto, was trained in Soweto, South Africa and is a registered sangoma. After 10 years of work in Southern Africa, she returned to Toronto where she continues her practice as a traditional healer and pursues graduate studies in medical anthropology.


Dr. Ted Lo is a community psychiatrist, Assistant Professor consulting to the Culture, Community and Health Studies Program at the University of Toronto.


When: Friday, March 9th at 7:30 p.m.


Where: Workman Theatre, CAMH 1001 Queen St. W. at OssingtonTickets: $10 (book early to reserve a seat)


Advance Tickets: Send cheque to FACT, 375 Bay Mills Road, # 516, TorontoOn M1T 2G6Payment must be received by Friday, Feb. 23, 2007.


Same day Tickets go on sale at the Workman theatre 30 minutes prior to the screening.For more information, call FACT 416-299-5113 or see http://www.the/ facts.orgFor further details, please see the attached poster. And thanks for passing this on to anyone else who might be interested.FACT is a non-profit

Tuesday, February 20, 2007

Marudio - Wapenzi wa Matako Makubwa



Naona blog ya 'Matako Makubwa' ilikuwa na hits nyingi sana, nilibandika kwanza 12/2005. Hivyo nimeamua kuirudia.

Nimesikia wazungu wakisema hiyo kupenda matako makubwa eti ni 'cultural thing' kwa watu weusi, na hawajakosea. Ni mila na desturi ya mwafrika kupenda matako makubwa. Na kuyasifia. Hata wengi wa waMarekani weusi wanapenda mpaka kutunga nyimbo za 'bootylicious'. Huwa nacheka nikiona mzungu anasifia mwanamke ambaye huko nyuma kapigwa pasi. Yaani fleti. Lakini kuna wesui ambao wamekuwa 'zungunized' na wanapenda matako fleti. Shauri zao!

Matako Makubwa Oyee!



************************************************************************

From my 12/2005 Blog:


Wapenzi wasomaji, leo nimeamua kuzungumzia suala ya matako makubwa. Tafadhali msione kama ni matusi lakini hapa USA ni issue kubwa, maana watu wanayachukia!

Nimeona nizungumzie suala ya matako makubwa kwa vile jana kazini, mzungu aliyekondeana mno kasema ni mnene na akila keki eti yote itaenda matakoni. Nilishangaa na kusikitika sana.Uzuri kwa wazungu ni kuwa na matako fleti kama vile yamepigwa pasi. Sijui kwa nini. Mtu anashepu ya mbao, mwanamke hana hips kakaa kama dume vile eti ndo uzuri. Kumbe ni kwa sababu hao models na wacheza sinema wako hivyo!

Basi wasichana na akina mama wanajinyima chakula kusudi wakonde na eti wapendeze. Ndo maana magonjwa kama Bulimia na Anorexia zimeshamiri hapa. Lakini ukitazama sinema za miaka ya nyuma kama za 1930's na 1940's, wanawake walikuwa na shepu na walikuwa wamejaa na hata wanaume wa kizungu walikuwa wanasifia. Mpaka 1950's kulikuwa na mcheza sinema Marilyn Monroe, alikuwa na zinga la figure 8, na wanaume wote walikuwa wanampapatikia. Ama kweli mambo yanabadilika. Hivi sasa wanasema eti walikuwa ni obese yaani wanene!

Mbona mimi naona matako fleti kama chapati ni mabaya na hayapendezi? Au ni kwa sababu nimekulia Africa? Brothas (waMarekani Weusi) wanapenda mwanamke awe na matako ya maana! Akipita mwanamke mwenye mbarikio utasikia brothas wakisifia, "umm, umm umm!" Kuna siku nilisikia wanaume wa kizungu wakijadili sababu ya wanaume weusi kupenda matako makubwa, walisema ni "cultural thing". Kwa kweli ni culture yaani utamaduni! Kama umekulia katika mazingara ya kupenda kitu utakipenda. Na ndo maana kuna weusi USA wanataka kuwa na shepu iliyokondeana kama mzungu kumbe haiko katika 'genes' zake. Wajitahidi kupunguza mzigo lakini wapi, iko pale pale.

Sisi wanawake wenye asili ya Afrika tumebarikiwa huko nyuma. Yaani boxi, siha, wowowo, booty, na nasikia waGhana wanaita yokohama, matako makubwa yana majina mengi. Waafrika tunaona kama ni urembo, lakini wazungu na waliokulia uzunguni wanaona kinyaa. Wanasema eti ni dalili ya ulafi na uvivu! Lakini kama ni dalili ya ulafi mbona hata mwanamke mwembamba mwafrika anaweza kuwa na kamzigo huko nyuma?

Ubaya mwenye matako makubwa anaweza kubaguliwa kwa vile bosi anaweza kuona kuwa ni 'ugly' (mbay) na mwenye nacho anachafua mazingira ya ofisi. Kweli kabisa!Hayo matako makubwa ni 'genes' za sisi waafrika. Lakini ajabu kuna siku nilisikia wazungu wakisema eti waafrika tuna matako makubwa kwa sababu ya utumwa. Eti mabibi zetu walinyimwa chakula hivyo matako ndo ilikuwa 'godown' ya mafuta ya akiba. Nadhani ni uzushi kama ile ya ngamia kuweka maji kwenye nundu zake!

Mimi mara nyingi nimeambiwa nina matako makubwa, niyapunguze kwa kwenda gym kufanya mazoezi. Hayo mazoezi haisadii kitu ni makubwa vile vile! Lakini msione kama naona haya, wala! Mtu akiniambia nina matako makubwa namwambia mbona kama ni madogo, na ningependa yawe makubwa zaidi! Wanabakia kushangaa hasa nikiwaambia kuwa Afrika, matako makubwa ni uzuri.Na amini usiamini kuna opresheni ya kuyapunguza inaitwa Liposuction. Wanawake wengi weusi na wazungu wamefanya hiyo liposuction ya matako, akiwemo mwimbaji Janet Jackson. Ubaya, ni kuwa ukishafanya hiyo liposuction, mafuta yataenda kwingine mwilini, hivyo utakuwa na shepu ya ajabu!

Sisi waafrika tunapenda kuringia huo mbarikio wa matako makubwa. Nilipokuwa nacheza ngoma shuleni na jeshini, tulikuwa tunatia nguo ndani ya bukta kusudi tuonekana na matako makubwa kweli kweli! Lakini, mara nyingi mitaani hapa USA, nimesikia akina dada wakifokewa, "You got a big a-s!" Kuna siku nilikuwa kwenye kituo cha Subway hapa Boston, kapita mama fualni Mganda, aisei alikuwa amejaliwa kweli huko nyuma, mpaka nikaona wivu. Basi ungeona wazungu walivyokuwa wanamtazama kwa mshangao ungecheka. Ila nilishuhudia baba fulani Mmarekani Mweusi akimtazama kwa furaha na kawa kama vile anamezea mate.

Nampenda sana mecheza sinema, Whoopi Goldberg. Nilikuwa nasoma jinsi akienda kwenye audition au akiwa kwenye movie shoot, wazungu wanamwambia kuwa ana matako makubwa au avae nguo ya kuzificha. Yeye alichoka, na mwishowe kusema, " Mimi ni mwanamke mweusi, nina matako makubwa niache kama nilivyo!" Wanawake wote tungedai heshima kama Whoopi nadhani wazungu wangeheshimu matako yetu makubwa.

Tatizo linigine la kuwa na matako makubwa USA ni kupata nguo. Ukienda kununua sketi au gauni uanweza kukuta mbele refu nyuma umepanda. Au unavaa hiyo nguo lakini kwenye hips na matako haipiti! Hii ni kwa sababu nguo imeshonwa kwa ajili ya wazungu wenye matako fleti. Na kupata Jeans inayofiti ni vigumu. Mtu ambaye atatengeneza nguo 'molded for the black woman' atapata wateja kweli kweli, maana tunalilia nguo kama hizo.

Pamoja na yote haya sasa wazungu wameibuka na staili ya kuwa ka ka-butt. Yaani jeans inakuwa na pedi ndani kusudi mtu aonekana ana matako. Loh! Watu hawaridhiki! Sijui tuseme asante J-Lo (mwimbaji Jennfier Lopez) au nini. Kwanza walikuwa wanamcheka J-Lo na matako yake makubwa lakini naona watu wanaanza kuyapenda. Mpaka kuna opresheni sasa ya kuongeza matako. Wacha wafanye haitapendeza kama matako natural tulyiozaliwa nayo waafrika.

Matako Makubwa Oyee!

Sunday, February 04, 2007

Leo ni SuperBowl - Wanaume wanakuwa Wajinga!

Leo ni siku ya SuperBowl. Yaani msimu wa mchezo wa football unaisha leo. Wanaocheza ni timu za Chicago Bears na IndianapolisColts. SuperBowl inachezwa mji ambayo haina uhusiano na timu wanazoshindana, maana lazima watu wangeuana. Mwaka huu inachezwa Miami, Florida.

Mimi siyo mshabiki wa football wa Marekani. Naona kama wanaumizana, kazi kuangushana. Mara unaona mtu kazolewa kavunjika mguu, mkono au mgongo!

Lakini wanaume hapa USA wanaipenda kweli. Mpaka wasichana wanaotafuta wapenzi, mume wanaambiwa wajifunze kuelewa huo mchezo na itakuwa rahisi kumpata!

Lakini nacho shangaa ni hivi, wanaume wanakuwa wajinga hawajali nini zaidi ya mambo ya hiyo SuperBowl. Wengine wananua tiketi za kwenda huko na mshahara wa miezi kadhaa, mradi wanaenda. Pia TV Kubwa kubwa zinauzwa sana kipindihiki, wanunuzi wakuu wanaume wanaotaka kuangalia Superbowl.

Magazeti, na TV wanaongea habari ya SuperBowl tu mpaka inachosha. Ukienda Grocery store, (dukani) unakuta wanaume wamejaa huko wananunua vyakula vya party kama potato chips, nachos, salsa, chicken wings, cold cuts platters, vinywaji kama soda na bia na nyama za kufanyia barbecue. Hata kwenye baridi unakuta wanaume wako nje wanafanya barbecue. Kwenye football wanita ‘tailgating’

Ajabu wikiendi ya SuperBowl kunakuwa na seli nzuri ya chakula. Mameneja huko Corporate Offices wanakuwa na huruma na kuwapunguzia bei nini? Halafu kila sehemu utasikia kuna SuperBowl party hata majumbani mwa watu. Mabaa zenye TV zinafanya kazi nzuri kweli siku ya SuperBowl.

Niliuliza akina mama wa kizungu kwa nini wanaume wanapenda sana SuperBowl na kupika wao wenyewe siku hiyo. Wakasema ni siku ya mwanaume kuonyesha kuwa ni mwanaume bila kujali wanawake. Haya SuperBowl ikisha watatukumbuka sisi wanawake.

Mama moja kaniambia habari ya chakula fulani wanachopika hao tailgaters, inaitwa jambalaya. Hicho chakula kina wali, sausage, nyanya, vitunguu, pilipili hoho, na viungo kadhaa. Halafu wanatia vipande vya nyama ya kaa. Eti hiyo kaa inaongeza ladhaa. Ukweli eti ina harufu kwa uke wa mwanamke, ndo maana wanaishangalia. Unaona wanaume wananusa halafu wanshangalia. Fikiria mbuzi beberu anvayotanua tanua pua akitaka mambo. LOH!

Hapa Boston timu yetu New England Patriots, hawakufanikwa kwenda. Mbona wanaume walilia machozi walivyoshindwa! Haya tuone nani atashinda Colts au Bears. Na kwa mara ya kwanza timu zote mbili zina kocha mweusi.

UPDATE- Washindi ni INDIANAPOLIS COLTS

Score ilikuwa 29-17.


Huwezi kujua ajali itatokea lini

Ajali ni ajali. Hupangi itatokea lini au itatokea nini. Ukweli ukiamka huwezi kujua Mungu au shetani amekupangia nini siku hiyo.

Zaidi ya wiki mbili zilizopita nikiwa nakwenda kazini nilianguka kwenye ngazi za subway Central Square hapa Cambridge. Hata sikumbuki vizuri ilikuaje, sikuwa nakimbia wala kuwa na haraka, mwendo wa kawaida tu. Nilikuwa nateremka kwenda kwenye geti kusudi nisubiri treni. Ghalfla nilianguka, kwa bahati kuna ile sehemu pana ya katikati ndo nikaishia hapo na sikwenda chini kabisa. Ngazi zenyewe zimechongwa na mawe. Loh, magumu! Baada ya kuanguka nilishindwa kuinuka. Nikasema hayo ni malipo kwa ajili ya kucheka uile tangazo ya bi kizee akisema, “I’ve fallen and I can’t get up!) (nimeanguka na siwezi kuinuka), japo sijaiona miaka mingi. Mzungu mwanaume aliyekuwa anapanda zile ngazi alinisaidia kuinuka. Alivyokuwa ananinsaidia nikasikia maumivu makali kwenye mguu na kushindwa kutembea kabisa. Nikamwambia nadhani nimevunjika mguu. Huyo mzungu alipiga simu polisi, na polisi kaja, halafu wakaamua kuniitia ambulance.

Wale EMT (Emergency Medical Technicians) walinipakia kwenye kiti maalum ya wagonjwa na kunibeba mpaka kwenye stretcher barabarani ndo wakanipakia kwenye ambulance. Nikapelekwa hospitalini donidoni ikiwa inalia.

Basi mle ndani nikawa nalia. Niliamka mzima, sasa nimevunjika mguu! Nikawaza je, ningechelewa kidogo ningeanguka, je, ninegwahi kidogo ningeanguka? Je, nitakuwa mzima tena, je, nitaweza kucheza densi tena? Nikasema nina bahati lakini maana kuna wengine wanapata ajali ya gari na wanakufa. Au wanakatika kiungo. Fkiria mtu unaagana na mpenzi wako mtaonana au mtapigiana simu baada ya muda kadhaa, halafu simu inapigwa, mwenzako kapata ajali. Nilikuwa na mawzao mengi lakini nilishukuru kuwa sikumia kiasi cha kupoteza fahamu.

Hospitalini walinihudumia mara moja. Nilikuwa nimevaa suruali, walivyopandisha wakaona kuwa ngozi imechunwa kwenye gotii. Nilibakia kushangaa maana suruali haikuchanika. Baadaye walinipeleka X-ray. Bahati nzuri hakuna mfupa iliyovunjuika lakini nilikuwa nimeumia misuli tu kwenye goti. Wakanipa magongo, na madawa ya kupunguza maumivu na nikaenda zangu nyumbani kwa teksi. Nilikosa kazi siku mbili na bahati nzuri wikiendi ikaja. Nikapata nafasi nzuri ya kumpumzika. Baada ya hapo ikabidi nirudi kazini na magongo. Na mjue huko kwenye treni hakuna aliyenipisha kiti hata waliokaa viti maalum vya wagonjwa. Wengine wanakuaona halafu wanajidai wanasoma gazeti.

Lakini nashukuru sikuumia zaidi, na daktari kasema baada ya wiki kadhaa maumivu yatakwisha kabisa. Namshukuru Mungu kuwa sikuumia zaidi.