Showing posts with label Bi Kidude. Show all posts
Showing posts with label Bi Kidude. Show all posts

Wednesday, April 17, 2013

Rest in Eternal Peace Bi Kidude - Kungwi Mkuu/ Malkia wa Taarab



REST IN ETERNAL PEACE BI KIDUDE!

QUEEN OF TAARAB! KUNGWI MKUU WA TANZANIA!


The Late Fatuma binto Baraka aka. Bi Kidude (1910(?) - 2013)



Read more about Bi Kidude HERE

Friday, September 07, 2012

Bi Kidude Hajafariki, Amelazwa Hospitalini Zanzibar

Bi Kidude


Habari za kizushi zilizosambaa kwa kasi ya ajabu kuhusu hali ya bi kidude kwamba amefariki dunia ni za uongo. Ndugu na jamaa wa Bi Kidude  wamekanusha uzushi huo na  wameweza kutoa ufafanuzi kwamba bi kidude amelazwa kwenye hospitali ya Hindu Mandal visiwani Zanzibar na bado anaendelea na matibabu yake.

Bila shaka Bi Kidude ataishi maisha marefu.

Wednesday, July 09, 2008

Siti Binti Saad 1880-1950 - Kumbukumbu


Bibi Siti Binti Saad ni mmoja wa waanzilishi wa Taarab nchini. Alitokea Zanzibar, na aliweza kuimba katika lugha za kiarabu, kihindi na Kiswahili. Alikuwa mwimbaji wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kutengeza santuri za nyimbo zake. Studio ilijengwa Zanzibar kwa ajili yake.

Alitengeneza santuri 150 (78 rpm). Si rahisi kupata nyimbo zake siku hizi.
Siti alikuwa mtoto wa watumwa. Alizaliwa huko Fumba, Zanzibar 1880 na alikuwa na maisha magumu hapo mwanzoni kabla ya kuwa mwimbaji maarufu. Alifariki dunia siku ya Julai 8, 1950 na kuzikwa kesho yake huko Zanzibar. Bi Kidude ni mwanafunzi wake.

Karibuni mtembelee website niliyotengeneza siku nyingi kuhusu historia na maisha ya Bibi Siti Binti Saad.

Wednesday, June 25, 2008

Bi Kidude naye ni Supa Modo!




Mwimbaji taarabu mkongwe na Kungwi mkuu wa Tanzania, Bi Kidude ameingia kwenye fani mpya! Umodo! Ameonyesha waTanzania kuwa umodo si kwa vijana tu, hata wazee wamo!
Bi Kidude alionyesha vitu vyake hivi karibuni kwenye fesheni show ya Mustafa Hassanali. Kuona picha zaidi za hiyo show tembelea blogu ya Father Kidevu!
Hongera Bi Kidude! YOU GO GIRL!

Saturday, November 24, 2007

Bi Kidude ana miaka mingapi?

Hivi Bi Kidude ana miaka mingapi? Sasa anadai kuwa ana mika 113. Lakini anasema hajui alizaliwa lini. Mimi nilimwona Zanzibar mwaka 1993 na wakati huo alisema ana miaka 80. Kwa hiyo nahisi kama ana miaka 94.

Aliolewa kwa mara ya kwanza katika miaka ya 1930's. Alikuwa mwanafunzi wa marehemu Siti Binti Saad ambaye alifariki 1950.

Ni Kungwi na mwenyewe kwa mafundisho ya Unyago. Huenda ni kweli wazungu wanavyosema, "sex makes you younger" (yaani ngono inakufanya uwe kijana).

Je, umemwona kwenye show zake. Ngoma zikianza kulia anageuka kijana!

GO BI KIDUDE!