Showing posts with label Mzee Thomas Kizigha. Show all posts
Showing posts with label Mzee Thomas Kizigha. Show all posts

Wednesday, July 23, 2008

Msiba wa Mzee Kizigha

Mwandishi Mwandamizi wa Tanzania Standard Newspapers Ltd (TSN) wachapishaji wa gazeti la Daily News na HabariLeo, Charles Kizigha, akiwa amebeba msalaba baada ya Ibada maalum ya kumuombea Marehemu Baba yake mzazi, Mzee Thomas Marijani Kizigha ambaye anatarajiwa kuzikwa wiki hii nyumbani kwao Usangi mkoani Kilimanjaro. Imepangwa asafirishwe kesho kwa ndege. Kwa picha zaisi tembelea Michuzi Blog.

*************************************************************

Nimeona hii habari ya mziba wa Mzee Kizigha kwenye Michuzi blog. Nilifanya kazi na mwanae Charles Kizigha, miaka mingi Daily News. Kwa kweli lazima nimpe pole Kaka Charles maana ni majuzi tu alifiwa na mama yake mzazi. Msiba ni msiba lakini kufiwa na wazazi wote wawili katika kipindi kifupi duuh. Poleni familia.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema mbinguni. AMEN.