Saturday, November 26, 2016

Aliyekuwa Rais wa Cuba , Fidel Castro Afariki Dunia

Rais Castro na Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1977
Aliyekuwa Rais wa Cuba, Fidel Castro, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90.  Castro alifariki usiku wa kuamkia leo.  Mdogo wake, Rais Raoul Castro aliwatangazia waCuba kuwa Castro amefariki saa nne na nusu usiku.  Alisema kuwa maiti ya kaka yake itachomwa moto leo (cremation) huko Cuba. Kutakuwa na Misa ya kumkumbuka  Taifa la Cuba itakuwa na siku kadhaa za kuomboleza.
Rais Raoul Castro alivyowantangazia wananchi:
The commander in chief of the Cuban revolution died at 22:29 hours this evening (03:29 GMT Saturday)," he said. "Towards victory, always!" he added, using a revolutionary slogan.
Marehemu Castro anakumbukwa kwa kuwa Dikteta. Alipindua serikali ya Cuba mwaka 1959, na hakutoka madarakani hadi mwaka 2006.  Alimwachia madaraka mdoo wake Raoul.  Castro alifanya mengi kusaidi nchi za Afrika ikiwemo Tanzania. Nchi ya Marekani waliweka vizuizi vingi juu ya Cuba ili kujaribu kumkomesha Castro lakini walishindwa.
Video ya Ziara ya Rais Castro nchini Tanzania kwa hisani ya AP



Saturday, November 19, 2016

Rest in Peace Sharon Jones



The Late Singer Sharon Jones 1956-2016

   NEW YORK (AP) - Sharon Jones, the stout powerhouse who shepherded a soul revival despite not finding stardom until middle age, has died. She was 60.

   Jones' representative, Judy Miller Silverman, said Jones died Friday at a Cooperstown, New York, hospital after battling pancreatic cancer. Loved ones and members of her retro-soul band, the Dap-Kings, were among those surrounding her, Silverman said.

   The story of Jones' battle with cancer, first diagnosed in 2013, was told in Barbara Kopple's documentary, "Miss Sharon Jones!" released earlier this year. Though she triumphantly returned to the stage in 2015 after the cancer went into remission, Jones late last year announced its return. Still, Jones mounted another comeback with the defiant single "I'm Still Here" and hit the road again this summer with the Dap-Kings even while undergoing chemotherapy.

   "You got to be brave," a debilitated Jones told the Associated Press in July , in between tour stops. "I want to use the time that I have. I don't want to spend it all laid up, wishing I had done that gig."

   Jones' death was immediately noted on social media and throughout the music industry. The British producer Mark Ronson, who brought the Dap-Kings in to play backing band to Amy Winehouse on her breakthrough album, "Back to Black," said, "Sharon Jones had one of the most magnificent, gut-wrenching voices of anyone in recent time."

   The youngest of six children, Sharon Lafaye Jones was born on May 4, 1956, in Augusta, Georgia. Her family lived in nearby North Augusta, South Carolina, across the Savannah River from the birthplace of James Brown. Jones, who would grow into a dynamic, show-stopping performer, grew up idolizing the Godfather of Soul and would later be frequently tagged as "the female James Brown."

   But for decades, such a fate was unimaginable. On "I'm Still Here," she sings of being turned down by music executives for being "too short, too fat, too black and too old."

   After growing up in Brooklyn (her mother moved to escape an abusive husband), Jones regularly sang gospel at her church, performed for years in a wedding band and sang back-up for various session bands. To make ends meet, she worked as a corrections officer at the Rikers Island jail complex and was a bank security guard.

   But in one recording session, she caught the attention of Gabriel Roth and Philip Lehman. The two, blown away by Jones' fiery voice, made her the lead singer of their newly formed Dap-Kings and launched the Bushwick, Brooklyn-based label, Daptone Records, around her unlikely star power.

   They debuted with 2002's "Dap-Dippin' With Sharon Jones and The Dap-Kings," released when Jones was 46. Three more albums followed in the ensuing decade, and two compilations. Standouts included a soulful rendition of Woody Guthrie's "This Land Is Your Land" and the single "100 Days, 100 Nights," in which she belts: "100 days, 100 nights to know a man's heart/ And a little more, before, he knows his own."

   The sound, backed by walls of horns and tightly guided by bandleader Roth, was propelled by Jones' grit and ferocity. For her, soul and survival went hand in hand. Her torrid performances began, like Brown's, with a prolonged introduction from her bandmates.

   Jones never disparaged the better-selling British soul revival led by Ronson and Winehouse that coincided with her rise. But she wasn't shy about claiming to be the more genuine article.

   "We've been there, and we're still doin' this," Jones told New York magazine in 2010. "In another few years, what are they gonna be doin'?"

   Their sixth album, "Give the People What They Want" earned Jones her first Grammy nomination for best R&B album. Their last album, "It's a Holiday Soul Party," was released last year.

   Kopple witnessed the charismatic Jones light up hospital wards while undergoing chemo. "When people are around or there's an audience, that gives her fuel and she forgets her pain," the director said ahead of the release of "Miss Sharon Jones!"

   Even while suffering the effects of her cancer and its treatments, the workmanlike Jones toured relentlessly

   "It's therapy," Jones said of performing in July. "I know I need rest and sleep. But I want to work and that is our job."




Makamu wa Rais Kuzindua Kampeni ya Uchunguzi wa Bure wa Saratani ya Matiti

Rais wa Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania (MEWATA), Dkt.Serafina Mkuwa (kulia), akitoa taarifa kwa wanahabari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya uchunguzi na matibabu ya Saratani ya Matiti na mlango wa kizazi mkoani Mwanza.

Kampeni hiyo itazinduliwa kesho katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza na Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan na baadaye kufanyika kwa siku mbili bure.
Na BMG
Kutoka kushoto ni Dkt.Mary Charles ambaye ni Makamu wa Rais MEWATA, Mganga Mkuu mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonald Subi, Rais wa MEWATI, Dkt.Serafina Mkuwa, Mwenyekiti Kamati ya Kampeni na Mjumbe kamati tendaji MEWATA, Dkt.Magdalena Lyimo pamoja na Mratibu wa huduma za afya ya uzazi na mtoto mkoa wa Mwanza, Secilia Mrema.
Pia watumishi wa afya mkoani Mwanza wamepatiwa mafunzo kwa ajili ya kusaidia utoaji wa huduma za uchunguzi wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi
Na George Binagi-GB Pazzo
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu, kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kampeni ya uchunguzi na matibabu ya saratani ya matiti na mlango wa kizazi bila malipo mkaoni Mwanza.

Rais wa Chama cha Madaktari Wanawake nchini MEWATA, Dkt.Serafina Mkuwa, ameyasema hayo hii leo Jijini Mwanza wakati akitoa taarifa ya kampeni hiyo kwa wanahabari.

Amesema baada ya ufunguzi wa kampeni hiyo, akinamama na wasichana mkoani Mwanza, watapata fursa ya kufanya uchunguzi na matibabu ya Saratani ya matiti na mlango wa kizazi kwa muda wa siku mbili ambazo ni kesho na kesho kutwa katika vituo vinne ambavyo ni Uwanja wa Furahisha, Vituo vya Afya Makongoro, Karume pamoja na Igoma Jijini Mwanza ambapo huduma zitakuwa zikitolewa kuanzia majira ya saa moja asubuhi.

Tatizo la saratani ya matiti na mlango wa kizazi bado ni changamoto kubwa mkoani Mwanza ambapo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonald Subi, anabainisha kwamba takwimu zilizopatikana katika halmashauri za Ukerewe, Buchosa pamoja na Kwimba, zinaonesha kwamba kati ya wanawake 1,294 waliochunguzwa, 58 wanamabadiliko ya awali ya saratani na 18 wanamabadiliko makubwa ya saratani na wamepewa rufaa kwenda hospitali ya rufaa Bugando kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Hata hivyo Dkt.Subi amewahimiza wananchi kuepuka matumizi ya tumbaku, sigara pamoja na pombe kali ambayo huchangia ongezeko la magonjwa ya saratani ya matiti na mlango wa uzazi kwa akinamama huku akiwahimiza kufanya uchunguzi angalau mara moja kwa mwaka ili kubaini tatizo mapema kwani tiba ya mapema husaidia kupambana na magonjwa hayo.

Chama cha Madaktari Wanawake nchini kimeshirikiana na Wizara ya Afya, Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza pamoja na wadau wengine wakiwemo Gender Health, PSI pamoja na Tayoa katika kufanikisha huduma hiyo ya uchunguzi na matibabu ya saratani ya matiti na mlango wa kizazi bila malipo mkoani Mwanza.

Sunday, November 13, 2016

Mafunzo Kwa Wasanii wa Filamu Mkoani Mwanza Yazaa Matunda


Kulia ni Mohamed Nyengi ambaye pia ni Afisa Uendeshaji na Masoko kutoka Shirika la Pensheni la PPF Kanda ya Ziwa, akifuatilia semina hiyo iliyoandaliwa na Bodi ya Filamu nchini kwa ajili ya wasanii wa filamu mkoani Mwanza.
Na BMG

Na George Binagi-GB Pazzo
Mafunzo kwa wasanii wa Filamu yaliyoandaliwa na Bodi ya Filamu nchini mkoani Mwanza, yamefungua milango mipya ya mafanikio katika soko la filamu mkoani Mwanza, baada ya Shirika la Pensheni la PPF kuahidi kuwajengea studio ya kisasa wasanii hao ikiwa watajiunga kwa wingi na shirika hilo.

Akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa wasanii hao kujiunga na huduma za PPF, Afisa Uendeshaji na Masoko wa shirika hilo Kanda ya Ziwa, Khatibu Mussa, amesema mbali na wasanii hao kunufaika na mafao yanayotolewa na shirika hilo, pia wanaweza kunufaika zaidi kwa kujengewa studio ya kisasa kwa ajili kurekodia kazi zao ambapo ameahidi kufikisha suala hilo mbele ya uongozi kwa ajili ya utekelezaji.

Baada ya kauli hiyo, Mzee Fumbuki Lubasa ambaye ni Mkufunzi Mstaafu kutoka Chuo cha Ualimu Butimba, idara ya Fasihi kwa Kiingereza na Sanaa, alisimama na kuahidi kutoa bure kiwanja chenye thamani ya takribani shilingi Milioni 20 ili ikiwa PPF itakubali kujenga nyumba kwa ajili ya studio ya wasanii wa filamu mkoani Mwanza.

Hayo yanajiri ikiwa ni juhudi za Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, aliyewataka wasanii wa filamu mkoani Mwanza kuboresha soko la filamu kwa kuwa na studio bora na ya kisasa kwa ajili ya kurekodia kazi zao pamoja na kazi nyingine ikiwemo utengenezaji wa vipindi bora na vyenye maudhui ya mtanzania kwa ajili ya kuoneshwa kwenye runinga mbalimbali nchini.
Mohamed Nyengi ambaye pia ni Afisa Uendeshaji na Masoko kutoka Shirika la Pensheni la PPF Kanda ya Ziwa, akifafanua jambo kuhusu umuhimu wa wasanii wa filamu mkoani Mwanza kujiunga na mfuko wa PPF. Kulia pia ni Afisa Uendeshaji na Masoko kutoka Shirika la Pensheni la PPF Kanda ya Ziwa, Khatibu Mussa Khatibu.
Mzee Fumbuki Lubasa (kulia) ambaye ni Mkufunzi Mstaafu kutoka Chuo cha Ualimu Butimba Jijini Mwanza, idara ya Fasihi kwa Kiingereza na Sanaa. Pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Sanaa Asilia. 

Alikuwa akizungumza wakati wa warsha ya mafunzo kwa wasanii wa filamu mkoani Mwanza ambapo ametoa kiwanja chenye thamani ya takribani shilingi Milioni 20 ili wasanii wa filamu Mwanza wajengewe studio ya kisasa ya kurekodi kazi za sanaa ikiwemo filamu.
Mzee Fumbuki Lubasa (kushoto) akisalimiana na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fissoo, baada ya kujitokeza na kutoa kiwanja kwa ajili ya wasanii wa filamu Mwanza kujengewa studio ya kisaa ya kurekodia kazi za sanaa.
Mzee Fumbuki Lubasa (kushoto) akisalimiana na Afisa Uendeshaji kutoka PPF Kanda ya Ziwa, Mohamed Nyengi, baada ya kujitokeza na kutoa kiwanja kwa ajili ya wasanii wa filamu Mwanza kujengewa studio ya kisaa ya kurekodia kazi za sanaa.
Mzee Fumbuki Lubasa (kushoto) akisalimiana na Afisa Uendeshaji na Masoko kutoka PPF Kanda ya Ziwa, Khatibu Mussa Khatibu, baada ya kujitokeza na kutoa kiwanja kwa ajili ya wasanii wa filamu Mwanza kujengewa studio ya kisaa ya kurekodia kazi za sanaa.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fissoo, akiwahamasisha wasanii wa filamu mkoani Mwanza kujiunga katika vyama vyao na kuanza kunufaika kupitia kutokana na kazi zao.
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, akizungumza kwenye warsha ya mafunzo kwa wasanii wa filamu mkoani Mwanza yaliyoandaliwa na Bodi ya Filamu nchini.
Mkufunzo kutoka Chuo Kikuu Dodoma, Idara ya Habari na Ubunifu, Deodracias Nduguru, akiwafunza wasanii wa filamu mkoani Mwanza namna bora ya kujitangaza na kutangaza kazi zao ili kujulikana zaidi.
Wasanii wa filamu akiwemo Mjumbe wa Shirikisho la Filamu Taifa kutoka mkoani Mwanza, Hussein Kimu (kulia) akiwa pamoja na Myovela Mfwaisa (kushoto).
Meneja Mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA, Innocent Mungy, akiwasilisha mada kuhusu namna bora ya matumizi ya Mitandao ya Kijamii kwenye warsha ya mafunzo kwa wasanii wa filamu mkoani Mwanza.

Amesema wasanii hao wakiitumia vyema mitandao ya kijamii wataweza kukuza soko lao la filamu ikiwemo kutangaza kazi zao na hivyo kuongeza mauzo ya kazi zao na kujiongezea kipato kupitia matangazo mbalimbali.
Wasanii wa filamu zaidi ya 300 mkoani Mwanza wakifuatilia mafunzo kutoka kwa Meneja Mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA, Innocent Mungy, ambaye amewasilisha mada kuhusu namna bora ya matumizi ya Mitandao ya Kijamii.
Bonyeza HAPA Kuhusu Mafunzo Hayo.

Mazishi ya Marehemu Mzee Richard Binagi Yafanyika Jijini Dar es Salaam

Mazishi ya Mzee Richard Binagi (88) aliyefariki dunia Jumanne Novemba 08,2016 Jijini Dar es salaam baada ya kuugua, yamefanyika jana Jumamosi Novemba 12,2016 nyumbani kwake Kipunguni Jijini Dar es salaam. Alikuwa askari mstaafu wa JWTZ.
Na BMG
Taratibu za kuuaga mwili wa Mzee Binagi zikifanyika
Askari wa JWTZ wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Mzee Richard Binagi
Askari wa JWTZ wakiusindikiza malaloni mwili wa Mzee Richard Binagi
Gwaride la heshima
Gwaride la heshima
Askari wa JWTZ wakitoa heshima zao 
Wanafamilia (Profesa Lloyd Binagi na mkewe) wakiweka shada la maua
Wanafamilia (Mzee Chacha Binagi na mkewe) wakiweka shada la maua
Wanafamilia (Mama Binagi) akiweka shada la maua
Wanafamilia (Zakari Binagi na mkewe) wakiweka shada la maua
Wanafamilia wakiweka shada la maua
Wanafamilia wakiweka shada la maua
Wanafamilia wakiweka shada la maua
Wanafamilia
Wanafamilia
Wanafamilia
Ndugu, jamaa na marafiki
Bonyeza HAPA Kuhusu Msiba

Saturday, November 12, 2016

Kumbukumbu - Mh. Samuel Sitta Alipokutana na WaTanzania Cambridge, MA Mwaka 2014

Mh. Samuel Sitta akiwa nyumbani kwangu Cambridge, MA, USA
Siku ya jumamosi, 6/15/14 jioni, Mheshimiwa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba na Waziri wa Afrika Mashariki​​, Mheshimiwa Samweli Sitta alikutana na baadhi ya viongozi wa Jumuiya za waTanzania wa New York na Massachusetts. Mkutano ulifanyika Cambridge, Massachusetts.  Katika mkutano huo Mh. Sitta aliongea kuhusu maswala ya Katiba na Uraia Pacha.  Pia aliongea kuhusu jinsi waTanzania wa diaspora watakavyoweza kusaidia kuijenga Tanzania. Mh. Sitta alikuwa Boston kwa ajili kozi fupi katika Chuo Kikuu cha Harvard.

Kwa picha na habari zaidi tembelea VIJIMAMBO BLOG. 


Kutoka Kushoto - Mr. Sangiwa, Mr. Temba, Dr. Malima, Mh. Sitta, Mr. Sangiwa, Mr. Tome, Mr. Mhellla, Chemi
Mh. Sitta akiwa mwingi wa furaha baadaya kuongea na WaTanzania mjini Cambridge, MA


Wananchi Wajeruhiwa Katika Ajali Iliyohusisha Magari Manne Kongowe Temeke jijini Dar es Salaam Leo

div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
 Wananchi wakiangalia ajali iliyohusisha magari manne na pikipiki iliyotokea daraja la Mzinga Kongowe, Temeke jijini Dar es Salaam leo mchana. Katika ajali hiyo watu kadhaa walijeruhiwa.
 Wananchi wakiangali basi dogo aina ya Coster ya abiria namba T 415 DCC ikiwa imeharibika vibaya baada ya kugongwa.
 Wananchi wakiwa eneo la ajali
 Wananchi wakiwa eneo la ajali.
 Ofisa wa Jeshi la Polisi akiwa eneo la ajali akichukua taarifa.
Prado yenye namba  T 177 AHH iliyohusika katika ajali hiyo.

Na  Dotto Mwaibale

WATU kadhaa wamejeruhiwa vibaya katika ajali iliyohusisha magari manne na pikipiki iliyotokea daraja la Mzinga Kongowe Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Ajali hiyo ilitokea saa sita mchana na kuhusisha magari hayo lori la mafuta aina ya Scania lenye namba T 617 AQQ, Coster ya abiria namba T 415 DCC inayofanya safari zake kati ya Kilwa Masoko na Mbagala, Prado yenye namba  T 177 AHH, pikipiki na lori jingine. 

Ofisa wa Polisi aliyekuwepo eneo la ajali ambaye alitambulika kwa jina moja la Emanuel alisema chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika.

"Nimefika sasa hivi bado hatujajua chanzo cha ajali wala watu waliopoteza maisha na kujeruhiwa" alisema ofisa huyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto alipopigiwa simu ili kuthibitisha ajali hiyo alikiri kutokea  hata hivyo alisema alikuwa hajapata taarifa kamili kutoka kwa Mkuu wa Kikosi cha Usalama wa Wilaya hiyo ambaye alikuwepo eneo la tukio.

Kwa mujibu wa mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo walisema majeruhi walikimbizwa Hospitali ya Manispaa ya Temeke kwa matibabu.

The great escape.

Wimbo Mpya wa Kabago Akiwa na Harmad Tanzania Watoka Rasmi

Mkongwe wa Hip Hop nchini Kabago ameachia rasmi hii leo wimbo wake uitwao Tanzania akiwa na mkongwe mwenzake Hardmad, wimbo unaitwa Tanzania. 
Kupitia BMG sikiliza wimbo huo maana ni wimbo bora.
Bonyeza HAPA Kuupakua au bonyeza Play hapo chini kusikiliza.

Mh. Zitto Kabwe Amkumbuka Marehemu Mh. Samuel Sitta

Mh. Zitto Kabwe akiongea na Mh. Samuel Sitta nje ya Karimjee Hall Miaka ya Nyuma

Makala hii imeandikwa na Zitto Zuberi Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo

ALFAJIRI ya Novemba 7, 2016, tuliamka na kukutana na habari za kusikitisha ya kwamba mzee Samwel John Sitta, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametangulia mbele ya haki.

Mimi, kwa sababu ya heshima zangu kwake, nilikuwa nikimwita Babu. Ninafahamu kwamba alikuwa mgonjwa kwa kitambo kidogo akisumbuliwa na saratani ya tezi dume. Habari hizi zilisambaa kwa kasi kubwa kupitia mitandao ya kijamii. 

Hatimaye taarifa rasmi ikatoka kuthibitisha habari hizo.
Sitta aliitumikia nchi yetu kwa muda mrefu na kwa uadilifu mkubwa sana. Sisi wengine pia kwa kiasi fulani kukua kwetu kisiasa kumetokana na utumishi wake uliotukuka kwa nchi yetu alipokuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Babu yangu huyu ananigusa mimi binafsi moja kwa moja. Alikuwa mtu wangu wa karibu. Tukiwa bungeni akiniandikia kitu alikuwa akitumia neno hilo “babu” kwa mwandiko wake mzuri usiotoka kwenye kumbukumbu zangu kabisa.
Labda siku zijazo, ‘vi- note’ hivi vinaweza kuchapishwa pindi watafiti watakapokuwa wakiandika historia ya nchi yetu na Bunge letu.

Aliniapisha kiapo cha ubunge tarehe 29/12/2005. Maneno ambayo aliniambia baada ya kunikabidhi Kanuni za Bunge na Katiba ya Nchi niliyaandika kwenye daftari langu la kumbukumbu siku hiyohiyo jioni.

Baada ya kula kiapo cha Utii na cha Uaminifu, kawaida wabunge hupewa mkono na mwapishaji na kupewa nyaraka za kazi. Kwa upande wangu, Sitta alinikumbatia na kuniambia “ utakuwa kiongozi muhimu sana kwa nchi yetu. You have a bright future”.

Maneno haya hayajawahi kutoka katika kumbukumbu zangu na kila nikipata misukosuko yangu kisiasa huyakumbuka na wakati mwengine yeye mwenyewe alikuwa akinipigia na kunikumbusha na kunitia moyo. Babu alikuwa mlezi wa wanasiasa vijana.

Sitta pia naweza kusema amenilea kwa kunisomesha. Mwaka 1996 nilikuwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Galanos jijini Tanga nikisomea mchepuo wa Historia, Jiografia na Uchumi (HGE).
Hali ya hewa ya Tanga haikunipenda, hivyo nikawa naumwa umwa sana. Pia nilitaka kusoma Hesabu badala ya Historia.

Wakati wa likizo ya mwezi Disemba mwaka 1996, nilitoka Tanga nikaenda Dar es Salaam, Wizara ya Elimu kuomba uhamisho kwenda shule yenye Somo la Hesabu, kidato cha Tano na Sita.
Nikakataliwa. Lakini nikaambiwa kuwa Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari wakati ule, Alexander Ndeki, alisoma na Sitta. Kipindi hicho Sitta akiwa Mkurugenzi wa Investments Promotion Centre (IPC) kabla haijabadilishwa jina kuwa Tanzania Investments Centre (TIC).

Nikaenda ofisi za IPC mahala ambapo leo ni CRDB Tawi la Azikiwe. Nilipofika Katibu Muhtasi wake akaniuliza kama nina miadi na bosi wake, nikasema hapana. Akaniambia hawezi kukuona. Nikasisitiza sana na kumlilia dada yule aniruhusu dakika chache tu. Akaniruhusu.

Nilipofika Sitta aliniuliza shida zangu kwa heshima kubwa. Nikamwambia kwamba ninataka kuhama shule. Akaniomba matokeo yangu ya Kidato cha Nne, nikampa maana nilikuwa natembea nayo.
Alipoyasoma akaniambia, “ wewe hupaswi kuhangaika kutafuta shule maana kwa matokeo yako unaweza kusoma shule yeyote nchini ya chaguo lako”.

Akainua simu akampigia Ndeki. Kisha akaniandikia kikaratasi niende wizarani muda uleule. Nilipofika wizarani nikapewa uhamisho kwenda Shule ya Sekondari Mazengo.

Nilipotoka nje ya wizara, nikakutana na kijana mwengine anaomba uhamisho, yeye anatoka Mazengo anataka kwenda Tosamaganga, Iringa. Akaniambia, achana na Mazengo hakuna Mwalimu wa Uchumi na hali ya vyoo ni mbaya sana. Nikarudi kwa Mkurugenzi.

Mzee aliyenipa uhamisho aliponiona narudi na kumwambia sitaki Mazengo akachukua fomu zangu za uhamisho na akachukua ‘whiteout’ akafuta Mazengo na kuweka Tosamaganga huku akisema kwa hasira “ nyie watoto wa wakubwa bwana”.

Sikujali nikaenda zangu Tosa kusoma Uchumi, Jiografia na Hesabu (EGM). Tangu wakati huo, Sitta akaendelea kufuatilia maendeleo yangu shuleni hapo, kisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadaye Taasisi ya InWent nchini Ujerumani.

Nilipotoka Ujerumani kusoma masomo ya Juu ya Biashara ya Kimataifa mwaka 2004, ilipaswa niwe na mradi wa kitaaluma. Nikachagua kuunganisha kampuni za Kijerumani na zile za Tanzania kwa kuandika mradi wa kuchukua wafanyabishiara 20 kutoka Tanzania na kuwaunganisha na wengine 20 kutoka nchi za Jumuiya ya Ulaya.

Ilibidi kupata Taasisi ya Tanzania kwa ajili mradi huo na Sitta akawa mstari wa mbele kuhakikisha mradi unafanikiwa na tukautekeleza kwa umakini kwa msaada wa afisa wa TIC aitwaye Phina Lyimo.

Mwaka mmoja baadaye, tukakutana na Sitta bungeni, yeye akiwa Mbunge wa Jimbo la Urambo Mashariki na mimi nikiwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini. Ulezi wake ukaendelea mpaka mauti yalipomkuta wiki hii. Nimempoteza Babu mlezi.
Sitta alikuwa mwana mageuzi (reformer) na kupitia uanamageuzi wake alifanya mabadiliko makubwa sana katika uendeshaji wa Shughuli za Bunge.

Sisi tuliohudumu kwenye Bunge la Tisa, tukimwita Spika wa Kasi na Viwango, tuliona wenyewe juhudi zake za kuliweka Bunge katika nafasi yake ya Kikatiba. Licha ya kuhakikisha kuwa maslahi ya wabunge yanakuwa yanayolingana na hadhi ya Bunge, alihakikisha pia kuwa Bunge linaisimamia Serikali sawasawa.

Haikuwa kazi rahisi sana kwani kulikuwa na mvutano mkubwa sana kati ya Spika Sitta na Waziri Mkuu, Edward Lowasa, katika kuleta mabadiliko hayo.

Tulikuwa tunaambiwa kuwa mvutano ule ulitokana na tetesi kwamba Sitta ndiye alipaswa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na hivyo kuwa na msuguano na aliyeteuliwa kushika nafasi hiyo.
Sio Sitta wala Lowasa ambaye alithibitisha ama kukanusha tetesi zile. Sitta ametangulia mbele ya haki, labda Lowasa ataweza kusemea hili siku za usoni.

Sitta alitumia fursa ya msuguano huo kufanya mabadiliko makubwa ya kanuni za Bunge na kutoa uhuru mpana wa mawazo ndani ya Bunge na kuhakikisha kuwa Taarifa za Kamati za Bunge na hususan Kamati za Usimamizi wa Serikali zinakuwa zinasomwa na kujadiliwa ndani ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni.

Wakati wa Bunge la Nane, taarifa za CAG hazikuwahi kusomwa hata mara moja. Ni kutokana na mabadiliko haya ya kanuni ndipo Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC ) ilianzishwa mwezi Machi, mwaka 2008. Nilichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Kamati ile na kuingia kwenye Kamati ya Uongozi ya Bunge ambayo kipindi hicho tuliiona kama Kamati ya wabunge wazee.

Namna nilivyoingia kuwa Mwenyekiti wa POAC nayo ni hadithi nyengine ya namna ya malezi ya kiuongozi yaliyofanywa na Spika Sitta.

Sikuwa nimejaza fomu kuomba Kamati ya POAC. Wakati huo ulikuwa ni wakati wa vuguvugu la Buzwagi (Mkataba wa Madini uliosainiwa kwa siri na Waziri wa Nishati Hotelini nchini Uingereza ).
Nilikuwa mjini Bagamoyo kwenye kazi za Kamati ya Bomani nikiwa na Harrison Mwakyembe na Ezekiel Maige. Spika wa Bunge akanipigia simu, akaniambia “ Babu, kesho kuna uchaguzi wa Kamati za Bunge.

“Nimekuteua Kamati ya POAC ambayo ni kamati mpya itakayokuwa chini ya Kambi ya Upinzani. Najua hukuomba kuwa mjumbe wa kamati hii, lakini nahitaji damu changa kwenye Kamati ya Uongozi ya Bunge.

“Naomba unikubalie na kesho uwepo Dar es Salaam kwa ajili ya uchaguzi na ugombee. Utashinda maana nimeshafanya kazi yangu”. Sikuwa na namna ya kukataa japo nilitaka sana kuendelea kuwa Kamati ya Fedha na Uchumi chini ya Dk. Abdallah Kigoda, ama Kamati ya Nishati na Madini chini ya William Shelukindo.

Ombi la mzee ni amri. Nikawa Mwenyekiti wa POAC na kuwa mmoja wa washauri wakuu wa Spika wa Bunge. Kamati ya PAC ikawa chini ya John Cheyo na Kamati ya LAAC ikawa chini ya Dk. Willibrod Slaa. Ilikuwa ni Bunge lenye meno kwelikweli.

Sitta alikuwa mbabe. Ubabe wake ulimpelekea kufanya maamuzi ambayo wakati mwingine yalimweka kwenye matatizo na wananchi. Mfano mzuri ni suala la Hoja Binafsi ya Buzwagi na Hoja ya Wizi wa Fedha Benki Kuu ( EPA).

Mwanzoni, Spika alikuwa upande wa wabunge wenye hoja hiyo, mimi na Slaa kiasi cha kuziboresha hoja zile kwa kalamu yake mwenyewe. Wabunge wa chama chake hawakuwa wanapenda hoja hizi na hivyo Lowasa akamweka kwenye wakati mgumu sana wa kuegemea upande wa serikali.
Hoja ya Slaa akaitupa kuwa ‘ ni makaratasi ya kuokoteza’. Hoja yangu akaiingiza bungeni na akasimamia kusimamishwa kwangu Bunge.

Wananchi walimkasirikia sana. Siku moja usiku, nikiwa nyumbani kwa Freeman Mbowe Mikocheni, Samwel Sitta, akanipigia simu kulalamika kuwa wafuasi wangu wanamtukana kwa sms. Akaniambia niwakataze. Nilimkubalia tu, lakini sikuwa na uwezo huo.

Spika Samwel Sitta akawa ni Spika pekee wa nchi yetu aliyeshuhudia uundwaji wa Serikali mbili ndani ya miaka mitano ya Uspika wake. Mzee Msekwa yeye alikaa miaka 10 na Waziri Mkuu mmoja, ingawa mwaka 1993-1995 naye aliona mabadiliko ya Mwaziri Wakuu, kutoka John Malecela kwenda kwa Msuya.

Baada ya kujiuzulu kwa Lowasa, Sitta hakurudi nyuma tena. Aliendelea kuwa Spika wa viwango mpaka alipomaliza muda wake katika Bunge la Tisa.
Spika Sitta alikuwa mwepesi kuomba msamaha alipokosea.

Nakumbuka siku moja mwaka 2009 alimfukuza bungeni Cheyo kwa makosa ambayo mzee Cheyo hakufanya. Baadhi yetu tukakasirishwa na kitendo kile.

Nikaenda kumwona Sitta ofisini kumwuliza kulikoni amdhalilishe mwenzake namna ile. Akanieleza kuwa hakuwa sawa na atamwomba radhi Cheyo.

Tukiwa kwenye Kamati ya Uongozi ya Bunge, kwa ajenda zake za kawaida tu, Sitta akamwomba radhi Cheyo. Nikikumbuka kisa hiki nacheka sana maana Jaji Frederick Werema aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali alicheka mpaka kuanguka chini. Sababu?

Sitta aliketi kwenye kiti chake, wenyeviti wote wa Kamati tukiwa tumetulia tuanze kikao. Mzee Sitta akasema “ John, naomba radhi kwa tukio lililotokea bungeni wiki iliyopita.
“Sijui nilikuwa nina nini siku hiyo, nadhani nilisumbuliwa na watu wanaopitapita jimboni kutaka kunitoa, nisamehe mzee mwenzangu”.

Baada ya maneno hayo ukumbi mzima ulitawaliwa na vicheko na Cheyo akamkubalia radhi yake huku naye akicheka na yakaishia hapo. Wazee hawa wawili wameandika pamoja kitabu “ Bunge lenye Meno”. 

Nimwelezeje zaidi Babu? Nimwelezeje zaidi Spika huyu wa Kasi na Viwango? Mwanasiasa shupavu, jasiri, mwenye ngozi ngumu, mbabe, mnyenyekevu inapobidi na mwenye uthubutu.
Tangulia Babu. Tangulia Mtemi wa Unyanyembe Samwel John Sitta. 

Raia Mwema

Miss Tanzania 2010, Genevieve Mpangala Kusaidia Kurejesha Heshima ya Elimu Tabora

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010 Genevieve Mpangala amejitosa kusaidia kurejesha heshima ya mkoa wa Tabora katika elimu hasa kwa wasichana ambao ndio nguzo kubwa kwa familia na maendeleo ya taifa.

Mrembo huyo ameamua kufanya hivyo kwa kutembelea shule mbili za Tabora Girls na Isevya kuongea na wanafunzi, kuwapa moyo na kuangalia matatizo yanayowasumbua katika kujipatia elimu.

Akizungumza na Moblog amesema kwamba amekuwa na masikitiko makubwa na matokeo ya mitihani ya kitaifa ya sekondari kwa miaka mitatu ilhali simulizi za Tabora miaka iliyopita ni za kufurahisha sana uikionesha kwamba mkoa huo ndio kitovu hasa cha elimu.

Anasema ukisoma nyaraka mbalimbali unaona jinsi Tabora ilivyokuwa ngome ya elimu huku watanzania wengi wakifika hapo pia kupata elimu ya sekondari.

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010, Genevieve Mpangala akizungumza wa shule ya sekondari Tabora Girls hivi karibuni.

“Kwa kweli pamoja na masimulizi mazuri kuhusu elimu Tabora miaka ya 80 na 90 ,nilichagua Tabora girls kwa sababu ni shule aliyosoma mama yangu mzazi form 1 mwaka 1977 mpaka 1980 mpaka na aliisifia sana shule yake hiyo na nikapenda niweze kuwa karibu nao kuhakikisha wanafunzi wote wanamaliza,na Isevya ilikua chaguo la pili kwasababu ilikua ni shule ya kutwa (day) na nilipendelea kuongea na wanafunzi hao” alisema Genevieve.

Mkoa wa Tabora ambao unapatikana kati ya Magharibi ya Tanzania kwenye uwanda wa latitudo 40-70 Kusini na longitudo 310 - 340 mashariki ukipakana na mikoa ya Shinyanga, Katavi, Singida, Kigoma na Dodoma ni mji ulioanzishwa na wafanyabiashara wa Kiarabu kwenye miaka ya 1850 ukijulikana kama Kazeh .

Kihistoria Kazeh ambayo ilikuwa kitovu cha biashara ya utumwa, mwaka 1871 robo ya mji ilichomwa moto na kuvurugwa na mtawala wa wanyamwezi Mirambo .

Ingawa mwaka 1885 hadi 1891 wajerumani walijaribu kutawala, historia zinasema kwamba mji huo ulikuwa na vurugu kubwa lakini baadae ukatawaliwa na wajerumani wakafanya mji wa utawala kabla ya vita kuu ya kwanza kuingia na wao kung’olewa.
Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010 Genevieve Mpangala akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi na mwalimu wao alipofanya ziara shuleni hapo.

Pamoja na historia yenye misukosuko ya Mkoa wa Tabora ambao ni moja ya mikoa yenye eneo kubwa unategemea sana kilimo kufanikisha maisha lakini kwa miaka mingi mkoa umekuwa ukididimia kimaendeleo na kijamii.

Mkoa wa Tabora ambao umekua wa mwisho kwa miaka mitatu mfululizo mwaka 2013,2014 na 2015 unahitaji nguvu kubwa ya kujiondoa katika shida ya kuporomoka katika elimu

Mrembo Genevieve anasema ziara yake katika shule hizo imemfumbua macho na kuona haja kubwa ya kuendelea na programu za kufufua matumaini.

Pamoja na kuwashukuru walimu kwa ushirikiano waliompa aliwataka wanafunzi kuweka mkazo katika imani, matumaini na kutekeleza ndoto zao katika uwanda mkubwa zaidi.
Aidha pamoja na kuzungumza "HAVE FAITH,HOPE FOR MORE AND DREAM EVEN BIGGER", pia aliwaasa kuwa elimu ni msingi mzuri wa maisha na kuwa wasiharakishe na kupotoshwa na mambo ya kidunia kwani haya maisha yapo.

Akiwa na wasichana wa shule ya Tabora Girls walimweleza changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni pamoja na kutokuwepo na uzio kwenye shule yao hiyo, uhaba wa vitabu, upungufu wa walimu, uhaba wa upatikanaji wa habari mubashara, kwa wanafunzi kwamba hawana king'amuzi,kwa wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi wanauhitaji wa msaada wa kofia pamoja na mafuta ya kuwakinga na jua.

Matatizo hayo yanatokana zaidi na kwamba wengi wao wanatoka kwenye mazingira duni. Changamoto nyingine ni pamoja na kuwa na zahanati ambayo ina uhaba wa vifaa mfano:vyandarua vya kutosha pamoja na vitanda,pia kwa wanafunzi ambao wanaulemavu wa macho ambao ni hafifu na vipofu kabisa hivyo kuna uhaba wa brail paper.

Ziara fupi ya Mrembo wa Tanzania 2010 Genevieve Mpangala kwa shule mbili za jijini Tabora za Isevya Secondary School na shule ya vipaji maalum ya wanawake Tabora girls.

Amesema katika mazungumzo yake na wanafunzi hao amebaini pia kwamba kutofanya vyema kwa wanafunzi pia kunasababishwa na wanafunzi hao kutumia madawa ya kulevya, utoro, mimba za shuleni na wazazi kuozesha mabinti katika umri mdogo kabla ya wao kumaliza shule.