Saturday, December 31, 2016

Heri ya Mwaka Mpya 2017!

Wadau, Mungu yu Mwema, tumefika 2017!

Nawatakia wadau wote Heri ya Mwaka Mpya! 


Saturday, December 24, 2016

Scrooge Albert Finney 1970 DVD - kwa Wenye roho Mbaya! Mtatubu!

Bing Crosby - It's Beginning to Look A Lot Like Christmas

Krismasi Njema!

Nawatakia wadau wote, Krismasi Njema! Mbarikiwe!

Merry Christmas!

Barua ya Kitapeli - Mtaibiwa Sana!

Nafahamu watu ambao wanadhani huo upupu ni kweli.  Eti utapata mamilioni ya madola ukitoa habari ya akaunti yako benki, au ukilipa dola $2000 ili upate mamilioni! Uchu wa pesa mbaya! Mtaibiwa sana!

********************************************

  • Dec 23 at 10:50 AM
Message body
HSBC BANK N.A.
140 Broadway
New York, NY 10005, USA

                                                          Payment Release Instruction from Federal Reserve Bank of New York

Acting on our capacity as the international correspondent bank to the International Monetary Fund Organization, this is to officially notify you that we have received a confirmation advice from the International Monetary Funds External Auditors Committee, World Bank, United Nations Organization and the Federal Reserve Bank of America respectively via International Payment Voucher Number: IMF/FRBWDC/BOA-93WB82UN567-G requesting our bank to direct the HSBC BANK USA N.A, a subsidiary of the Federal Reserve Bank of America to disburse your due wining/inheritance and contract payment valued at Ten Million Three Hundred Thousand United States Dollars (US10.3M) in your favor via their branch in New York.

In consideration of the above, you have been issued with this Exclusive Reference Identification Number (IMF/FRB-NY/9USXX10751/09), Vide Transaction No.: WHA/EUR/202 and Transfer Allocation No.: FRB/X44/701LN/NYC/US, Password: 339331, Pin Code: 78569, Certificate of Merit No: 104, Release Code No: 0876; Immediate HSBC Telex Confirmation No: -222568; Secret Code: XXTN014. Having received these vital payment numbers, you are instantly qualified to receive and confirm your payment within the next 72hrs. As necessary clearance has been granted from the International Monetary Funds External Auditors to release the funds to you with immediate effect.
In view of this directive received from the International Monetary Funds (IMF), we have on our own part verified your payment file as directed to us, and your name is next on the list of outstanding fund beneficiaries to receive their payment at this Third quarter of year 2016. With that being done, you are required to urgently contact the HSBC USA N.A. in New York through their International Funds Release Supervisor:

Contact Person: Sir Nelson Haggin.
(Head, Funds Release Supervisor)
Email: nelson.haggin116@gmail.com
Direct Office Line:  (+16465689796)

And reconfirm your international payment voucher number and your reference identification number respectively before that office with a view to the final remittance approval and subsequent crediting of your bank account to the tune of funds as stated herein.
We wish to inform you of the need for you to also re-confirm the following information before the HSBC BANK USA N.A. in New York to enable the officer in-charge to proceed with the preliminary arrangements that will enhance the immediate release of your funds. Owing to security reasons, be clearly informed that we will not respond to any phone calls/general inquiries placed to our bank with regards to the remittance of your funds by beneficiaries as we are barred from doing so, you are therefore advised to communicate only with the accredited officer for further remittance advice.

1) Full Name
2) Full Address;
3) Your contact telephone and fax number;
4) Your Age and Profession;
5) Copy of any valid form of your Identification;
6) Your Bank name;
7) Your Bank Address;
8) Account name and Number;
8) ABA/Routing Number;
10) Swift or Sort Code/IBAN

Thank you for your anticipated co-operation.
TREAT AS URGENT.

MIS. MARIE DUNCAN
DIRECTOR OF FUNDS CLEARANCE UNIT.
FEDERAL RESERVE BANK

Unyanyasaji wa Kijinsia: Mchango wa UMIss Tanzania Unaonekana?

Na Elias Muhongo

Tukiwa tunaangalia tangazo la biashara la ‘BIG BOSS’ nikashtukia mwanangu mmoja akilalamika: “Hapo si tunajinyanyasa kweli?”. Nikamuuliza ana maana gani? Akasema “ Baba angalia sana tangazo hilo. Huyu mama anamfahamu boyfriend wake lazima, ndiyo maana alikuwa hakupotea nyumba. Lakini kukutana na harufu ya manukato anayotumia boyfriend wake akaamua kuondoka na aliyejipaka (manukato hayo)? Ni unyanyasaji wa kijinsia na hapo tunajinyanyasa wenyewe”. Mjadala ulikuwa mkali lakini nikomee hapo na kuendeleza mawazo yangu kuhusu unyanyasaji wa kijinsia, hasa unyanyasaji wa wanawake.
Nimeangalia mijadala mingi kipindi hiki na kuilinganisha na kipindi fulani kilichopita. Wakati wa maandalizi ya mkutano wa Beijing 1990, nilishiriki sana maandalizi hayo hapa nchini. Nakumbuka akina mama kufikia hatua ya kuainisha aina mbali mbali za unyanyasaji unaowakabili wanawake. Kupigwa na waume zao. Kusafiri mbali kutafuta maji. Huduma duni za afya wakati wa uzazi na uzazi wa mpango, nakadhalika. Lakini pia walijiambia ukweli mwingine wasiojiambia siku hizi. Walijiambia jinsi inavyokuwa vigumu kukutana na mwanamke aliye madarakani. Jinsi ilivyo vigumu mwanamke kumpigia kura mwanamke mwenzake licha ya wingi wao.
Tulijadili na jinsi katika michezo kama dansi akina mama wanavuliwa nguo na kujianika huku wenzao (wanaume) wanacheza wamejivalia nguo.

Wagombea Miss Tanzania 2009

Ninaamini kuwa huenda baadhi ya manyanyaso yamepungua. Lakini ukichunguza sana utakuta yale wanayojinyanyasa yanaendelea na hayapigiwi kelele kama yale wanayonyanyaswa.
Tuangalie na huu unyanyasaji wa kijinsia kupitia ‘Miss Tanzania’. Nakumbuka katika historia ya Miss Tanzania tangu viruhusiwe baada ya utawala wa Mwalimu Nyerere, naweza kudhibitisha kuwa ni mwaka mmoja ambao Tanzania iliwahi kuwakilishwa na mtanzania halisi licha ya kupingwa na watanzania wengi. Ni mwaka Tanzania ilipowakilishwa na Mtanzania mwenye asili ya India. Huyo alionyesha asili yake na utanzania wake. Lafudhi yake ilikuwa ya mtanzania mwenye asili ya India. Myondoko yake ilikuwa ya Mtanzania mwenye asili ya India. Rangi ya ngozi yake iliwakilisha Mtanzania mwenye asili ya India. Nywele za kichwa chake ziliwakilisha mtanzania mwenye asili ya India.

Nani anitajie mwingine? Anitajie Mis Tanzania ambaye aliiwakilisha Tanzania nje ya Tanzania na waangalizi wakaiona Tanzania? Sitarajii. Maandalizi ya Miss Tanzania yanamuandaa mwakilishi wetu kuuondoa utanzania ndani mwake. Maandalizi huanzia Willayani. Yanapokamilika ngazi ya Taifa mshindi na washiriki wote wanakuwa wamekamuliwa utanzania ndipo (mshindi) anakabidhiwa bendera ya Tanzania kwenda kuwakilisha kitu kisichojulikana. Huwezi kuuona utanzania katika lafudhi yake. Huwezi kuuona utanzania katika myondoko yake (gait). Huwezi kuuona utanzania katika asili ya ngozi yake wala nywele zake. 

Lakini kila mashindano hayo na maandalizi yake yanapokuwepo hukosi kuhisi unyanyasaji wa wazi na wa siri. Mavazi wanayovaa ni unyanyasaji wa ajabu usioendana na Utanzania. Lakini wasikie waandaaji wakijitetea kuwa hakuna eushwa ya ngono zinazoendelea katika shughuli hiyo. Nani haoni kuwa hayo hayawezi kukosekana? Huu wote ni unyanyasaji wa kijinsia unaoendelea kwa hiyari ya wanyanyaswaji na wanaharakati usioweza kupigiwa kelele kwa sababu tu wafadhiri wa miradi ya uanaharakati ndio wadhamini wa unyanyasaji huo.

Kuna wakati niliwahi kufikiri badala ya mashindano ya Miss Tanzania kwa nini kusianzishwe mashindano ysa mapishi ya kitanzania. Inahitaji kuandaa vigezo vya kuamua namna ya kuamua kati ya chakula cha kihaya na kipare. Mpare atapika kande na mhaya ndizi zilizochanganywa magarage mabichi na nyama iliyokauka watu watakula na kuuona utanzania. Ikishindikana basi shindanisha wapishi mbali mbali wa chakula aina moja. Mapishi yetu hayawezi kuchakachuliwa kama ambavyo utamaduni wetu unachakachuliwa kupitia mashindano haya ya Miss Tanzania.

Elisa Muhingo

Thursday, December 22, 2016

Zanzibar ilitoa Msaada Kwa Uiingereza!!!!

Jamani tumezoea kuwa wapokea misaada. Lakini je, mlikuwa na habari kuwa wakati wa Vita Kuu ya pili vya dunia (World War 2) Zanzibar ilitoa msaada wa chakula Kwa waingereza wenye nja? Wakati Ile Zanzibar ni Sultanate.




Saturday, December 17, 2016

Zilipendwa - Pata Pata

Huu wimbo wa Pata Pata ilikuwa kiboko enzi zile. Uliimbwa na MSwazi, Miriam Makeba aka Mama Africa.



Namna na Kuepuka Matumizi Makubwa ya Fedha Kiindi cha Sikukuu


Na Jumia Travel Tanzania

Kwa kawaida kipindi cha sikukuu ni wakati ambao watu wengi huwa na matumizi makubwa ya fedha kwa ajili ya kusherehekea pamoja na wapendwa wao, famila, jamaa na marafiki.

Jumia Travel (www.travel.jumia.com) ingependa kukushauri kwamba ni vema ukawa na mpango madhubuti unaoeleweka wa namna gani pesa yako itakavyotumika ili pindi mwaka mpya utakapoingia uwe mwenye furaha na sio huzuni.

Tenga Bajeti Mapema

Kuna namna nyingi za kutenga bajeti kwa ajili ya matumizi yako kama vile manunuzi ya zawadi kwa watoto, wazazi, kutoa msaada pengine na mengineyo ndani ya nyumba. Endapo utapanga mapema itakusaidia sana kujua utahitajika kutumia kiasi gani kipindi hiki badala ya kukurupuka sikukuu zinapowadia.

Fuatilia Mwenendo wa Matumizi Yako

Kutenga bajeti pekee tu haitoshi bila ya kuwa na mbinu sahihi ya kufuatilia mwenendo mzima wa jinsi pesa inavyotumika. Tenga pembeni bajeti ya sikukuu kwa kufungua akaunti ya benki ili isiingiliane na ya matumizi ya kawaida. Unaweza kutumia mbinu mbalimbali kuhakikisha unafanikiwa katika hili, kwa mfano kuwa na programu ya simu, ambayo utakuwa unaweza kufuatilia kwa ukaribu mwenendo wa matumizi na kiasi cha pesa kilichobaki popote na muda wowote ulipo.

Punguza Matumizi Yasiyokuwa na Tija

Unaweza kuepuka au kupunguza matumizi ambayo si ya lazima ndani ya kipindi hiki ili kufidia gharama kwenye vitu vingine. Kwa mfano, kama ulikuwa na mazoea ya kwenda na familia yako kwenye hoteli ya kifahari kwa ajili ya mapumziko kila wikendi pengine gharama yake ni TSHS 100,000/- kwa wiki ambayo ni sawa na TSHS 400,000/- kwa mwezi, unaweza kuacha kwa mwezi huu ili kuitumia kwa mambo mengine.

Pendekeza Utaratibu wa Kununuliana Zawadi kwa Siri

Kwa bahati mbaya familia nyingi za kiafrika sio wenyeji wa utamaduni huu wa kununuliana zawadi kwa siri au ‘Secret Santa’ kama inavyojulikana kwa lugha ya Kiingereza.  Mbinu hii ina manufaa makubwa sana kama utataka kuepuka gharama kubwa za kumnunulia zawadi kila mwanafamilia, kwa mfano, pengine una baba, mama, kaka, dada, binamu, wajomba na mashangazi unaweza ukautambulisha utaratibu wa kila mtu kumnunulia zawadi mwenzio kwa siri na kumkabidhi siku ya sikukuu. Nadhani inaweza kuleta msisimko zaidi na kila mtu akafurahia.

Epuka Mila Zitakazo Kugharimu


Kuna baadhi ya makabila bado yana taratibu ambao huwalazimu wanakoo kukutana kwa pamoja ifikapo kila mwisho wa mwaka. Watu hulazimika kusafiri na kutumia gharama kubwa kwa karamu ambazo huandaliwa na kujikuta mwaka unaanza wakiwa hawana fedha za kutosha. Unaweza kuepuka hayo yote kwa kufanya vitu vya kawaida ambavyo familia yako itavifurahia na kuvipenda.

Kuwa Mwangalifu na Ofa za Mauzo

Inabidi kuwa makini sana na ofa zinazotolewa na wauzaji wa bidhaa mbalimbali ndani ya kipindi hiki cha sikukuu. Wafanyabiashara ni werevu sana kwani hutumia mbinu mbalimbali za kuuza bidhaa zao kwa kuweka mabango makubwa ya ‘Ofa Ofa!’ huku bei ikiwa ni ileile sawa na siku za kawaida. Kuepuka hili unapaswa kufanya tafiti mapema kwa kutembelea maduka au mitandao ili kujua kama ni kweli kuna unafuu kwenye hizo bei zinazotangazwa.

Jitahidi Kutokuzidisha Manunuzi Yako


Kutokana na ofa kemkem ndani ya kipindi hiki cha sikukuu wateja wengi hujikuta njia panda kwa kushindwa kujizuia kuzidisha manunuzi wanayoyafanya. Inashauriwa kuwa na orodha pamoja na bajeti ya vitu unavyotaka kwenda kuvinunua ili pindi umalizapo usizidishe kwa kutamani vingine. Kama ikiwezakana fanya manunuzi mapema kabla ya sikukuu yenyewe ambapo kutokana na punguzo kubwa la bei ukajikuta unataka kununua kila bidhaa.

Mwisho kabisa Jumia Travel (www.travel.jumia.com) 
inakukumbusha kufanya tathmini ya pesa na matumizi uliyoyafanya ili kujua kama ulikuwa ndani ya bajeti kama ulivyojipangia au la. Kwa kufanya hivyo, utakuwa na mkakati mzuri wa kuanza mwaka mpya bila ya msongo wa mawazo.

Kongamano la Kumuenzi Fidel Castro


Nilibahatika kuhudhuria japo kwa muda mfupi Kongamano ya Kumuenzi Marahemu Rais Fidel Castor wa Cuba, iliyofanyika mjini Dar es Salaam, Tanzania, jumapili iliyopita December 11, 2016 kwenye hall ya Taasisi ya Watu Wazima. (Symposium to Honor the Legacy of Fidel Castro).  Waliongolea jinsi Castor alivyotoka kwenye familia ya matajiri lakini alipenda kusaidia na kunyanua maskini.  Pia jinsi Cuba ilivyosaidia Tanzania.


Jenerali Ulimwengu Akiongea
Audience Participants
The Symposium Leaders

Mfuko wa PPF Wadhamiria Kuwafikia WaTanzania Wote Wakiwemo Wasnatasnia wa Filamu

Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Meshack Bandawe, akizungumza kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wadau wa filamu na michezo ya kuigiza mkoani Mara. 

Mafunzo hayo yalanza Disemba 14 na yanafikia tamati leo Disemba 16, 2016 katika ukumbi wa shule ya Sekondari Mara Mjini Musoma. Yameandaliwa na Bodi ya Filamu nchini ili kuwajengea uwezo wadau wa filamu ili kuzalisha kazi zenye ubora.
#BMGHabari
Wadau wa filamu mkoani Mara wakimsikiliza Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe, wakati akiwaeleza umuhimu wa kujiunga na mfuko huo
Afisa Masoko PPF, Evance Baguma, akiwasilisha mada kwa wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara
Wadau wa filamu mkoani Mara wakifuatilia mada kutoka kwa Afisa Masoko PPF, Evance Baguma
Wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara wamefurahishwa na mada kuhusu mifuko ya hifadhi ya jamii kutoka PPF na kuonesha mwitiko mkubwa wa kujiunga na mfuko wa Pensheni wa PPF.

Mfuko wa Pesheni wa PPF umesema umedhamiria kuhakikisha kwamba wananchi wengi walio kwenye sekta zisizo rasmi ikiwemo wajasiriamali wananufaika na mafao ya hifadhi za jamii kupitia huduma ya Wote Scheme.

Meneja wa mfuko huo Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe, ameyasema hayo Musoma mkoani Mara, wakati akieleza umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko huo mbele ya wadau wa filamu mkoani humo.

Amesema wananchi wasio kwenye sekta rasmi wakiwemo wajasiriamali wanayo fursa ya kujiunga na mfuko wa PPF na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu, mikopo ya elimu, maendeleo pamoja na mafao ya uzeeni kwa kila mwanachama kuchangia shilingi elfu 20 kwa mwezi ambazo mwanachama hulipa kadri awezavyo.

Naye Afisa Masoko PPF, Evance Baguma, amesema lengo la mfuko huo kuanzisha huduma ya Wote Scheme kwa wajasiriamali ni kuondoa dhama potofu kwa baadhi ya wananchi kwamba anayeweza kunufaika na huduma za mifuko ya hifadhi za jamii ni lazima awe mtumishi wa taasisi binafsi ama serikali.

Wadau wengi wa filamu mkoani Mara wamefurahishwa na ufafanuzi wa mfuko huo ambapo wamebainisha kwamba awali walikosa fursa mbalimbali za mifuko ya hifadhi za jamii ikiwemo PPF kutokana ufahamu duni waliokuwa nao.
Tazama picha zaidi HAPA

Katibu Tawala Moani Mara Ahitimisha Mafunzo kwa Wadau wa Filamu Mkoani Humo

Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (katikati) akizungumza hii leo kwenye kilele cha mafunzo ya siku tatu kwa wadau wa filamu mkoani humo. Mafunzo hayo yalianza juzi Disemba 14,2016 kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari Mara Mjini Msoma.

Yaliandaliwa na Bodi ya Filamu nchini kwa lengo la kuwajengea welezi wanatasinia wa filamu ili kuzalisha kazi zenye ubora na hivyo kukidhi ushindani katika soko la ndani na nje ya nchi ambapo zaidi ya washiri 200 walionufaika na mafunzo hayo wamepatiwa vyeti. Tayari mafunzo ya aina hiyo yamefanyika mikoa ya Morogoro na Mwanza na yataendelea katika mikoa mingine.
#BMGHabari
Wanatasnia wa filamu mkoani Mara wakimsikiliza Katibu Tawala mkoani humo, Adoh Mapunda, wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia hao. Ameahidi kutoa fulana (Tshirt) 250 kwa ajili ya wanatasnia wa filamu mkoani Mara waliohudhuria mafunzo hayo ambapo zitawasaidia hususani kuwa na sare ya aina moja wakikutana kwa pamoja
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao, amesema sekta ya filamu ina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wanatasnia wake na taifa kwa ujumla hivyo Bodi za filamu mikoani zihakikishe zinasimamia maendeleo ya tasnia hiyo.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso, amebainisha kwamba wadau wa filamu wakiwemo watayarishaji, waongozaji, wahariri pamoja na waigizaji wamefundishwa vyema mafunzo hayo ili kuzalisha kazi bora.
Mgeni rasmi, Katibu Tawala mkoani Mara, Adoh Mapunda (wa pili kulia), akipokea cheti cha utambuzi kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao, akipokea cheti cha utambuzi
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso
Mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo, Bi.Deograsia Ndunguru, kutoka Chuo Kikuu Dodoma, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari Genoveva kutoka Idara ya Habari Serikalini, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Katibu wa Chama cha Waigizaji mkoani Mara, Johnson Ibambai, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwakilishi wa Mkuu wa Shule ya Sekondari Mara, akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba yake kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari Amicus Butunga, akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba ya TBC kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari George Binagi akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba ya 102.5 Lake Fm kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (mwenye suti) na viongozi wengine wakiwa pamoja na washiriki wa mafunzo ya filamu mkoani Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (mwenye suti) na viongozi wengine wakiwa pamoja na washiriki zaidi ya 200 wa mafunzo ya filamu mkoani Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Mwigizaji Dan Msimamo kutoka Tarime amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuinua ubora wa filamu mkoani Mara na hivyo kukuza soko lake
Mwigizaji Justar Lucas kutoka Tarime amesema mafunzo hayo yamewaongezea weledi na kutambua kwamba filamu ni ajira na ikitumika vyema husaidia kukuza kipato cha wanatasnia wa filamu na taifa kwa ujumla.
Mwigizaji Innocent Mbalwa kutoka Bunda ameishukuru Serikali kupitia Bodi ya Filamu kwa kutoa mafunzo hayo ambapo amesema yatafungua milango mipya kwenye tasnia ya filamu mkoani Mara.
Mwigizaji Jackline James kutoka Musoma amesema mafunzo hayo yamemsaidia kutambua kwamba filamu ni ajira tofauti na alivyokuwa akidhani awali kwamba tasnia hiyo ni sehemu ya burudani.
******************
Katibu Tawala mkoani Mara, Adoh Mapunda, amewahimiza wanatasnia wa filamu mkoani humo kuwa wabunifu katika uzalishaji wa kazi zao ili kupanua soko la filamu ndani na nje ya nchi.

Mapunda ametoa rai hiyo hii leo, wakati akihitimisha mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia wa filamu mkoani Mara, yaliyoandaliwa na Bodi ya Filamu nchini ili kukuza welezi katika uzalishaji wa kazi bora na zenye maudhui yanaykubalika katika jamii.

"Ubunifu ndio unahitajika hivi sasa, watu wengi wanahitaji ubunifu binafsi na siyo "kucopy" na "kupaste" kazi za wengine". Amesisitiza Mapunda na kuongeza kwamba serikali itatoa ushirikiano wa dhati katika kuboresha tasnia hiyo ya filamu kwani hivi sasa hutoa ajira na kukuza uchumi kwa taifa.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nuru Millao, ameziagiza Bodi za Filamu za mikoa kuhakikisha kwamba zinatimiza wajibu wake ipasavyo ili kuboresha zaidi sekta hiyo.

Naye Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisso, amewahimiza wadau wa filamu mkoani Mara wakiwemo watayarishaji, waongozaji, wahariri pamoja na waigizaji walionufaika na mafunzo hayo, kuyatumia vyema ili kukuza soko lao la filamu.

Kwa upande wake Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, amewasisitizia hao kutumia mafunzo hayo ili kuzalisha filamu na vipindi vya luninga vyenye ubora ili kunufaika na uhitaji uliopo.

Akisoma maazimio ya wanatasnia wa filamu mkoani Mara, Katibu wa Chama cha Waigizaji mkoani humo, Johnson Ibambai, ametaja baadhi ya maazimio hayo kuwa ni pamoja na kuiomba serikali kuweka mitaala ya filamu kuanzia shule za msingi na vyuo vya ufundi VETA ili kusadia utoaji wa elimu hiyo ya filamu.
Tazama picha zaidi HAPA