Showing posts with label Msiba kansa. Show all posts
Showing posts with label Msiba kansa. Show all posts

Thursday, February 10, 2022

Tanzia - Dr. MweleNtuli Malecela

 



Dr.  Mwele Ntuli Malecela  1963-2022

Nimepokea kwa huzuni na masikitiko habari ya kifo cha dada yangu wa Ubatizo Dr. Mwele Ntuli Malecela.  Amefariki Geneva, Switzerland jana.  Alikuwa na sumbuliwa na ugonjwa wa Kansa tangu mwaka 2019.   Kwa maneno yake mwenyewe..kansa iligundulika ikiwa tayari imekwisha sambaa mwilini.

Wakati wa kifo chake, Dr. Malecela, alikuwa anafanya kazi World Health Organization, kama Mkurugenzi wa Udhibiti wa  Magonjwa ya Yasiopewa Kipaumbele.  Kabla ya hapo alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti za Kiafya Tanzania (NIMRI). 

Tanzania na Africa kwa ujumla imepata hasara. Tumempoteza mtaalamu aliyeboboea katika fani yake.

Poleni sana familia ya Malecela.  Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.


Kwa  habari zaidi BOFYA HAPA

Wednesday, March 06, 2013

Rais wa Venezuela, Hugo Chavez Afariki Dunia!



Wadau, leo tumempoteza mtetezi wa maskini, Rais Hugo Chavez wa Venezuela. Alikuwa na miaka 58. Aliugua ugonjwa wa kansa (saratani).

Alikuwa anatoa mafuta bure kusaidia maskini wa Marekani katika kipindi cha baridi. Huko matajiri hawana taimu na maskini.

Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.

Katika kideo, Rais Chavez anamwita Rais Bush  Jr. shetani huko Umoja wa Mataifa.

Kwa habari zaidi za kifo cha Rais Chavez soma:  http://www.cnn.com/2013/03/05/world/americas/venezuela-chavez-main/index.html?hpt=hp_t1