Showing posts with label Well. Show all posts
Showing posts with label Well. Show all posts

Saturday, October 01, 2022

Mnaifahamu Tanzania Life Project ?




Tanzania Life Project ni NGO inayaosaidia wananchi wanaoishi kwenye vijiji vilivyo n ukosefu wa maji kupata maji.   Wanachimba visima ili kusaidia kupata maji na kuepuka kutembea misafa mirefu kutafuta maji

Nilipotoka Tanzania nilikutana na baadhi ya watu waliojitolea (Volunteers) walioenda  Dodoma, Tanzania kusaidia wanavijiji.

Kwa kweli niliguswa sana na moyo wao wa kusaidia watu kupata maji.  Ninakumbuka enzi zile...Tabora maji yalikuwa ya shida sana. Ukiyapata yana rangi ya maziwa. 

Zaidi ya kuchimba visima, wanatoa ruzuku kwa wafanyabiashara wadogo wadogo, na wantaoa elimu kwa wanawake na wanaume kwa ajili ya kuimarisha maisha yao.


tKwa habari zaidi BOFYA HAPA: 

Friday, July 28, 2017

Tigo Imechangia Kisima kwa wakaazi wa Mji Mpya mkoani Morogoro



Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo (katikati) akikata utepe kuzindua kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Meneja wa huduma za jamii Tigo, Halima Okash, Ofisa Mkuu wa Ufundi na Taarifa wa Tigo (CTIO) Jérôme Albou,  na  Diwani wa mji mpya Wence Kalogelezi

Mkazi wa Mji mpya akiwa kabeba ndoo ya maji mara baada ya uzinduzi wa kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.




Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo (katikati) akihutubia wakazi wa Mji mpya mara baada ya  kuzindua kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.



Mkuu wa wilaya ya Morogoro mjini, Regina Chonjo akiwa katika picha ya pamoja  na Wakazi wa Mji Mpya Mkoani Morogoro mara baada ya uzinduzi w kisima hicho.

 kisima kilichotolewa msaada na kampuni ya Tigo chenye thamani ya shilingi milioni 17/- kwa hospitali ya Mji mpya jana mjini Morogoro.


·        Uchangiaji huu ni ishara ya shukurani kwa wakaazi hao kwa kuzima moto katika kituo cha data cha Tigo.

Tarehe 27 Julai 2017 – Tigo Tanzania imechangia kisima chenye thamani ya TZS milioni 17 kwa hosipitali ya Mji Mpya na maeneo yanayoizunguka katika mkoa wa Morogoro kama mkono wa shukurani kwa wakaazi kwa kuhatarisha maisha yao wakati wakipambana na moto ambao ulilipuka katika kituo cha data cha kampuni katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa Tigo, uchimbaji wa kisima hicho pia ulikuwa sambamba na nia ya kampuni hiyo kusaidia ustawi wa jamii ambako Tigo inaendesha  shughuli zake.
Akizungumza katika sherehe za makabidhiano zilizofanyika katika hospitali ya mji mpya katika manispaa ya mji wa Morogoro Afisa Ufundi na Taarifa wa Tigo (CTIO) Jerome Albou alielezea matarajio yake kwamba kisima hicho kitawafikisha mbali sana katika kuondoa suala la upungufu wa maji katika hospitali na pia kutoa maji safi na salama ya uhakika kwa jamii inayokizunguka.
“Tunawashukuru sana watu wa Mji Mpya kwa kuonesha kujali na kujitoa wakati wa kupambana na moto ambao karibu uteketeze kabisa kituo cha Data mapema mwaka huu. Kweli Tigo ina deni kwa wanajamii, serikali ya mtaa na viongozi wa ulinzi na usalama wa manispaa kwa kuitika  kwa wakati kuhakikisha kuwa hakuna uharibifu mkubwa unasababishwa wakati wa moto,” alisema Albou.   
“Kwa hiyo msaada huu, unakuja kutimiza ahadi walioiweka Tigo kwa wakazi wa Mji mwema wa kuwapatia maji safi na salama kama namna ya kutambua juhudi zao katika kulinda mali za kituo hicho cha data.”
Albou alibainisha kwamba uchangiaji huo unakamilisha idadi ya vijiji 20 ambavyo vimenufaika kutokana na jitihada za Tigo za kutoa maji safi na salama nchi nzima, ikiwa inawasaidia zaidi ya watu 187,000.
Mwaka huu, Tigo ina mpango wa kuchimba visima zaidi katika maeneo yanayohitaji ambayo zaidi ya watu 350,000 wanatarajiwa kunufaika katika jitihada zetu za kusaidia juhudi za serikali za kuondoa upungufu wa maji safi na salama nchini.
Makabidhiano yalishuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr Kebwe Stephen Kebwa ambaye aliishukuru Tigo kwa kufikiria kutoa msaada huo. Alisema kwamba kisima hicho kitasaidia utoaji wa huduma bora za kiafya katika hospitali ya Mji Mwema na kusaidia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Aliwaomba wasamaria wema wengine kujitokeza na kuunga mkono juhudi za kuondoa upungufu wa maji katika mkoa huo.
Tunapenda kuishukuru Tigo kwa kutusaidia katika juhudi zetu za kutoa huduma za kiafya za uhakika katika eneo hili kwa kutatua tatizo lililokuwepo la upungufu wa maji. Tunaamini kwamba upatikanaji wa maji safi na salama karibu na wakaazi pia itaongeza uzalishaji wa kiuchumi hasa kwa wasichana na wanawake ambao hawatakuwa wanapoteza muda mwingi wa kutafuta maji safi na salama sehemu zingine. Hii itawapatia wasichana fursa ya kuhudhuria masomo kwa uhuru na kuipa jamii fursa ya kuhudhuria kwa ufanisi katika shughuli zao za maendeleo ya Taifa,  Alisema Dr Kebwe. 

Saturday, August 25, 2012

An Important Lesson!



One day a farmer's donkey fell down into a well. The animal cried piteously for hours as the farmer tried to figure out what to do. Finally, he decided the animal was old, and the well needed to be covered up anyway; it just wasn't worth it to retrieve the donkey.

He invited all his neighbors to come over and help him. They all grabbed a shovel and began to shovel dirt into the well. At first, th
e donkey realized what was happening and cried horribly. Then, to everyone's amazement he quieted down.

A few shovel loads later, the farmer finally looked down the well. He was astonished at what he saw. With each shovel of dirt that hit his back, the donkey was doing something amazing. He would shake it off and take a step up.

As the farmer's neighbors continued to shovel dirt on top of the animal, he would shake it off and take a step up. Pretty soon, everyone was amazed as the donkey stepped up over the edge of the well and happily trotted off!

MORAL :
Life is going to shovel dirt on you, all kinds of dirt. The trick to getting out of the well is to shake it off and take a step up. Each of our troubles is a steppingstone. We can get out of the deepest wells just by not stopping, never giving up! Shake it off and take a step up.

Remember the five simple rules to be happy:

1. Free your heart from hatred - Forgive.

2. Free your mind from worries - Most never happens.

3. Live simply and appreciate what you have.

4. Give more.

5. Expect less from people but more from God.

You have two choices... smile and close this page, or pass this along to someone else to share the lesson .

God bless us all!

Wednesday, September 23, 2009

Mwanamke Afariki Dar Akiwa Anasaka Maji!


Nilipokuwa Tabora Girls (81-83), maji yalikuwa ya shida na mara nyingi tulienda kisimani kuchota maji na kufua nguo zetu. Kuchota maji kwenye kisima kama hiyo pichani ina ufundi wake! Nilipokuwa jeshini Masange JKT nilianguka ndani ya kisima. Nilikuwa peke yangu siku hiyo na sikuwa na jinsi ya kutoka. Kila nikijaribu kutoka naanguka tena mpaka nilichoka. Bahati yangu kulikuwa na afande karibu ambaye alikuwa anafua nguo zake, alinisaidia kutoka. La sivyo sijui ningetokaje maana matope yalikuwa yanateleza kweli maana yalikuwa 'clay soil'.

Hivyo, nimesikitika sana kusikia habari ya huyo mama aliyekufa akiwa anatafuta maji. Huenda alipata matatizo ya moyo. Kujitusha ndoo nzito kichwani ni kazi kweli ukiwa na umri mkubwa.

Lakini naomba niwaulize. Miaka karibu 50 ya Uhuru na bado wananchi wengi hawana maji safi ya bomba, inabidi wachote maji kwenye visima na kukinga maji ya mvua! Wengine wanaletewa maji na boza. Wengine inabidi wanunue maji kwa wanaopita na mikokoteni. Kweli ni maendeleo?


******************************************************
Kutoka ippmedia.com

Mwili wa bibi mwenye umri wa miaka 60, umekutwa ukiwa jirani na kisima cha maji katika maeneo ya Pugu Stesheni Jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile amesema mwili huo ulikutwa jana mishale ya saa 12:00 jioni katika maeneo ya Pugu Stesheni, jirani na makazi ya bibi huyo.

Amemtaja marehemu kuwa ni Selina Joseph, 60, mkazi wa Pugu Stesheni.

Akisimulia tukio hilo, Kamanda Shilogile amesema pembeni ya mwili huo kulikuwa na ndoo ya maji.

Amesema chanzo cha kifo hicho bado hakijafahamika na kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Amana.

Hata hivyo taarifa kutoka kwa baadhi ya wananchi wa maeneo hayo zinadai kuwa bibi huyo alikutwa na mauti akiwa katika harakati za kusaka maji ambayo yamekuwa kero kubwa katika eneo hilo.

Kufuatia tukio hilo, wananchi hasa akinamama wameiomba Serikali kuangalia namna ya kuwasaidia.

CHANZO: ALASIRI