Sunday, March 17, 2013

Mjengwa asitisha mahusiano na Ludovick Joseph kwa Tuhuma za "Kuhusika na matukio ya kigaidi'

TAARIFA RASMI KUTOKA Mtandao Wa Kijamii Wa MJENGWA BLOG

Sunday, 17 March 2013 | Written by Mjengwa Blog

Ndugu zangu,
Kutokana na kuwepo kwa taarifa rasmi za kipolisi zenye kumtuhumu Ludovic Joseph kuhusika na matukio ya kigaidi.

Uongozi wa Mtandao wa Kijamii wa Mjengwablog unasitisha rasmi, kuanzia leo Jumapili, Machi, 17,2013, kuwa na Ludovick Joseph kama msaidizi wa Mtandao wa Kijamii wa Mjengwablog na website ya Kwanza Jamii.

Maggid Mjengwa,
Mmiliki wa Mjengwablog /Kwanzajamii

3 comments:

  1. Baada ya kuwekwa video ya kupanga mbinu za kuteka na kutesa inayo
    muonyesha mkurugenzi wa usalama wa Chadema kwenye mitandao ya kijamii
    tumeshuhudia uharaka wa jeshi la Polisi kumkamata, kumhoji na kumuweka
    ndani kiongozi huyo, lakini pia hayakupita masaa 48 wakamkamata kijana
    mwingine mwenye jina la Ludovick Joseph kwa kuhisiwa kuwa ameshiriki
    kwa namna moja au nyingine kwenye uttengenezaji wa video hiyo japo
    naye inasemekana siku aliyo tekwa Kibanda naye alitekwa na
    kunyang'anywa vitendea kazi vyake pamoja na nguo alizo kuwa amevaa.

    Kwa kuwa nchi iko kwenye mtanziko wa mauwaji ya raia wasio kuwa na
    hatia ikiwa ni pamoja kutekwa na kuteswa kwa wanahabari na wengine
    kuuwawa kinyama nimejikuta najiuliza maswali kadhaa.

    1. Jeshi la polisi linashindwa nini kumkamata Mwigulu Mchemba aliye
    wahi kusema kwenye vyombo vya habari kuwa ana mkanda unao onyesha
    viongozi wa chadema wakipanga mauwaji?! Kwa nini jeshi la Polisi
    lisipate mahali pa kuanzia kwa kumkamata kiongozi huyu wa ccm?! Kama
    wamemkamata Rwekatare, wanashindwa nini kumkamata Mwigullu?

    2. Kwa kuwa mitandao ya kijamii imekuwa chanzo cha kupatia taarifa
    jeshi la polisi (kama video inayo muonyesha Rwekatare na hatimaye
    kumkamata), je polisi inashindwa nini kumkamata Sheikh Illunga ambaye
    naye video yake ya kuhamasisha waumini wa dini yetu (Kinyume na
    mafundisho ya Quran) iko bado kwenye mitandao ya kijamii na watu
    wakiendelea kuangalia na kusikiliza uchochezi wake?, mkumbuke kuwa
    kuna tishio la viongozi wa dini nyingine kuuwa.

    Naamini Tanzania ni yetu sote na hakuna aliye mtanzania zaidi kuliko
    mtanzania mwingine. Kila mwenye makosa afikishwe kwenye vyombo vya
    sheria na sheria zisiwe zenye meno kwa baadhi ya watu na sheria
    hizohizo zisigeuke kibogoyo kwa watu wengine.

    Tumeona mateso ya Dr Ulimboka na wahusika kutajwa kwenye baadhi ya
    vyombo vya habari lakini mpaka leo wahusika hawaja chukuliwa hatua
    zozote.

    ReplyDelete
  2. Habari zinatisha, kumbe LJ ni kijana wa Usalama wa Taifa?

    ReplyDelete
  3. Distancing from oneself! Mjengwa mnafiki sana!

    ReplyDelete