Tuesday, March 31, 2015

Tanzia - Dr. Aleck H. Che-Mponda, Baba yangu mzazi

Wadau, ninasikitika kutangaza kifo cha Baba yangu mzazi, Dr. Aleck H. Che-Mponda, kilichotokea katika hospitali ya Massana mjini Dar es Salaam, jana jioni (March 30, 2015).  Mipango ya mazishi inafanyika.  Alikuwa anumwa ugonjwa wa Saratani (Cancer ya Mifupa).

Habari ziwafikie ndugu na marafiki wote popote walipo.

Rest in eternal peace, Dr. Aleck H. Che-Mponda (1935-2015)





Sunday, March 29, 2015

Watanzania - Wakimbizi Ulaya!

 
Malazi ya Wakimbizi huko Ujerumani


Nimepata kwa E-Mail:

 Hivi karibuni nilikuwa safarini Nchini Ujerumani. Na moja ya mambo niliyoyakuta ni kwamba siku hizi nchini humo kumefunguliwa makambi sehemu mbali mbali ya wakimbizi. Wengi wao ni kutoka nchi za Afrika. Nadhani mnasikia mara kwa mara kuhusu wakimbizi hawa ambao huenda Ulaya kwa njia ya hatari ya Meli. Wengi hufa bahari kwa hali mbaya ya hewa au hata kwa kutoswa.

Nchini Ujerumani nilikuwa katika Jiji la Munich. Nilibahatika kuona moja ya kambi hiyo, ila kwa bahati mbaya sikuruhusiwa kuingia. Niliambiwa kadiri ya orodha yao kuna WATANZINIA WAWILI. Nilipopata habari hiyo nilishituka sana. Hata aliyenipa habari hiyo aliona sikuwa tena katika hali ya kawaida. Ndipo akaniuliza nchini kwenu kuna matatizo gani hata watu wakimbie huko? Hakika sikuwa na jibu. Sababu za ukimbizi nchini mwako zinaweza kuwa za Kisiasa, yaani kutokana na utawala mbovu watu wanaamua kukimbia kuokoa maisha yao. Au hali hali nyingine yoyote inayohatarisha maisha. Mimi ninajiuliza nchini Tanzania kuna hali gani ya kuhatarisha maisha ya watu hadi wakimbie wakaishi kwenye makambi Ugaibuni? Hakika nilisikitika sana.

Ila kwa vyovyote wanazo sababu zao za kimsingi kukimbia na hata kujiorodhesha kama wakimbizi. Wito wangu kwa vijana; hakika wengi wanadhania Ulaya ni sehemu poa. Kuna fedha za kumwaga na maisha huko ni rahisi. Kiukweli ni kujidanganya. Hapa Tanzania unaweza kwenda sokoni ukaokota hata matunda au mbogamboga ukaponea. Ukafanya kibarua chochote kitu hata kufanya usafi kwenye zizi au bustanini au hata kuiba kwa wale wenye ujuzi huo. Kwa wenzetu hayo hayapo. Hakuna cha kibarua. Hakuna mazingira unayoweza kuiba kirahisi. Kila duka na soko kuna makamera. Hali ya hewa ni mbaya. Muda mwingi katika mwaka ni baridi kali. nk. Witoa kwa vijana kama unataka kuteseka maisha yako yote kimbilia Ulaya.

Walioko kule wako makambini. Hawaruhusiwi kusafiri, hawaruhusiwi kufanya kazi ila wanafugwa tu kwa kupatiwa chakula na mahitaji mengine ili waishi. Wanangoja ufanyike utaratibu wa kurejeshwa makwao. Je huko si kupoteza muda na kuhatarisha maisha zaidi. Kinachoniuma zaidi ni je, hapa Tanzania kuna mazingira gani magumu kiasi hicho hata wajiorodheshe kuwa wakimbizi? Kama kuna mwenye maelezo ya sababu ningeshukuru.

K

Saturday, March 28, 2015

Afariiki Baada ya Kuchomwa Sindano ya Kuongeza Saizi ya Matako





Wadau, huko Texas mwanamke Mmarekani mweusi amepoteza maisha yake kwa kupenda kuchoma sindano za kuongeza saizi ya makalio.  Huyo dada alichoma sindano kadhaa na  kweli matako yake yaliongezeka. Lakini alitaka zaidi! Hatimaye sindano hizo zikamwua!  Sindano zenyewe zina Super glue na fixa fleti ya matairi!   Mpende mungu alivyowaumba. Na hao madaktari feki waliokuwa wanamchoma wamekimbia. Wakaikamatwa watashitakiwa kwa mauaji.

**************************
Wykesha Reid went to the Deep Ellum salon for the same reason many others did: She wanted to add curves.
“Everybody else got big booties,” Patricia Kelley, 70, who had raised Reid since she was a baby, said Reid told her. “So she wanted a big booty.”
Reid, 34, a nursing home staffer, joined a growing number of people who are turning to black-market buttocks injections — which are much cheaper and riskier than plastic surgery — to get their bodies closer to pop-culture idols such as BeyoncĂ© and Kim Kardashian.
Reid went to the salon in the 3800 block of East Side Avenue three times for the injections with no problems.
“Your butt’s getting too big,” Kelley recalled telling her. “But she got hooked on them booty shots.”
On Feb. 18, Reid returned to the salon for a fourth visit, Kelley said Thursday. But something went wrong. Police found her body inside the business at 7 the next morning. The building had been cleaned out and her purse and cellphone were missing, Kelley said.
Now Reid’s family hopes someone will be brought to justice in her death.
Police issued arrest warrants late Wednesday on charges of practicing medicine without a license for Denise Ross, 43, and Jimmy Clarke, 31, who also is known as Alicia.
Ross and Clarke are wanted in connection with a case in which a woman who received butt injections suffered pain, soreness and psychological problems but survived.

Kusoma habari kamili BOFYA HAPA:

Asiimilia 40 ya Wanwake Zanzibar Wanaishi Maisha Duni

DSC_0081
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi (aliyefunikwa mwamvuli) akiwasili kwenye sherehe ya siku ya wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicious Women Group na kufanyika ndani ya ukumbi wa Salama, Bwawani Hotel mwishoni mwa wiki.
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
UTAFITI uliofanywa na taasisi ya wanawake nchini Zanzibar ya Zanzibalicious Women umeonyesha kuwa asilimia 40 ya wanawake Zanzibar, wanaishi katika mazingira duni ya umasikini kwa kutojitambua na kukosa elimu ya uelewa jinsi ya kukabiliana na mazingira waliyomo.
Akisoma risala siku ya wanawake mbele ya mgeni rasmi mke wa rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mama Mwanamwema Shein , katika siku ya wanawake hafla iliyofanyika hoteli ya Bwawani, Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Shekha Hilal alisema hali hiyo ni changamoto kubwa na sasa kunatafutwa namna ya kumfikia mwanamke huyu ambaye ameshagota katika jamii yetu.
“Mama Shein asilimia hii ni kubwa saana, na sisi kama wanawake ambao tayari tumejaaliwa elimu na tunajitambua, ikiwa ni pamoja na tayari tumepiga hatua kimaendeleo katika nyanja mbalimbali, tumeguswa sana sana na suala hili.” Alisema Shekha.
Zanzibalicious ni umoja wa wanawake wanaoishi Zanzibar,ulioanzishwa mwaka 2011,na kusajiliwa rasmi mwaka 2013, ikiambatana na uzinduzi uliofanyika tarehe 28 Machi 2014.
DSC_0227
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein akiwasili kwenye sherehe ya siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicous Women Group mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Salama, Bwawani Hotel.
Mweka hazina huyo alisema kwamba wanajiuliza maswali mengi kama mwanamke huyo elimu ya kujikwamua imemfikia au kama kuna jitihada zozote za kumfikishia elimu hiyo.
“Je hili ni jukumu la serikali peke yake? Au sisi tunatakiwa tujumuike na serikali? mheshimiwa mgeni rasmi tumeona ya kwamba tuungane pamoja na serikali katika kutekeleza suala hili.” Alisema Shekha akielezea nia ya taasisi hiyo ya kuondoa umaskini miongoni mwa wanawake nchini Zanzibar.
Alisema taasisi yao inajipanga kutoa elimu za aina mbili ili awali kumuwezesha kujikimu kupitia ujasiriamali, kwa kumpatia elimu kwa vitendo,kwa mfano:-ushonaji,ufugaji na utengenezaji wa bidhaa mbali mbali na pili kumtoa katika hali ya upweke ili elimu atakayopata imfikishe kwenye mifuko mbali mbali pamoja na mfuko wa Rais Dk. Ali Mohammed Shein .
Alisema katika program hiyo wanatarajia baada ya miaka 2 wanawake 100 watakuwa wanajitegemea wenyewe na kuwa mabalozi katika kuelimisha wanawake wengine zaidi.
DSC_0471
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein akisoma hotuba wakati wa sherehe ya siku ya wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicous Women Group na kufanyika ndani ukumbi wa Salama, Bwawani hoteli mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akifuatiwa na Mwenyekiti mstaafu wa Zanzibalicious Women Group, Bi. Ummukulthum Ansel.
“Na kama kila mwanamke akiweza kuelimisha wanawake katika kaya yake ,baada ya miaka kadhaa, Zanzibar itakuwa na wanawake walioweza kujikomboa katika dimbwi hili la kuishi maisha duni.” Alisema.
Akizungumzia mafanikio ya asasi hiyo alisema kwamba imefanikiwa kutoa elimu na kuwawezesha kina mama kuunda vikundi vidogo vidogo vya maendeleo kwa kuanzisha miradi mbalimbali, kwa mfano kina mama wa Chaani na Matemwe.
Aidha imetoa misaada ya hali na mali kwa waathirika wa madawa ya kulevya ikiwa ni moja ya kumkwamua mwanamke na kutoa misaada mbali mbali kwa wanawake wasiojiweza ikiwemo hospital kuu ya Mnazi mmoja na kina mama wajane.
Alisema pamoja na mafanikio hayo bado wanawake wanakabiliwa na changamoto za ndoa za utotoni, uzazi salama, ukatili wa kijinsia,mfumo dume, ubaguzi na mimba za utotoni.
Mhe.Mgeni rasmi, Umoja huu umekuwa ukiendesha shughuli zote tokea mwaka 2011 kwa kutegemea michango yetu sisi binafsi.
DSC_0314
Baadhi ya wakinama waliohudhuria sherehe hiyo wakionekana kufurahishwa na hotuba ya Mke wa Rais wa Zanzibar (hayupo pichani).
Changamoto hii imesababisha kutokutimiza kwa malengo yetu kwa muda tulioupanga kutokana na kukosa fedha za kutosheleza utekelezaji wa malengo hayo.
Akijibu risala hiyo Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein, ameikumbusha jamii kuunganisha nguvu zao kuwakomboa wanawake kujiendeleza kimaisha na kujiongezea kipato.
Alisema hatua hiyo itaongeza kasi ya kuimarisha ustawi wa familia na jamii hususan wanawake wanaoishi vijijini ambao wanakabiliwa na changamoto zaidi.
Alisema sherehe ya siku ya wanawake duniani inakuwa na maana zaidi kama juhudi zitafanyika kuangalia changamoto na kujipanga kuzifanyia kazi.
“Rai yangu ni kuwa tuwazingatie zaidi akina mama wanaoishi vijijini na wenye mahitaji maalum kutokana na kukosa fursa kama hizo za kuwaendeleza kimaisha”, alisisitiza.
DSC_0344
Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Bi. Shekha Hilal akisoma risala kwa mgeni rasmi Mke wa Rais wa Zanzibar (hayupo pichani) Kulia ni Mwenyekiti wa Zanzibalicous Women Group, Bi. Evelyne Wilson.
Aidha, aliongeza kuwa wanawake ni jeshi kubwa ambalo likiandaliwa vyema linaweza kushinda katika mapambano yanayokusudiwa huku akisisitza mshikamano ili kufikia malengo yanayowekwa.
Akizungumzia ujumbe wa sherehe hizo ambao ni kuhamasisha hatua mathubuti kumwendeleza na kumtambua mwanamke, alitoa rai kwa wanawake kushirikiana na serikali katika kampeni za kupambana na madhila wanayokabiliana nayo ikiwa ni pamoja na ukatili wa watoto na wanawake.
Kuhusu uzoefu wake katika maisha na malezi ya watoto, alisema amebahatika kupata watoto 11 ambao amewalea katika mazingira mbalimbali ikiwa ni kwenda na kurudi kazini na kuwa pekee huku mumewe akiwa safarini kikazi.
Aidha, aliwataka wanawake kuwa wastahamilivu katika malezi ya watoto hasa watoto Njiti ambao huzaliwa kabla ya kufikisha muda.
Hata hivyo aliwaonya wanawake wanaojali kujiremba na kuwa sahau watoto na kukumbusha kwa ‘watoto ni wageni’ kwamba wanahitaji matunzo na ukarimu mkubwa kutoka kwa wazazi wao.
IMG_6571
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akizindua Mfuko wa Zanzibalicious Women Group kwa kuchangia shilingi milioni tano, wakati wa maadhimisho ya sherehe ya wanawake duniani visiwani Zanzibar yaliyoandaliwa na Zanzibalicious Women Group na kufanyika katika ukumbi wa Salama uliopo Bwawani Hotel Zanzibar. Kulia ni Mwenyekiti wa Zanzibalicious Women Group, Bi Evelyne Wilson Baruti.
DSC_0082
Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Shekha Hilal akinakili majina ya watu waliokuwa wakichangia kwenye harambe ya mfuko wa Zanzibalicous Women Group uliozinduliwa rasmi na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (hayupo pichani).
DSC_0074
Mbunifu nguli wa mavazi Mama wa mitindo, Asia Idarous akinadi moja ya nguo alizotengeneza kwa ajili ya kuchangia mfuko wa Zanzibalicious Women Group.
DSC_0075
Mke wa Naibu Waziri wa Afya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bi. Zakhia Kombo akitangaza dau la kununua nguo hiyo iliyokuwa ikinadiwa kwenye harambe ya mfuko wa ZWG iliyozinduliwa na Mama Mwanamwema Shein.
DSC_0091
Meza kuu kwenye picha ya pamoja na Zanzibalicous Women Group.
Unaweza kutembelea mtandao wao na kuona shughuli mbalimbali walizozifanya hapa http://www.zanzibalicious.org/
DSC_0388
Mmoja wa wadhamini ZANLINK wanaotoa udhamini kwa Zanzibalicious Women Group wakisikiliza kwa makini yaliyokuwa yakijiri ukumbini hapo. Kwa picha zaidi bofya link hii

Friday, March 20, 2015

Muswada Binafsi wa Baraza la Vijana la Taifa Kujadiliwa Bungeni

Mh. John Mnyika


MUSWADA BINAFSI WA BARAZA LA VIJANA LA TAIFA KUJADILIWA BUNGENI TAREHE 31 MACHI 2015
Nashukuru wote ambao mmekuwa mkifuatilia hatma ya muswada binafsi wa Baraza la Vijana la Taifa niliouwasilisha tarehe 31 Oktoba 2013.
Vijana na wadau wa maendeleo ya vijana mzingatie kwamba muswada huo hatimaye umepangwa kusomwa kwa mara ya pili na kujadiliwa Bungeni Jumanne tarehe 31 Machi 2015 katika Mkutano wa 19 wa Bunge.
Muswada huo ulisomwa kwa mara ya kwanza katika Mkutano wa 14 wa Bunge tarehe 21 Disemba 2013. Maoni kutoka kwa wadau yalikusanywa Oktoba 2014 na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii.
Baraza la Vijana la Taifa pamoja na malengo mengine litawezesha vijana kuanzia kwenye vijiji/mitaa mpaka taifa kuweza kuwa na vyombo vya kuwaunganisha vijana kwa kike na wa kiume kwa ajili ya maendeleo yao na ya taifa.
Aidha, Baraza hilo litafuatilia pia kwa karibu utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya vijana ikiwemo kuhusu ajira, elimu na sekta zingine katika Halmashauri, Serikali kuu, katika vyombo mbalimbali vya maendeleo na wadau wa maendeleo.
Pia, Muswada huo utawezeshwa kuanzishwa kwa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana na kulipa jukumu Baraza la Vijana kufuatilia kwa karibu utendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana; kuhakikisha kwamba fedha zinatengwa za kutosha na kufika kwa walengwa kuwawezesha vijana kujiajiri, kukuza vipaji vyao na kushughulikia maendeleo yao kwa ujumla.
Kujadiliwa kwa muswada huo ni hatua ya pekee katika historia ya harakati za vijana nchini kwa kuzingatia kuwa Sera ya zamani ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 ilitamka kwamba kutaanzishwa  Baraza la Vijana na suala hilo kurudiwa katika Sera mpya ya mwaka 2007.
Hata hivyo Serikali imekuwa ikikwepa kuhakikisha kwamba matakwa hayo ya sera tajwa yanatekelezwa kwa wakati pamoja na kuwa suala hilo linahusu mustakabali wa maendeleo ya vijana nchini.

Natambua mchango wa vijana na taasisi zote za vijana mlioshiriki katika maandalizi ya muswada huu, unaitwa binafsi kwa sababu tu ndio neno linalopaswa kutumika kwa mujibu wa Kanuni za Bunge lakini ukweli ni kwamba huu ni muswada wenu; mimi ni mwakilishi.

John Mnyika (Mb)
20 Machi 2015

Saturday, March 07, 2015

Waganga wa Kienyeji 32 wakamatwa Tanzania - Mauaji ya Albino

Siku ya Alhamisi ,watu wanne walihukumiwa kifo kwa mauaji ya mwanamke albino mwaka wa 2008 katika jimbo hilo.

Serikali iliwapiga marufuku waganga wa kienyeji mwezi Januari kama mojawapo ya kampeni ya kusitisha mauaji hayo.

Kwa habari Kamili BOFYA HAPA: 

Albino Children in Tanzania

Albino wazusha vurugu Ikulu ya Dar es Salaam Magogoni

Vurugu zilizofanywa na baadhi ya walemavu wa ngozi Albino katika Ikulu ya Tanzania zimesababisha kuahirishwa kwa kikao kati ya viongozi wao na Rais Jakaya Kikwete.

Rais Kikwete alikuwa akitarajiwa kufanya mkutano na viongozi wa Albino Tanzania TAS aliowaalika kuzungumzia hoja zao kutokana na mauaji ya walemavu hao yanayoendelea nchini humo.

Lakini heka heka iliyotokea katika eneo la mapokezi iliwalazimu maafisa wa Ikulu kuwatawanya walemavu hao.

Ni muda mfupi baada ya ukaguzi kuanza kufanyika katika moja ya lango la kuingilia Ikulu, kundi moja la walemavu hao waliokuwa katika moja ya chumba wakaanzisha malalamiko kwa sauti huku viongozi wao wakiwa wanajiandaa kuruhusiwa na kuingia ndani.

Kelele hizo na mabishano hayo miongoni mwa walemavu hao kwa mbali ikaanza kuonekana ni dosari namba moja hasa baada ya kupandisha mori na kila mtu kuanza kusema lake kupinga ushiriki wa viongozi hao.

Kutokana na vurugu hizo maafisa wa Ikulu waliwatawanya Walemavu hao kutoka nje ya Geti, na hapo ikawa mwanzo wa sakata jipya baada ya kuanza kulumbana na viongozi wao na hatimaye kuanza kupigana na mambo yakawa hivi.

Baada ya kutulizwa ugomvi kilichofuata ni nyimbo za kupinga uhalali wa viongozi wao. Hata hivyi vurugu hizi zinatazamwa tofauti na baadhi ya walemavu hao, ambao wanasema ni vurugu hizo zimepoteza fursa ya kuwasilisha matatizo yao kwa Rais

Chanzo: BBC swahili
--

Wanawake wana Kazi Ngumu Waheshimu

Thursday, March 05, 2015

Rais Kikwete Akutana na Uongozi wa Chama cha Albino

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na viongozi wa Chama Cha Albino Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo. Walioketi kushoto ni Waziri wa Sheria na Katiba Dkt Asha Rose Migiro, Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Mathias Chikawe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe George Mcheche Masaju Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabirika Mushi na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Bw. Emmanuel Achayo 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifafanua jambo wakati akiongea na viongozi Wa Chama Cha Albino Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi Wa Chama Cha Albino Tanzania baad ya kukutana nao pamoja na Waziri wa Sheria na Katiba Dkt Asha Rose Migiro, Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Mathias Chikawe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe George Mcheche Masaju Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabirika Mushi na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Bw. Emmanuel Achayo Ikulu jijini Dar es salaam leo. PICHA NA IKULU

Sunday, March 01, 2015

Captain John Komba Obituary

Kutoka Daily News 

 Mbinga West MP Komba is No More

Published on Sunday, 01 March 2015

By DEOGRATIAS MUSHI 

The late Captain John Komba 

 Mbinga West Member of Parliament and Member of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) National Executive Committee (NEC) Captain John Damian Komba is no more. He died at TMJ hospital in Dar es Salaam Today, where he had been admitted few hours before he breathed his last.

The Tanzania One Theatre (TOT) Secretary General Mr. Gasper Tumaini said that medical reports show that Komba was suffering from Pressure and Diabetes. According to him, Captain Komba was admitted to Sanitas Medical Clinic in Dar es Salaam a week ago, and after two days his health improved and he was discharged. Secretary, Mr Nape Nnauye meanwhile, expressed shock and sadness over the sudden passing of Capt Komba saying that the void he has left behind would be difficult to fill.

Speaking at a press conference yesterday, Mr Nnauye said that the party’s National Chairman, President Jakaya Kikwete, had received the news with great shock. He said that the president has sent condolences to the late Capt Komba’s family and noted that he knew the deceased well because he had worked with him for many years. “Capt Komba was a veteran cadre, an artist, a music composer and he will be dearly missed.

He composed a song during the 38th anniversary of the party which touched many hearts, now it seems it was his way of saying goodbye,” he said. He said that he would forever be thankful to the late Komba because it was he who convinced his late father to enroll him into the party after completing national service and that the party sent heartfelt condolences to his family and friends.

 Captain Komba was born on March 18, 1954, then joined Lituhi primary school in 1963. After completing standard seven in 1970, he joined Songea boys secondary school where he completed in 1974, then joined Cleruu Teachers Training College where he attained teaching certificate in 1976. In 1978 he joined Monduli Military Cadet Training Unit in Arusha where he got a diploma, and then studied at Magdeburg Path in Germany where he got a diploma in politics. Captain Komba then joined Washington International University in 2006, where he was awarded BA in political science in 2008. During his life time, Captain Komba served Tanzania People's Defence Forces as Army Officer from 1978 to 1992.Before he had been employed by the Ministry of Education(1977 and 1978). Between 1992 and 2005 Captain Komba was TOT Executive Director, doubling also as CCM Chief Culture from 1992 to date. He served as Mbinga West member of Parliament from 2005, and also as member of CCM's National Executive Committee (NEC) from 1987 to date.

While in Parliament, Captain Komba once questioned why Tanzania did not unite with Burundi and DR Congo since the three governments of Rwanda, Uganda and Kenya had teamed up and set up an alliance within the community. He even threatened to embark on a rebellion if the Constituent Assembly (CA) could adopt a three-government system as it was proposed in the second draft constitution. He also questioned the rationale of Tanzania remaining in the EAC in light of actions which clearly sidelined it.

 He was once quoted saying he would be the last person to endorse the three-tier Union model and that he would defend the status quo at all costs. "Woe unto you if you will be persuaded to buy the idea of a three-government system. I will retreat into the forest to fight for the two-tier Union structure," he warned amid laughter. His body has been preserved at Lugalo hospital, pending funeral arrangements.

Team Michuzi Production Yarekodi Kwa Weledi wa Hali ya Juu Mnuso wa Tanzania Bloggers Party Serena Hotel Jijini Dar es Salaam

Ankal akiwa na MD wa Michuzi Media Group (kulia kwake) pamoja na kikosi kazi cha Team Michuzi Production chini ya Production Manager Barbra Kilugira (wa tatu kushoto) ambayo ilipata heshima ya kurekodi mnuso wa kihistoria wa Tanzania Bloggers Network (TBN) Meet and greet Party katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia March 1, 2015. Mnuso huu ulifanikiwa sana kwa udhamini mkubwa wa VODACOM TANZANIA (wadhaini wakuu), NMB, COCACOLA, RAHA.COM na SERENA HOTEL.