



Hivi karibuni, mcheza sinema maarufu wa hapa Marekani, Denzel Washington na familya yake walitembelea Brook Army Medical Center, mjini San Antonio, Texas (BAMC). Hiyo hospitali ni ya jeshi na inahudumia hasa wagonjwa walioungua moto. Wengi wameumia katika vita vya Iraq na wamesafirishwa kutoka Ujerumani.
Kuna nyumba kadhaa za familia za wagonjwa kukaa wakiwa wamefika kuangalia wagonjwa wao.
Mara nyingi zinakuwa zimejaa. Familia wanakaa pale kwa gharama ndogo au bila malipo kutokana na uwezo wao. Ni bei rahisi kuliko kufikia hospitalini.
Denzel aliliuliza bei ya kujenga nyumba moja ni bei gani. Aliambiwa. Alishangaza wanajeshi alipotoa andika hundi enye pesa za kutosha za kujenga nyumba moja.
Sasa watu wanashangaa. Kwa nini akina Britney Spears, Madonna, Robert Downey Jr. , Tom Curise, wakifanya vituko wanatolewa ukurasa wa kwanza wa magezeti. Denzel akitenda wema wako kimya!
Sasa watu wanashangaa. Kwa nini akina Britney Spears, Madonna, Robert Downey Jr. , Tom Curise, wakifanya vituko wanatolewa ukurasa wa kwanza wa magezeti. Denzel akitenda wema wako kimya!


