Showing posts with label Film Camera. Show all posts
Showing posts with label Film Camera. Show all posts

Saturday, December 17, 2016

Mfuko wa PPF Wadhamiria Kuwafikia WaTanzania Wote Wakiwemo Wasnatasnia wa Filamu

Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Meshack Bandawe, akizungumza kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wadau wa filamu na michezo ya kuigiza mkoani Mara. 

Mafunzo hayo yalanza Disemba 14 na yanafikia tamati leo Disemba 16, 2016 katika ukumbi wa shule ya Sekondari Mara Mjini Musoma. Yameandaliwa na Bodi ya Filamu nchini ili kuwajengea uwezo wadau wa filamu ili kuzalisha kazi zenye ubora.
#BMGHabari
Wadau wa filamu mkoani Mara wakimsikiliza Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe, wakati akiwaeleza umuhimu wa kujiunga na mfuko huo
Afisa Masoko PPF, Evance Baguma, akiwasilisha mada kwa wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara
Wadau wa filamu mkoani Mara wakifuatilia mada kutoka kwa Afisa Masoko PPF, Evance Baguma
Wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara wamefurahishwa na mada kuhusu mifuko ya hifadhi ya jamii kutoka PPF na kuonesha mwitiko mkubwa wa kujiunga na mfuko wa Pensheni wa PPF.

Mfuko wa Pesheni wa PPF umesema umedhamiria kuhakikisha kwamba wananchi wengi walio kwenye sekta zisizo rasmi ikiwemo wajasiriamali wananufaika na mafao ya hifadhi za jamii kupitia huduma ya Wote Scheme.

Meneja wa mfuko huo Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe, ameyasema hayo Musoma mkoani Mara, wakati akieleza umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko huo mbele ya wadau wa filamu mkoani humo.

Amesema wananchi wasio kwenye sekta rasmi wakiwemo wajasiriamali wanayo fursa ya kujiunga na mfuko wa PPF na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu, mikopo ya elimu, maendeleo pamoja na mafao ya uzeeni kwa kila mwanachama kuchangia shilingi elfu 20 kwa mwezi ambazo mwanachama hulipa kadri awezavyo.

Naye Afisa Masoko PPF, Evance Baguma, amesema lengo la mfuko huo kuanzisha huduma ya Wote Scheme kwa wajasiriamali ni kuondoa dhama potofu kwa baadhi ya wananchi kwamba anayeweza kunufaika na huduma za mifuko ya hifadhi za jamii ni lazima awe mtumishi wa taasisi binafsi ama serikali.

Wadau wengi wa filamu mkoani Mara wamefurahishwa na ufafanuzi wa mfuko huo ambapo wamebainisha kwamba awali walikosa fursa mbalimbali za mifuko ya hifadhi za jamii ikiwemo PPF kutokana ufahamu duni waliokuwa nao.
Tazama picha zaidi HAPA

Wednesday, June 13, 2012

Taarifia Kuhusu Sinema 'American Dream'

We are currently casting for a Bongowood film, American Dream.  It is the story of a young Tanzanian man who comes to America in search of his fortune only to find life is not what he expected. Though filmed in USA, the film is geared for a Tanzanian audience.
If interested or you fit the role, please send a photo, age range and resume (Yaani CV kuhusu experience yako ya acting tu) to ndotousafilm@gmail.com. Most of the roles have Swahili dialogue, therefore knowledge of Swahili is a plus. 

Please note the film is tentatively scheduled to film in the New York and Boston area in August-September of this year.  Also, this is a no budget/low budget film. Food and gas money will be provided.

We look forward to hearing from you.  

American Dream (Ndoto ya Marekani)
Preliminary Cast Breakdown
[AMANI] LEAD/STAR male, African American, 25-35 years old, An eager Tanzanian man. Arrives in the USA as a student but is really interested in getting a better life for himself and provide for his family back home.
[RICHARD] LEAD male, African American, 25-35 years old Amani’s brother, has been in the USA for a while. Tries to help Amani.
[WALLET] LEAD male, African American, 35 - 50 years old, respected and established Tanzanian in the USA. He has papers, connections, money, the person everyone goes to him for help and advice.
[PATRICK] SUPPORTING male, African American, 25-35 lives with Wallet, he is studying at the University, works part time.
[KATE] SUPPORTING female, Caucasian, 25-35 years old, Richard’s girlfriend who get tired or his African ways
[UNIVERSITY ADMINISTRATOR] SUPPORTING male , Caucasian , 40+ years, stern University employee who plays by the rules.
[MAYA] LEAD Female, African American , 35-50 years old, Single parent, she has been in the USA a while. She can as a student, had a child, is established in the community. She is lonely, looking for love.
[PILI] SUPPORTING female, African American , 35-50 years old, is Maya’s gossiping friend and co-worker
[BOSS] SUPPORTING male, African American, 35-50 years old , an African who runs the Barbershop. He is a no nonsense guy.
[LULU] SUPPORTING female, African America 14-18 years or can play, this is Maya’s daughter. She loves her mother at the same time does not want to see her taken advantage of. Very suspicious of those who come around her mother, rejects African culture.
[ZERA] LEAD female, African American, 25-35 years old, outgoing adventurous young woman. She has been in the USA a while. Was physically abused by Grant who deep down she still loves.
[Grant ] SUPPORTING male, African American , 30- 40 years old, an African who wants to dominate his woman. Has a soft side and an evil side. He is openly jealous and possessive.
[IMMIGRATION ATTORNEY], male, Caucasian, 40+ years old> handles immigration cases and gives advice to the African community.

Sunday, March 21, 2010

Sinema - On the Mean Streets

Jumamosi niliigiza katika sinema fupi iitwayo 'On the Mean Streets'. Sinema hii imetungwa na mwanafunzi Brian Goodwin ambaye ni mwanafunzi Emerson College hapa Boston. Mimi niliigiza kama mwalimu wa Kiingereza wa Sekondari. Nakutana na kijana wa kizungu ambaye anadhani maisha ya Roxbury wa Boston ni ya ghetto na weusi wote huko ni maskini. Naishia kuchukia jinsi kijana wa kizungu alivyokuwa na mawazo finyu kuhusu Roxbury. Sinema inempigwa kama 16MM Format.

Kati ya Shots. Mimi kama Mwalimu Cheryl. Brian Goodwin aliigiza kama Pinkerton, mzungu mwenye mawazo finyu juu ya Roxbury.
Mshika Boom (Sauti), rafiki yangu na msanii mwanzangu katika kikundi cha Oscar Micheaux family Theater Charles 'Matumbi' Jackson, mimi na Brian. Charles aliigiza kama mlevi.

Tumemaliza shoot! Hapo ni mtaa wa Parker St. karibu na Roxbury Crossing. Huyo binti aliyeshika Camera alipata taabu sana maana ilikuwa nzito kweli. Walikuwa na tgripod, lakini kwenye script waliandika scene ipigwe kwa Handheld (Kamera Mkononi). Lakini binti alikuwa 'rpo' alisema ataipiga handheld!

Friday, June 12, 2009

Serikali Yaondoa Ushuru wa Kamera

ASANTE SANA RAIS WETU MPENDWA JAKAYA KIKWETE!

*************************************************
Kutoka ippmedia.com
Serikali yaondoa ushuru wa Kamera

Na Mwandishi wetu

12th June 2009

Serikali imeondoa ushuru wa forodha kwenye kamera maalum za kupiga picha za filamu ili kuhamasisha sekta ya filamu kwa nia ya kuongeza ajira na kipato kwa vijana hapa nchini.

Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Fedha na Uchumi Mustapha Mkullo wakati akisoma bungeni mjini Dodoma bajeti ya mwaka 2008 na 2009. Kwa mujibu wa Mkullo, kamera hizo zilizofutiwa ushuru ni zile maalum za kupiga picha za filamu zinazotambuliwa chini ya HS Codes 8525.80.00.

Hatua hiyo ya Serikali ya kuondoa ushuru imekuja baada ya hivi karibuni Rais Jakaya Mrisho Kikwete kukutana na watengenezaji na wacheza filamu wa Hollywood wakati alipotembelea Marekani kwa ziara ya kikazi.

Sekta ya filamu hapa nchini imekuwa ikipanda chati kwa haraka sana, ambapo vijana wengi wamekuwa wakijihusisha na shughuli za uchezaji na utengenezaji wa filamu mbalimbali.

Hatua hiyo ya Serikali itasaidia wawekezaji kuja nchini kuwekeza katika sekta hiyo kama sekta nyingine na kuinua fani hiyo ambayo ilikuwa chini sana.