Showing posts with label United States of Africa. Show all posts
Showing posts with label United States of Africa. Show all posts

Sunday, April 27, 2008

Kwame Nkrumah wa Ghana

Kwame Nkrumah na mke wake na machifu huko Ghana siku ya Januari 20, 1963


Ule ukumbi mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, unitwa Nkrumah Hall. Ilipewa jina hiyo kwa heshima ya rais wa Kwanza wa Ghana, Kwame Nkrumah.

Ghana ilikuwa nchi ya kwanza ya weusi kupata Uhuru barani Afrika. Ilipata Uhuru mwaka 1957 kutoka Uingereza. Mwaka 1960, Nkrumah alitangaza kuwa Ghana ni Jamhuri. Mwaka 1964, alisema yeye ni rais wa maisha ya nchi hiyo. Alikataza vyama vyote vya siasa isipokuwa chama chake.

Mwaka 1966 alipokuwa safarini China, alipinduliwa. Alikufa akiwa exile nchini Romania mwaka 1972.

Nkrumah alikuwa na ndoto ya bara Afrika kuwa, UNITED STATES OF AFRICA. Wadau mnadhani kuwa bara Afrika inaweza kuwa nchi moja kama majimbo ya Marekani? Tulivyo na lugha na utamaduni tofauti na ukabila sidhani kama itawezekana kwa sasa. Labda baada ya miaka 200!

Kwa habari zaidi za Kwame Nkrumah someni:

http://www.thenagain.info/WebChron/Africa/Ghana.html

http://news.bbc.co.uk/onthisday/hi/dates/stories/march/6/newsid_2515000/2515459.stm

http://www.africanews.com/site/list_messages/16337