Showing posts with label Governor Mark Sanford. Show all posts
Showing posts with label Governor Mark Sanford. Show all posts

Saturday, April 17, 2010

Gavana Deval Patrick Akutana na Waafrika wa Massachusetts

Leo, Gavana wa Massachusetts, Bwana Deval Patrick, aliongea na waafrika waishio Massachusetts. Mkutano huo uliitwa African Town Hall. Ilifanyika Tobin Comunity Center mjini Boston.

Waafrika walitokea kutoka nchi nyingi za Afrika, hasa waafrika kutoka Magharibi walikuwa wengi. Wakutoka Afrika Mashariki tulikuwa wengi pia, hasa waGanda. Lakini kama nilivyotabiri, hao wa Magharibi walijaribu sana kuiteka mkutano. Ila nashangaa watu wengine hawaelewi kuwa kuna tofauti kubwa sana kati ya serikali ya Mkoa (State Government), na serikali kuu ya nchi (Federal Government) ambayo inaongozwa na Rais Obama. Wengine hawakuewelewa kuwa mambo mengine yanahusu serikali ya mji wanaokaa na si mkoa.

Masuala makuu yaliongolewa, ni elimu kwa wahamiaji, bima ya afya, na umuhimu wa census hasa. Kuna waafrika walisema kuna wana majina ya kiislamu na walihofia kuwa wakijaza fomu watanyanyaswa. Wengine walisema kuwa hawana makatarasi na walihofia kukamatwa wakirudisha fomu. Wasaidizi wa Gavana pia walijaribu kuelimisha watu kuhusu umuhimu wa fomu hizo na kuwa haziendi uhamiaji. Kwenye bima ya afya alisema kuwa baada ya mwezi Agosti itakuwa rahisi zaidi kuipata. Pia alisema kuwa wanajitahidi kuruhusu wanafunzi wasio na makaratasi wanaokaa Massachusetts waweze kulipa ada ya 'In State' kama wakisoma katika State Colleges.


Gavana Patrick aliwaomba waafrika wampigie kura katika uchaguzi ujao na waombe ndugu na marafiki wampigie pia.

****************************************************************************


Wasichana wa KiGanda wakicheza ngoma ya asili kumwingiza Gavana kwenye Ukumbi. Gavana yuko nyyuma yao anasalimiana na watu.
Gavana Patrick akielezea hatua alizochukua kama Gavana ilikusaidia wahamiaji wanaokaa Massachusetts.

Gavana Patrick aliwahimiza waafrika wajaze fomu za Census. Aliwaambia watu wasijali kama wana makaratasi au hawana, maana si fomu ya uhamiaji bali fomu ya kujua kuna watu wangapi katika eneo fulani serikali iweze kuwapa huduma ya kutosha, kama shule, hospitali,polisi.

Hao waGanda walipiga ngoma wakati Gavana anaiingia ukumbini. Gavana alifurahi sana.

Huyo MKameroon, alichekesha watu pamoja na Gavana alipoomba waafrika wasinyangywe chakula chao cha asili wakitua katika uwanja wa ndege (Logan Airport) Boston. Gavana alimjibu kuwa ana imani kuwa chakula hicho ni kizuri, lakini hizo ni sheria za serikali kuu ya nchi (Federal) na yeye mwenyewe hawezi kuvunja sheria.

Viongozi wa kidini wa waafrika Massachusetts wakipiga picha na Gavana baada ya shughuli. Huyo mama Mngieria aliyeshika simu alikuwa alijaribu kuleta fujo wakati wa maswali na majibu. Dume MNigeria mwenzake kamkalisha chini!

Shughuli iliisha kwa fujo! Ilibidi walinzi wa Gavana wamzunguke na kumtoa kwenye mlango wa pembeni. Kisa, kila mtu alitaka kupiga picha naye. Jamani, Gavana alisukumwa!!!!! Ila lazima niseme sisi waTanzania ni wastaarabu sana. Sikumwona MTanzania akifanya fujo mle wala kushiri katika kundi la waliomsukuma na kumsakama ili apige picha naye. Shughuli ilianza vizuri, lakini iliisha vibaya!

Thursday, June 25, 2009

Gavana wa South Carolina Atoroka na Kimada

Governor Mark Sanford (South Carolina)

Bila shaka mmesikia habari za Gavana wa South Carolina kupotea kwa siku kadhaa. Alivyotokea alisema kuwa eti alienda kutembea (hiking) kwenye milima ya Appalachian. Kumbe kuna mtu alimwona kwenye uwanja wa ndege akitokea Argentina na kampiga picha!

Hapo sasa ilibidi gavana aseme ukweli. Alienda Argentina kumfuata kimada wake. Kimada mwenyewe ni mwanamke kutoka huko Argentina. Anasema kuwa alimjua huyo mwanamke kwa miaka minane, lakini alianza uhusiano wa kimapenzi naye mwaka jana. Alisema alienda Argentina mara tatu kumwona. Gavana Sanford ana mke na watoto wanne wa kiume, lazima wameaibika.

Habari zinasema kuwa mke wake aligundua habari ya mume wake kutembea nje ya ndoa na kamfukuza ndani ya nyumba yao kama wiki mbili zilizopita! Na pia eti hizo safari za Argentina zimelipiwa na walipa kodi wa South Carolina! Hmmm, naona itabidi jamaa ajiuzulu.

Hapa Marekani ingawa watu wengi wanatembea nje ya ndoa zao ni mwiko na jambo la aibu. Inaweza kumwangusha mtu mkubwa mwenye cheo. Siyo kama nchi zingine amabako dume akitembea nje ya ndoa eti ni jambo lakujivunia na inaonyesha eti ni mwanaume!

Cha kuchekesha zaidi jamaa ni Republican. Hao Republican wanajidai watakatifu, wapenda familia wasio na makosa...kazi kusema wenzao! Kumbe wao ndo mabingwa wa kutembea nje, na uhuni mwingine!

Kwa habari zaidi someni:

http://www.cnn.com/2009/POLITICS/06/25/sanford.fallout/index.html

http://www.washingtonpost.com/wp-dyn/content/article/2009/06/24/AR2009062402504.html

http://www.mercurynews.com/politics/ci_12678735


******************************************************************

Kusoma habari ya e-mails za mapenzi kati ya Gavana na kimada soma hapa:

http://www.thestate.com/sanford/story/839350.html

http://www.cnn.com/2009/POLITICS/06/24/south.carolina.governor.emails/index.html

"I could digress and say that you have the ability to give magnificent gentle kisses, or that I love your tan lines or that I love the curve of your hips, the erotic beauty of you holding yourself (or two magnificent parts of yourself) in the faded glow of the night's light -- but hey, that would be going into sexual details ..."
"...while all the things above are all too true -- at the same time we are in a ... hopelessly impossible situation of love...." he added.


DUH!!!!!