Saturday, July 30, 2016

Kumbe Donald Trump Kafanana na Mama Yake!

Mama Mzazi wa Mhogombea Rais Marekani, Mary Trump! (Cheki hizo Nywele)


Maalim Seif Sharif Hamad Kuongea na WaTanzania Boston Leo

Zanzibar Diaspora Association inapenda kuwaalika kwenye mkutano wa hadhara utakao fanyika Siku ya Jumamosi July 30th -
MAHALI: 42 Charles St Boston
MA 02122.
MDA: Kuanzia 5:pm mpaka 7:pm
Mgeni rasmi ni Katibu mkuu wa CUF. 
Maalim Seif Shariff Hamad
Nyote mnakaribishwa

Friday, July 29, 2016

Pastor Daniel Moses Kulola Kutembelea Marekani

"Greetings my friend, Again God has given to me a chance to come to America, this time i wont stay in USA for long time it is just for 2 weeks then i come back home Tanzania.

My schedule will be in Boston from 9th to 14th August then 15th August to Dallas, Houston to 22nd, on 23rd to Arizona. my ticket back to Tanzania reads on 25th from Arizona to Boston and Boston to Tanzania.
I thought it is good to let you know so that you can pray for me and also call me for greetings". Pastor Kulola States.

Wednesday, July 13, 2016

Kazi Anayofanya Rais John Pombe Magufuli Tanzania

Ananyosha Nchi!


Hospitali ya Kutibu Kansa Kujengwa Bukoba

MWEKEZAJI MZAWA AAMUA KUWEKEZA KAGERA KWA KUJENGA    HOSPITALI KUBWA YA KUTIBU MAGONJWA YA KANSA KATIKA MANISPAA YA BUKOBA

Mkoa wa Kagera kupiga hatua kubwa kimaendeleo baada ya kujitokeza mwekezaji mzalendo ambaye ni Mshauri Mkuu wa Kampuni ya VIP Engineering and Marketing Company Ltd ya Jijini Dar es Salaam Bwana James Rugemalila kuanza mchakato wa kujenga kituo kikubwa (hospitali) ya magonjwa ya matibabu ya Kansa katika Manispaa ya Bukoba.

Bw. James Rugemalila akiambatana na ujumbe mzito na wataalamu wa afya kutoka nchi mbalimbali alifika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera tarehe 10/07/2015 na kuongea na Katibu Tawala mkoa Bw. Nassor Mnambila ambaye alimhakikishia juu ya kupata ardhi wanayohitaji na kuwa serikali ya mkoa itawaunga mkono katika hatua zote za kupatikana kwa kituo hicho.

Aidha Bw. Rugemalila na ujumbe wake walifika  Manispaa ya Bukoba na kuongea na Kaimu Mkurugenzi Bw. Lukiko Chibunu ambaye pia aliwahakikishia kuwa ardhi ipo na tayari wameitenga kwa ajili ya uwekezaji huo kama walivyoombwa na Bw. Rugemalila na walidhuru eneo husika Mtaa wa Makongo  karibu na Ziwa Victoria.

Ujumbe huo ulilidhishwa na eneo husika pia  Bw. Rugemalila aliambatana na Profesa Anthony Pais Mkuu wa Idara ya Upasuaji kutoka Bangalore India ambaye alisema Tanzania na Mkoa wa Kagera ni muhimu kuwa na kituo hicho kutokana na takwimu za Shirika la Afya ulimwenguni (WHO).

Profesa Pais alisema kuwa wagonjwa wa kansa 35000 wanatambuliwa kila mwaka duniani na asilimia 90%  ya wagonjwa wanatoka duniani kote na wagonjwa 3000 wanatoka Tanzania kila mwaka na hupelekwa nje ya nchi kutibiwa ambapo baada ya kituo hicho kujengwa itakuwa fursa kwa watanzania kupata matibabu hapa hapa nchini  na mkoani Kagera.

Vilevile Profesa Pais alisema kuwa Kampuni ya VIP Engenering and Marketing Ltd iliamua kujenga kituo hicho mkoani Kagera kwasababu walipoonyeshwa eneo la Makongo katika Manispaa ya Bukoba walipendezwa nalo sana pia mkoa wa Kagera umepakana na nchi zote za Afrika Mashariki ambapo ni moja wapo ya fursa katika uwekezaji.

Naye Bw. Anic Kashasha Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano na Mawasiliano katika Kampuni ya VIP Engineering Ltd alisema kuwa kituo hicho mara baada ya kukamilika kitajulikana kwa jina la (RUTAKWABYERA CANCER HEALTH CENTER) na kitakuwa na hadhi zote  za hali ya juu mpaka kawaida ili kutoa fursa kwa wananchi wote kupata huduma stahili.

Kituo hicho kwa kuanzia kitajengwa na kuanza na vitanda 100 na mara baada ya kukamilika kitakuwa na vitanda 500 pia zitajengwa hosteli za wananchi ambao watakuwa wanawaleta wagonjwa wao kupata mahala pakujihifadhi.  Kitaitwa kituo badala ya hospitali kwani kitakuwa kinaendesha uchunguzi, ugunduzi, na kutoa tiba na elimu juu ya ugonjwa wa Kansa.

Kituo cha Rutakwabyera kinatarajiwa kujengwa ndani ya miaka mitatu kuanzia sasa na gharama za mradi mzima zitajulikana mara baada ya ujenzi kuanza rasmi. Mkoa wa Kagera unazo Nyanja nyingi sana za uwekezaji wazawa na wawekezaji mbalimbali mnakaribishwa kuwekeza Kagera.

Saturday, July 09, 2016

Ukweli Kuhusu Ubaguzi Marekani

Ukiwa mweusi Marekani, ukiongelea ubaguzi unaambiwa unafikra za kitmuwa! Unaambaiwa uache kufikiria.  Wewe ni mbaguzi dhidi ya wzungu. Myehudi anaambiwa asisahau yaliyowapata wahenga wake! Khaa!



Saturday, July 02, 2016

Kumbukumbu - Steven Kanumba (1984 -2012)

Kaka Selles Mapunda akisafisha kaburi la rafiki yake, marehemu msanii Steven Kanumba, huko katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Kusoma Historia ya Marehemu Steven Kanumba BOFYA HAPA:

Marehemu Steven Kanumba (1984 -2012)