Showing posts with label Mitindo. Show all posts
Showing posts with label Mitindo. Show all posts

Saturday, July 26, 2014

WaJapani Sasa Wanataka Nywele Zetu!


 Wajanja, muwahi kufika Japani mkafungue saluni za kutenegeneza mitindo ya Afro.



Kutoka Facebook:

 
THE JAPANESE ARE NOW BUYING AFRO HAIR

This photo shows how the Japanese create 'the Afro Look' on their hair texture. (This is old news.)
But, apparently, they are now interested in buying our afro hair, so they can make it into wigs, weaving weft and bulks of hair for braiding. (Makes you wonder where our hair goes, once it is swept up, off the salon floor. Will salon owners be capitalising on the trade of our hair?.... Perhaps.)
MS Natural Notts TAKE ON THIS
We, 'Black folks' should have been the first to capitalise on this, i.e. developing a market for the trade of our afro hair, instead of leaving it on the salon floor, in retaliation to Asians capitalising on our distorted concept of beauty. E.g. The straight hair obsession by blacks, that fuels the global success of Asian human hair trading.
The ONLY reason our people missed this entrepreneurial idea, is because we HATE what naturally grows from our scalp..... Other ethnic groups have always been the first to appreciate every inch of us and to capitalise on our beauty, by any means necessary..... E.g. fake tans, fake buts, fake full lips, etc
WHEN WILL WE FULLY UNDERSTAND
Our natural assets are the measuring stick of beauty???


‪#‎BlackPeopleWeNeedToWakeTFUP‬!

Monday, September 22, 2008

Mwanamitindo Bora 2008

Kutoka Lukwangule Entertainment:

WALIMBWENDE 13 wamefuzu kutinga kwenye fainali za kinyang’anyiro cha michuano ya kumsaka mwanamitindo bora wa Afrika Mashariki kitakachofanyika Novemba 29 jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa waratibu wa kinyang’anyiro hicho Judy Felician alisema leo kuwa walimbwende hao 13 wataingia kambi mwezi ujao pamoja na washindi wengine kutoka nchini za Kenya Uganda, Rwanda na Burundi kupata washindi wanne ambao watakwenda kushiriki kwenye shindano jingine la uanamitindo nchini Ugiriki.

Judy alisema nchi za Kenya Uganda, Rwanda na Burundi zitatoa walimbwende watatu kila moja ambao wataungana kambini na walimbwende 13 wa hapa nchini katika kambi ambayo itaanza Oktoba 25 jijini Dar es Salaam.

Walimbwende 13 waliofuzu kutinga fainali ni Rihama Mohamed, Gloria Emson, Namrata Mandania, Nshoma Mkwabi, Sarah Kazaura, Cynthia Kimasha na Beatrice Wilbard.
Wengine ni Nelly Kamwelu, Doris Godfrey, Evanuru Isaack, Joyce Mbago na Irene Shirima . baadhi ya vigezo vilivyotumika kuwapata washiriki hao ni binti kuwa na umri kati ya miaka 18 hadi 22 na urefu wa sentimita 170-175, kifua cha upana wa sentimita 60.

Kwa mujibu wa Judy walimbwende hao 13 waliofuzu kutinga hatua ya fainali zitakazofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubileee jijini Dar es Salaam walipatikana katika michakato miwili tofauti iliyofanyika Agosti 30 na Septemba 20 na kuhusisha walimbwende kutoka shemu mbalimbali za Tanzania .

Aidha mratibu huyo alisema katika fainali hizo walimbwende wanne watakaoshika nafasi nne za juu watapelekwa nchini Ugiriki na kampuni ya G-Cat ya Uingereza kushiriki katika kinyang’anyiro kingine ambacho kitawakutanisha na wanamitindo wengine kutoka ulaya.
Judy alisema wakiwa Ugiriki wanamitindo hao watachuana kuwania kupata mkataba wa mwaka mmoja kuonyesha mavazi kwa mwaka mzima huko ulaya.

Akizungumzia mustakabali wa walimbwende ambao watashindwa kufuzu kwenda Judy alisema walimbwende hao watakuwa wakitumika katika shughuli mbalimbali za matangazo na masuala mbalimbali ya mitindo hapa nchini.

Shindano hilo linalenga kuwawezesha wanawake na kauli mbiu yake inasema ‘Wasichana wajihadhari na ujauzito katika umri mdogo, umalaya na utumiaji wa dawa za kulevya na Ukimwi’.