Friday, January 30, 2015

Nape Nnauye Aanza Amsha-Amsha ya Miaka 38 ya CCM Mjini Songea

 Wananchi wakiwa katika shamrashamra za kumpokea Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye leo kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Ruvuma mjini Songea leo, alipowasli kwa ajili ya kuanzisha amsha amsha ya Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM ambayo inafanyika Jumapili hii, Kitaifa mjini Songea kwa kuongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
 Mratibu wa Maadhimisho ya Miaka 38 ya CCM, Emaanuel John Nchimbi akiwasili kwenye Ofisi hiyo ya CCM mkoa wa Ruvuma leo kumpokea Nape
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye (kushoto) akiongoza wananchi kwenda katika maeneo mbalimbali kuzindua mashina ya Wajasiriamali wa CCM na kuhutubia mkutano wa hadhara, baada ya kuwasili leo mjini Songea
  Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye (kushoto) akiongoza wananchi kwenda katika maeneo mbalimbali kuzindua mashina ya Wajasiriamali wa CCM na kuhutubia mkutano wa hadhara, baada ya kuwasili leo mjini Songea
  Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye (kushoto) akiongoza wananchi kwenda katika maeneo mbalimbali kuzindua mashina ya Wajasiriamali wa CCM na kuhutubia mkutano wa hadhara, baada ya kuwasili leo mjini Songea
 Vijana wakiwa wameacha shughuli zao kumshangilia Nape alipokuwa akipita mitaani mjini Songea wakati akienda kufungua mashina ya wajasiriamali wa CCM na kuhutubia mkutnao wa hadhara
 Mwanamke akihanikiza kwa vigelegele kumshangilia Napa wakati wakipita kwenye moja ya mitaa maarufu ya mjini Songea wakati akienda kufungua matawi ya Wajasiriamali wa CCM na kuhutubia mkutano wa hadhara
 Kina Mama wakimshangilia Nape wakati akipita kwenye mita hiyo
 Nape akiwashukuru wananchi waliokuwa wakimshangilia wakati wakipita kwenye mitaa hiyo leo
 Baadhi ya viongozi wakimsubiri kumlaki Nape kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Songea mjini leo
 Nape akisalimiana na viongozi kwenye Ofisi hiyo ya CCM wilaya ya Songe mjini
 Nape akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya CCM Songea mjini leo
 Nape akikata utepe kuzindiuashina la wakereketwa wajasiriamali wa CCM katika Stendi ya mjini Songea
 Nape akipandisha bendera ya CCM kuzindua tawi hilo la CCM kwenye Stendi ya mabasi mjni Songea
 Nape akimsalimia Mjumbe wa Shina namba 12, Margareth Mtivila,  Songea mjini
 Nape akipandisha bendera kuzindua shina la wakereketwa wajasiliamali wa CCM Liziboni mjini Songea
 Ofisi ya CCM iliyozaa shina hilo la wakereketwa ilizinduliwa na Paul Sozigwa
 Nape akimkabidhi kadi ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Hadija Nyoni, baada ya kuzindua shina hilo. Jumla ya Vijana 89 walikabidhiwa kadi hizo
 Nape akizindua tawi la CCM Liziboni

 Nape akizindua Mradi wa Ujenzi wa mabanda ya Biashara Kata ya Lisiboni
 Nape akipanda mti wa kumbukumbu baada ya kuzindua ujenzi wa mradi wa vibanda hivyo vya Biashara, Liziboni
 Nape akiingia kwenye jengo la Ofisi ya CCM tawi la Mji Mwema, wilaya ya Songea mjini
 Nape akipaka rangi kwenye Ofisi hiyo ya CCM tawi la Mjimwema
 Nape akiwa katika picha ya pamoja na vijana wajasiriamali wa mradi wa kufuga kuku Mjimwema
 Nape akifungua shina la Wajasiriamali wa CCM Mjini Mwema
 Nape akikagua ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Ruwiko
 Nape akitoa pole kwa familia ya askari wa Magereza, wakati wa maziko ya askari huyo katika kata ya Ruwilo, wilaya ya Songea  mjini
 Nape akitazama picha ya askari huyo ambaye amefariki kwa ajali
 Nape akiwapa pole ndugu wa Marehemu huyo
 Nape akizindua shina la Wakereketwa wa CCM, tawi la Chuo Kikuu cha St. Joseph Songea mjini
 Bibi Riziki Ngonyani (92) wa mjini akishangilia wakati wa uzinduzi wa shina hilo la St. Joseph
Nape akiagana na baadhi ya viongozi wa CCM shina la Chuo Kikuu cha St. Joseph mjini Songea. Picha na Bashir Nkoromo

Sunday, January 25, 2015

Mwanaume Ajifanya Mwanamke Ili Apate Kazi Dar

 Kutoka Facebook

 
LAHAULA UMEISIKIA HII??? Katika hali isiyo ya kawaida kijana mmoja mwenye jina la Naftaeli Mbowe ameibua mapya jijini Daresalam. Kijana huyu ambaye ni graduate wa sociology katika moja ya vyuo hapa nchini alimaliza chuo mwaka 2011 na kufaulu vizuri sana. Kutokana na maisha ya kuiga akiwa chuoni alijitumbukiza kwenye siasa na kujidai ni mwanaharakati wa chadema hivyo kutokana na uwezo wake darasani aliweza kujenga hoja zilizomfanya akajulikana na uongozi wa juu wa CDM.

Alipomaliza chuo kijana huyu alichukuliwa na viongozi hawa wa ufipani kwa ahadi kuwa aendelee kukisaidia chama ambapo alipangwa kwenye department ya matusi mtandaoni kwa ujira wa kulipiwa chumba jijini daresalam na kulipwa shilingi laki moja kama posho ya mwezi. Chakula na vinywaji walikuwa wanapata kwenye getho walilopangiwa mtaa wa kimara Bucha. Kijana huyu amekuwa akifanya kazi hiyo kwa muda mrefu na yupo humu humu kundini kwa jina bandia. Kutokana na chama kufilisika siku za hivi karibuni kwa kuendekeza kesi za kupinga kila jambo la serikali na safari za viongozi zisizokuwa na tija vijana hawa walitelekezwa.

Kijana huyu toka mwaka 2013 amekuwa akisota mtaani bila mafanikio yoyote ndipo alipoamua kujibadilisha jinsia kwa kuvaa nguo za kike na kusuka rasta ili aombe kazi za uhasegirl na azma yake hii ilitimia. Aliajiriwa na mama mmoja asiyekuwa na mume maeneo ya ubungo msewe na hakuweza kumshtukia kwa muda wa miezi miwili kwani aliishi kwa umakini mkubwa sana. Juzi ijumaa limemtokea la kumtokea baada ya mtoto wa kiume wa mwenye nyumba kwenda kumpiga chabo akioga ili afaidi kuona maumbile ya beki tatu huyo.

Alishangazwa na alichokiona ikabidi amkasirikie mama yake sana kwa kumleta mwanamme ndani ya nyumba yao huku akisingizia ni mwanamke. Gadhabu zilimpanda zaidi kwa kuwa njemba hilo lilikuwa likilala na dada yake ndipo njama za kumuumbua bila mama yake kujua ziliposukwa.Alipotumwa sokoni mtoto wa mama wa kazi ambaye ni wa kiume aliamua kufuatilia nyuma ili kumuumbua, huku akiwa na wenzanke walimsimamisha na kumshushia kipigo cha maana ndipo alipoelezea kisa kizima.

Vijana wa chadema mliopo kwenye magetho mbali mbali okokeni sasa njooni ccm. mtaumbuka mjini hapa.

Barua ya Kitapeli

Hello,

I hope this email gets to you this time as this is my third time of sending it? I have tried without success to locate your contact address and telephone number and I resorted to communicate with you via email which is an unconventional means of relaying an important message such as this. Kindly accept my sincere apology if my email sounds offensive since you were not notified previously about this inquiry.

My name is George Wallace, I am an attorney and a Certified Private Investigator (CPI) accredited by Precise Business Consulting. We are presently conducting a standard process investigation and recommendation exercise on behalf of Credit Suisse Bank , a financial investment arm of Credit Suisse Group. This investigation is in respect of a deceased customer ( Names withheld ) who shares the same surname with you including circumstances surrounding his huge financial investments.

However, you may be interested to know that I got your impressive information after a very conscious search online for a suitable successor to the deceased customer while tracing extended family ancestry records and I have decided to contact you before concluding my investigation.

The customer died intestate and nominated no successor in title over the huge financial investments he made at Credit Suisse Bank and we have been assigned to recommend a beneficiary to secure his lodgment before the bank gets it confiscated in the next 20 working days.

The essence of this message is to request you to provide answers/comments on any or all of the four questions below:

1. Are you aware of any relative or extended family of yours born on the 17th of February 1946 who shares the same surname with you and whose last known location was the United Kingdom ?

2. Are you aware of any reasonable financial investments made by this person at Credit Suisse Bank , a financial investment arm of Credit Suisse Group?

3. Could you establish beyond reasonable doubt your eligibility to assume status of successor in title to the deceased if you are legally recommended to the Bank ?

4. Would you advance a substantial part of the funds as donations to charity if you are eventually approved by the bank as the lodgment beneficiary ?

Your answers to the questions above would help to determine our recommendation to Credit Suisse Bank towards legally appointing you to inherit this investment fund after previously certified investigation by the bank had yielded negative results that there was no known relation to the deceased customer.

Be advised that we are constrained at this point from giving you detailed information concerning the investigation process for security reasons.

I would provide you with additional information on receipt of your response.

Thank you for accommodating our inquiry.

Yours Faithfully,

Mr. George Wallace.

Note: Please do not respond to this INQUIRY if you have no idea about the above specified questions.

Saturday, January 24, 2015

Punguza Hasira!

Daktari aliingia hospitalini kwa haraka sana baada ya kuitwa kwa shughuli ya Upasuaji wa haraka, alipokea simu haraka, na kuvaa nguoza kazi na kuelekea moja kwa moja kwenye chumba cha upasuaji.
Wakati akielekea kwenye chumba cha upasuaji alimkuta Baba wa mtoto anazunguka huku na huku karibu na chumba hicho akimsubiria Daktari.
Baada ya kumuona tu, Baba mtoto akapayuka: “ Kwanini umechelewa kuja? Hufahamu kama maisha ya Mtoto wangu yapo hatarini? Hivi unayajua majukumu yako?”
Yule Daktari alitabasamu na kumwambia: “ Samahani sana, Sikuwa Karibu na Hospitali na nimejitahidi kuja kwa haraka sana baada ya kupokea simu kutoka hapa hospitalini….. Na kwakuwa nimeshafika ningekuomba upunguze jazba na hasira ili nifanye shughuli yangu” “Punguza hasira?!
Hivi ingekuwaje kama Mwanao ndiye angekuwa chumba cha upasuaji sasa hivi, ungeweza kupunguza hasira? Kama mwanao ndiye angekuwa anakufa sasa hivi ungefanyaje?” Yule Baba aliongea kwa hasira sana.
Yule Daktari alitabasamu tena na kumjibu: “Daktari hawezi kurefusha maisha ya Binadamu. Nenda katulie na umuombee mwanao, sisi tutajitahidi kadri kwa uwezo tulionao kwa Baraka za Mwenyezi Mungu”
“Kutoa Ushauri kwa vitu visivyo wahusu ni rahisi sana” Alinong’ona yule Baba mwenye mtoto.
Upasuaji ulifanyika kwa masaa kadhaa mara tu baada ya kumalizika Daktari alitoka akiwa anafuraha, “Asante Mungu! Mtoto wako amepona!” Kama una swali lolote utamuuliza Nurse!!” Bila ya kumsubiri Baba Mwenye mtoto kujibu chochote aliondoka kwa haraka kwenye eneo la upasuaji.
“ Kwa nini ni mkorofi sana huyu Daktari? Yaani hawezi hata kusubiri kidogo nimuulize maendeleo ya mwanangu” Baba wa mtoto alimjadili akiwa na nurse baada ya Daktar kuondoka.
Nurse akamjibu, huku akitokwa na machozi:
“Mtoto wake alifariki jana kwenye ajali ya gari, alikuwa katika mazishi ya mtoto wake wakati tunampigia simu aje Hospitali kwa ajili ya upasuaji wa mtoto wako. Amefanikiwa kuyaokoa maisha ya mtoto wako, kwahiyo ameondoka kuwahi mazishi ya mtoto wake.”

HEKIMA:

1. “USIMHUKUMU MTU YEYOTE…. SABABU HUYAJUI MAISHA YAKE NA KIPI
KILICHOMKUTA KWENYE MAISHA YAKE.


2. “TENDA WEMA KADRI UWEZAVYO BILAYA KUJALI HALI ULIYONAYO.

Mungu Akulinde Sospete Muhongo

MUNGU AKULINDE  SOSPETER MUHONGO

Na Happiness Katabazi

LEO  saa tano asubuhi, Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo alitangaza rasmi kujiuzuru nafasi hiyo ya uwaziri kwasababu ya zogo la Escrow.

Tangu mwanzo kupitia makala yangu msimamo wangu niliweka wazi Kuwa naunga mkono Utendaji kazi wa Profesa Muhongo na hata Leo hii ninavyoandika makala hii sitabadilisha msimamo wangu Kuwa Kwangu Profesa Muhongo ni Miongoni mwa Mawaziri wa Nishati na Madini ambao nimewashuhudia Kuwa ni mawaziri ambao wameacha alama ya kukumbukwa.

Pia tangu mwanzo nilisema wazi kupitia makala zangu mbalimbali kwa jicho la Sheria Katika zogo la Escrow Hakuna Mashitaka ya wizi Kama baadhi ya watu walivyokuwa wakiwa hukumu Moja kwa Moja watu  waliotajwa kwenye zogo la Escrow Kuwa ni wezi na kwamba Fedha za Escrow zimeibwa.

Hoja yangu ilipingwa  na baadhi ya watu waliokuwa wakisema Fedha za Escrow ni za umma na fedha hizo za Escrow zimeibwa na waliiba ni wezi wanastahili kushitakiwa kwa wizi, ilikuja Kufungwa mkono na Rais Jakaya Kikwete, Disemba 22 Mwaka Jana, Katika mkutano wake na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam, pamoja na mengine alisema hatukuwa na wizi Katika Fedha za Escrow na Fedha za Escrow siyo mali ya umma.

Pia mapema Mwaka huu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ili wafungulia  Kesi ya kupokea Rushwa kutoka kwa Lugemalila baadhi ya maofisa wa serikali ambao waliotajwa kwenye zogo la Escrow.

Tusubiri hatima ya Kesi hizo itapofika Tamati na tusubiri pia ushahidi utakaotolewa na Huyo Lugemalila  je Lugemalila akifika mahakamani atatoa ushahidi wa ni kweli au si kweli aliwapa rushwa? pia tusubiri utetezi wa washitakiwa hao na uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, utakapotolewa.

Profesa Muhongo ametaja baadhi ya Sababu zilizomsukuma kufikia uamuzi huo, Nampongeza kwa uamuzi huo licha amekuchukua wakati Tayari mashankupe na mapashukuna  wameishalipaka matope jina lake Mbele ya Jamii.

Waswahili wanasema penye ukweli, uongo ujitenga. Hivyo ipo siku ukweli wa hili zogo la Escrow utakuja kujulikana nani muhasisi wake?  Kwanini waliliasisi zogo hili?,Muhongo alishiriki kwa kiasi gani Katika jambo Hilo?Ni kweli Katika Utawala wa Muhongo Wizara ya Nishati ilipata Hasara na kwamba Hakuna jambo lolote la maendeleo alilolifanya?

Aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa wakati akitoa hotuba yake bungeni wakati ajijuzuru  pamoja na mambo mengi alisema ; ' Tukiruhusu kila mwanasiasa ajijuzuru kwa tuhuma tu ambazo hata hazijathibitika Hakuna mwanasiasa atakayebaki salama'.

Kweli sasa mantiki ya ubashiri huo wa maneno ya Mzee  Lowassa yameanza kutimia.

Hongera Muhongo kwa uamuzi huo Kwani utakupa fursa ya kwenda kufanya shughuli nyingine kwa Amani na utulivu kwa watu wenye akili timamu ambao wanamisimamo usiyoyumba na Kamwe hawaamini katika majungu na upashukuna.

Mema uliyoyafanya Katika Wizara ya Nishati na Madini,tutayakumbuka na tutaheshimu mchango wako katika sekta ya nishati na madini.

Utendaji kazi wako kumbe ulikuwa ukiwakera baadhi ya walafi .Na watu wanaofikiri sawa sawa tunajiuliza ni kwanini kila kukicha Mawaziri wa Wizara ya Nishati na Madini hasa katika serikali ya awamu ya nne wamekuwa wakishambuliwa wazi wazi na mwishoe wamekuwa wakijiuzuru au kuondolewa katika wizara hiyo?

Mbona Wizara Kama Wizara ya Maendeleo ya Jinsia na Watoto hata siku Moja hatushuhuudii wanasiasa uchwara wakikomalia Kuwa mawaziri wake wameshindwa kazi Kwani kila siku ripoti zinaonyesha watoto wadogo ,wanawake wanafanyiwa vitendo Vya kikatiri Kama kubakwa na Kuuwawa?

Ni Wizara ya Nishati na Madini tuu ndiyo inastahili kumulikwa ? .Jibu ni Jepesi hapa ni manyang'au yenye Nguvu za kifedha yalizibiwa mirija ya kufanya biashara zao kwa njia chafu Katika sekta ya Madini na Nishati.

Ikumbukwe Kuwa wale wote ambao mnatumia Hiari na uchafu wa kila aina kuwachafua wenzenu na kuakikisha wenzenu wanatoka madarakani kwaajili ya mashinikizo yenu, ipo siku na Nyie wakati wenu utafika wa kulipwa hapa hapa na Mungu malipo ya hizo hira Zenu na msije kulia na Mtu.

Nchi hii Ilipofika hivi sasa, majungu, fitna,ushirikina, uzandiki Ndio umetawala na umeshika hatamu.Watu wasiyo na hatia na siyo kwenye Nyanja za siasa tu wanaangamia kwa ushenzi huo.

Imekuwa nchi ya watu tunaopenda Ujinga Ujinga na uzushi halafu na mbaya zaidi tabia hizo zinafaywa na wanaume amba wanawake nyumbani eti tunajiaminisha nchi hii itapata maendeleo kwa haraka.

Wito wangu kwa Watanzania wanaishi nchi za nje na kufanya kazi katika taasisi za kimataifa nje ya nchi na wamesoma vizuri ,wasiwe wepesi sana kurudi nchi Kuja kufanyakazi Hasa za kisiasa kwa kisingizio eti serikali imewaomba sana Kuja Tanzania kufanya kazi.

Nawaomba mjifunze kwa yaliyowakuta wenzenu ambao walikuwa wakifanyakazi nje ya nchi akiwemo Profesa Muhongo ambaye alikuwa akifanya kazi nje ya nchi, serikali ya awamu ya nne chini ya Rais Jakyaa Kikwete ikamuona wa maana sana, ikamtaka arejee nchini aje alitumikie nchi na kweli alikuja kuitumikia lakini malipo aliyoyapata ndiyo hayo mmeyaona.

Ambayo minayafananisha na tabia zinazofanywaga na waswahili swahili huku mtaani za kumkodishia ngoma ya mdundiko mtu na kuja kumsuta mtu.
Au kumkodishia mapashukuna  kila kukicha wawe wanamchafua jina lake na kweli wamefanikiwa na waliokuwa wanatakiwa wadhibiti Hali hiyo wamekaa kimya.

Mke wangu IGP- Said Mwema na Mkurugenzi wa TAKUKURU ,Dk.Edward Hosea wakati Sakata la Fedha za EPA bado washitakiwa hawajapelekwa Mahakamani na wananchi walikuwa wakishinikiza wapelekwe.

Viongozi Hao ambao ni makachero wazuri tu walikuwataka wananchi wawe na subira na Kusema HIvi " Mafisadi ni watu hatari sana hivyo inatakiwa kwenda nao Polepole".  Ni kweli makachero hao walikuwa walikuwa wakijua wanavyosema na ndicho kilichomkuta Mtani wangu Muhongo.

Hivyo Muhongo muachie Mungu, yeye ndiyo muweza wa yote, endelea kulitumikia taifa Lako kwa uaminifu ila kwa taadhari pia  Kwani Tulipofika sasa watendaji waaminifu na wachapakazi nchi hii HIvi sasa nikama hawatakiwi.

Tusubiri tuletee Waziri wa Nishati na Madini ambaye uenda anaweza Kuwa malaika kutoka mbinguni ambaye Kamwe hataguswa na tuhuma yoyote Kama watangulizi wake Wizara hiyo walivyokabiliwa na tuhuma na kutakuwa kujiuzuru.

Pia tusubiri Huyo Waziri wa Nishati na Madini mpya ambaye atateuliwa  na Rais Kikwete ambaye ataweza kuendeleza Yale yaliyoachwa na Muhongo na alete mipango yake Mipya Katika Kipindi hiki kifupi kilichobakia  kuelekea uchaguzi Mkuu Oktoba Mwaka 2015. Na tumpe ushirikiano siyo kuanza kumchokona.

Mwisho namtakia kila la kheri Mtani wangu Profesa Muhongo Katika majukumu yake mapya.Hongera kwa uamuzi huo wa kujiuzuru licha kwa wale walikuwa tunafahamu mchango uamuzi huo umekusikitisha ila hatuna jinsi.

Wewe siyo wa kwanza kujiuzuru nafasi hiyo kwa Sababu umeona jina Lako lime nafika. Hata aliyekuwa Waziri wa serikali ya awamu ya Tatu, Dk.  Kitine naye Alifikia uamuzi wa kujiuzuru uwaziri kwa Madai Kuwa alitafuna Fedha za umma kwa kisingizio Kuwa Mkewe alikuwa Amelazwa Canada kwaajili ya matibabu na Katika mahojiano yake na Gazeti la Mtanzania la Jumapili la wiki iliyopita , Dk.Kitine akifanya mahojiano na Gazeti Hilo alilitaja kundi la wanamtandao na  ndiyo walioshiriki kumzushia fitna hiyo na walifanikiwa kumchafua kwasababu walikuwa wakiisoma Rais Benjamin Mkapa alikuwa akimwandaa Kuwa Rais wa Tanzania Mwaka 2005.

Lakini Kamati ya Bunge ya Wizara ya Mambo ya nje ilikuja kumsafisha na kunekana ni kweli Mke wake alikuwa ni mgonjwa na alilazwa huko Canada.

Narudia tena wale wote mabingwa wa kufanya binadamu wenzao kwa Lengo tu la kupata maslahi Fulani ikiwemo biashara, vyeo Mkae mkijua ipo siku Mungu atawaadhibu.

Kumbukeni hawa mnao wafanyakazi ufedhuli nao wana Mungu na Mungu wao wala siyo kipofu wala kiwete anayetembelea Magongo.Ipo siku Mtalipwa Ubaya mnaofanyia  wenzenu.Aminini  hivyo.

Mungu akutangulie Muhongo nenda kafanyekazi na wasomi wenzio achana na hawa wanaume 'wachambue Michele'  ambao wametawaliwa na husuda na fitna na unafki na vichwa vyao wanavitumia kwaajili ya Kufugia nywele badala ya kufikiri.

Mungu ibariki Tanzania

Chanzo: Facebook: Happy Katabazi
Januari 24 Mwaka 2015
0716 774494.

Profesa Muhongo Ajiuzulu

Akitangaza kujiunzulu mbele ya waandishi wa habari mapema leo Jumamosi Januari 24, 2015
Kutoka Jamii Forums

Aliyekuwa Waziri wa Nishati na madini, Prof. Sospeter Muhongo, ametangaza kujiuzulu Wadhifa wake wa Uwaziri Katika mkutano wake wa waandishi wa habari aliouitisha hii leo. Profesa Muhongo ametangaza hatua hiyo leo asubuni alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam. Amesema atabaki na Ubunge nafasi aliyo ipata kwa kuteuliwa na Rais Kikwete.

Akiongea na Waandishi wa Habari, Prof. Muhongo amezidi kusisitiza kuwa yeye hakuhusika na chochote kile katika sakata hilo lakini baada ya kutafakari sana akagundua kwamba, katika sakata hilo amenyooshewa kidole yeye kama Profesa Muhongo. “Mimi nashangaa leo watu kila kona wananiona mimi ni mwizi, yaani kama mimi ndio nimechukua mabilioni ya escrow wakati ukweli upo wazi. wakati wizara ya nisharti inaingia kwenye mkataba huo mimi sikuwepo kwenye nafasi ya uwaziri, lakini leo watu bado wananiona mimi ni mwizi.

Acha niaachie ngazi nafasi hii ya uwaziri kwani imekuwa ni shida sana, mimi ni mtu msomi nimepata tuzo sehemu mbalimbali duniani nasifika kwa kutoa ushahuri wenye tija, lakini leo naonekana mwizi, wakati historia yangu inaonesha mimi ni mtu msafi sina doa na wala sijawai hata kumwibia mtu, lakini watu wananiona mimi mwizi”alisema Profesa Muhongo, na ni kwa sababu hiyo ameamua kujiuzulu kwa kuzitaja sababu mbili kuwa ni:-

-Ana matumaini kuwa kuachia kwake ngazi, mjadala wa ‘escrow’ utakuwa umefikia tamati.
-Anafanya hivyo ili kukiweka safi Chama Cha Mapinduzi ambacho kimekuwa kinanyooshewa kidole.

Amesema kwa namna moja ama nyingine, sakata hilo si tu kuwa limekuwa likikigharimu Chama bali pia baada ya kutafakari aliwasiliana na mkuu wake wa kazi, Rais Jakaya Kikwete na familia yake na watu wake wa karibu kuwataarifu kuwa anajiuzulu.

Amesema akiwa katika nafasi hiyo, aliweza kufanya mengi ikiwa ni pamoja na kuwapeleka vijana wengi nje kusomea masuala ya gesi, nishati na sayansi kwa ujumla kwani ili Taifa liendelee, linahitaji kuwa na wataalamu katika sekta hiyo muhimu.

Waziri huyo mtaalamu wa miamba, amejiuzulu kufuatia shinikizo la muda mrefu la kumtaka afanye hivyo au awajibishwe, kufuatia mapendekezo ya bunge lililopita, lililoiagiza Serikali kuchukua hatua dhidi ya viongozi wote na watendaji waliohusika na kashfa ya akaunti ya Tegeta Escrow iliyobainisha kiasi cha fedha bilioni 302 kuchotwa BOT zilipokuwa zikihifadhiwa.

Mwishoni mwa mwaka jana, 2014, Bunge la Tanzania lilitoka na maazimio ya kutaka kuwajibishwa kwa mawaziri Profesa Sospeter Muhongo, Profesa Anna Tibaijuka, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema, kutokana na sakata la uchotaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa Benki Kuu (BoT) kwa kutaka mamlaka ya uteuzi kutengua uteuzi wao. Mbali na hao, yumo Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi na Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).

Profesa Muhongo anakuwa ni kigogo wa nne kufuata mkumbo baada ya Waziri Profesa Anna Tibaijuka kufukuzwa nafasi yake na Rais, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema kujiuzulu mwenyewe, huku Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi akisimamishwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuvunjwa.

Katika hotuba ya mwisho ya Rais Jakaya Kikwete, siku alipotengua uwaziri wa Profesa Anna Tibaijuka alisema amemeweka kiporo Profesa sospeter Muhongo wakati uchunguzi zaidi wa kashfa hiyo ukifanywa.

===============

Mapema leo hii Waziri Muhongo alikuwa ameitisha mkutano na Waandishi wa habari ==>Prof. Muhongo aita waandishi wa habari leo

Muungano ya Sasa


Thursday, January 22, 2015

Viongozi wa South Sudan Wafika Makubaliano

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Naibu Rais wa Afrika Kusini Cyril
Ramaphosa (kulia) na Bw. Bw. Deng Alor Kuol  wakifurahia wakati  Rais
Salva Kiir Mayardiy wa Sudan ya Kusini (wa pili kushoto) na Makamu wa
Rais wa zamani wa Sudan Dkt Riek Machar Teny (wa pili kulia) wakipeana
mikono na kubadilishana nyaraka baada ya kutia saini mkatana wa
makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudani Kusini
katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha Jumatano Januari 21, 2015
usiku.  PICHA NA IKULU


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

MKATABA wa kujenga tena umoja na kukiunganisha upya Chama Tawala cha Sudan Kusini cha Sudan People’s Liberation Movement (SPLM) ulitiwa saini usiku wa jana, Jumatano, Januari 22, 2015, katika sherehe ya kufana iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Ngurdoto, Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha.
Mkataba huo unaojulikana kama Agreement on the Re-unification of Sudan People’s Liberation Movement umepongezwa kuwa ni hatua muhimu katika kulitoa taifa changa la Sudan Kusini katika hali ya machafuko, vita vya wenyewe kwa wenyewe, kutoelewana na kutoaminiana, mambo ambayo yameligubika taifa hilo tokea mwishoni mwa 2013 wakati kutokuelewana kulipozuka ndani ya SPLM na hatimaye katika Serikali ya nchi hiyo.
Baada ya siku nzima ya mawasiliano na majadiliano baina ya pande zinazovutana ndani ya chama hicho pamoja na viongozi wa nchi jirani na rafiki na Sudan Kusini, viongozi watatu wa vikundi vinavyopingana ndani ya SPLM walitia saini Mkataba huo muhimu sana.
Viongozi waliotia saini ni Mheshimiwa Salva Kiir Mayardit, Rais wa Sudan Kusini ambaye pia ni Mwenyekiti wa SPLM na anayeongoza kundi linalojulikana kama SPLM in Government (SPLM-IG), Mheshimiwa Dkt. Riek Machar ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa SPLM na pia aliyekuwa Makamu wa Rais wa Sudan Kusini anayeongoza kundi la SPLM in Opposition (SPLM-IO) na Dkt. Deng Alor Kuol ambaye anaongoza kundi la SPLM Leaders- Former Detainees (SPLM Leaders – FD).
Sherehe hiyo ilishuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho ndicho kimesimamia mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo. Rais Kikwete pia ndiye mdhamini mkuu wa Mkataba huo.
Wengine walioshuhudia tukio hilo muhimu ni Rais wa Uganda, Mheshimiwa Jenerali Yoweri Kaguta Museveni; Rais Uhuru Muigai Kenyatta wa Kenya; Naibu wa Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa, Makamu Mwenyekiti wa zamani wa CCM Mheshimiwa John Samwel Malecela ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo na Katibu Mkuu wa CCM Mheshimiwa Abdulrahman Kinana ambaye alikuwa mwezeshaji wa mazungumzo.
Mazungumzo yaliyozaa Mkataba huo yalianza mwishoni mwa mwaka jana baada ya Rais Kikwete na Chama cha CCM kuombwa na Rais Kiir Mayardit kukubali chama hicho tawala cha Tanzania kutumia uzoefu na ujuzi wake wa miaka mingi wa uongozi na siasa kujaribu kuleta suluhu ndani ya SPLM.
Mazungumzo hayo ya kutafuta suluhu ambayo yamefanyika kwa awamu mbili, ya kwanza yakiwa yamefanyika Oktoba mwaka jana na pili yakiwa yameanza mwanzoni mwa mwezi huu, Januari 2015,  yameongeza thamani kwenye mazungumzo mengine yanayofanyika Addis Ababa, Ethiopia chini ya usimamizi wa taasisi ya IGAD na yanayojadili jinsi ya kurejesha amani nchini humo.
Viongozi wa SPLM wanaamini kuwa kwa sababu mgogoro wa kisiasa nchini mwao ulianzia ndani ya chama hicho na kwa sababu SPLM ndicho chombo pekee ambacho kinawaunganisha wananchi wote wa Sudan Kusini, basi busara inaelekeza kuwa suluhu ianze kutafutwa ndani ya chama hicho.
Mkataba wa jana, kimsingi, unalenga kuweka mazingira ya kujenga utulivu, maelewano, amani na umoja wa kudumu ndani ya chama hicho na nchini humo kwa kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mambo ya msingi yaliyokubaliwa kuhusu shughuli za siasa, uongozi na oganisheni ya chama hicho yanafanyika bila kukawia.
Mkataba huo pia unalenga kuhakikisha kuwa chama cha SPLM kinabuni na kutekeleza sera za kuondokana na ukabila, makundi yenye mitazamo finyu na mwenendo wa kijeshi katika siasa za Sudan Kusini.
Aidha, Mkataba huo unalenga kuhakikisha kuwa chama cha SPLM kinafanya mageuzi ya kuanza kujenga utamaduni wa kuvumiliana na ujenzi wa misingi ya demokrasia.
Mkataba huo pia unataka watu wote ambao walishiriki katika mauaji na umwagaji damu katika vita vya wenyewe kwa wenyewe wasiruhusiwe kugombea wala kushika nafasi ya uongozi wa umma ndani ya chama hicho.
Pia viongozi wote wa Sudan Kusini wanatakiwa, chini ya Mkataba huo, kuwaomba radhi wananchi wa nchi hiyo ya Sudan Kusini kwa kuruhusu nchi hiyo kuingia katika machafuko ya umwagaji damu mkubwa.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
22 Januari,2015

Tuesday, January 20, 2015

Meeting on South Sudan in Arusha





THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS



The warring factions of the Sudanese Peoples Liberation Movement (SPLM) of South Sudan will tomorrow (Wednesday, January 21, 2015) sign an agreement on the re-unification of their movement, in a major step towards resolving the current political crisis that has plunged the country into a tragic and unprecedented civil war.

          The Presidents of South Africa, Uganda and Kenya and the Prime Minister of Ethiopia will join Tanzanian President Jakaya Mrisho Kikwete in witnessing the signing to take place at the Ngurdoto Mountain Lodge in Arusha. 

          Both President Salva Kiir and Former Vice President Dr. Rick Machar will sign for their respectful SPLM factions. A leader of the SPLM-Former Detainees will also sign on behalf of his faction.

The agreement is result of an intra–SPLM Dialogue attended by delegations of the three SPLM Groups which has been taking place in Arusha under the auspices of Tanzania’s ruling party, Chama cha Mapinduzi (CCM).

Following a request by the chairman of SPLM, President Salva Kiir,  CCM agreed, last year, to mediate between SPLM groups – SPLM in Government, SPLM in Opposition and SPLM – Former Detainees – which appeared as a result of the political crisis.

 The talks in Arusha, which first took place between 12-20 October, last year, were chaired by former Chairman of CCM, John Samwel Malecela and facilitated by CCM Secretary General, Mr. Abdulrahman Kinana.
The latest talks, which resulted in the agreement, took place in both December last year and beginning January 8th this year. The agreement will be followed by the process of implementation during which time CCM will continue assisting.

The Process in Arusha sought at re-uniting SPLM and was therefore complimentary to the Peace Talks taking place in Addis Ababa, Ethiopia.
President Kikwete arrived in Arusha this evening (Tuesday, January 20, 2015) ready for the signing ceremony tomorrow.