Showing posts with label Gospel Singer. Show all posts
Showing posts with label Gospel Singer. Show all posts

Saturday, February 10, 2018

IMBA Diaspora Singing Auditions in Boston

An American idol Style Singing Competition is being held to to find the the next ' African' American Gospel Star.

It's called IMBA Diaspora. Imba in Swahili means sing.  Gospel Singers of African descent (Diaspora) are invited to participate.

Boston Auditions will be held on Saturday, February 24th, at the Double Tree by Hilton Hotel in (201 Everett Avenue) Chelsea, MA, 02150 from 11:00AM to 4:00PM.

Regional winners will be flown to North Carolina for the Finals in July, 2018.  The winner will get a Music and Video Recording Contract.

Auditions will be held in Atlanta, Boston, Illinois, Maryland, Minnesota, California, Texas, New York and North Carolina.

For more information visit www.imbadiaspora.org.  Or call Pastor Jared Mlongecha at 781-284-0510.


Saturday, July 26, 2014

Mwimba Injili Bahati Bukuku Apata Ajali ya Gari!


 
 
 
 
Msanii wa Injili Bahati Bukuku (40) ni miongoni mwa majeruhi watatu wa ajali ya gari iliyotokea iliyotokea leo katika barabara ya Morogoro – Dodoma eneo la ranchi ya Narco Wilaya ya Kongwa .

Majeruhi wengine ni Edson Mwakabungu (31) ambaye alikuwa dereva na Frank Christopher (20).
 
Kwa mujibu wa taarifa ya kamanda wa polisi wa mkoa wa Dodoma David Misime  ajali hiyo ilitokea saa tisa alfajiri.
 
Alisema taarifa za wahusika zinasema kwamba gari walilokuwa wakisafiria Bukuku, IT 7945 aina ya Toyota Nadia likiendeshwa na Edson Mwakabungu mkazi wa Tabata Dar es salaam liliacha njia na kugonga gema baada ya kugongwa na gari inayodaiwa kuwa ni Fuso.
 
Kamanda Misime amesema kwamba Bukuku analalamika maumivu sehemu mbalimbali za mwili huku Frank akiwa na michubuko usoni na mkono wa Kulia.
Aidha amesema kwamba watu wote hao wamelazwa  katika Hospitali ya Wilaya ya Kongwa kwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.
 
 Kwa mujibu wa Kamanda Misime mwimbaji huyo na wenzake walikuwa wanatokea Dar es Salaam ambapo dereva alikuwa anelekea DRC – Kongo, huku Bahati Bukuku na Frank Christopher walikuwa wanakwenda Kahama kwenye tamasha la injili.
 
Source: Sifa Lubasi, Dodoma