Thursday, February 16, 2012

Matatizo ya Kijiji cha Nanja Wilaya ya Monduli

Nafanya kazi katika Asasi inayotoa elimu ya UKIMWI na Afya ya Uzazi kwa jamii iliyopo Arusha. Mwishoni mwa mwezi huu tulifanya survey ya UKIMWI katika vijiji vya Nanja na Makuyuni vilivyopo wilaya ya Monduli kwa ajili ya mradi tunaotaka kuanza hivi karibuni.

Kilichonisukuma kuandika katika jukwaa hili ni matatizo tuliyoyakuta katika kijiji cha Nanja

HAWANA MAJI

Yaani hakuna kisima wala bomba la maji hivyo hutegemea maji ya mvua ambayo watu wachache ndio wanamatenki ya kuvunia maji hayo. Katika kipindi ambacho si cha mvua hununua maji ndoo ya lita kumi kwa tsh 300 hadi 500.

HAWANA KITUO CHA AFYA

Hakuna kituo cha afya/Zahanati wala clinic ya kutibu wanakijiji. Ikitokea kuna mgonjwa mpaka wampeleke Monduli,Makuyuni au Mto wa mbu ili waweze kupata matibabu. Kwa upande wa kinamama wajawazito wengi wao huzalishwa na wakunga wa jadii hivyo kuna uwezekano mkubwa wa vifo vya mama a mtoto.

Ombi langu kwa wanabidii kama kuna mtu aliyewahi kufanya utafiti au ana uzoefu wa maeneo haya ya Nanja aieleze jamii kuhusu sehemu hii kwakua watanzania wenzetu wanateseka.

Nawakilisha

Malima P. Macha
PM - CHAWAKUA

Chupi Bomber Afungwa Maisha

Umar Farouk Abulmutallab baada ya kukamatwa na FBI
Yule kijana MNigeria, aliyejaribu kulipua ndege na bomu alivaa ndani ya chupi yake siku ya Krismasi mwaka 2009 amepata kifungo cha maisha.  Umar Farouk Abdulmutallab, alikuwa na miaka 25 alivyojaribu kulipua hiyo bomu ya chupi. Haikulipuka kama alivyotarajia na badala yake kaunguza nyeti zake, bolo na mapumbu!  Hivi ni mwanaume gani wa kiafrika asiyethamini nyeti zake?! Alikuwa tayari kujiua na kuua watu wengine eti kwa ajili ya dini! Atakuwa punguani huyo, wala si dini. Mwache akae huko gerezani maisha atakuwa mke wa Big Bob.***********************************


DETROIT (AP) — A Nigerian man on a suicide mission for al-Qaida was sentenced Thursday to life in prison for attempting to blow up an international flight with a bomb in his underwear as the plane approached Detroit on Christmas 2009.

The mandatory punishment for Umar Farouk Abdulmutallab, the well-educated son of a wealthy banker, was never in doubt after he surprised the courtroom and pleaded guilty to all charges on the second day of trial last fall.

Abdulmutallab sat with his hands folded under his chin, leaning back in his chair as the sentence was announced.

In October, Abdulmutallab said the bomb in his underwear was a "blessed weapon" to avenge poorly treated Muslims around the world. It failed to fully detonate aboard an Amsterdam-to-Detroit flight but caused a brief fire that badly burned his groin. Passengers pounced on Abdulmutallab and forced him to the front of Northwest Airlines Flight 253 where he was held until the plane landed minutes later.

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI!

Tuesday, February 14, 2012

Ni Katerero au Katelelo? - WAKUBWA TU!


Leo ni Valentine's Day! Mfurahishe mpenzi wako! 

***********************************************************
Dada Dina anatutoa ushamba hapa!  Asante sana Dada Dina kwa somo nzuri sana.

Kutoka Dinahicious Blog:

Katelelo


"Dada Dinah habari ya kazi. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kazi unayoifanya ya kuelimisha jamii kuhusu ngono na mambo ya mapenzi kwa ujuma.

Leo katika pita pita mtaani nimekutana neno linaloitwa KATELELO. Nasikia ni jina la style ya kufanya sex maarufu huko Bukoba. Nimemwuliza rafiki yangu wa huko Bukoba anielezee, amebakia tu kucheka, kacheka kweli, amekataa kunieleza inafanywaje.

Basically nasikia ni Cli-toris Stimulation technique ambayo nasikia mwanamke akifanyiwa hata kama tangu azaliwe hajawahi pata orgasm atapata tu. Tena zaida ya yote nasikia mwanamke anaweza mwaga maji hadi LITA 3 au hata 4.

Jamani hiki kitu kipo kweli? Sasa kama kipo jamani mke wako au mpenzi wako akitombwa na hao jamaa wa katelelo si ndio atakukimbia tena kibaya zaidi awe hapati orgasm akisex na wewe.

Please dada Dinah pamoja na wadau wote kama hiki kitu ni kweli na kuna mtu anajua basi naomba na mimi animegee huo utalaam.

Asante, Mdau kutoka A-TOWN"

Jawabu: Asante, Katelelo ipo na nina uhakika wengi huwa wanaifanya ila majina ndio hutofautiana au hawaipi jina zaidi ya "nilimsugua kisimi", "nilichapwa kisimini" "nilinyonywa/lambwa kisimi".

Swala la lita tatu za maji sina uhakika linasababishwa na "katelelo" bali ni maumbile zaidi kwamba wapo wanawake wanamwaga maji na wengine wanatoa ute mwingi lakini sio kisai cha kuleowesha godoro.

Sasa ni hivi, Kitendo cha kucheza na kisimi kwa utaalamu na mirindimo tofauti mpaka mwanamke anamaliza ndio kinaitwa "katelelo", kitendo hiki hakina tofauti sana na "kumshukia" mwanamke yaani kucheza na kisimi kwa kutumia ulimi japokuwa ulimi ni mtamu zaidi kwa vile ni laini kutokana na mate kinywani vilevile unanyonya kila baada ya "vibrashi" vichache, bila kusahau kuna "speed" amabyo huongezwa na kupunguzwa.

Kitendo hiki hufanywa kwa kufuata mikao fulani kama ilivyo kwenye "kumshukia Chumvini" na mikao hiyo ni kama vile "Doggy" Inaweza kuwa ya kupiga magoti au ya kuinama, kulala chali na kupanua miguu, kukaa kochini au kitini na kupanua miguu.....kama hakionekani basi mwana mama itamlazimu kutumia mikono yake ili kupanua maeneo yake nyeti ili uweze kufanyia kazi "kiharage".

Kuna namna ya ukamataji wa uume ili kufikia lengo, kuna wale wanaoushikilia karibu zaidi na kichwa hali inayoongeza ukubwa wa "kichwa" na ugumu hali inayo ongeza utamu alafu ndio wanasugua (hii kama inauma vile eeh), wacha niseme ku-brashi Kisimi, ku-brashi huko hutofautiana (nitakuambia jisni ninavyoendelea)

Pia kuna wanaume wengine hushikilia uume kama vile wanavyo kojoa (sio manii bali mkojo maji) au wanavyouingiza ukeni lakini sasa wanaishia kisimini tu na kufanya ile-brashi. Sasa wakati unaendelea na ku-brashi unatakiwa kuongeza manjonjo na "spidi" ili kumpa mpenzi wako utamu makini.

Unaweza kuwa unachovyesha kichwa pale ukeni (unapoingia uume) pale mwanzo wa uke kuna utamu wake ambao ni tofauti au niseme ni zaidi ya ule wa kisimi japokuwa huwezi kufikia kilele.......wakati "unamkaTelelo" Kisaikolojia atakuwa anasikilizia Utamu wa ajabu bila kujua tofauti, yeye atakuwa akijua unacheza na sehemu ya juu ya uke wake ambayo ni Kisimi.

Ikiwa mwanamke unaefanyanae ni mmoja kati ya wale wenye kutoa maji mengi (nasikia baadhi ya Wahaya,Wachaga, Wanyakyusa (kwa Tz), Waganda, Warundi na Wanyarwanda) hii ni kwa ajili ya kula ndizi nini hehehehehe......basi wakati anakaribia utaanza kuona maji yakiongezeka na akifika kabisa basi ndio vile......usisahau kuanika Godoro.

Wanawake wengi wa Kiafrika wanapenda sana mtindo huu wa ufanyaji ngono kwa vile ni rahisi kufika kileleni kuliko aina nyingine ya ufanyaji hasa ukizingatia kuwa asalimia kubwa ya wanawake hawana uwezo wa kusikilizia/kupata utamu wa ngono kwenye maeneo mengine (mwanzo wa uke, Kipele G, Kuta za uke na eneo linaolitwa AFE).

Kisimi ni eneo pekee la linaloweza kumfanya mwanamke kupata uzoefu wa utamu wa ngono kwa haraka kuliko sehemu nyingine za uke wake hata kama kajaaliwa kusikilizia utamu ikiwa maeneo mengine manne yakifanyiwa kazi vema.

Natumai maelezo yangu na yawachangiaji wengine yatakuwa yamekusaidia kwa kiasi fulani....

Kila la kheri!

Happy Valentine's Day!

Nawatakia wadau wote siku njema na enye furaha tele na yule umpendaye leo hii siku ya Valentine's Day! 

Msisahau kufanya mapenzi kwa usalama!

Saturday, February 11, 2012

Whitney Houston Afariki Duna!!!!

(Pichani Marehemu Whitney Houston nwaka 2004)

Whitney Houston, superstar of records, films, dies



LOS ANGELES (AP) — Whitney Houston, who ruled as pop music's queen until her majestic voice and regal image were ravaged by drug use, erratic behavior and a tumultuous marriage to singer Bobby Brown, has died. She was 48.

Houston's publicist, Kristen Foster, said Saturday that the singer had died, but the cause and the location of her death were unknown.

News of Houston's death came on the eve of music's biggest night — the Grammy Awards. It's a showcase where she once reigned, and her death was sure to cast a heavy pall on Sunday's ceremony. Houston's longtime mentor Clive Davis was to hold his annual concert and dinner Saturday; it was unclear if it was going to go forward.

At her peak, Houston the golden girl of the music industry. From the middle 1980s to the late 1990s, she was one of the world's best-selling artists. She wowed audiences with effortless, powerful and peerless vocals that were rooted in the black church but made palatable to the masses with a pop sheen.

Her success carried her beyond music to movies, where she starred in hits like "The Bodyguard" and "Waiting to Exhale."

She had the perfect voice and the perfect image: a gorgeous singer who had sex appeal but was never overtly sexual, who maintained perfect poise.

She influenced a generation of younger singers, from Christina Aguilera to Mariah Carey, who when she first came out sounded so much like Houston that many thought it was Houston.

But by the end of her career, Houston became a stunning cautionary tale of the toll of drug use. Her album sales plummeted and the hits stopped coming; her once serene image was shattered by a wild demeanor and bizarre public appearances. She confessed to abusing cocaine, marijuana and pills, and her once pristine voice became raspy and hoarse, unable to hit the high notes as she had during her prime.

"The biggest devil is me. I'm either my best friend or my worst enemy," Houston told ABC's Diane Sawyer in an infamous 2002 interview with then-husband Brown by her side.

 http://music.yahoo.com/news/whitney-houston-superstar-records-films-dies-005927033.html

Zilipendwa - How Will I Know



Rest in Peace Whitney Houston (1963-2012)

Friday, February 10, 2012

Warsha ya Uandishi wa Miswaada ya Filamu - UDSM

WARSHA YA UANDISHI WA MISWAADA YA FILAMU/SCREENPLAY WORKSHOP
(Level 1)


Je? Unajua kuwa hadithi za Filamu zozote hujengwa kwa wahusika, wahusika ndiyo wabeba lengo zima la filamu?  Je, wajua jinsi ya kuwa jenga wahusika wako ili waweze kubeba lengo la hadithi ya Filamu kiufasaha? Je,unajua kuwa ukikosea kumjenga mhusika mkuu katika hadithi ya Filamu yako ni vigumu hadithi ya Filamu bora?

Basi ukitaka kuyajua yote haya karibu katika warsha ya uandishi wa miswada ya filamu pale IDARA YA SANAA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM Kuanzia tarehe 13-15 Februari 2012. Kuta kuwa na Warsha ya Uandishi wa Miswaada ya Filamu/Screenplay Workshop (Level 1) Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kila siku kuanzia saa 3 asubuhi hadis aa 8 mchana , Cheti cha Ushiriki kitatolew amwishoni mwa mafunzo.

Warsha itakuwa kwa Kiswahili (na Kiingereza ikibidi)na mshiriki anaweza kuwa mtu yoyote anayependa kuandika miswada ya filamu (amateur scriptwriter) au mwandishi anayechipukia (upcoming scriptwriter)

Hima wadau wote wa Tasnia ya Filamu ,Sanaa, Sanaa za Maonyesho na Uandishi wa ubunifu msikose nafasi hii muhimu ya warsha mafunzo daraja la kwanza ilikujijengea misingi mizuri ya Uandishi wa Miswaada ya Filamu.

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na warsha hii tafadhali wasiliana na IDARA YA SANAA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM , Ndg. John Mwakilama SimuN amba0714 13 22 49, na barua pepe: mwakilamajohn@yahoo.com

Thursday, February 09, 2012

Mkurugenzi wa TAMWA Ananilea Nkya Akamatwa na Polisi

UPDATE:  Dada Nkya ametoka kwa Dhamana jioni hii!

Dada Nkya akishika bango jana, Picha kwa hisani ya Global Publishers

Kutoka The Guardian:

Senior Tanzanian journalist arrested

The director of the Tanzania Media Women's Association (Tamwa), Ananilea Nkya, was arrested early today in Dar es Salaam.

She was detained along with several activists and journalists during a public demonstration calling for the government to resolve an ongoing doctors' strike.

Several hospitals have been closed during the strike by junior doctors and medical interns, which began on 30 January. They are protesting about pay and working conditions.

Some specialists have also joined the strike, and the Tanzanian government has come under mounting pressure to resolve the dispute.

The reason for Nkya's arrest remains obscure. She did make a statement yesterday about the need "to make the public disabuse themselves of the commonly held belief that prominent people care little about what is going on because they can access medical attention outside Tanzania."

But concerned supporters do not believe that to have been the reason for her detention.
Sources: Daraja/AllAfrica.com/IPPmedia/The Citizen

Maazimio ya Kikao Kati ya Waziri Mkuu na Madaktati Leo CPL

Asante Da Subi kwa Kuleta Taarifa Hii:


Tamko la Kamati: MAAZIMIO YA KIKAO CHA WAZIRI MKUU; MADAKTARI

09/02/20120 Comments Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari inayoongoza mgomo wa Madaktari, Dkt. Stephen Ulimboka baada ya kuzungumza na madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es salaam, Februari 9, 2012. (Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu)
TAARIFA KWA UMMA NA MADAKTARI WOTE NCHINI JUU YA MAAMUZI YALIYOFIKIWA LEO FEBRUARY 9, 2012 KUFUATIA MKUTANO KATI YETU NA WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA KATIKA UKUMBI WA CPL, HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

Kamati ya muda ya kushughulikia madai ya madaktari nchini inapenda kuwajulisha madaktari wote pamoja na kada nyingine zote za afya nchini juu ya kile ambacho kimejiri katika siku ya leo ya tarehe 09.02.2012 ikiwa ni matokeo ya kikao wanataaluma wa kada za afya na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda na baadaye kufuatiwa na kikao kati ya madaktari na kada nyingine za afya.

Ifahamike kuwa kama Kamati tulipata mwaliko wa kushiriki katika Mkutano huo ambapo ilitarajiwa kuwa Mhe, Waziri mkuu atafika kwa nia ya kutoa mrejesho wa madai ya madaktari yaliyowasilishwa mezani kwake mnamo tarehe 23.01.2012. Madai yetu yalikuwa manane na Mh Wazizri mkuu aliweza kutoa maelezo ya dai moja baada ya lingine.

Miongoni mwa madai ambayo mpaka sasa yamepatiwa majibu ya kuridhisha ni pamoja na;

Kuwawajibisha watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, wakiwemo Katibu Mkuu Mama Blandina Nyoni , na Mganga Mkuu wa Serikali Dr. Deo Mtasiwa. Aidha Mh waziri mkuu alisema kuwa ameshalifikisha kwa Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania suala zima la kuwawajibisha watendaji wa wakuu wa kisiasa wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambao ni Waziri Mh Hadji Mponda na Naibu Waziri Mhe. Lucy Nkya.

Kama sehemu ya maridhiano, Mh Waziri Mkuu pia aliahidi mbele ya mkutano kuwa hakutawepo na unyanyasaji au vitisho vya aina yoyote ile kwa wale wote walioshiriki katika kushinikiza Serikali kutatua kero hizo. Aidha kama sehemu ya maridhiano, Mh waziri Mkuu pia alifuta zuio la madaktari kutokufanya mikutano. Lakini pia, Mh waziri Mkuu alisema kuwa Serikali haina kusudio la kumfukuza kazi mtumishi yeyote wa afya yule kazi aliyeshiriki katika mchakato huu wa kuishikiniza Serikali kutafuta ufumbuzi madai ya madaktari nchini.

Aidha, Mh waziri Mkuu amesema “Interns” wote waliokuwa wamehamishwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wamesharudishwa bila masharti katika hospitali hiyo ili kuendelea na program kama kawaida. Hili pia linaambatana na kulipwa na kupewa stahiki zao zote.

Pia suala la madaktari na familia zao kuwa na Kadi ya Bima ya Afya ya kijani( Green Card) limekubaliwa na kwa sasa tusubiri utekelezaji.

Pia ilikubaliwa kuwa madaktari watapata fursa ya kukopeshwa magari kama watumishi wengine wa umma.

Mbali na madai hayo, pia Mh. Waziri Mkuu alitoa ufafanuzi juu ya madai yanayuhusu maslahi ya watumishi wa afya ikiwa ni pamoja na Mishahara na Posho na stahiki mbalimbali. Lakini hata, Mh waziri Mkuu hakutoa majibu ya moja kwa moja ya kiwango gani kitakachoweza kulipwa na Serikali kama mishahara, posho na stahiki mbalimbali kwa minajili kwamba bado zinafanyiwa kazi na kamati ya wataalamu aliyoiunda ili waweze kumshauri. Aidha, Mh waziri Mkuu alisema kuwa kwa wakati huu inaweza kupandisha “on call allowances” za kada mbalimbali za afya kutoka shilingi 3,000 – 10,000/= na kufikia kati ya shilingi 5,000 hadi 25,000. Madaktari bado wanaona ongezeko hili halilingani na ukubwa wa kazi ifanywayo pindi mtumishi wa afya anapokuwa “on call” na hivyo basi kuendelea kupendekeza kuwa “on call” allowance iwe ni 10% ya mshahara wa mtumishi husika.

Pia Mhe, Waziri Mkuu hakuweza kueleza kinagaubaga mkakati kazi wa uboreshaji wa huduma za afya wapatayo wananchi wa Tanzania.

Baada ya tamko hilo la Serikali kumalizika, Mh Waziri Mkuu na ujumbe wake waliondoka, na Mkutano huo ukaendelea kwa Kamati kufanya Mkutano na madaktari wote, lengo ikiwa kujadili tamko hilo na kutoa maazimio.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu, madaktari walikubaliana kwamba; kwa kuwa Serikali imeanza kuonyesha nia ya kutatua tatizo hili kwa kutekeleza baadhi ya maazimio yetu, wajumbe kwa niaba ya madaktari wote nchi nzima tulikubaliana na kuazimia yafuatayo;

Kurudi kazini mara moja kuanzia kesho tarehe 10.02.2012 bila masharti yeyote.

Kamati ya jumuiya ya madaktari kama sehemu ya MAT kuendelea kukaa mezani ya majadiliano na Serikali ili kuanza kupitia madai hasa yale yanayohusu maslahi.

Kukutana tena tarehe 03.03.2012 ili kupata mrejesho wa kiwango cha utekelezaji wa madai hayo kwa mujibu wa vikao vya majadiliano na makubaliano na hatimae kuchukua hatua zaidi.

Kujadili utekelezaji juu ya Kuwawajibisha Waziri na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi na Jamii.

Mwisho kabisa Madaktari wote kwa ujumla wake walilaani na kukemea kitendo cha Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwahoji wanaharakati wa haki za kibinaadamu na mashirika ya kijamii wakiwemo Dr. Hellen Kijo-Bisimba na Mama Ananilea Nkya na wanaharakati wengine wote waliokumbwa na kamata kamata hiyo na hivyo basi tunalitaka jeshi hilo kuwaachilia huru mara moja bila masharti yeyoye.

Pamoja Tunaweza

Imetolewa na Kamati ya muda ya kushughulikia madai ya madaktari Tanzania

Dr, Ulimboka Stephen
Mwenyekiti.

Monday, February 06, 2012

Bibi Yake Rais Obama Apata Ajali ya Gari Kenya!

Wadau, Bibi yake Rais Barack Obama, amaepata ajali ya gari Kenya. Bibi Obama ana miaka 91.
Mungu yu mwema na hakuumia sana.  Kweli alikuwa na malaika alivypata ajali.

********************************

A man looks inside the car that President Barack Obama's grandmother Sarah was in when it rolled in Kisumu, Kenya, Feb. 4, 2012. (Courtesy Nation Media)
 President Obama's Grandmother in Car Accident

By Bazi Kanani

NAIROBI - President Obama's grandmother, Sarah Obama, is home recovering at her home in western Kenya after an accident that, judging by the condition of the vehicle, could have been much worse.

"God is with me, because if you could have seen the wreckage that we came out of safe, one would wonder," Sarah Obama said Monday.

Police in the town of Kisumu say the 91-year-old was traveling to her home in the village of Kogelo Saturday night when the driver lost control, and the vehicle rolled into a ditch.

All five people in the car, including her two bodyguards, were taken to a hospital for treatment. All were released with minor injuries.

A hospital spokesperson says Sarah Obama was bruised and in shock when she arrived at the hospital. She was released about two hours later.

"You can see I was not injured save for this small scar on my right hand and I am not even using a walking stick," Obama said.

She said friends from as far away as the United States and the Middle East have been calling to check on her, but she assures them, "Hakuna tabu!" That means 'no problem' in Swahili.

Sarah Obama is the step-mother of President Obama's Kenyan father. She has been to the U.S. a few times, and the President has been to the village to visit with her and other relatives three times. In his memoir, "Dream from my Father," Obama called her "Granny."

Mimba na Siri ya Precious

Imeletwa na Mdau YM:

Mimba na Siri ya Precious

MIMBA
Mimba ilitungwa baada ya baba kutoa hongo kwa kimada

Ili kuthibitisha kama ni mimba kweli kimada akatoa rushwa kwa daktari ili apimwe harakaharaka kwa kuwa kulikuwa na msongamano wa wagonjwa

Kila alipoenda kliniki wakati wote wa Ujauzito alitoa 'chai' ili ahudumiwe vizuri na wauguzi na madaktari

Hata wakati wa kujifungua akatoa 'chai' kwa manesi apate huduma safi

BAADA YA KUJIFUNGUA
Baada ya kujifungua aliendelea kutoa hongo awe wa kwanza kuhudumiwa, mwanae awe wa kwanza kuchomwa sindano za Chanjo n.k.

Mwanae akaitwa 'Precious'

ELIMU KWA PRECIOUS
Kuandikishwa chekechekea akatoa hongo ili Precious apate nafasi katika shule nzuri kwa kuwa nafasi zilikuwa chache, Precious anaangalia

Kuandikishwa shule ya msingi mchezo uleule, Precious anaangalia

Tena sekondari akatoa 'Chai' kwa mwalimu wa Hisabati ili Precious apate alama nzuri

Chuo kikuu Precious hali ikawa ngumu, akagawa uroda kwa mkufunzi ili apate alama nzuri

KAZI
Precious akagawa uroda ili apate kazi, akapata

Precious akatishiwa mara kwa mara kufukuzwa kazi kutokana na utendaji mbovu kinga ikawa ni kugawa uroda

Akatumia nafasi yake kwa manufaa yake binafsi

Kwa tamaa ya vitu vya thamani kuliko mshahara wake akaendelea kupokea rushwa

NDOA
Kwa kuwa wazazi wake (baba yake) hakuwa mwaminifu katika ndoa yake (Precious ni mtoto wa kimada), naye Precious hakuona sababu ya kuwa mwaminifu ktk ndoa

Watoto wake wote walifuata mlolongo kama wa kuzaliwa kwake

KIFO

Hata alipougua ghafla , hongo ikatumika apate huduma bora lakini Mungu alimpenda zaidi

Walipoenda kuchonga jeneza, wakakuta kuna order nyingi ikabidi watoe 'Cha Juu' ili kuchukua jeneza lilokuwepo tayari

Wakati wa mazishi Kwaya iliyotakiwa kuimba wakati wa Maombolezo ilikuwa na safari , ikapewa 'cha juu' ili kuahirisha safari

MWISHO

Kwaya ikaimba na Kumsifia Precious alivyokuwa 'mtumishi mwema wa Mungu', tena wakamwomba Mungu ampokee kwa mikono miwili , amuepushe na Moto wa milele.

Risala ikasomwa, na kusifia utumishi wake uliotukuka, tena kaacha pengo lisilozibika.


TAKE HOME MESSAGE
Wazazi 'huwapakaza' watoto wao matope ya dhambi toka pale mimba inapotungwa hata baada ya kuzaliwa

Watoto wote huakisi tabia walizojifunza toka kwetu, kama wazazi (Observational Learning)

Kama hatuwezi kuwa wawazi hasa pale kaburini hata kwa mtu aliyekufa na sifa mbaya akasifiwa basi tunahalalisha matendo mabaya aliyoyafanya marehemu.

Ili Kupambana na Rushwa twahitaji kuanzia wakati wa Ujauzito, mtoto azaliwe bila rushwa, akue bila rushwa n.k

KWA LEO NI HAYO TU!!!

Aolewa na Wanaume Wawili huko Katavi!

Sijui ilitoka kwenye gazeti gani. Lakini kwa kweli nimependa ushujaa wa huyo Mama Kaela!

********************************************************
MWANAMKE AOLEWA NA WANAUME WAWILI


MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani hapa, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, zililifikia gazeti hili na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Wakiwa kijijini hapo mume wake aliendelea kufanya kazi ya ukulima wakati yeye mama (Veronica), pamoja na kilimo hujihusisha na upishi na uuzaji wa pombe ya kienyeji ya iitwayo kayoga.

Mwanamke huyo ambaye amesema ana watoto wanne, Alfred (20), binti mwenye miaka 16 (ambaye ameolewa) na wengine wawili wa kiume, mmoja akisoma darasa la sita na mdogo ana miaka saba, amesema hana shida na waume wake.

Ingawa wanandoa hao walizungumza kwa hadhari, majirani walikiri kuwa mwanamke huyo anaishi na wanaume hao wawili kwa amani na kwamba mwanamke huyo ndiye mwenye sauti na si waume zake.

“Si siri tena sasa, tumeshawazoea, kwani wanaishi kwa amani ila yule mume mdogo anaishi kwenye nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake, lakini anashinda kwa mume mkubwa, ambapo inajulikana kijijini hapa kuwa ni nyumba kubwa. “Basi pale ni mambo yote, kula na kunywa, mama huyu amewapangia zamu wanaume hao kama afanyavyo mume mwenye wake wengi. Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni,” alisema mkazi mmoja kwa masharti ya jina lake kutoandikwa gazetini. Ilielezwa, kwamba wanaume hao wana akili timamu na hawatumii kilevi cha pombe kama ilivyo kwa mke wao.

Hata hivyo, mume mkubwa anapewa sifa za upole tofauti na mume mdogo anayetajwa kuwa mkorofi kiasi cha mara kadhaa kumchapa makofi mkewe anapomuudhi.

Majirani wanadai kwamba Mama Kaela na mumewe Paulo, walipofika kijijini hapo, walipokewa na kuishi maisha ya kawaida, lakini baadaye mama huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Arcado, ambaye naye alilazimika kuachana na mkewe wa ndoa anayefahamika kijijini hapo kwa jina la Mama Pere.

Ilielezwa na mashuhuda hao kwamba mume mkubwa alipobaini uhusiano huo, alikuja juu, lakini mwanamke huyo inadaiwa alimweleza mumewe huyo, atake asitake lazima wataishi wawili, vinginevyo ataachana naye, ndipo mume mkubwa alipokubali kuishi na mume mwenza.

Katika maisha ya kawaida katika familia hiyo, inaelezwa kwamba katika baadhi ya siku ikitokea kuwa mama huyo amechoka kupika, mume mdogo huchukua jukumu la kupika na kumwandalia chakula na maji ya kuoga mume mkubwa.

“Lakini mara nyingi kwa mfano, ikiwa ni zamu ya mama huyo kulala kwa mumewe mkubwa, basi humfulia nguo zake kisha anakwenda kwa mumewe mdogo nako anamfulia nguo.

“Ndivyo wanavyoishi, nasi sasa tumewazoea ila yule mama ni mkali na ana sauti pale kwake kwa wanaume wale ila tunaona kama ana wivu sana kwa huyu mdogo ambaye naye pia ana wivu kwa mkewe huyo, labda anahofia kuwa mama huyo anaweza kuongeza mwanamume mwingine,” anasema mmoja wa majirani hao.

Hakuna mazuri yasiyokuwa na machungu, japo familia hiyo inaelezwa kuwa na amani, mtoto wao mdogo nusura avuruge uhusiano wa wanandoa hao, baada ya kuibuka mzozo wakati wa maandalizi ya ubatizo wake.

Kwa sababu anazojua mama, ingawa inafahamika kuwa wote ni watoto wa mume mkubwa, mke huyo katika hati za ubatizo aliandikisha ubini wa mtoto huyo kuwa ni Mlele (akimaanisha kuwa mtoto wa mume mdogo), lakini mume mkubwa aliweka pingamizi kanisani akidai yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo, yeye na Arcado ni waumini wa madhehebu ya Katoliki wakati Paulo ni Mpentekoste. Madai ya mzozo wa uhalali wa `ubaba’ wa mtoto huyo, yalithibitishwa na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, akiwamo mwalimu wa dini wa Kigango cha Kanisa Katoliki Uruira, Mashaka Abel. Walisema miaka sita iliyopita, mtoto huyo akiwa na umri wa mwaka mmoja, alifanyiwa taratibu za ubatizo, lakini ilishindikana, kutokana na wanaume hao, kila mmoja kudai ndiye baba mzazi wa mtoto.

“Lilikuwa jambo la kustaajabisha sana, kwani familia hiyo ilifanya maandalizi yote ya sherehe ya ubatizo wa mtoto huyo, lakini siku hiyo kanisani wakati huo ilikuwa ni kigango cha Katumba ambacho sasa ni Uruira, sakata lilianzia pale Padri alipomwuliza mama wa mtoto huyo ubini wa mtoto naye akasema ni Mlele.

“Hapo ndipo mume mkubwa alipopinga na kudai kuwa mtoto yule si wa Arcado bali wake na yeye ndiye baba halali. Padri hakuamini, aliuliza tena na tena na majibu yakawa ni yale yale, ndipo ubatizo ukashindikana,” alisema Katekista Abel.

Kazi ya kutafuta undani wa ndoa hiyo haikuwa rahisi kutokana na mazingira ya woga na usiri uliokusudiwa kubaki, ambapo awali mama alisema kwamba mume wake ni Paulo pekee japo siku ambayo mwandishi wa habari hizi alifika kijijini hapo na baadaye nyumbani kwa wanandoa hao na kumkuta mume mdogo (Arcado akimsaidia mkewe kukoroga pombe. Awali katika utambulisho, walidai kuwa ni mtu na mdogo wake na kusita kuzungumzia maisha yao ya kifamilia.

Mke wao ambaye alionekana wazi kuwa ni msemaji mkuu alifoka na kuja juu, akidai kuwa hayuko tayari kuzungumzia uhusiano wake na wanaume hao wawili, ingawa alikiri kuwa wanaishi pamoja.

"Kwa hiyo umefunga safari yote hii kutoka huko ulikotoka ili uje kwangu mie Veronica … nasema sitaki kabisa mtu kuja hapa na kutaka kunivurugia mpangilio wa maisha yangu, kwanza nani alikueleza hayo, wambea wakubwa hao yanawahusu nini watu hao?” alihoji.

“Mie mume wangu ni huyu Paulo basi … sasa leo umeniachia vurugu ndani ya nyumba nitapigwa na huyo mume wangu Paulo, kwani mmenishikisha ugoni?” alifoka Mama Kaela. Hata hivyo, mume mkubwa alidai kuwa hatamwadhibu mkewe huyo na kwamba wataendelea kuishi pamoja na mdogo wake Arcado kwa amani. Hata hivyo, akina mama wengi kijijini hapo wanalaani kitendo cha mama huyo kuishi na wanaume wawili ambapo waliomba uongozi wa Kanisa uingilie kati, ili mama huyo aweze kufunga ndoa na mume mmoja.

Lakini kwa upande mwingine, baadhi walimpongeza mwanamke huyo wakidai kuwa kitendo hicho ni cha kijasiri kwa mwanamke, kumudu kuishi na wanaume wawili na kuwa na mamlaka juu yao.

Ndugu wa Arcado wao wanalaani kitendo cha ndugu yao kuolewa na mama huyo, wakidai kuwa walishamshauri na kumuahidi kuwa endapo ataachana na mama huyo watamwozesha mwanamke mwingine, lakini yeye Arcado, amedai kuwa yuko tayari kufa, lakini si kuachana na mama huyo, kwani ndiye ubavu wake wa maisha.

“Sasa tumebaki tunamwangalia tu huyu ndugu yetu Arcado, tumemshauri, lakini mkaidi, hatusikilizi. Basi nasi hatuna la kufanya zaidi ya kumwangalia,“ alisema mmoja wa ndugu wa karibu wa Arcado. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Florence Katobasho, alikiri kuwa mwanamke huyo anaishi kinyumba na wanaume wawili na wanaishi kwa amani kwani hajawahi kufikishiwa malalamiko yoyote kuhusu wanandoa hao.

“Ni ukweli usiopingika, kwamba Mama Kaela anaishi na wanaume hao wawili … lakini kwa kuwa sijafikishiwa malalamiko yoyote kuhusu maisha ya wanandoa hao, mimi kama kiongozi hapa sina la kufanya na siwezi kuwafukuza, kwa kweli wanaishi kwa amani, mengine ni yao,” alisema Mwenyekiti wa Kijiji

SOMA   ZAIDI http://www.fotobaraza.me/profiles/blogs/mwanamke-aolewa-na-wanaume#ixzz1lVfLAlP4

Saturday, February 04, 2012

Afrika Ilivyo Ibiwa!

Hii katuni haina haja ya maelezo!

Bei ya Bidhaa Yapanda Ghafla Dar!

Kuna mdau ameleta maoni aliyoona leo kuhusu vitu kupanda bei kutokana na bei ya umeme kupanda.

******************************************************


Kwa masikitiko makubwa, ninalazimika kuandika ujumbe huu kufuatia ninayoyaona sokoni leo.

Kwa bahati mbaya, anaeathiriwa na mabadiliko yote haya ni mlaji wa mwisho ambae ni mwananchi.. Kupanda kwa gharama ya umeme, kumeongeza bei za vitu kwa takribani asilimia 25 hadi 40.

Mfano, maji ya Azam (1 lt) yalokuwa yanauzwa kwa Tzs 500 sasa ni Tzs 600. Yale ya (1/2 Lt) yanauzwa Tzs 400 na yale ya (1/4 Lt) yanauzwa Tzs 250. Bei hizi ni kuanzia leo. Maji hayo kwa bei ya jumla yamepanda kwa takriban Tzs 700 kwa kila carton.

Kwa bahati mbaya, makampuni mengine ya ya maji ya kunywa kama Kilimanjaro, Sayona na Maisha nayo yako mbioni kupandisha bei. Bei ya cement na nondo nayo imepanda na viwanda hivyo navyo vinajipanga kupandisha bei ili kufidia gharama ya umeme.


Viwanda vya bia navyo vimepandisha bei jana kwa Tzs 6000 kwa crate kwa bei ya jumla. Bia ya Serengeti haijapanda lakini nayo iko njiani kupanda. Kwa ufupi, mfumko wa bei (Inflation) itafikia 23% hadi 25% mwezi huu kama serekali haitachukua hatua za ziada kupunguza machungu hayo ya umeme.

Kwa ufupi, tunahitaji mabadiliko makubwa sana ya safu yote ya uongozi wa nchi hii, tangu serekalini hadi kwenye mashirika ya umma, ili kuleta tija na kuwa na maamuzi yasiyo ya kisiasa.

TUFANYE NINI kubadili hali yetu ya maisha kwenye mfumko wa bei unaosababishwa na kupanda kwa bei za mafuta na umeme?

Mdau EK