Showing posts with label Actors. Show all posts
Showing posts with label Actors. Show all posts

Saturday, October 19, 2019

Please Help Lay Boston Actor Charles L Jackson to Rest!

UPDATE - Charles L. Jackson was laid to rest in his family plot in Springfield, MA on Friday November 1, 2019.   may he rest in eternal peace. Amen.



Please help lay Charles Lee Jackson to rest. He died on October 7, 2019 in his apartment in Dorchester, Massachusetts. His body wasn't found until Wednesday, October 9, 2019 and his notified on October, 10, 2019. His family is struggling to put the money together to give him a proper burial. A GOFUNDME has been set up. Please help if you can. Charles did a lot of background acting work, he also did numerous play in Roxbury, and Boston. He was a father and grandfather. Rest in peace Charles (1955-2019)

https://www.gofundme.com/f/his-final-scenelaying-to-rest-charles-l-jackson

GO FUND ME FOR CHARLES L. JACKSON
The Late Charles Lee A Jackson at Revere Beach in 2011.  

Saturday, December 17, 2016

Mfuko wa PPF Wadhamiria Kuwafikia WaTanzania Wote Wakiwemo Wasnatasnia wa Filamu

Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Meshack Bandawe, akizungumza kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wadau wa filamu na michezo ya kuigiza mkoani Mara. 

Mafunzo hayo yalanza Disemba 14 na yanafikia tamati leo Disemba 16, 2016 katika ukumbi wa shule ya Sekondari Mara Mjini Musoma. Yameandaliwa na Bodi ya Filamu nchini ili kuwajengea uwezo wadau wa filamu ili kuzalisha kazi zenye ubora.
#BMGHabari
Wadau wa filamu mkoani Mara wakimsikiliza Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe, wakati akiwaeleza umuhimu wa kujiunga na mfuko huo
Afisa Masoko PPF, Evance Baguma, akiwasilisha mada kwa wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara
Wadau wa filamu mkoani Mara wakifuatilia mada kutoka kwa Afisa Masoko PPF, Evance Baguma
Wadau wa filamu na maigizo mkoani Mara wamefurahishwa na mada kuhusu mifuko ya hifadhi ya jamii kutoka PPF na kuonesha mwitiko mkubwa wa kujiunga na mfuko wa Pensheni wa PPF.

Mfuko wa Pesheni wa PPF umesema umedhamiria kuhakikisha kwamba wananchi wengi walio kwenye sekta zisizo rasmi ikiwemo wajasiriamali wananufaika na mafao ya hifadhi za jamii kupitia huduma ya Wote Scheme.

Meneja wa mfuko huo Kanda ya Ziwa, Meshack Bandawe, ameyasema hayo Musoma mkoani Mara, wakati akieleza umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko huo mbele ya wadau wa filamu mkoani humo.

Amesema wananchi wasio kwenye sekta rasmi wakiwemo wajasiriamali wanayo fursa ya kujiunga na mfuko wa PPF na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu, mikopo ya elimu, maendeleo pamoja na mafao ya uzeeni kwa kila mwanachama kuchangia shilingi elfu 20 kwa mwezi ambazo mwanachama hulipa kadri awezavyo.

Naye Afisa Masoko PPF, Evance Baguma, amesema lengo la mfuko huo kuanzisha huduma ya Wote Scheme kwa wajasiriamali ni kuondoa dhama potofu kwa baadhi ya wananchi kwamba anayeweza kunufaika na huduma za mifuko ya hifadhi za jamii ni lazima awe mtumishi wa taasisi binafsi ama serikali.

Wadau wengi wa filamu mkoani Mara wamefurahishwa na ufafanuzi wa mfuko huo ambapo wamebainisha kwamba awali walikosa fursa mbalimbali za mifuko ya hifadhi za jamii ikiwemo PPF kutokana ufahamu duni waliokuwa nao.
Tazama picha zaidi HAPA

Katibu Tawala Moani Mara Ahitimisha Mafunzo kwa Wadau wa Filamu Mkoani Humo

Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (katikati) akizungumza hii leo kwenye kilele cha mafunzo ya siku tatu kwa wadau wa filamu mkoani humo. Mafunzo hayo yalianza juzi Disemba 14,2016 kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari Mara Mjini Msoma.

Yaliandaliwa na Bodi ya Filamu nchini kwa lengo la kuwajengea welezi wanatasinia wa filamu ili kuzalisha kazi zenye ubora na hivyo kukidhi ushindani katika soko la ndani na nje ya nchi ambapo zaidi ya washiri 200 walionufaika na mafunzo hayo wamepatiwa vyeti. Tayari mafunzo ya aina hiyo yamefanyika mikoa ya Morogoro na Mwanza na yataendelea katika mikoa mingine.
#BMGHabari
Wanatasnia wa filamu mkoani Mara wakimsikiliza Katibu Tawala mkoani humo, Adoh Mapunda, wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia hao. Ameahidi kutoa fulana (Tshirt) 250 kwa ajili ya wanatasnia wa filamu mkoani Mara waliohudhuria mafunzo hayo ambapo zitawasaidia hususani kuwa na sare ya aina moja wakikutana kwa pamoja
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao, amesema sekta ya filamu ina mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa wanatasnia wake na taifa kwa ujumla hivyo Bodi za filamu mikoani zihakikishe zinasimamia maendeleo ya tasnia hiyo.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso, amebainisha kwamba wadau wa filamu wakiwemo watayarishaji, waongozaji, wahariri pamoja na waigizaji wamefundishwa vyema mafunzo hayo ili kuzalisha kazi bora.
Mgeni rasmi, Katibu Tawala mkoani Mara, Adoh Mapunda (wa pili kulia), akipokea cheti cha utambuzi kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi.Nuru Millao, akipokea cheti cha utambuzi
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fisso
Mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo, Bi.Deograsia Ndunguru, kutoka Chuo Kikuu Dodoma, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari Genoveva kutoka Idara ya Habari Serikalini, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Katibu wa Chama cha Waigizaji mkoani Mara, Johnson Ibambai, akipokea cheti cha utambuzi kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwakilishi wa Mkuu wa Shule ya Sekondari Mara, akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba yake kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari Amicus Butunga, akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba ya TBC kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Mwanahabari George Binagi akipokea cheti cha utambuzi kwa niaba ya 102.5 Lake Fm kutoka Bodi ya Filamu nchini.
Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (mwenye suti) na viongozi wengine wakiwa pamoja na washiriki wa mafunzo ya filamu mkoani Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Katibu Tawala mkoa wa Mara, Adoh Mapunda (mwenye suti) na viongozi wengine wakiwa pamoja na washiriki zaidi ya 200 wa mafunzo ya filamu mkoani Mara wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Mwigizaji Dan Msimamo kutoka Tarime amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuinua ubora wa filamu mkoani Mara na hivyo kukuza soko lake
Mwigizaji Justar Lucas kutoka Tarime amesema mafunzo hayo yamewaongezea weledi na kutambua kwamba filamu ni ajira na ikitumika vyema husaidia kukuza kipato cha wanatasnia wa filamu na taifa kwa ujumla.
Mwigizaji Innocent Mbalwa kutoka Bunda ameishukuru Serikali kupitia Bodi ya Filamu kwa kutoa mafunzo hayo ambapo amesema yatafungua milango mipya kwenye tasnia ya filamu mkoani Mara.
Mwigizaji Jackline James kutoka Musoma amesema mafunzo hayo yamemsaidia kutambua kwamba filamu ni ajira tofauti na alivyokuwa akidhani awali kwamba tasnia hiyo ni sehemu ya burudani.
******************
Katibu Tawala mkoani Mara, Adoh Mapunda, amewahimiza wanatasnia wa filamu mkoani humo kuwa wabunifu katika uzalishaji wa kazi zao ili kupanua soko la filamu ndani na nje ya nchi.

Mapunda ametoa rai hiyo hii leo, wakati akihitimisha mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia wa filamu mkoani Mara, yaliyoandaliwa na Bodi ya Filamu nchini ili kukuza welezi katika uzalishaji wa kazi bora na zenye maudhui yanaykubalika katika jamii.

"Ubunifu ndio unahitajika hivi sasa, watu wengi wanahitaji ubunifu binafsi na siyo "kucopy" na "kupaste" kazi za wengine". Amesisitiza Mapunda na kuongeza kwamba serikali itatoa ushirikiano wa dhati katika kuboresha tasnia hiyo ya filamu kwani hivi sasa hutoa ajira na kukuza uchumi kwa taifa.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nuru Millao, ameziagiza Bodi za Filamu za mikoa kuhakikisha kwamba zinatimiza wajibu wake ipasavyo ili kuboresha zaidi sekta hiyo.

Naye Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisso, amewahimiza wadau wa filamu mkoani Mara wakiwemo watayarishaji, waongozaji, wahariri pamoja na waigizaji walionufaika na mafunzo hayo, kuyatumia vyema ili kukuza soko lao la filamu.

Kwa upande wake Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba, amewasisitizia hao kutumia mafunzo hayo ili kuzalisha filamu na vipindi vya luninga vyenye ubora ili kunufaika na uhitaji uliopo.

Akisoma maazimio ya wanatasnia wa filamu mkoani Mara, Katibu wa Chama cha Waigizaji mkoani humo, Johnson Ibambai, ametaja baadhi ya maazimio hayo kuwa ni pamoja na kuiomba serikali kuweka mitaala ya filamu kuanzia shule za msingi na vyuo vya ufundi VETA ili kusadia utoaji wa elimu hiyo ya filamu.
Tazama picha zaidi HAPA

Thursday, November 19, 2015

Mwanahabari Nashon Kenedy Awapa Siri Ya Mafanikio Wasanii wa Mwanza

Kulia ni Mwanahabari Nashon Kenedy kutoka gazeti la kiswahili la Habari Leo na lile la kiingereza la Daily News akiongea katika hafla ya kuzaliwa kwa Yusuph Kisiba a.k.a Yuskiss ambae ni Mtengenezaji wa Filamu katika Kampuni ya Shafineyz Film Production ya Jijini Mwanza.
Na:George Binagi-GB Pazzo wa Binagi Media Group
Mwanahabari Nashon Kenedy kutoka gazeti la kiswahili la Habari Leo na lile la kiingereza la Daily News amewashauri wasanii wa maigizo Jijini Mwanza, kubadilika na kuigiza filamu zinazogusa maisha halisi ya Kitanzania na kuachana na uigizaji wa filamu zisizo na uhalisia wa maisha ya Kitanzania hususani filamu za mapenzi. 

Kenedy aliyasema hayo jana katika hafla ya kuzaliwa kwa Yusuph Kisiba a.k.a Yuskiss ambae ni Mtengenezaji wa Filamu katika Kampuni ya Shafineyz Film Production ya Jijini Mwanza ambapo alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo ambayo pamoja na wageni wengine, pia ilihudhuriwa na wasanii mbalimbali wa muziki na filamu kutoka Jijini Mwanza.

"Japokuwa maisha yetu yanategemea mapenzi, lakini mimi nawashauri kwamba acheni kuigiza filamu za mapenzi kila siku kama mnahitaji kufanikiwa. Igizeni filamu zinazoeleza maisha halisi ya kitanzania kama vile kuonyesha matatizo yanayowakabili wananchi, na hapo ndipo mtaweza kuwa tofauti na waigizaji wengine jambo ambalo litawasaidia kufikia katika mafanikio yenu". Alibainisha Kenedy.

Katika hafla hiyo, Kisiba aliwashukuru wale wote walioungana nae katika kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa ambapo aliahidi kuitimiza ahadi yake ya kuhakikisha kuwa soko la uigizaji wa filamu Jijini Mwanza linafufuliwa kupitia Kampuni anayofanyia kazi ya Shafineyz Film Production kwa kuwa ni aibu kukosekana kwa soko la filamu Jijini hapa ikilinganishwa na majiji mengine nchini kama vile Jiji la Dar es salaam. 
Tazama HAPA Picha za Hafla hiyo

Thursday, October 16, 2014

Nafasi ya Kuwa Katika Sinema Boston

Jodi Purdy CASTING & PRODUCTION NOTICES
BOSTON AREA ONLY

Seeking Ethnic Family for Birthday Party scene to be shot on Saturday 10/18 or Sunday 10/19 in your home - must be able to sing Happy Birthday in your language - PAYING GIG!!
Please send photos of family - mom, dad, grandparents, kids, teens and your contact info asap to: zandrakcasting@gmail.com Subject: Ethnic Family

Wednesday, April 06, 2011

Wasanii na Wadau wa Filamu Tanzania Wapata Mkombozi wa Kweli

NA JUSTIN KASYOME

www.kasyome.bogspot.com+255 7141696655

Ukizungumzia tasnia ya filamu za Kitanzania kwa kuwataja wanaharakati au wadau wanaooiinua na kuipigania filamu, ni nadra sana kuacha kuwataja waigizaji maarufu, vikundi vyenye majina makubwa, taasisi, vyama au makampuni.

Steven Kanumba "The Great", Vincent Kigosi "The Greatest", Suzan Lewis "Natasha", Charles Magari "Mzee Magari", Blandina Chagula "Johari" na wengine wengi, ni miongoni mwa waigizaji ambao ni lazima uwataje kama ukitakiwa kuwataja waigizaji "wanaipiga tafu" tasnia ya filamu nchini.

Wadau wengine ni kwa mfano, makundi ya Mambo Hayo na The Spendid, yaliyotamba enzi zao na kuibua changamoto ambazo hadi sasa zinaonekana. Mengine ni Kaole Sanaa Group na Jakaya Arts Group.

Taasisi kama kituo cha Utamaduni cha Muungano wa Urusi na Tanzania (Russian - Tanzania Culture Center), taaisisi ya watu wa Ujerumani (Goethe Institute), Game 1st Quality, Steps Entertainment, BASATA, COSOTA na TAF.

Pamoja na wadau na wanaharakati mbalimbali, msanii bado hana mafanikio! bado ni omba omba! Wengi wenye maisha mazuri, si kutokana na filamu! Ni kutokana na background ya familia yake au kipato chake kingine nje ya filamu! wakiwa kwenye vyombo vya habari wanaficha ukweli ili wajikweze kwa kuwa wengi wao wanaingia kwenye taaluma ya filamu "kuuza sura"!

Mzalishaji, anaeumiza kichwa kutafuta mtaji na kuandaa bajeti ya filamu, uandaaji hadi kukamilika, bado hana sauti wala nguvu sokoni! Anafanya kazi kwa shinikizo la woga wa soko! Hana uhakika wa soko lake endapo atakuwa jeuri! kinachobaki ni kuweka mikono nyuma awapo mezeni ili filamu yake isambazwe! Haijalishi atalipwa kiasi gani!
Msambazaji, anatupiwa lawama za unyonyaji, Buguruni na Ubungo, filamu za elfu tano dukani, zinauzwa elfu moja moja! Muigizaji, ndugu jamaa na marafiki wanazinunua kwa wingi!

Mnunuzi wa mwisho bado anafuata mkumbo wa nguvu ya msambazaji bila kujali ubora filamu kuanzia kwa mtunzi wa hadithi, muigizaji, muongozaji, mpiga picha, mbamaji, mazingira na taaluma ya filamu yote! Ananunua filamu kwa mazoea ya majina na hadithi!

Idea For Action Tanzania (IFA Tanzania), mradi uliobuniwa kitaalamu, ni miongoni mwa wadau wa kweli na wa dhati kabisa katika kiwanda cha filamu za kitanzania.
Ni mradi wa kuibua na kuendeleza vipaji vya sanaa kwa kutoa elimu ya sanaa na ujasiriamali, bure, bila ada yoyote! Kila mdau wa sanaa anaalikwa kuhudhuria mafunzo.

Mafunzo haya yatolewayo kwa lugha anayoielewa kila mtanzania (Kiswahili) yanakwenda kwa muda wa miezi mitatu. Mlengwa anatakiwa kujiunga muda wowote na kuanza mafunzo baada ya kujaza fomu ya kujiunga. Hakuna umri, kabila, dini wala kiwango cha elimu kinachofaa kupata mafunzo isipokuwa yeyote mwenye mapenzi mema na sanaa na anayejua kusoma na kuandika, anapaswa kujiunga.

Baada ya kumaliza mafunzo, mwanafunzi anasimamiwa na wataalamu kufanya mafunzo kwa vitendo kwa vitendo ili kuthibitisha uelewa wake na kutunikiwa cheti cha awali cha kuhitimu.

Mwisho, mhitimu akipenda ataunganishwa na makampuni au taasisi wadau kufanya kazi kwa mkataba wa miaka miwili ili kuzidi kuapata uzoefu wa kazi ya sanaa na atabakiwa kuwa mwanachama wa mradi wa IFA Tanzania maisha yake yote kwa kushirikaina na mradi pale atakapohitajika, kuomba ushauri katika kuanzisha na kuendesha miradi mbali mbali ya sanaa na mambo mengine ya kimaendeleo.

Mradi huu ambao ni endelevu, umegawanywa katika vitengo vinne vya filamu, muziki, vichekesho na biashara. Tuzungumzie kitengo cha filamu. Ndani ya kitengo hiki, zinafundioshwa mada nane,saba ni taaluma ya filamu na moja na ujasirimalia wa filamu (Interprenuereship in Film Production)

Mada hizo saba ni Utunzi na Uandishi wa Hadithi (Screenwriting), Uigizaji na Upangaji wasanii (Acting and Casting), Upigaji wa picha (Cinematography), Ubunifu wa Sauti (Sound Designing), Ubunifu wa Uzalishaji (Production Design), Uongozaji/Uzalishaji/Masoko (Directin/Producing/Marketing) na Uhariri(Editing).

Malengo makubwa ya IFA Tanzania, kitengo cha filamu ni matatu. Kutoa taaluma ya filamu ili mnufaika aitambue filamu na kujitambua awapo ndani ya filamu.
Hilo mosi.
Pili, kutoa elimu ya ujasiriamali baada ya taaluma ili kugundua, kutambua na kutumia fursa mbalimbali zilizopo na kupata mafanikio kabla ya kumpelekea msambazaji!
Msambazaji awe mdau wa mwisho kwa mapato ya mzalishaji wa filamu za kitanzania! Tofauti na ilivyo sasa, ambapo mzalishaji ni lazima akampigie magoti msambazaji! Tena kwa kazi iliyomtoa jasho!

Tatu, ambalo ni kubwa zaidi, kuokoa utamaduni wetu. Uzalendo, haki na utaifa uwekwe mbele zaidi wakati elimu na burudani ikiimilishwa kitaalamu kama dhima kuu ya filamu ambayo ni kazi ya sanaa katika jamii.
Malengo ya mradi ni kumzalisha mtaalamu wa filamu mwenye mbinu za ujasiriamali ili atazame, azalishe au kushirikishwa katika filamu zinazozungumzia visa vya vita, magonjwa, upelelezi, tatizo la ukosefu wa ajira, njaa, afya, elimu n.k.
Iweje filamu za kitanzania ziwe na ujumbe wa kisa kimoja cha mapenzi pekee? Je, Je ni makosa kuzungumzia visa vingine? Utamaduni wetu wa sasa kwa vizazi vijavyo, utakuwaje? Tunaijenga Tanzania ijayo au tunaibomoa?

Tunasikitishwa sana na mfumo wa filamu zetu kiutendaji na kibiashara. Tunapoteza utamaduni kwa faida fulani fulani. Nani alaumiwe kati ya muigizaji, mzalishaji, msambazaji au mnunuzi wa mwisho?

Justin Kasyome, anaendelea, IFA Tanzania, ni mradi wa kizalendo, tunapigania utamduni wa mtanzania kwa kutengeneza faida inayokubalika katika mfumo mzuri kimasoko. Watanzania tujikomboe, elimu pekee ndio silaha yetu. Kwa pamoja tutshinda na kumwondoa adui yetu.
IFA Tanzania, inapatikana ndani ya majengo ya Chuo Cha Elimu Kuu Sanaa, eneo la Sinza Legho, barabara ya Shekilango, mkabala na Club ya Sun Cirro. Au kwa mtandao wa www.ifatanzania.blogspot.com

Monday, September 13, 2010

Kazi ya Acting Kwa Watoto - African Boy and Girl

African Boy and Girl

Mon, 09/13/2010

(Non-Union Only)

A young African or African American boy and girl
(age 7-12) are needed to narrate several kids films
about Africa. The work is unpaid but can serve as an
educational experience. Please send e-mail photo.
Thank you.
Elmer Hawkes
www.worldstogether.com
info@worldstogether.com

Contact Details:
Elmer Hawkes
Worlds Together
617 354-2207

info@worldstogether.com

Thursday, March 18, 2010

Ray na Vincent Wanatafuta Waigizaji wa Kike Wapya!

Waigizaji wasichana wanahitajika RJ Company

03/18/2010


Kama unajihisi wewe ni mrembo basi kwa sasa tunatafuta wasanii wapya wa kike katika ofisi za RJ COMPANY zilizoko SINZA MORI. Lengo ni kuwapata wasanii wa kike ambao ni wapya katika tasnia ya filam nchini ili waje kushiriki katika filam mpya itakayoandaliwa na kampuni ya RJ. Umri ni kuanzia miaka 18 mpaka 28. Pia unaweza kutuma picha zako kabla hufika ofisini ili tuweze kukuona jinsi ilivyo.Muda wa ofisi ni saa 4 kamili asubuhi mpaka saa 12 jioni kwa siku za Jumatatu mpaka Ijumaa na siku za Jumamosi kuanzia saa 4 kamili asubuhi mpaka saa 8 mchana. HAKUNA GHARAMA ZOZOTE ZILE UTAKAZOLIPISHWA KWANI KAMPUNI INAJITOSHELEZA.

WASILIANA NA VINCENT aka RAY KUPITIA:Tel: +255 714 082729P.O. Box 11347
Email: vincentkigosi@gmail.com
Website: www.rjtanzania.com

*****************************************

Hapo napingana na Ray. Yaani watu zaidi ya miaka 28 hawawezi kuwa warembo? Angesema anatafuta kuanzia 18+. Katika sinema unahitaji waigizaji wa kila umri. Mambo ya vijana kujifanya wazee haipendezi. - Chemi