Showing posts with label Britney Spears. Show all posts
Showing posts with label Britney Spears. Show all posts

Friday, December 21, 2007

Jamie Lynn Spears ana mimba! Ana miaka 16!


Bila shaka mmesikia habari za huyo binti Jamie Lynn Spears, ambaye ni mdogo wake Britney Spears. Ana mimba na ana miaka 16 tu. Baba wa mtoto Casey Aldridge, ana miaka 19. Anatoka Mississipi. Sehemu zingine hapa USA hiyo ni kosa la jinai kumtia mtoto mimba, na angeitwa sex offender.

Jamie Lyyn sasa anaitwa, kila jina chafu ya kiingereza ambayo unaweza kufahamu ya neno malaya. Kaitwa tramp, whore, ho, slut, skank. Wanasema ni nyege mwasho kama dada yake Britney.

Familia yake wametukanwa kuwa ni wazungu wasio na thamani. Wameitwa Cracker, white trash, trailer trash, bayou swamp trash, washamba, inbred (kuzaana wenyewe kwa wenyewe katika ukoo) doh! Wanasema "The apple doesn't fall far from the tree" ( Yaani tuna la apple haianguki mbali na mti wake). Yaani sikujua kuwa wazungu wanaweza kutukanana hivyo!

Wamekasirika kwa sababu Jamie Lynn Spears ni mdogo wake Britney Spears. Jamie Lynn ana TV show kwenye Nickolodeon inaitwa Zoey 101. Wasichana wanaipenda kweli na wazazi wengi walimwona kama mtu wa kumwiga. KUMBE!

Halafu alikuwa anajifanya ni Mkristo mwema. Mtakatifu hawezi kuvunja amri za Mungu. Yaani awe bikira mpaka siku ya kuolewa. Sasa hiyo mimba inaonyesha watu alikuwa anafanya nini. Inatoboa siri, hakuna cha ubikira hapo.

Na jambo la kuongeza chumvi hapa. Mwezi wa saba gazeti la National Enquirer walitoa stori kuwa huyo binti ana mimba. Nickolodeon walitafuta mawakili na kuandika barua kali kuwa watawa-sue kwa ajili ya kuchafua jina la binti mwema, Mkristo safi kama Jamie Lynn. Sasa inaelekea huenda hiyo habari ya mimba ilikuwa ya kweli na aliitoa.
Sasa watu wanasema kuwa Nickolodeon ni wanafiki maana angekuwa ni msichana mweusi show yake ingesimamishwa mara moja. Lakini wameruhusu iendelee kuonyeshwa.

Mama yao alikuwa anaandika kitabu kuhusu malezi bora. Publishers wa hicho kitabu wamesimamisha mkataba waliokuwa naye maana inaelekea hawezi kumlea mtu.

Karibuni mtoe maoni hapo.

Kwa habari zaidi someni:



Thursday, October 04, 2007

Britney Spears Anyang'anwa Watoto Wake na Serikali



Mwimbaji Britney Spears amenyang’anywa watoto wake na Serikali. Kisa wanaona kuwa hafai kulea watoto. Kwanza anashindwa muda gani na hao watoto, maana anakuwa amelewa. Mara alipigwa picha hajavaa chupi na dunia yote iliona hao watoto walitoka wapi. Nadhani alichoka na hao watoto maana jana ilikuwa awe mahakamani kujitetea na hakutokea. Badala yake paparazzi walimwona anatembea na gari yake barabarani.

WaTanzania walioko hapa USA wengi wanajua sheria za hapa. Hakuna kumchapa mtoto. Hapa Boston mtoto wa MBongo aliulizwa kama anapigwa na wazazi wake. Alijibu ndiyo. Mbona karibu serikali wamchukue huyo mtoto. Mwisho walikimbia mji.

Sasa huyo Britney na mapesa yake yote anaweza kulipa maaya wa kuwalea lakini bado walioona kuwa hafai kulea. Watu wa karibu naye walidai kuwa anatumia madawa ya kulevya mbele ya watoto, anatembea uchi mbele ya watoto na mengine. Pia walidai anawalisha ‘junk food’ kama soda na chips.

Sasa hivi watoto wanalelewa na baba yao, mcheza densi, Kevin Federline, ambaye ana watoto wengine wawili zaidi aliyezaa na mwanamke mweusi na mcheza sinema, Shar Jackson.

Watu wanadai kuwa huenda Kevin, alimshitaki Britney kwa sababu mwisho wa mwezi huu ndo mwisho wake kupokea posho ya dola $20,000 kutoka kwa Britney. Wanasheria wanasema kuwa Kevin ataweza kuendelea kupokea hizo $20,000 na zingine kila mwezi kama akiweza kutunza watoto vizuri.

Maisha ya Britney ni ya ajabu. Miaka Mingi alidai ni bikira na alikuwa mfano wa kuigwa. Mara kasema alishavunjwa huo ubikira siku nyingi. Mara Aliolewa kwa muda wa siku tatu tu na kijana aliyesoma naye shule ya msingi. Baada ya hiyo ndo kunvunjwa ndo tulisikia kuwa amemwibia Shar Jackson, baba watoto wake. Britney ana vituko.