Showing posts with label Jason Hilton. Show all posts
Showing posts with label Jason Hilton. Show all posts

Wednesday, August 13, 2008

Walimu wa sinema 'stunts'



Hao ndo walifundisha akina Peter Omari, Shaffi Abdul na Charles Magali stunts zao kwenye sinema Bongoland II. Nilishangaa waigizaji Bongo walivyoniambia kuwa eti watu wanapigana kweli hadi kuumizana wakiwa kwenye shuti. Hizi sinema za Hollywood hakuna kuumizana ingawa utadhani mtu kapigwa kweli kweli.

Tulivyokuwa Bongo niliwashauri watu wajifunze hizo stunts maana walikuwa wanatoa mafunzo bure. Zaidi ya kipigana aliwaonyesha kidogo defensive driving (yaani kuendesha gari kwa stunt). Hapa Marekani watu wanalipa maelfu ya dola kujifunza.

Mwalimu Jason Hilton alitaka kufundisha wabongo wengi lakini hakuna aliyejitokeza zaidi ya waliokuwa kwenye sinema. Nilivyowauliza vijana fulani kama wanataka kujifunza waliuza eti watalipwa shilingi ngapi. Somo inatolewa bure halafu unataka ulipwe? Si ukachukua huo utalaamu uliyopata na uende ukatengeneza pesa? Au, ni wazo baya kwangu?

Wednesday, January 23, 2008

Mapigano katika sinema ya Bongoland II


Peter Omari na Charles Magali wakifanya mazoezi kabla ya kushuti scene

Jason Hilton coaches Shaffi & Mzee Olotu for a fight scene
Jason Hilton coaches Mzee Olotu on how to fall during a fight scene
Jason Hilton plays 'Kung Fu' with curious neighborhood kids while filiming in Manzese
Josiah Kibira discusses with Jason Hilton and Shafii on the logisitics of a fight scene

Watu wanangojea kwa hamu sinema ya Bongoland II.

Kwenye crew ya Bongoland II kulikuwa na mtaalamu wa mambo ya stunts (kupigana, kuanguka nk katika sinema) anaitwa Jason Hilton. Nilivyokuwa Bongo niliwaambia baadhi ya wasanii kuwa wawe makini kujifunza maana alikuwa anatoa somo bure. Hapa Marekani ukitaka masomo ya stunt unalipia hasa.

Kwa kweli kuna umuhimu wa mwalimu wa kufundisha stunts kwa wasanii Bongo. Nilishangaa sana nilipoambiwa kuwa eti katika sinema za Bongo, ukiona watu wanapigana au mtu kazabwa kibao basi wanafanya kweli hadi kuumizana! Hollywood mnaona watu wanapigana kumbe hakuna mtu aliyeguswa. Mfano kwenye ile sine ya Aftershock:Beyond the Civil War ambayo nimo, utadhani jamaa wanapigana kweli. Kumbe jamaa hakuguswa hata kidogo. Nakumbuka walivyoifilm na final product nikashangaa kweli utadhani jamaa kaua!

Website ya Jason Hilton ni: http://www.tumblemonster.com/pages/gallery.html

Hapa mnaweza kuona clip fupi ya mapingano kutoka sinema ya Bongoland II.

Note inachukua muda ku-load.

http://www.tumblemonster.com/video/TMPStuntSchoolReel.mov

Tuesday, July 31, 2007

Bongoland II - Manzese


Picha hizi zinatoka Kwenye site ya Sam Fischer, ambaye ni Cameraman kwenye sinema ya Bongoland II. http://web.mac.com/samfischer/iWeb/Site/Africa%20Photos%202.html
Hapo juu Star wa Bongoland II Peter Omari, na actor mwingine wanajiandaa kuacti scene kwenye gari.
Scene inapangwa. Hapa Sam Fischer anapanga jinsi atakavyopiga picha ya scene ya kupigana.

Stunt Coordinator, Jason Hilton, akicheza Kung Fu na watoto wa Manzese.


Hapa wanapadisha camera kwenye crane.



Akina Sam walitengeneza Crane kwa ajili yakupandisha camera na kupiga scene kutoka juu. Ila bahati mbaya crane ilivunjika na haikuweza kutumika.




Uchochoro wa Manzese. Amini msiamini, zamani hii ilikuwa barabara ambayo magari yalikuwa yanapita. Baba mdogo alikuwa ana drive hapo na kupaki gari yake kwenye gereji yake. Sasa asante ujenzi holela hakuna barabara tena.



Muongozaji na Mwandishi wa sinema ya Bongoland II, Josiah Kibira, akifika kwenye nyumba ya Manzese.




Hapa Timu ya Bongoland II wana survey kama nyumba itafaa kwenye filamu. Nyumba hiyo ni ya marehemu baba yangu mdogo, Prof. Crispin Hauli. Na inatumika kwenye sinema ya Bongoland II kama nyumba ya 'Uncle'.