Wednesday, July 30, 2014

Unajua Una Damu ya Aina Gani?

Je, unajua una damu ya aina gani?  Unajua unaweza kumpa nani damu, au unaweza kupokea damu kutoka kwa nini? Hebu mchecki Chart hii.  Ukienda kutoa damu Red Cross waulize una damu ya aina gani.

Tuesday, July 29, 2014

Heri ya Iddi!


Nawatakia wadau wote waIslamu Iddi Njema! Eid Mubarak!

Saturday, July 26, 2014

Mwimba Injili Bahati Bukuku Apata Ajali ya Gari!


 
 
 
 
Msanii wa Injili Bahati Bukuku (40) ni miongoni mwa majeruhi watatu wa ajali ya gari iliyotokea iliyotokea leo katika barabara ya Morogoro – Dodoma eneo la ranchi ya Narco Wilaya ya Kongwa .

Majeruhi wengine ni Edson Mwakabungu (31) ambaye alikuwa dereva na Frank Christopher (20).
 
Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda wa polisi wa mkoa wa Dodoma David Misime  ajali hiyo ilitokea saa tisa alfajiri.
 
Alisema taarifa za wahusika zinasema kwamba gari walilokuwa wakisafiria Bukuku, IT 7945 aina ya Toyota Nadia likiendeshwa na Edson Mwakabungu mkazi wa Tabata Dar es salaam liliacha njia na kugonga gema baada ya kugongwa na gari inayodaiwa kuwa ni Fuso.
 
Kamanda Misime amesema kwamba Bukuku analalamika maumivu sehemu mbalimbali za mwili huku Frank akiwa na michubuko usoni na mkono wa Kulia.
Aidha amesema kwamba watu wote hao wamelazwa  katika Hospitali ya Wilaya ya Kongwa kwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.
 
 Kwa mujibu wa Kamanda Misime mwimbaji huyo na wenzake walikuwa wanatokea Dar es Salaam ambapo dereva alikuwa anelekea DRC – Kongo, huku Bahati Bukuku na Frank Christopher walikuwa wanakwenda Kahama kwenye tamasha la injili.
 
Source: Sifa Lubasi, Dodoma

WaJapani Sasa Wanataka Nywele Zetu!


 Wajanja, muwahi kufika Japani mkafungue saluni za kutenegeneza mitindo ya Afro.



Kutoka Facebook:

 
THE JAPANESE ARE NOW BUYING AFRO HAIR

This photo shows how the Japanese create 'the Afro Look' on their hair texture. (This is old news.)
But, apparently, they are now interested in buying our afro hair, so they can make it into wigs, weaving weft and bulks of hair for braiding. (Makes you wonder where our hair goes, once it is swept up, off the salon floor. Will salon owners be capitalising on the trade of our hair?.... Perhaps.)
MS Natural Notts TAKE ON THIS
We, 'Black folks' should have been the first to capitalise on this, i.e. developing a market for the trade of our afro hair, instead of leaving it on the salon floor, in retaliation to Asians capitalising on our distorted concept of beauty. E.g. The straight hair obsession by blacks, that fuels the global success of Asian human hair trading.
The ONLY reason our people missed this entrepreneurial idea, is because we HATE what naturally grows from our scalp..... Other ethnic groups have always been the first to appreciate every inch of us and to capitalise on our beauty, by any means necessary..... E.g. fake tans, fake buts, fake full lips, etc
WHEN WILL WE FULLY UNDERSTAND
Our natural assets are the measuring stick of beauty???


‪#‎BlackPeopleWeNeedToWakeTFUP‬!

Ugonjwa wa Chikugunya Marekani

 Ugonjwa wa Chikugunya unayosambaza na Mbu sasa uko Marekani!  Mbu wanaosambaza wanaitwa Andes na wanauma watu mchana.  Wana sayansi wanasema kuwa asili ya Ugonjwa wa Chikungunya ni Tanzania.

******************************************************

Aedes Mosquito

By Maggie Fox

Chikungunya has been reported in a Florida man and woman who had not recently traveled, health officials said Thursday — the first indication that the painful virus has taken up residence in the United States.

Health experts had said it was only a matter of time before the virus, carried by mosquitoes, made its way to the U.S. It’s been spreading rapidly in the Caribbean and Central America. It's infected 350,000 and killed 21.

Sign up for top health news direct to your inbox.

There have been other U.S. cases but all have been among people who had recently traveled to affected regions.

“Seven months after the mosquito-borne virus chikungunya was recognized in the Western Hemisphere, the first locally acquired case of the disease has surfaced in the continental United States,” the Centers for Disease Control and Prevention said in a statement.

"The first locally acquired case of the disease has surfaced in the continental United States.”

Florida health officials later said there were two cases: a 41-year-old woman in Miami-Dade County and a 50-year-old man in Palm Beach County.

“Since 2006, the United States has averaged 28 imported cases of chikungunya (chik-un-GUHN-ya) per year in travelers returning from countries where the virus is common. To date this year, 243 travel-associated cases have been reported in 31 states and two territories,” CDC said.

“However, the newly reported case represents the first time that mosquitoes in the continental United States are thought to have spread the virus to a non-traveler. This year, Puerto Rico and the U.S. Virgin Islands reported 121 and two cases of locally acquired chikungunya respectively.”

Chikungunya is not usually deadly, but it can cause a very bad headache, joint pain, rash and fever. Its name in the Makonde language, spoken in Tanzania and Mozambique in Africa, means “that which bends up,” because patients are often contorted with pain. They can spend weeks in bed, racked with pain.
The virus only arrived in the Western Hemisphere in December, on St. Martin.

The Aedes aegypti and Aedes albopictus mosquitoes that spread chikungunya are found across the southern United States and as far north as New York. A. albopictus is commonly known as the Asian tiger mosquito and itself only came to the United States in recent decades.

So what’s the difference between a traveler carrying it and a locally transmitted case? The virus grows in human blood and when a mosquito bites an infected person, it can spread it to others. So an infected person can carry the virus to new places and it spreads that way. Officials have been cautioning that the virus could become established in the U.S. , much as West Nile virus did starting in 1999.

There's no vaccine against chikungunya and the only treatment is rest and pain relief.

“The arrival of chikungunya virus, first in the tropical Americas and now in the United States, underscores the risks posed by this and other exotic pathogens,” said Roger Nasci, who heads CDC’s Arboviral Diseases Branch. “This emphasizes the importance of CDC’s health security initiatives designed to maintain effective surveillance networks, diagnostic laboratories and mosquito control programs both in the United States and around the world.”

CDC and the Florida Department of Health said they are looking for other locally acquired cases.

"More chikungunya-infected travelers coming into the United States increases the likelihood that local chikungunya transmission will occur."

“It is not known what course chikungunya will take now in the United States. CDC officials believe chikungunya will behave like dengue virus in the United States, where imported cases have resulted in sporadic local transmission but have not caused widespread outbreaks,” CDC said. Dengue has been seen in Florida and South Texas.

“None of the more than 200 imported chikungunya cases between 2006 and 2013 have triggered a local outbreak. However, more chikungunya-infected travelers coming into the United States increases the likelihood that local chikungunya transmission will occur."

The good news is people are immune after one infection.

And a recent study suggests the United States has a bit of time on its side. The strain of chikungunya circulating in the Caribbean is the Asian strain, and it’s only adapted to be carried by the Aedes aegypti mosquito, says Scott Weaver of the University of Texas Medical Branch, who’s been studying the virus for years. And so far, that mosquito can only be found in the far southern U.S.

Monday, July 21, 2014

Tapeli Lililojidai Kishoka wa TANESCO Adakwa Live Mlimani City

10500539_819006161445574_7780628803053090260_n

Pichani juu na chini ni Kishoka wa Tanesco aliyekamatwa Mlimani City.

Na Mwandishi wetu

TAPELI lililokubuhu kwa masuala ya kulaghai watu kwa njia ya kujifanya kishoka washirika la Umeme Nchini, Tanesco, jana asubuhi limedakwa baada ya kuwekewa mtego walipokuwa wakitaka kutapeli kwa mmoja wa Afisa wa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma- Ledama.

Kwa mujibu wa Bi. Usia akieleza tukio hilo, alidai kuwa tapeli huyo alifika asubuhi akiwa na wenzake sita, nyumbani kwake wakasema wanatoka Tanesco wamekuja kucheki mita ya Luku. Hata hivyo wakakorokocha wakasema mita imechezewa kwa hiyo wanakata Umeme na kung'oa mita, eti waliona kwenye GPS yao kuwaUmeme hauendi vema.

“wakasema fidia na kurudisha umeme kiofisi ni milioni 8! ila tukiwapa milioni 2 wataturudishia. nikawauliza kama mita imechezewa mbona tunanunua umemewa laki 3 kwamwezi? si ingepaswa tulipe kidogo? wakasema wakati mwingine wakiweka hiyo resistance (eti ndo kifaa cha kuiba Umeme) huwa kinafyatuka halafu Umeme unakwenda zaidi! “ alielezea Bi. Usia.

Na kuongeza kuwa vishoka hao wakakata Umeme wakaondoka, tujipange. tujadiliana na mzee tukapata mashaka maana walikuwa wakali halafu wanalazimisha mambo, wamevaa vitambulisho lakini wamevigeuza kwahiyo havisomeki. tukapiga simu Tanesco kuwauliza wakasema hao ni vishoka tuitePolisi, basi tukawapigia simu waje wachukue laki tano waturudishie Umeme, mengine Jumatatu. wakaja fasta wakarudisha Umeme, nikawaambia naenda aTM wasubiri nikawaacha na mzee nikatoka mbio mpaka Polisi chuo nikawahadithia wakanipa Polisi 3 nikaja nao nyumbani, tukawakuta wameondoka.

Mzee akawapigia simu waje hela imepatikana wakasema tukutane Mlimani City, tukafanikiwa kukamata mmoja wengine wakakimbia. tumemuacha selo, tukaandikisha maelezo. tunasubiri hatua itakayofuata.

10417599_819006198112237_2101442257557265538_n  

Hapa likiwa chini ya ulinzi na pingu mkononi.

--

Saturday, July 19, 2014

Wema Sepetu 'Amlipua' vibaya Kajala -





Wema Sepetu (R) na Kajala

Kutoka BONGO MOVIES. COM

Ikiwa ni siku chache zimepita baada ya mwigizaji  Kajala kudai kuwa mrembo Wema Sepeteu ni Mnafiki, hatimaye Mwanadada Wema Sepetu , amemlipua aliyekuwa shosti wake, Kajala Masanja ‘K’ ambaye wiki iliyopita alimwita mnafiki, habari  ambayo  ilisambaa  katika  mitandao  mbalimbali  ya  kijamii.

Katika habari hiyo, Kajala alikaririwa akisema kwamba licha ya watu wengi kuamini wamepatana, hakuna ukweli kwani rafiki yake huyo ni mnafiki kufuatia kutomthamini na kutokuwa karibu naye kama zamani likiwemo suala la kumsifia mtu ambaye alikuwa na ugomvi na Kajala (Dacutee).

Akizungumza na mwanahabari wetu, Wema alisema alishangaa kuona Kajala anamwita mnafiki wakati hakuwahi kupatana naye tangu walipotofautiana kipindi cha nyuma kama alivyosema.
“Nashangaa Kajala ananiambia mimi ni mnafiki ‘ok fine’ na huo unafiki wangu unakuja pale nilipomu-wish Dacutee siku yake ya kuzaliwa, alitakaje eti? Yaani kwa kuwa yeye ana bifu la kumchukulia bwana’ke na mimi nijiingize kwenye bifu lao?

“Au tofauti zangu mimi na yeye, Aunty Ezekiel aingilie, itakuwa sahihi kweli kama wanavyofanya hao watu wake anaozurura nao siku hizi? Wanaingilia vitu ambavyo hawavijui kiundani wake? Nasema siyo sahihi kabisa mimi nitabaki kama Wema Sepetu na yeye atabaki kama Kajala Masanja na asifikirie kuwa nitakuja kuwa kama zamani na yeye halafu kama anamaindi kuhusiana na Dacutee mbona Petit Man ambaye ana uhusiano naye aliweka picha.

BOFYA HAPA KUSOMA HABARI KAMILI BONGO MOVIES.COM

Hadhi ya Elimu Imeshuka Tambaza Sekondari!

 Hapo zamani za kale.... jamani si zamani sana, Shule ya sekondari Tambaza ilikuwa inongoza kwa kutoa elimu ya hali ya juu.  Sasa hakuna tena.  Wanafunzi wa Form Six wameanguka vibaya ,mithani ya kitaifa. Nasikia hata maabara hawana tena na ni shule ya Sayansi!   Jamani!  Enzi zetu O level  tu tulikuwa na maabara, na kulikuwa na walimu na Lab Assistants!  Laakini baaya ya UPE hizo maabara ziligeuzwa kuwa madarasa!

*******************************************

KUTOKA THE CITIZEN

Tambaza teachers Flee over Form 6 National Exam Fiasco


Tambaza Secondary School, which performed poorly in this year’s Form Six examination. PHOTO | SAUM MWALIMU       

By Saumu Mwalimu, The Citizen Reporter

Posted  Friday, July 18  2014 at  11:06
In Summary
An air of sadness and disbelief engulfed the formerly top- performing school when The Citizen visited yesterday.

Dar es Salaam. While other schools were celebrating success in this year’s Advanced Certificate of Secondary Education Examination, things were different at Tambaza High School in Dar es Salaam.
An air of sadness and disbelief engulfed the formerly top- performing school when The Citizen visited yesterday.
Tambaza was for many years among the best schools in Tanzania, but it has steadily declined, and is among the ten worst performers nationally this year. The results have shocked the school community, and this was confirmed by the head teacher yesterday. Groups of students and teachers were seen huddled together, discussing the fiasco in hushed tones.
The teachers, however, hurriedly walked away as this reporter approached them to get their views on the school’s poor performance.
The headmaster, Mr Hussein Mavumba, was found going through the results in his office. He described the school’s performance as “shocking and beyond belief”.
“It is too early to say anything but as the head of this school, it is frustrating. We are doing some scientific analysis to establish why this happened...where we have gone wrong so that we can chart our next course of action.
“I’m required to explain this to my seniors, so I’m currently busy preparing a report, but it’s not easy to believe what has happened,” Mr Mavumba said.
Speaking to this reporter on condition of anonymity, some students blamed the school’s poor performance on an acute shortage of science teachers.
“Here we take science combinations, and yet we don’t have science teachers. We don’t even have even laboratories and the necessary equipment,” said one of the students.
Other students said the results were demoralising.
“It is disappointing to see your school perform so badly, but we should take this as a challenge and see where we have gone wrong,” another student said.

KWA HABARI KAMILI BOFYA HAPA:

Ugaidi Kenya - Watu 87 Wamekufa!

   NAIROBI, Kenya (AP) - Seven people were killed when gunmen attacked a bus at the Kenyan coast where previous attacks had left 87 people dead, the Kenya Red Cross said Saturday.

   The attack Friday night came at Corner Mbaya, 5 kilometers (3 miles) from the coastal town of Witu in Lamu county, the humanitarian group said. Two of those killed were security officials and five were civilians, the Red Cross said. Authorities believe many of the passengers in the 52-seater bus fled into a nearby forest.

   Al-Qaida-linked al-Shabab militants from Somalia claimed responsibility for the attack.

   "The attack was carried out in response to the Kenyan government's claim that all the areas that have recently been subject for attacks were secured after having deployed troops," the group said.

   Al-Shabab said the attackers were sending a message to Kenya that they cannot stop the group's operations in coastal areas.

   Al-Shabab has vowed to carry out attacks on Kenyan soil to avenge the presence of Kenyan troops fighting the militants in Somalia.  In September, four al-Shabab gunmen attacked an upscale in Nairobi, the Kenyan capital, killing 67 people.

   Al-Shabab has also claimed responsibility for previous attacks along the coast but the Kenyan government claims local political networks are responsible.



Massachusetts Itapokea Watoto Wahamiaji Haramu Ambao Hawakuja Nchini USA na Wazazi Wao

 Imekuwa kero na sasa nbi balaa.  Watoto wahamiaji haramu (illegal aliens) kutoka Amerika ya Kati zaidi ya 57,000 wameruka mpaka wa Mexico kuingia USA. Wana umri wa miaka mitatu hadi 17. Wamekuja bila wazazi wao. Wazazi wao wanawatuma halafu wanawambia wahakikishe wanakamatwa.  Sasa, wataoto wamekuwa wengi  kiasi kwamba serikali ya Marekani inakosa sehemu ya kuwaweka. Gavana wetu hapa Massachusetts, Gov. Deval Patrick, amekubali kuwapokea baadhi yao. Watu wameanza kuchachamaa maana wana dai wahamiaji haramu wamezidi kunyonyua huduma za wananchi wa kawaidia na waliokuja kihalali hasa mashule, na kliniki za afya.

Wanadai wazazi wao wanawatuma kwa vile Raidi Obama alitoa msamaha kwa watoto wahamiaji haramu waliokuwa hapa USA  ambao walikuwa hapa tayari.

**************************************

BOSTON (AP) - Gov. Deval Patrick on Friday proposed two possible locations in Massachusetts to temporarily shelter unaccompanied children crossing the nation's southern border.

   Camp Edwards military base on Cape Cod and Westover Air Reserve Base in Chicopee will be reviewed by officials from the U.S. Department of Health and Human Services to see if either is suitable for housing the children, most of whom are coming from Central America, Patrick said.

   Only one site would be selected, if any facility in Massachusetts is chosen.

   Patrick said the federal government is looking for places that can house up to 1,000 children for four months.

   He said each child would stay for an average of about 35 days and that all expenses will be picked up by the federal government while they are being processed for deportation, reunification or asylum.

   The children would receive food, care and education while at the facility, Patrick said, and will not attend local schools. All children would receive a medical screening before entering the state, including all essential vaccines.

   Patrick said no final decision has been made yet on whether either facility would be suitable as a shelter or when any children may start arriving.

   Chicopee Mayor Richard Kos said he's also concerned about the humanitarian plight, but said locating children at Westover Air Force Base doesn't make sense, citing insufficient housing and few facilities needed to care for children.

   "It does not work for those children, and it does not work for the city of Chicopee," Kos told reporters at city hall Friday afternoon according to The Republican newspaper. "We are more than skeptical."

   More than 57,000 children have crossed into the country over the southern border since the fall, mostly from El Salvador, Guatemala and Honduras. Some U.S. residents have opposed housing the children within their communities, spurring protests in California and Arizona.

   Patrick, who at times appeared emotional during a morning press conference, said the country and the state have a moral responsibility to look after the unaccompanied minors.

   "There are children alone in a foreign land," Patrick said. "This good nation is great when we open our doors and our hearts to needy children and diminished when we don't."

   Patrick said that any memorandum of understanding signed with the federal government will specify that the federal government will be responsible for the cost of running the facility, what period of time the facility would be open, and the conditions under which there could be an extension.

   Patrick said other states have received similar requests from the federal government to aid in what he called a "humanitarian crisis."

   State Rep. Brad Jones, the House Republican leader, said in a statement on Thursday that he will convene a meeting next week to discuss the potential impact on Massachusetts of what he called a "national immigration crisis."

   President Barack Obama has requested $3.7 billion in emergency spending to help address the situation at the border. Congressional Republicans have been pushing to significantly pare down that request.

   There is precedent for Massachusetts offering temporary shelter in crisis situations. In 2005, 235 Hurricane Katrina evacuees were housed at Camp Edwards until they could be placed in permanent housing.

   In Connecticut, state officials recently rejected a federal request to temporarily house up to 2,000 immigrant children from Central America at a mostly vacant facility built for developmentally disabled adults, pointing in part to what they said was the facility's size and deteriorating condition.

Friday, July 18, 2014

Ndege Iliyobeba Wanajeshi Kutoka Marekani Yatua Kwa Dharura Uganda!



The Plane  on the Road at Mityana Highway in Uganda - Photo from Facebook
KAMPALA, Uganda (AP) - A Ugandan police spokesman says a small aircraft carrying U.S. military personnel has made an emergency landing on a road after running out of fuel.

   Phillip Mukasa said Friday that the Piper aircraft with eight people on board - including two crew members - was returning to Uganda's Entebbe airport when it had to make an emergency landing in Mityana town, some 67 kilometers (about 41 miles) from the Ugandan capital of Kampala.

   No one was hurt and the aircraft wasn't damaged, he said, although motor traffic flow was seriously disrupted.

   He said the aircraft had been headed to South Sudan but it couldn't land there and had to return to Uganda.

   It was not immediately clear why the pilot could not land in South Sudan.
  

Thursday, July 17, 2014

Mwanamke Kutoka Kenya Agongwa na Gari na Kufariki Boston

  Wikiendi iliyopita, mwanamke kutok Kenya aligongwa na gari aina ya Pick-Up na Kufariki papo hapo! Tunachijua ni kuwa anaitwa Nancy na alikuwa na miaka 32.

Kutoka WHDH.com 

DORCHESTER, Mass. (WHDH) - A woman was hit and killed by a motor vehicle in Dorchester early Saturday morning.

Officers arrived at the intersection of River Street and Washington Street at around 5 a.m. for reports of a collision where they found the 32-year-old victim with life threatening injuries.

She was transported to Carney Hospital where she later succumbed to her injuries.

Neighbors said she was on her way to work, the first of two jobs, when she was struck. Everyone who knew her raved about her work ethic.

"She worked two jobs," said Carl Cahoon. "She got up at five in the morning went down and got the bus and did her first job."

Cahoon added that there was a purpose behind that work.

"I know she was saving her money to get her son to come back  from Kenya...8-year-old child," Cahoon said. ""Always working, always talking about 'I can't wait to get my son'...she was saving the money to have her son fly here and unfortunately it's not happening now."

Police have not identified the vehicle involved in the crash. Anyone with information is strongly urged to contact the Boston Police Homicide Unit at (617) 343-4470 or leave an anonymous tip at (800) 494-TIPS.

Monday, July 14, 2014

Mwache Mzee Balali Apumzike Kwa Amani!

Jamani, nimeshangaa tangu wiki iliyopita  kuna mzozo kuwa Marehemu Daudi Balali aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu yu au la.  Mzee Balali amefariki! Ni marehemu!  Rest in Peace Mzee Daudi Balali (1942-2008)!

Kama hamwamini basi tumeni maombi ya death certificate huko alipokufa, Maryland, USA. Kama cheti haitoshi basi mlipe hela kwenda mahakamani kuomba kaburi lake lifukuliwe na mfanye testi kwenye mabaki mtakayokuta. Inaweza kuwagharamia dola $65,000!

Kuna mtu ana Twitter akaunti ya Utani! Kuna watu wameapa eti ni Marehemu Mzee Balali anayeandika!
Kaburi la Mzee Balali huko Silver Spring, Maryland, USA
Kutoka Gazeti la Mwananchi:

Mkazi wa Kijiji la Luganga, Wilaya ya Mufindi, Iringa, alikozaliwa Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daudi Ballali analazimika kutumia saa 32 kufika katika kaburi la kiongozi huyo lililopo eneo la Silver Spring, Maryland nchini Marekani.

Ndugu wa Ballali wanaweza kutaka kwenda kuona kaburi la ndugu yao, kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawakuwahi kupata fursa ya kumzika Gavana huyo ambaye alikuwa kiongozi wa juu kabisa wa taasisi kubwa inayosimamia masuala ya fedha na uchumi wa nchi.

Mwandishi wa gazeti hili alisafiri kwa saa 24 kutoka Dar es Salaam hadi Washington, Marekani ambako alithibitisha pasi na shaka kwamba Ballali alizikwa Mei 21, 2008 katika makaburi ya Gate of Heaven, baada ya kufariki dunia akiwa nyumbani kwake Maryland, Mei 16, mwaka huo.

Safari hiyo ya siku kumi, ilianza Alhamisi Juni 26, 2014 hadi Jumapili, Julai 6. Mwandishi wa habari hizi aliligundua kaburi hilo baada ya kwenda makaburi ya Gate of Heaven kwa siku tatu mfululizo.

Siku ya kwanza, mwenyeji wa mwandishi ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sasa alimfikisha katika makaburi hayo, lakini kaburi la Ballali halikuonekana na hata mwandishi alipokwenda siku ya pili peke yake, kaburi hilo pia halikuonekana kwa kutokana na ukubwa wa eneo hilo.

Siku ya tatu, Mwandishi wa Mwananchi alilazimika kuomba msaada wa Ofisi ya Makaburi ya Gate of Heaven, ambayo ilimsadia kuonyesha eneo lilipo kaburi hilo, hivyo kuwezesha kupata picha zake.

Kaburi lake liko katika msitari wa mwisho kabisa na Ukanda wa Kijani wa miti iliyozunguka makaburi ya Gate of Heaven, likiwa limeandikwa jina la kiongozi huyo, pamoja na maneno ya Kiingereza yanayosomeka “When the heart weep for what it has lost, the soul rejoices for what it has found”.

Maana ya maneno hayo ni kwamba “wakati moyo ukiomboleza kwa kile kilichopotea, roho hufurahi kwa kile kilichopatikana”. Kaburi hili limezungukwa na makaburi mengine kadhaa ambayo si ya Watanzania, kwani kwa haraka kutokana na mazingira yalivyokuwa, Mwandishi wa Mwananchi hakuweza kuona kaburi jingine lenye majina yenye asili au kuwa na mwelekeo wa asili ya Tanzania.

Uthibitisho huu ni tofauti na hekaya za miaka nenda rudi zilizogubika kifo cha kiongozi huyo, ambaye tangu alipoondoka nchini kwenda Marekani Agosti 2007, hakuwahi kurejea na badala yake zilisikika taarifa za kuugua kwake, kifo chake na baadaye mazishi yake yaliyokuwa ya siri kubwa yakiwahusisha ndugu wa karibu pekee.

Kutokana na mazingira hayo, kumekuwapo na uvumi kwamba Ballali hakufa na pengine amefichwa kusikojulikana, madai yanayochagizwa na mtu aliyejitokeza katika mitandao wa kijamii ya Twitter na facebook, akidai kwamba yeye ni Ballali na kwamba hajafa, huku akisisitiza kuwa wakati ukiwadia ukweli utafahamika.

Mtu huyo asiyefahamika hadi sasa alianza kujitokeza Twitter, Oktoba Mosi, 2012 pale aliposema “Nitakutana na Rais Kikwete (Jakaya) na ujumbe wake wiki hii hapa Marekani”. Mtu huyo alidai kwamba alikuja nchini Tanzania na kukaa karibu na Hoteli ya Hyatt Kempinski Kilimanjaro na baadaye kuondoka ghafla kwa kile alichokiita sababu za kiusalama.

Novemba 13 mwaka huo alituma ujumbe akisema:“In Dar es Salaam, Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kempinski Kilimanjaro Hotel. Feels good to be close to my former office, BoT,” akimaanisha kwamba niko Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, najisikia vizuri kuwa karibu na ofisi yangu ya zamani BoT.

Mtu huyo ambaye sasa tunaweza kuthibitisha kuwa ni feki amekuwa akiendelea kutuma ujumbe akijitambulisha kwa jina hilo la Ballali.

Ballali alifariki dunia kama ilivyotagazwa, lakini ilikuwaje akaenda safarini Washington, ugonjwa wake na hata kifo chake kilikuwaje? Je ndugu zake wanasemaje, safari ya kwenda Marekani ilikuwaje? Fuatilia mfululizo wa habari hii itakapoendelea kesho.



Source: Mwananchi

*********

 

Wazungu Watajirika Kwa Kuuza Bangi Kihahali Marekani!

 Wazungu Marekani watajarikia kwa kuuza bangi kihalali sasa.  Mnaona hizo kliniki za 'Medicinal Marijuana' zinavyoshamiri Marekani? Je. wale weusi waliofungwa kwa kuuza bangi tena kidogo sana wataendelea kufungwa? Hivyo vifungo vimeharibu maisha ya watu, na familia nyingi pia.

Dr. Farrah Gray awapasha!


 
www.FarrahGray.com

Sunday, July 13, 2014

Mahojiano na washiriki wa maonyesho ya Utamaduni wa Kenya

Kati ya Juni 25 na Julai 6, jiji la Washington DC lilikuwa mwenyeji wa maonyesho ya kila mwaka ya yanayohusu maisha a watu na jamii mbalimbali.
Mwaka huu, nchi ya Kenya ilishirikishwa, wakionyesha utamaduni wao na changamoto za kuzidumisha katika zama hizi za sayansi na teknolojia.
Kwanza Production ilipata fursa ya kutembelea maonyesho hayo na kuzungumza na baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo ambapo walieleza mengi ya kufurahisha.
KARIBU UUNGANE NASI

Zaidi ya washiriki 100 kutoka nchini Kenya waLIkuja hapa jijini kuonyesha mambo mbalimbali kama kutengeneza vyungu kwa ufinyanzi, uchongaji vinyago, mapambo ya shanga, useremala, nakshi za majengo, ujenzi wa majahazi, mapishi , muziki na mengine yanayotunza utamaduni wa nchi hiyo
Maelezo ya ujenzi na sehemu za JAHAZI (DHOW) toka kwa Ali Skanda aliyetoka Lamu Kenya
Na mtangazaji mkongwe abdushakur Aboud mbele ya Jahazi lililoletwa kwenye makumbusho ya hapa Washington DC kutoka Lamu nchini Kenya
Mtaalamu wa mapambo yatokanayo na shanga na usimamizi wa filamu nchini Kenya Emmah Irungu
Mwandishi wa habari kutoka Kenya BMJ Mureithi

Drug Lord Akatamatwa Zanzibar! Alikuwa na Zaidi ya Kilo 5,000 za Unga!

 Duh! Kilo 5,605 za Unga!!!!  Street Value Je?

******************************************

Kutoka Ippmedia.com

Police arrest drug baron in Zanzibar

12th July 2014

Abeid Aman Karume International Airport
 
Police in Zanzibar arrested Ali Sleyum Rashid at the Abeid Aman Karume International airport on Wednesday in connection with possession of 5.605 kilogrammes of cocaine.

Rashid (39) who had boarded Oman Air flight No WY.717 that landed at the airport from Muscat was arrested at around 2: 45 pm.

The police were also holding four airport employees believed to be close friends of the suspect. It was not immediately stated if the four employees acted as accomplices.

Speaking to the press yesterday in Zanzibar, the Isles Director of Criminal Investigation Yussuf Ilembo said the police worked on a tip off from some sources to search his luggage immediately after arrival.
He said they found 14 hand bags for women before they found cocaine stacked in each of them.

The suspect had travelled using passport number AB 363906 issued on December 29, 2009 by the Immigration Department head office in Dar es Salaam.

 He said the passport showed the suspect travelled to many countries, including Brazil, China, Hong Kong, Japan, South Africa and some Arab states.
SOURCE: THE GUARDIAN

Saturday, July 12, 2014

Chidi Benz Ampiga Ray C

Jamani, jamani, jamani! Mambo gani tena haya! Dume anampiga dada wa watu namna hii! Halafu bado huyo dume anaitwa Staa! Huyo ni mhalifu na anstahili kuwa jela kwa kitendo alichokifanya kwa Ray C.  Mmeona hatua zilizichukuliwa dhidi ya Chris Brown alivyomtwanga Rihanna? Nilipokuwa TAMWA, nilishughulikia sana maswala ya uoneveu dhidi ya akina mama. Loh! Huyo jamaa siyo Chid Benz ni Chizi Benz!

*********************************************

Kwa habari kamili ya Tukio Tembelea GLOBAL PUBLISHERS:


http://api.ning.com/files/Jlj7Yacjzg3*Iyvt90DSt5oT20Lf6U4hQjUZP8Q9QGKLl7Ba9HNopUt0VXWvUSXeDCKIuek51EB2qvq0z85a*SGDrfCArDwR/chdi.jpg
Huyo ni Mwanaisha ambaye alipigwa kabla na Chid Benz

Bongo Flava Star - Rehema Chalamila aka. Ray C
 
Ray C Hospitalini Baada ya Kipigo


Na Musa Mateja
Uonevu! Rapa mwenye ‘swagger’ za Ja-Rule Bongo, Rashid Makwilo ‘Chid Benz’, anadaiwa kukwaa kisanga kingine kibaya baada ya kukurupuka kutoka nyumbani kwake na kwenda kumvamia staa mwenzake, Rehema Chalamila ‘Ray C’ nyumbani kwake anapoishi na kumtwanga makonde ikiwa ni siku chache tangu jamaa huyo apate msala mwigine wa aina hiyo.

 TUJIUNGE NYUMBANI KWA RAY C
Ilidaiwa kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita nyumbani kwa Ray C, Changanyikeni jijini Dar es Salaam ambapo ilisemekana kwamba Chid Benz alimvamia mishale ya saa 4:00 usiku kwa gia ya kumsaka mzazi mwenzake aliyemtaja kwa jina moja la Mariam.


CHID BENZ ATAKA KUMUONA MWANAYE
Ilidaiwa kwamba Chid Benz alisema kuwa alizungumza na mpenziye huyo kwamba alitaka kwenda kumuona mwanaye ambapo Mariam alimjibu kwamba kwa muda huo alikuwa nyumbani kwa Ray C  Changanyikeni.

UNGA WATAJWA
Sosi wetu alidai kwamba baada ya kujibiwa hivyo, Chid Benz alianza kulalama na kumwambia anamfuata palepale kwa nini usiku ule alale kwa Ray C, wakati ana uwezo wa kwenda nyumbani au amekwenda kwa staa huyo ili kunywa dawa zao za kuondoa sumu ya madawa ya kulevya ‘unga’,
 jambo ambalo jamaa huyo siku zote huwa hataki hata kulisikia masikioni mwake.


CHID BENZ AWAVAMIA
“Huwezi kuamini baada ya muda kama wa saa moja, Ray C na Mariam wakiwa ndani wakitazama TV, ghafla mlango ulisukumwa kwa nguvu kisha akaingia Chid Benz na kumdaka Mariam na kuanza kumshushia kipigo.“Yaani huo mshtuko walioupata walidhani wamevamiwa na Al-Shabaab.
KIBAO CHAMGEUKIA RAY C
“Mungu mkubwa kwa sababu Mariam alifanikiwa kuchoropoka na kukimbilia chumbani ndipo kibao kikamgeukia Ray C.
“Ray C akiwa anashangaa ghafla naye alipokea kipigo kikali kutoka kwa Chid na kumsababishia majeraha mbalimbali mwilini.
RAY C AKIMBILIA KWA MAJIRANI
“Baada ya kuona maji yanazidi unga, Ray C alitafuta upenyo na kukimbilia kwa majirani huku akipiga kelele za kuvamiwa, mara moja majirani waliambatana naye mpaka nyumbani kwake.
“Walipofika Chid Benz alikuwa ametumia staili za kininja kwa kuruka geti na kutokomea kusikojulikana huku akiwaacha Ray C na Mariam wakiangua vilio kwa kipigo kikali walichopokea.
RAY C AVUJA DAMU
“Ray C aliumia mkono na mguu ambao ulionekana ukivuja damu. Mariam alikuwa akililia mbavu zake kuchakazwa kwa makonde mazito na upande mwingine baadhi ya vyombo vya ndani vikionekana kuvunjwa na vingine kusambaratishwa kufuatia tafrani iliyozuka muda mfupi baada ya Chid Benz kutia maguu nyumbani hapo,” chanzo kilishusha madai hayo mazito.

RAY C ATIRIRIKA SAKATA LILIVYOKUWA

Akizungumzia na gazeti hili Alhamisi iliyopita juu ya sakata hilo, Ray C alisimulia mkasa mzima: “Kweli Chid Benz alikuja nyumbani kwangu na kunivamia.
“Alinipiga vibaya sana na kuvunja baadhi ya vitu vya ndani kwangu, jambo ambalo lilinishangaza zaidi ni namna alivyopafahamu nyumbani kwangu hadi kuja kunifanyia fujo nikiwa na mzazi mwenzake, Mariam ambaye nilitoka naye ofisini kwangu.
“Ujue jana (Jumatano) tulikuwa na kazi sana ofisini kwangu mimi na Mariam, sasa kutokana na kubanwa na kazi kweli muda ulienda sana hivyo nikamwambia Mariam akalale kwangu.
“Kwa kuwa muda ule ilikuwa ngumu kwenda kwao Mbezi Beach, Mariam alikubali na tulikwenda wote nyumbani kwangu.

“Huko nyuma Mariam alikuwa mwathirika wa madawa ya kulevya lakini baada ya kusikia mimi nimeacha, naye aliachana nayo na kuanza kutumia dawa za kuondoa sumu.
“Tumeendelea kutumia naye dawa na sasa ameshapona kabisa hivyo kuna baadhi ya kazi nimekuwa nikimshirikisha kunisaidia kwenye ofisi yangu. Pia alishawahi kumshawishi Chid Benz ili aje kutumia dawa lakini jamaa alikataa na kumfanyia vurugu sana huku akimkataza kuwa na mimi kwa madai mimi ndiyo namfanya amwambie kuachana na utumiaji dawa za kulevya.
“Sasa jana alipojua hivyo nadhani Chid Benz alikuja kutimiza dhamira yake ambayo siku nyingi alikuwa akiahidi kunipiga.”

SOO LIPO POLISI

Ray C alisema baada ya tukio hilo alikwenda kuripoti kwenye Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Kinondoni na kufunguliwa jalada la kesi ambapo Chid Benz anasakwa na polisi.
Juhudi za kumpata Chid Benz hazikuzaa matunda kwani simu yake haikuwa hewani hivyo jitihada zinaendelea na kama ana ufafanuzi au utetezi anaweza kutupigia.

CHID BENZ NI TATIZO?

Chid Benz anadaiwa kuwa ni tatizo kwani tukio hilo la Ray C amelifanya wakati akiwa na tukio la pili kwa wanawake kwani kwenye Mahakama ya Mwanzo, Ilala ana kesi mbichi aliyoshitakiwa kwa kosa la kumpiga mrembo aitwaye Mwanaisha.
Mbali matukio hayo pia Chid Benz ana rekodi ya kukorofishana na wasanii wenzake kama Kalapina na marehemu Ngwea.

KWA HABARI ZAIDI TEMBELEA EDWIN MOSHI BLOG

La Kufanya Ukisimamishwa na Polisi Trafiki Tanzania - Know Your Rights


Kuna nini Mbeya? Watu 135 Wameuawa!

Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi
KWA HISANI YA LUKWANGULE BLOG:

WATU 135 wameuawa katika matukio tofauti yaliyotokea mkoani Mbeya katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Julai mwaka huu.
 
Kiasi hicho cha matukio ya mauaji ni sawa na pungufu ya matukio 21 sawa na asilimia 14 ikilinganisha na yale 156 yaliyotokea katika kipindi kama hicho mwaka jana.
 
Akitoa taarifa ya utendaji wa jeshi la polisi mkoani Mbeya, Kamanda wa polisi mkoani hapa Ahmed Msangi alisema katika takwimu hizo mauaji yaliyotokana na wananchi kujichukulia sheria mikononi yalikuwa 33.
 
Alisema mauaji yaliyosababishwa na imani za kishirikina yalikuwa 23 sawa na matukio ya mauaji yaliyotokana na sababu nyingine huku matukio ya mauaji yaliyosababishwa na wivu au ugoni yalikuwa 20.
 
Matukio ya mauaji yaliyotokana na ugomvi wa majumbani yalikuwa 16, matukio ya ugomvi vilabuni 11 na matukio ya kulipiza kisasi yalikuwa tisa.
Alisema katika kipindi hicho wahamiaji haramu 159 walikamatwa kati yao 152 walikuwa raia wa Ethiopia, 23 raia wa Burundi,10 Wasomali, saba Wapakistani, wawili kutoka Malawi na mmoja akiwa ni raia wa Msumbiji.
 
“Katika kipindi hicho tumeweza kukamata bunduki 19 ambapo gobori zilikuwa 15, bastola mbili zilizotengenezwa kienyeji, Riffle moja na SMG moja. Pia zilikamatwa silaha mbili baada ya majambazi kuuawa katika jaribio la kufanya unyang’anyi. Silaha hizo ni SMG yenye namba 3514 na AK-47 namba 592058 na risasi 25 kwenye magazini,” alisema Kamanda Msangi.
 
Aliongeza kuwa katika kipindi hicho kiasi cha lita 479 za gongo pamoja na mitambo 16 ya kutengenezea pombe hiyo vilikamatwa.
 
Kilo 296 na gramu 678 na miche 314 ya bangi zilikamatwa sambamba na mashamba matatu ya bangi yenye ukubwa wa jumla ya ekari moja na robo.

Mkutano wa Injili Mijini Morogoro Na Pastor Daniel Moses Kulola

Pastor Daniel Moses Kulola anamaliza Mkutano wa Injili, huko Chamwino, Morogoro.



Kutembelea Blogu ya Pastor Daniel Moses Kulola BOFYA HAPA:

Masanja Mkandamizaji in the House

 
Hata waimbaji Kutoka China walishiriki

Tuesday, July 08, 2014

Brazil Wapondwa Vibaya na Ujerumani Katika Mashindano ya World Cup!

Katika Mashindano ya Kombe la Dunia huko Brazil, Brazili ilipondwa vibaya sana na Ujerumani!  Brazil wameanguka  1-7.  Duh! Hata Pele ana aibu!

Kwa habari za Ushindi wa Ujerumani BOFYA HAPA:

Shabiki wa Brazil akilia machozi baada ya Brazil Kutolewa katika mashindao ya World Cup. Unaweza kuona picha zaidi kwa  KUBOFYA HAPA:

Saturday, July 05, 2014

Mahojiano ya Kwanza na Diamond Platinumz Baada ya BET Awards

Diamond Platnumz na DMK kwenye utoaji tuzo za BET Los Angeles
Photo Credits: DMK Global Promotions' facebook page
Karibu katika mahojiano ya Kwanza Production na Damond Platnumz. Msanii mwenye mafanikio makubwa kutoka nchini Tanzania
Amejiunga nasi kwa njia ya simu punde baada ya kuhudhuria utoaji tuzo za BET ambako yeye alikuwa mmoja wa waliokuwa wakiwania tuzo hizo.
Kazungumza mengi kuhusu TUZO HIZO.
Alipopokea na alivyopokea uteuzi wake, aliloliona kwenye tuzo hizo, ulinganishaji wake katika utoaji tuzo hizi na za Tanzania / Afika, alichojifunza, faida ya kuja kushiriki hili na hata mikakati yake ijayo kuhakikisha kuwa muziki wa Tanzania unafika mbali zaidi.
SWALI jingine alilojibu ni kuwa....ni kweli kuwa ili muziki wa Tanzania ushinde tuzo ni lazima uwe na mahadhi ya Afrika Magharibi (kama muziki wake wa Number One) ama Afrika Kusini 
Amejiunga nasi kwa msaada wa promota Dickson Mkama almaarufu DMK ambaye pia ndiye meneja wa msanii huyo hapa nchini.
KARIBU


Friday, July 04, 2014

Leo ni SIkukuu ya Uhuru Marekani - Independence Day

1123156635066_united_states_independence_day_picture.jpg (465×308)

HAPPY INDEPENDENCE DAY! 

238 Years of Independence from the British!

 1776 - 2014


Wadau, leo Marekani inasherekea miaka 238 tangu Uhuru kutoka kwa Waingereza!

Thursday, July 03, 2014

'Specific threat' of attack at Entebbe airport

KAMPALA - The US embassy in Uganda warned Thursday of a "specific threat" by an unknown group to attack the international airport serving the capital Kampala.

The alert came as travellers flying to the United States from Europe and the Middle East faced tighter security because of new concerns about the development of explosives that could circumvent airport security.

"The US embassy has received information from the Uganda police force that according to intelligence sources there is a specific threat to attack Entebbe International Airport by an unknown terrorist group today, July 3rd, between the hours of 2100-2300 (1800 GMT to 2000 GMT)," the statement said.

Although it did not name any group, Al-Qaeda linked Shebab insurgents have claimed recent attacks in Kenya and Djibouti.

Uganda has troops in Somalia as part of the African Union force fighting the Shebab and is on high alert amid fears of attacks by the Islamist militants.

'Specific threat' of attack at Entebbe airport



Uganda in danger of Terrorist Attack!

CULTURAL WARS TRAILER - Sinema Mpya Iliyotengenezwa na waTZ New York!



The new movie, “Cultural Wars”, is now available on DVDs and there is also an online option to purchase your electronic copy for your Ipad.  To get your DVD or electronic copies please visit the following websites:
 
 
The trailer for the movie is available to watch for free at:http://www.youtube.com/watch?v=B2rnWOufA38
 
This is a must-watch family movie that narrates a love story in New York City. It is also a D. J. Mhella production’s first full-length feature. Mhella is an independent filmmaker and he needs your support in making his filming dreams come true. Your support through buying this movie will be appreciated.
 
For any support and questions please write to: DJMhellaproduction@gmail.com