Monday, June 30, 2014

Ukeketaji Tanzania - Female Circumcision


FLASH MASSAGE DIASPORA:
 
Kilio cha mwanamziki/mwanahabari mkongwe Freddy Macha hatimaye kimesikika na kuwagusa viongozi wa ngazi zisizokamatika.Ni sawa na kuyaona machozi ya kilio cha njiwa.Kama ni mila,jadi,itikadi za dini kuwepo na utafiti wa kiafya kupunguza maumivu na mateso ya ukeketwaji wa watoto wa kike hata utamaduni wa kambi za jando maporini kwa watoto wa kiume yafanyike kwa madaktari bingwa katika madahawati ya serikali kupitia usimamizi wa kadi za bima maalumu-NSSF kwa jamii kupunguza msongamano
wa vifo kwa watoto ambao kwa miaka ya siku hizi wanazaliwa tayari wamekomaa kama vijana wa Taifa.
   



FREDDY MACHA-KITOTOBLOG
Kumbukumbu:




image

SHEREHE KUSAIDIA UJENZI WA JUMBA LA KUHIF...
Ijumaa tarehe 30 Mei, London. Ukumbi wa hoteli iliyoko kitongoji cha Hackney, kaskazini ya London ulishuhudia usiku wa muziki, chakula na vinywaji. Kila aliyeingi...

Preview by Yahoo


SOURCE: MIKIDADI-DENMARK

Sunday, June 29, 2014

Barua Kutoka kwa Mume wa Flora Mbasha kwenda kwa Mchungaji Gwajima

 Nimepata kwa Email:

"Mchungaji ...yapata kama wiki mbili zilizopita nilihoji kupitia vyombo vya habari juu ya ‘utajiri' wa ghafla wa mkewangu Mara baada ya mgogoro kutokea kati yangu na yeye, bila kupoteza muda mkewangu akanijibu kupitia gazeti moja la udaku kuwa amechangiwa fedha kiasi cha milioni 9 na waumini kanisani kwako.

Mchungaji, naomba uelewe kuwa nafahamu juu ya mipango yote mnayoipanga kuliko unavyodhani!! Kwanza ni kweli kuwa mlipitisha harambee ya kumchangia mkewangu, lakini kiwango kilichopatikana kilikuwa ni milioni 2 na laki tatu na si milioni tisa kama mlivyotangaza!! Lakini mlitangaza uongo huo makusudi iwe rahisi kutimiza malengo yenu ya kidhalimu mliyoyapanga juu yangu!!

Mnamo tarehe 3 mwezi juni mwaka huu, mlifungua akaunti mpya kwa jina la mkewangu katika benki ya crdb morogoro, na siku nne baadae mkewangu aliingiziwa fedha kiasi cha milioni 18 kutoka akaunti ya MWANAMAPINDUZI FOUNDATION ambayo hyo accnt ipo nmb mwanza! Ambapo asasi hii inamilikiwa na mchungaji wako msaidizi Maximilian Machumu pamoja na mbunge wa viti maalumu kutoka mikoa ya kaskazini!

Nashukuru kama ulimpa fedha hizi kwa nia ya kumsaidia, lakini hofu yangu ni kuwa kwanini kitendo hiki kifanyike kwa kificho?? Kwanini mtumie njia za siri ambazo si rahisi watu kujua kama mmempa fedha??

Pia napatwa na mashaka zaidi kwani siku moja baada ya fedha hizi kuingizwa taarifa ya benki inaonyesha kuwa kiasi cha milioni sita cash zilitolewa na siku hiyo hiyo wapo waandishi watatu wa magazeti ya udaku ambao wanaonekana waliingiziwa fedha kiasi cha milioni moja kila mtu na aliyedeposit hizo fedha ni moja ya viongozi wako hapo kanisani!! Kuna nini hapo??

Mchungaji, naomba tusizunguke mbuyu! Ni dhahiri shahiri kuwa umekuwa na uhusiano wenye utata na mkewangu kwa muda mrefu sasa!

Binafsi nilianza kupata wasiwasi mwaka jana mwezi desemba tulipoenda katika mkutano wako wa injili pale morogoro! Mimi na mkewangu tulifikia hoteli ya kingsway msamvu na wewe ulifikia Nashera Hotel maeneo ya forest hill!!

Baada ya siku tatu za mahubiri mkutano wako ulipigwa marufuku na serikali kwasababu ya maneno yakichochezi uliyokuwa unahubiri, hvyo ikatulazimu waimbaji wote turejee dar es salaam!!

Lakini uliniomba mkewangu abaki na wewe kwani ulipanga uwe unawafanyia watu maombi pale kanisani kwako kihonda kwa muda wa siku nne!! Nilikubali na nikamuacha mkewangu nyumbani kwa dada yako pale mazimbu!! Lakini kesho yake dada yako alisafiri kwenda mwanza na ikabidi mkewangu arudi hotelini kingsway!!

Kwaa taarifa nilizonazo na nimezithibitisha kupitia wahudumu wa pale hotelini ni kuwa mkewangu hakuwahi kulala pale hata siku moja ingawa chumba kililipiwa kwa siku zote zile!! Unaweza kunijibu alikuwa analala wapi?? Je unaweza kunieleza kwanini mkewangu alikuwa analetwa nashera hoteli na taxi kila siku usiku!! Sibahatishi katika hili kwani hata namba ya dereva taxi ninayo!!

Yote haya nilivumilia, na hapa kati kati kuna mengi sana yametokea lakini nikajifanya mjinga nikajishusha nikavumilia kwa lengo la kulinda ndoa yangu isiharibike lakini naona wenzangu hambadiliki wala hamjishitukii sana sana mapenzi ndio yanzidi kuwa motomoto kati yenu!! Ulikuwa unategemea nivumilie mpaka lini, nijishushe kiasi gani, niwe mjinga kiasi gani Nilikuvumilia sana mchungaji lakini sasa imefika point hapana, imetosha lazima nikuondelee uvivu watanzania na dunia ikufahamu jinsi ulivyo na kitendo ulichonifanyaia na unataka kuniziba mdomo kwa kunitishia jela miaka 30!!!

Wewe ni mpuuzi na shetani anaishi ndani yako... na nataka nikuahidi kitu kimoja kuwa NITAKUSHINDA! Najua utanisumbua sana kutokana na hela zako but at the end, I will be the last man standing!! Narudia tena, nitakushinda.!!

Bila kusahau naomba niongee na wewe pia mkewangu, hivi ni nini kilichokukuta ndani ya moyo wako How did we get here?? Je ni fedha zilizokufanya ukengeuke kiasi hicho au kuna kingine?? Kama unanichukia mimi kiasi hiki je, uwahurumii hata watoto wetu?? Mbona tunawatengenezea mikosi wakiwa wadogo hivi?? Hivi unadhani watoto wanajisikiaje watakaposikia kuwa baba ameenda jela kwa kosa la kubaka lakini aliyechongesha muvi yote hiyo ni mama?? Hivi kisaikolojia hawa watoto watakuwaje Si watakuwa huku wanatuchukia sisi wote wawili kwa aibu na mikosi hii tunayowatengenezea Kwanini tunataka kuwataabisha watoto kwa dhambi ambayo hawajaitenda

Yes nafahamu nimekukosea mengi and am very sory for that, lakini basi embu kumbuka mkewangu nimekuvumilia mambo mangapi mkewangu, kumbuka makosa mazito uliyonifanyia lakini nikakusamehe ni sijamsimulia hata ndugu yako ama ndugu yangu ili kulinda heshima yako!! Kumbuka jinsi tulivyopogana na changamoto mbalimbali mpaka leo hii umefikia kuwa moja ya icons wa muziki wa injili hapa nchini?? Kumbuka shida, manyanyaso, dhuluma, kuchekwa na kudharauliwa ambako tumepitia mpaka leo hii tuko hapa!!!

Mkewangu, kwa miaka yote hii nimekubali nionekane bushoke tu huku watu hawajui kuwa mimi ndiye ninayechora ramani ya kila ishu yako!! Mimi ndiye nimekuwa nafatilia na kufanikisha kila kitu chako from scratch!!!

Lakini nimekubali jamii inione bushoke kwani nilikuwa najua nini mimi na wewe tunatengeneza kwa maisha yetu ya sasa na baadae!!! Nini kilichokubadilisha mkewangu Fedha Au huyo mchungaji mwanamazingaombwe

Hivi kweli kabisa umefikia hatua ya kulipa waandishi wa habari ili wanikandamize nionekane sifai katika jamii Ni nini kilichokuoata mkewangu??

Naomba uelewe kuwa binafsi siogopi kwenda jela kwasababu ya hiyo muvi mliyonizushia, kwani ni bora nikakae jela kuliko kuishi huru huku mkininyanyasa kiasi cha kuondoa utu wangu kama bidamu, lakini kinachoniuma ni familia yetu!! Kwanini watoto wateseke kwa sababu ya tamaa zetu binafsi!! Nikifikiria hilo naumia sana!

Najua kwa sasa inaonekana kama vile ni impossible kwa mimi na wewe kurudiana tena, lakini binafsi naamini tunaweza!! Najua haitakuwa rahisi kwani tumeharibu mno, lakini ni heri ya kujaribu kuliko kuendelea kufanya huu upuuzi tunoufanya sasa!!

Kumbuka hiki tunachokifanya sasa hatujajipaka matope sisi tu pekee, bali mziki wote wa injili Tanzania, na tusipotubu tukajirudi Mungu atatuhukumu kwa dhambi hii!! 
Kumbuka kuwa hakuna kati yenu atakayeshinda katika hii vita, vyombo vya habari pekee ndivyo vitakavyo nufaika lakini mimi, wewe na mchungaji wote tuta loose!!

Mwisho nimalizie na wewe mchungaji, tulipokutana mara ya kwanza nilikuchukulia kama kaka na kama mlezi wetu wa kiroho!! Lakini umegeuka shetani mwenye pembe saba, umeparaganyisha familia yangu, umeleta maumivu makali kwenye ukoo!!

Nakuonya tena kwa mara nyingine, muache mkewangu!! Huyo ni mkewangu, nilimtolea mahali mimi mwenyewe na wazazi wake waliniamini na kunikabidhi!!! Nasema niachie mkewangu!!

Wewe ni nyoka, imefika time watanzania wakujue ukweli wako wewe mbwa mwitu mkali uliyevaa ngozi ya kondoo!!!

Umedanganya watu vya kutosha na umefarakanisha ndoa nyingi sana kwa sababu ya kiburi cha pesa zako chafu za sembe!! Umeudhalilisha ulokole kiasi cha kutosha imefika time tuwaeleze watanzania ukweli na wakufahamu kuwa wewe ni nyoka!!

Sitakubali kuona ukiendelea kuitesa familia yangu, nitapambana na nitakushinda!!! Siogopi fedha zako wala connection ulizonazo, ni bora nife nikiwa nimesimama kuliko kuishi nimepiga magoti!

Nitapambana na wewe mpaka mwisho ili historia isomeke vizuri ili hata wanangu wakiwa wakubwa wajue kuwa baba yao sikuwa lofa kiasi cha kupiga magoti na kuelekeza shingo kibla kuruhusu mdhalimu kama wewe uichinje familia yangu, bali licha ya umasikini wangu nilisimama kiume na kupigana kutetea familia yangu!!!

Narudia tena mchungaji, nitapambana na nitakushinda.."
Global Publishers
 
 
--

Saturday, June 28, 2014

Ujambazi Geita

Nimepokea taarifa hizi kwa Email:

Taarifa kutoka kwa mdau S.A.

June 24, 2014

Wadau,
Jioni ya leo majambazi wamempiga risasi mbili kifuani na tumboni mfanyabiashara maarufu kwa jina la Warwa na inasemekana amefariki dunia papo hapo kwenye duka lake la uwakala wa mitandao ya kutuma na kupokea pesa maarufu kama mpesa, airtel money na tigo pesa lililopo soko kuu kwenye barabara ielekeayo kwenye benki za nmb, nbc na posta.
Mpaka sasa mji wa Geita umekumbwa na taharuki kubwa kutokana na tukio hilo. Mpaka kufikia saa mbili usiku huu bado kulikuwa na makundi ya watu wengi kwenye eneo la tukio na kwenye maeneo ya hospitali kuu ya wilaya ya Geita.
Inasikitisha sana maana inasemekana kuwa pamoja na polisi kuwa karibu na eneo hilo lakini majambazi hao wamefanikiwa kutoroka kwa kutumia pikipiki. Vishindo vya risasi zinazoamika kumuua ndugu Warwa vilisikika mbali kutoka kwenye eneo hilo la tukio.
SA.

************************

June 25, 2014

Wadau,
Taarifa zilizopo Geita zinaoonyesha kuwa majambazi hao waliuwawa jana ile ile, walipoondoka na pikipiki, walikuwa wakifuatwa kwa nyuma kwa mbali na madreva pikipiki ambao waliwatonya polisi uelekeo walikokuwa wanakimbilia!

Inasemekana walikuwa wanakimbilia uelekeo wa Nyang'wale, polisi wa Geita wakawajulisha wenzao wa Nyang'wale ambao nao wakawatangizia hao jamaa barabarani na kuwaua.
Utambuzi wa maiti za majambazi hao wawili ulionyesha kuwa mmojawapo ni mpwa wa marehemu aliyevamiwa na kuuwawa! Na hii ni baada ya dada wa Warwa kumtambua kijana huyo kuwa ni mwanae!

Habari zaidi zinasema kuwa, kabla ya kupigwa risasi zile kifuani na tumboni, marehemu Warwa alimtambua mpwa wake huyo na kutamka kuwa, "....hata wewe ..... umejiunga na ujambazi kuja kunivamia mimi mjomba wako?", na huenda hiyo ilikuwa sababu ya kuuwawa kule na kijana huyo!
Taarifa zilizopo hapa Geita zinasema jana hiyo hiyo, ndani ya muda mfupi sana, kulikuwa na matukio mawili ya ujambazi, hilo la hapo kwa marehemu Warwa na jingine kwa mfanyabiashara wa jumla wa bia ndugu Inyasi, ambaye yeye hakukutwa dukani bali mke wake na watu wengine. Hapo waliishia kupora fedha na bostora iliyokuwemo kwenye droo na kukimbilia kusikojulikana.
Haijajulikana kama matukio haya yalifanywa na watu walewale au tofauti, lakini inasemekana yana uhusiano. Inasemekana kiasi kikubwa cha fedha kiliporwa, na wadau wanatonya kuwa huenda pesa hiyo ilikuwa ni zaidi ya shilingi mil. 50!
SA.

TAMWA kutoa Elimu Kupambana na Ulevi Kupindukia

TAMWA kutoa elimu kupambana na ulevi Kupindukia
Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Valerie Msoka akisisitiza jambo katika mkutano na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo.
KITUO cha Usuluhishi (CRC) kinachofanya kazi chini ya Chama cha Wanahabari Wanawakecha (TAMWA) kimejipanga kutoa elimu kwa jamii kuhakikisha kinapambana na matumizi ya pombe kupindukia kwa jamii suala ambalo limezidisha vitendo vya ukatili wa jinsia unaofanywa na watumiaji pombe kupindukia.

Akizungumza na wahariri wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Valerie Msoka alisema utafiti uliofanywa na Shirika la IOGT International unaonesha kuwa kiwango cha unywaji pombe jijini Dar es Salaam ni asilimia 47.6 kwa wanaume na asilimia 29 kwa wanawake huku ikibainika kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya vitendo vya ukatili na matumizi ya pombe kupita kiasi. 

Bi. Soka alisema takwimu zinaonesha kuwa wanawake ambao waume zao wanalewa mara kwa mara wengi wao wanakumbana na ukatili unaohusisha vipigo, kuumizwa na ukatili wa kingono kwa asilimia 77, huku kiwango cha ukatili kwa wanawake ambao waume ama wenzi wao hawanywi pombe ni asilimia 33.

"...Utafiti uliofanywa na shirika la IOGT International unaonyesha kwamba kiwango cha unywaji pombe katika jiji la Dar es Salaam ni asilimia 47.6 kwa wanaume na asilimia 29 kwa wanawake...lakini takwimu kutokana na utafiti wa Demographia na Afya Tanzania (TDHS) 2010...unaonesha wanawake ambao waume zao wanalewa mara kwa mara wengi wao wanakumbana na ukatili unaohusisha kipigo/kuumizwa na ukatili wa kingono kwa asilimia 77," alisema.

Aidha aliviomba vyombo vya habari kushirikiana na TAMWA kutoa elimu kwa jamii kupunguza matumizi ya pombe kupindukia kwani licha ya ukatili huo familia pia zimekuwa zikiathirika kiuchumi juu ya matumizi ya pombe huku baadhi ya watoto wakikosa huduma za msingi kutoka kwa baadhi ya wazazi ambao ni walevi kupindukia.

Alisema TAMWA inatekeleza mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na wasichana unaosababishwa na pombe huku lengo kuu ikiwa ni kuhakikisha maisha ya wanawake na watoto yanaboreshwa kwa kuimarisha sheria na kupunguza ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe kupindukia.

Hata hivyo alisema tayari chama hicho kimeanza kufanya utafiti mwingine katika Wilaya ya Kinondoni kuangalia madhara yanayotokana na unywaji wa pombe kupindukia ili kuangalia hali halisi ya matumizi ya pombe eneo hilo na madhara ambayo yamekuwa yakitokana na matumizi hayo.

Alisema malengo mengine ya mradi ni pamoja na kuboresha maisha ya wanawake na watoto kwa kuimarisha sheria na kupunguza ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe katika wilaya ya Kinondoni na pia kujenga uelewa miongoni mwa jamii juu ya madhara yatokanayo na unywaji wa pombe kupindukia. 

Mkurugenzi huyo Mtendaji wa TAMWA aliongeza kuwa mapambano hayo pia yatasaidia, kukabiliana na matumizi ya pombe na kutoa taarifa kwa vyombo husika kuhusu ukatili dhidi ya wanawake unaotokana na matumizi ya pombe, ikiwa ni pamoja na kujenga uwezo wa jamii kukabiliana na ukatili unaosababishwa na unywaji wa pombe dhidi ya wanawake na watoto.

Salamu za Ramadhani Kutoka Sec. of State John Kerry

 
U.S. Secretary of State, John Kerry

Secretary of State John Kerry on Ramadan Kareem

Press Statement

John Kerry
Secretary of State
Washington, DC
June 27, 2014




As the holy month of Ramadan begins, I wish the millions of Muslims here at home and so many more all around the world Ramadan Kareem.

Ramadan is a time for peaceful reflection and prayer, a time for acts of compassion and charity -- universal values and aspiration ingrained in every human heart.

Across the globe, Muslims will assemble and celebrate a rich tradition with fasting and prayer, as generations have done every year since the time of the Prophet Muhammad. Here in America, Muslims will commemorate Ramadan in ways that reflect the great diversity of our country and the spirit of community that binds us together.

The diversity and patriotism of America’s religious communities are sources of strength for all of us, and our freedom to worship is a powerful reminder of the traditions we share. E Pluribus Unum – From Many, One. And from many faiths, we stand together in one shared country.\

Along with many of our Ambassadors all over the world, I will host an Iftar celebration at the State Department in Washington, DC. This event will bring together leaders from across the Muslim community to join together and reflect on our shared values.

On behalf of the U.S. Department of State, I wish all Muslims around the world a peaceful Ramadan and joyful month.

Tahadhari kwa Waegeshao Magari Jijini Dar

Kutoka kwa Taji Liundi

TAHADHARI:

Inanisikitisha sana kuandika tahadhari hii kwenu rafiki zangu. Haistahili kuwa tahadhari. Lakini SASA HIVI katika mitaa mbalimbali jamaa zetu wa TANROADS wanapita kukamata na kupiga FINE magari yaliyoegeshwa "vibaya". Fine ni Tsh 220.000.

Hili ni tatizo kubwa sana na RUSHWA inafukuta kwenye zoezi hili. Mtanzania wa kawaida HAWEZI kulipa kiasi hicho kama ameegesha KANDO YA BARABARA zetu za kawaida, mfano pale Sinza Palestina.

Hao jamaa wanadai inabidi uwe umewasha TAA ZA TAHADHARI NA UWEKE TRIANGLE.
Sawa. Lakini si kawaida kabisa na zoazoa yao leo ni hatari. Wanatembea na Noah kubeba madereva/abiria waliokamatwa.

MAONI YANGU: Tusinyanyasane! Sio uungwana. Wananchi tunasota ile mbaya. Huko mitaani tunahangaika kujikwamua kiuchumi.

TANROADS kama Wakala wa Serikali inatakiwa ITOE MATANGAZO YA ELIMU KWA UMMA KABLA YA KUCHUKUA HATUA ZA KISUMBUFU NA KIHALIFU KWA KUCHOCHEA RUSHWA(wanakubali hadi Tsh 60/70elfu ukiongea nao).

Kwa kawaida, wangetakiwa wapite hata na PA watangaze: "Ndg wananchi katika eneo hili, mnaombwa kuegesha magari yenu kwa utaratibu huu kandokando ya barabara kuu. Hakikisha umewasha taa za dharura na weka Triangle mita...nyuma ya gari".

Hii ingeondoa usumbufu wa KUMWELEKEZA kila mkosaji.

Tumieni TBC!! RADIO Uhuru nk. Ombeni Matangazo ya kijamii kwenye Radio binafsi.
Kinachotokea ni shambulio la kihalifu kwa WaTanzania wasio na hatia. Kwa mara nyingine tena naandika kuhusu uendeshaji mambo KIHOLELA. Uholela huu unanyanyasa waTanzania.
Marafiki zangu humu mlio na wadhifa na uwezo wa kufwatilia hili..fanyeni hivyo. Mtagundua nazungumza UKWELI!!

Sijapendezwa!

Eneza TAHADHARI hii.

Tanzia - Nkwabi Ng'wanakilala

Kutoka Jamii Forum

The late Nkwabi Ng'wanakilala

Aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la Habari Tanzania SHIHATA na mhadhiri wa chuo kikuu cha mtakatifu Agustino, Nkwabi Ng'wanakilala amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza alipokuwa anaugulia matatizo ya figo yaliokuwa yanamsumbua kwa takribani wiki tatu. Mungu ailaze roho ya comrade mahala pema!

Thursday, June 26, 2014

Aliweka Implant Ndani ya Matako Yake! Imeharibika!

Wadau, siku hizi wazungu wanataka kuwa na matako makubwa kama waafrika!  Sasa ona jinsi tako la huyo dada ilivyohabrika! Implant inajigeuza ni balaa!  Itabidi aende kwa dakatari waitoe!

******************************************************


GARANI MW1 - Eti ni Dawa ya Kutibu UKIMWI Kutoka Malawi

Eti, kuna dawa ya kutibu UKIMWI huko Malawi.  Hii dawa ni unga ambao unaweza kuchanganya na chakula chako.  Waliotengeneza wanadai kuwa pamoja na kutibu, muathirika atakuwa na hamu ya kula chakula kingi na atakuwa na kiu mara kwa mara.

 Lakini watu wamejitokeza na kusema hiyo dawa ni feki na haitibu ugonjwa wowote!

Wadau, watu wanaotaka kupona watakuwa na hamu ya kutumia kitu chochote ambacho kinaweza kuwatibu! Mnakumbuka Kikombe cha Babu?  Mnakumbuka waliozuka na vilombe baada ya hapo?  Nakumbuka miaka ya 90 kuna mtau alidai ana dawa Nairobi! Wagonjwa walimiminika kule! Watu wanachezea tumaini ya wagonjwa!  Ni dhambi!

Mnaweza kusoma habari ya  wanaodai GARANI MW1 ni feki kwa KUBOFYA HAPA:


******************************************************

GARANI MW1 - Herbal AIDS MEDICINE



GARANI MW1 is a herbal preparation that is being used to treat people that have HIV and AIDS. It has strong antiviral properties and therefore also positively affects immune system. The medicine improves the immune system by increasing ones CD4 cell count because viral replication is reduced/halted. The body is then able to fight opportunistic infections that come due to the compromised immunity.  The viral load is reduced to undetectable levels and people have tested non reactive to the HIV tests using both anti body and HIV DNA/ PCR tests. 
 As Garanimw1 is available in powder form, it is taken through porridge made from maize flour with no sugar or salt, one tea teaspoon per day, once a day for three consecutive days, repeated after a period of two weeks from the same pack. Some have become totally cured after taking only one pack while others may need to repeat the dose at 1 month intervals.  
DISEASES

Frequent and nonstop headaches, chest pains and breathlessness, chronic undefined coughs, skin rashes, other skin conditions, cancer, hair loss, swollen lymph nodes, painful legs, asthma, unexplained weight loss, numbness in the legs and other body parts, hormonal imbalances, general body weaknesses and pains, chronic wounds, diabetes, high blood pressure, loss of memory, cancerous growths, anaemia, skin discolorations and many others. 
 
 There are many people that have taken the medicine but did not have the HIV virus and have reported success stories on diseases and conditions such as diabetes, high blood pressure, asthma, stomach ulcers, sickle cell, and other abdominal swellings in the body, amenorrhea and others. Some people who had lost their shape due to the effects of ARVs (lipodystrophy) have regained it even while taking the drugs.  
INSTRUCTIONS

1.The full course of the medicine is three teaspoons of the powder taken over a period of three days, one teaspoon per day for three days – put in porridge with no sugar or salt. The remaining powder should be taken after two weeks in the same manner until it is finished. One should choose time when to take the medcine
 2. The porridge should be put in a bowl or cup before adding the medicine and not in a pot.
3.For couples, both should take the medicine and abstain from sex or use condoms correctly and consistently until they go for the HIV test when time is due  
4.One can go for test after 12 months. This is the HIV antibody test in which a small amount of blood from a finger prick is tested since antibodies may persist in the blood for several months even after when the disease causing organism has disappeared from the blood stream.  
5.HIV DNA PCR test can be done after 10 months which looks into the presence of the actual virus.  
6.If one is on ARVs or any other medication they should continue taking the medicine and one will be advised to stop taking the ARVs by a qualified physician when all the above tests are done and are negative 
 7.The known effects of the medicine is that others may develop increased appetite and thirst therefore food and water should be taken as required.
 NOTE: For better and faster results, the dosage should be repeated at 1 month interval for two or more times with condom use at all times although one dose

Wednesday, June 25, 2014

Mbunge Shukuru Kawambwa Yuko Canada - Hajafa! Ilikuwa Uzushi

 
Mb. Shukuru Kawambwa

Kutoka Facebook

TAARIFA TOKA BAGAMOYO
Ndg Watanzania,WanaBagamoyo na wapenda maendeleo, kwa niaba ya CCM-Bagamoyo na Ofisi ya Mbunge-Jimbo la Bagamoyo napenda kuleta kwenu Masikitiko yetu kwa niaba ya Chama na Familia ya Mheshimiwa Mbunge Shukuru Jumanne Kawambwa kutokana na Usumbufu ambao umesababishwa na habari zinazoenezwa Mitandaoni kwamba Mheshimiwa Kawambwa amekumbwa na Umauti akiwa njiani anaelekea Mwanza.

UKWELI
Mheshimiwa Shukuru Jumanne Kawambwa yupo Nchini Canada Akitimiza majukumu yake. Hivyo Watanzania na wana Bagamoyo mnaombwa radhi kwa usumbufu uliotokea na kwamba Mheshimiwa Mbunge yuko na Afya njema na utekelezaji wa Majukumu unaendelea kama kawaida.


Katuni za Siasa - Editorial Cartoons

Kuna Mambo Huko KATUNI INASEMA BLOG:  Hebu cheki katuni za kisiasa huko!  Chini ni sampuli.

BOFYA HAPA KUONA KATUNI ZAIDI

Kijana Michael Said aka Wakudata anajitahidi sana.


Tuesday, June 24, 2014

Peoples Bank of Zanzibar Launches Online Service

(Zanzibar, Tanzania)  The people's Bank of Zanzibar Limited (PBZ Ltd) which is one among the oldest commercial banks in Tanzania and the only indigenous bank in Zanzibar wholly owned by the people of Zanzibar has today expanded its online remittance services to Tanzania from abroad by launching a new service for mobile phone subscribers in the country.

The new service enables members of Tanzanian Diasporic communities to transfer money to their loved ones in Tanzania directly to their mobile phones. Thus, anyone with a mobile phone in Tanzania can now receive money securely and promptly from overseas regardless of his/her location in the country. Similar service is already enjoyed by other East African countries.

The service is carried-out in collaboration with a widely renowned and an award-winning London-based financial services institution calledWorld Remit

The People's Bank of Zanzibar couldn't have planned a better timing for the launch of this new service than at the moment when the local Tanzanian mobile networks just signed the 'interoperability agreement' which allows mobile money customers to transfer cash to each other regardless of whether they are using Tigo Pesa, Airtel Money or Ezy Pesa on their mobile handsets.

With such an agreement in place, many families in the Diaspora will now be enticed to send e-money back home to the e-wallet accounts of their relatives even if the relatives live in remote villages. This will definitely promote a nascent ‘cashless’ economy in Tanzania and will help to drive forward e-commerce and socio-economic development in the country.
According to the People’s Bank of Zanzibar, from January 31st, 2013, when the first remittance worth only TShs 31,252.00 was sent from Toronto, Canada, up to date around one billion Tanzanian Shillings have already been remitted to Tanzania from different Diaspora communities through the People’s Bank of Zanzibar using cash pickup at the counter, bank deposit and airtime top-up services.

Visiting any branch of the bank in Tanzania today one would not fail to notice queues of customers beaming with smiles as they happily wait to pick up their cash sent by their relatives and friends from Europe. These queues are now part of the history of the People's Bank of Zanzibar, as no one would from tomorrow go to stand on a queue when he knows quite well that he can receive cash from abroad directly in the palm of his/her hand.

Monthly records of the People's Bank of Zanzibar show that the number of remittances from different Diaspora communities are increasing month after month with Canada leading. Of late, UK which has the largest population of Tanzanians abroad has also caught up with the spirit after lagging behind for sometime and if it continues with the same tempo might soon surpass Canada. 

The remittance services provided by the People’s Bank of Zanzibar were originally destined only for the recipients of those cities where the bank had its branches, viz, Pemba, Zanzibar and Dar Es Salaam. But, with the launching of this new service today, a new window has been thrown open for more than 27 million Tanzanians who own mobile phones in the country.

According to the officials of the bank in Zanzibar, the system has begun today to transfer funds to Tigo mobile phone numbers only (Tigo Pesa accounts), while the process of finalizing agreements with the other 3-BIG mobile providers in the country goes on.

Recipients are required to pre-register for mobile money service with their mobile phone providers prior to the usage of the service.

Remittance services through the People’s Bank of Zanzibar from USA to Tanzania are expected to start by the end of the year.

To all those who toiled, moiled and operated as one high performing team for the successful launching of the service today, we say it loud to them - AHSANTENI SANA!


Source: Zanzibar Ni Kwetu

Saturday, June 21, 2014

Ajali Mbaya Imetokea Lugalo Leo - Watu Saba Wamakufa






 Taarifa na picha kitoka kwa Mdau OS:


Ajali mbaya ya gari imetokea mchana huu, katika maeneo ya Lugalo jijini Dar es Salaam. Katika ajali hiyo, inakadiriwa zaidi ya watu saba wamefariki dunia.

Mashuhuda wanasema, ajali hiyo imesababishwa na gari aina ya dalala iliyokuwa ikitokea maeneo ya Tegeta kuja Mwenge. Gari hiyo ililigonga dalala nyingine kabla ya kulivamia roli na baadaye gari nyingine aina ya Toyota Discover.

JK: Vyama Vingi Vimepanua Wigo wa Kisiasa


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

JK: Vyama vingi vimepanua wigo wa kisiasa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa mfumo wa vyama vingi vya siasa ni mzuri, umeleta matumaini kwa kupanua wigo na kufungua zaidi uwanja wa kisiasa pamoja na kuiwajibisha Serikali.

Hata hivyo, Rais Kikwete amesema kuwa ili mfumo huo uboreshwe zaidi na uweze kuimarisha misingi mikuu ya maendeleo ni lazima uendeshwa kwa watu kufuata sheria na wala siyo kuingiza matumizi ya nguvu ambayo yanaweza kuvuruga nchi.

Rais Kikwete ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama aliyasema hayo jana, Ijumaa, Juni 20, 2014, wakati alipotoa Mhadhara (Lecture) kuhusu Usalama wa taifa – The Security of a Nation- kwenye Chuo cha Taifa cha Ulinzi  - National Defence College (NDC) Kunduchi, mjini Dar Es Salaam.

Rais Kikwete alikuwa anajibu swali la mwanafunzi wa kozi ya pili kwenye chuo hicho kutoka Kenya ambaye alitaka kujua jinsi gani vyama vingi vya siasa vinavyoathiri umoja wa kitaifa na kuibadilishaTanzania kufuatia miaka zaidi ya 30 ya Tanzania kuwa nchi yenye kuleta matumaini kwa nchi nyingine za Afrika na Waafrika.

Rais kikwete alisema: “Vyama vingi ni vizuri. Mfumo wa vyama vingi unaleta matumaini kwa kupanua wigo wa kisiasa ambao haukuwa mpana kiasi hicho huko nyuma. Sasa mtu anaweza kuamua kujiunga na chama chochote cha siasa anachokipenda yeye.”

Aliongeza rais Kikwete: “Ni mfumo ambao unaiwajibisha Serikali. Ni mfumo mzuri kwa upanuzi wa demokrasia. Sasa watu wanaweza hata kuamua kupunguza bajeti ya safari za Rais nje ya nchi. Wanadhani kuwa Rais anaweza kufanikiwa zaidi na Tanzania kupita hatua za maendeleo haraka zaidi kama Rais atabakia amejifungia ndani ya nchi.”

Rais Kikwete alizidi kujibu swali hilo: “Jambo la maana ni kwamba tunahitaji aina mbali mbali ya mawazo. Mawazo ya namna hiyo hayaathiri demokrasia. Mawazo ya namna hiyo yanasaidia hata chama changu kuimarika zaidi.”

Hata hivyo, Rais Kikwete amesema kuwa mfumo huo utavurugika endapo baadhi ya watu wataendekeza matumizi ya nguvu na hoja za nguvu badala ya kupambana kwa hoja na nguvu ya hoja.

“Wasiwasi wangu ni kuingiza matumizi ya nguvu katika ujenzi wa demokrasia. Ni makosa kwa watu kukimbilia kutumia nguvu baada ya kushindwa kwenye hoja. Na hili halivumiliki na likitokea basi Serikali itaingilia kati kudumisha amani.”

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM

21 Juni, 2014


Rais wa Malawi Afunga Pingu za Maisha Leo! Ana miaka 74


Photos from the Wedding of President Peter Mutharika June 21, 2014
Malawi’s newly elected head of state is set to marry on Saturday. President Peter Mutharika will wed his longtime fiancée Gertrude Maseko, a former parliamentarian, at a private ceremony according to Peter Mukhito, co-chairman of the presidential wedding organizing committee.

The couple and some of their “well-wishers” are expected to fund the wedding, after Mutharika ordered government officials to ensure that no state funds are used to organize the nuptial ceremony.

Mukhito said foreign dignitaries, members of the diplomatic corps, friends of the couple and residents of the region Mutharika hails from have been invited to be guests at the wedding this weekend.

“The wedding would be officiated here in Blantyre and after a reception will follow at Ndata Farm,” said Mukhito. “The bill is being footed by the president himself and some well-wishers. In fact, His Excellency has directed that no government money should be used on this wedding…we have religiously followed the directive from the president that no government money should be used for the wedding.”

Mutharika, 74, is a widower with two daughters and a son. He was however accused of being gay during the run up to last month’s general election.