Showing posts with label Kifo Msiba. Show all posts
Showing posts with label Kifo Msiba. Show all posts

Saturday, December 31, 2022

Papa Mstaafu Benedict wa XVI (16) Afariki Dunia



                                                      Hayati Papa Benedict XVI

 Papa Mstaafu Benedict XVI amefariki dunia leo asubuhi huko Vatican, Italia.  Ilitanganzwa mapema wiki hii kuwa afya ya Papa Benedict XVI ilikuwa imezorota.  Amefariki kwenye Monestari ya Vatican.  Alikuwa na miaka 95. Jina aliyozaliwa nayo ilikuwa Joseph Ratzinger. Alizaliwa Ujerumani mwaka 1927.

Atazikwa Alhamisi Ijayo huko Vatican baada ya Misa itakayosimamiwa na Papa Francis.  Papa Benedict XVI hakutaka mazishi enye makuu. 

Papa Benedict XVI  alistaafu ghafla mwaka 2013.   Alikuwa Papa wa kwanza kustaafu katika miaka 600 iliyopita ya Vatican. Kwa kawaida mtu anaachia upapa akifa.  Papa (Pope) ni mkuu wa kanisa Katoliki duniani.

Mungu Ailaze Roho ya Papa Benedict XVI mahala pema peponi.  Amen



Sunday, February 13, 2022

Tanzia - Professor Samahani Kejeri

Mwanahistoria na Mtembeza Watalii maarufu, "Professor" Samahani Kejeri, amefariki dunia, leo Februari 13, 2022, katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Alikuwa amelazwa kwa ajili ya matibabu ya kansa.

Binti yake, Furaha Kejeri amethibitisha  habari hiyo, Mazishi yatafanyika kesho, Jumatatu, Februari 14, 2022 nyumbani kwa marehemu, Magomeni, Bagamoyo. (Siyo Magomeni ya Dar es Salaam)

Prof. Kejeri alipewa jina la "Professor" kutokana na ufahamu wake wa Historia ya Bagamoyo.  Alikuwa anatunza vitabu, "friend books" ambazo zimesainiwa na watu ambao aliwatembeza Bagamoyo.  Mimi mwenyewe nilikutana naye mara la kwanza mwaka 1988, nikiwa mwanafunzi wa Tanzani School of Journalism.  Tulienda Bagamoyo kwenye Field Trip na alitutembeza na kutoonyesha sehemu muhimu za kihistoria ya Bagamoyo ikiwemo "hanging tree" ambako wajerumani walikuwa wananyonga weusi.  

Prof. Kejeri pia aliigiza katika sinema Maangamizi the Ancient One kama Mganga Simba Mbili.  Sinema hiyo ilikuwa ya kwanza kutoka Tanzania kuwa katika mashindano ya Academy Awards (Oscars) Hollywood.

Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi. Amin



Prof. Samahani Kejeri, Prof. Amandina Lihamba na Msanii Barbara O katika sinema Maangamizi the Ancient One

Prof. Samahani Kejeri Explains History of His Name - YouTube



Thursday, February 10, 2022

Tanzia - Dr. MweleNtuli Malecela

 



Dr.  Mwele Ntuli Malecela  1963-2022

Nimepokea kwa huzuni na masikitiko habari ya kifo cha dada yangu wa Ubatizo Dr. Mwele Ntuli Malecela.  Amefariki Geneva, Switzerland jana.  Alikuwa na sumbuliwa na ugonjwa wa Kansa tangu mwaka 2019.   Kwa maneno yake mwenyewe..kansa iligundulika ikiwa tayari imekwisha sambaa mwilini.

Wakati wa kifo chake, Dr. Malecela, alikuwa anafanya kazi World Health Organization, kama Mkurugenzi wa Udhibiti wa  Magonjwa ya Yasiopewa Kipaumbele.  Kabla ya hapo alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti za Kiafya Tanzania (NIMRI). 

Tanzania na Africa kwa ujumla imepata hasara. Tumempoteza mtaalamu aliyeboboea katika fani yake.

Poleni sana familia ya Malecela.  Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.


Kwa  habari zaidi BOFYA HAPA

Saturday, December 25, 2021

Congo Restaurant bombed on Christmas Day!



Bomu imelipuka kwenye mgahawa Kongo Magharibi..watu saba wamekufa!

BENI, Congo (AP) -  A bomb has exploded at a restaurant as patrons gathered on Christmas Day and killed at least seven people in eastern Congo. Mayor Narcisse Muteba told The Associated Press that the victims included two children and that investigations were underway to find the perpetrators. There was no immediate claim of responsibility for the attack though Islamic extremists claimed a suicide bombing back in June that caused no other casualties. The town has long been targeted by rebels from the Allied Democratic Forces which traces its origins to neighboring Uganda. But an Islamic State group affiliate claimed responsibility for two explosions in Beni in June.

\

FOR MORE INFORMATION CLICK HERE:

Saturday, April 17, 2021

Buriani Prince Philip (1921-2021) - Mume wa Malkia wa Uingereza

 Leo  mume wa Malkia wa Uingereza, Prince Philip, amezikwa katika kanisa la Mt.George huko Windsor Castle, Uingereza.  Prince Philip alifaikri tarehe 9 Aprili akiwa na miaka 99.  Alikuwa mume wa Malkia Elizabteh kwa miaka 73. 

Niliwahi kuongea na Prince Philip. Mwaka 1979, nikiwa mwanafunzi wa  shule ya sekondari Zanaki,  tulikuwa Ikulu, kuwapokea.  Enzi zile, kama anakuja kiongozi wa nchi ya nje, wanafunzi walikuwa wanatumiwa kupanga  njia kumlaki   

Basi, malkia na familia yake walishuka kwenye gari, na walitembea kwa miguu kwenye  kapeti nyekundu kuingia Ikulu.  Prince Philip alisimama, na kutangalia sisi wanafunzi.  Akauliza,  nyie ni wanafunzi wa shule gani, kwa Kiingereza,  Wanafunzi waliokuwa karibu na mimi walikimibia.  Nikamjibu,  " We are students from Zanaki Girls Secondary School.  (sisi ni wanafunzi kutoka shule ya sokndari Zanaki".  Akauliza  shule ilikuwa inaitwa nini zamani, nikamwambia, Aga Khan Girls.  Alisema  asante, na kuendelea kuingia Ikulu.  Doh!  Niliongea na Royalty!  nilirudi yumbani kwa furaha na kuwasimulia wazazi wangu na marafaiki jinis nilivyoongea na Prince Philip.

Kwenye ziara ile ya mwaka 1979, Malikia alisali na sisi, katika Kanisa la Mt. Albano, Dar es Salaam.  

Mungu ailaze roho ya marehemu Prince Philip.  

Kuona video fupi ya ziara ya Malkia Elizabeth II na familia yake East Africa mwaka 1979  BOFYA HAPA:

 Wanafunzi na wakazi wa Dar es Salaam, wakiwashangalia Malkia Elizabeth na familia yake wakielekea Ikulu alipotembelea Tanzania mwaka 1979,


Malkia Elizabeth II na hayati Prince Philip wakiwapungia waTanzania baada ya ziara yao mwaka 1979.


Maisha ya Prince Philip

Saturday, April 11, 2020

JIhadhari na Ugonjwa wa Coronavirus



Mgonjwa wa Coronavirus akipata matibabu hospiatlini
Wadau,  tafadhali jikinge dhidi ya ugonjwa wa Coronavirus (COVID-19).  Huo ugonjwa unaua!   Hauchagui rangi, umri, au kama wewe ni maskini au tajiri!

Shemaji yangu, Dennis Whitlow, amefariki kwa coronavirus hapa Boston usiku wa kuamkia jumatatu. Hakuna aliyeruhisiwa kumwona hospitalini hadi amefariki.   Nafahamu wagonjwa wengi, wengine wamepona, wengine wamefariki!  Kuna babu wa miaka 88 aliyefariki niliyekuwa namfahamu na kijana mwenye afya mwenye miaka 28 ambaye amefariki. Coronavirus hauchagui.

Tafadhali mfuate masharti. Ukae mbali na mtu mwingine, kaeni majumbani na ukitoka funika  mdomo na pua!  Nawa mikono kila mara. Usiguse uso wako.

Kifo cha coronavirus ni sawa na kifo cha maji, mapafu yanajaa maji, mwili unashindwa kupata hewa (oxygen).


Mungu Atunusuru!


Kirusi cha Coronavirus
Kaburi la pamoj a ya waliofuka kwa Coronavirus mjini New York

Saturday, July 27, 2019

TANZIA - Agnes Kabigi

Wadau, Agnes Kabigi alikuwa rafiki yangu pamoja na mwandishi wa habari mwenzangu.   kweli nina huzuni leo.  Mungu ailiaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.

HABARI KUTOKA https://www.habarimtaa.com/2019/07/picha-mwili-wa-agnes-kabigi-waagwa.html
Mwili wa Meneja Mawasiliano wa asasi inayolenga kutokomeza UKIMWI kwa watoto na familia Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI), Bi. Agnes Kabigi umeagwa leo Jumamosi Mjini Kahama na kusafirishwa kwenda jijini Dar es salaam kwa ajili ya mazishi.

Agnes Kabigi alifariki dunia aliyefariki dunia jana mchana Ijumaa Julai 26,2019 baada kuanguka ghafla wakati akitekeleza majukumu yake akiwa katika Hospitali ya wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Agnes Kabigi ni mwandishi Mwandamizi aliyewahi kufanya kazi katika Magazeti ya Uhuru,Mzalendo na Nipashe na mpaka umauti unamkuta alikuwa anafanya kazi katika shirika la AGPAHI linalojihusisha na mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI ambalo linafanya kazi zake katika mikoa ya Shinyanga,Mwanza,Simiyu na Mara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa shirika la AGPAHI,wakati wa kuaga mwili wa marehemu,Mfanyakazi wa AGPAHI mkoa wa Shinyanga,Kasablankhahr Herman amesema mwili wa Agnes utasafirishwa kwa ndege majira ya saa 10 leo jioni kutoka Mwanza hadi Jijini Dar es salaam kwa ajili ya mazishi.

Agnes alizaliwa tarehe Julai 13,1967.
Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Agnes Kabigi . Amina

Saturday, September 22, 2018

Tanzia - Jah Kimbute


KUTOKA FACEBOOK:

Yohana Blacklista
TANZIA: MFALME WA REGGAE JAH KIMBUTE AFARIKI DUNIA DAR ES SALAAM

Habari zilizotufikia katika chumba chetu cha habari usiku huu zinasema kwamba gwiji wa muziki wa reggae nchini Jah Kimbute amefariki dunia nyumbani kwake Msasani jijini Dar es salaam, mshirika wa karibu wa marehemu David Msitta Manju, amethibitisha.
Akiongea nasi kwa njia ya simu kutoka Mwanza aliko kikazi, Manju amesema amepata habari usiku huu kwamba Jah Kimbute amefariki dunia Alhamisi jioni nyumbani kwake.
Amesema kwamba amepata taarifa hizo toka kwa mkewe aliyeko jijini Tanga na kwamba mipango ya mazishi itajulikana leo asubuhi baada ya ndugu kukusanyika.
Mke wa marehemu pia alithibitisha habari hizo akiwa Tanga, na kusema kila kitu kitafahamika baada ya ndugu wa Jah Kimbute kukutana.
Amesema marehemu alikuwa akiishi na mwanae nyumbani kwake Msasani na kwamba jana jioni alipokwenda chumbani kwake alimkuta amefariki.
"Hizi habari tumezipata usiku huu na sasa ndugu wa marehemu ambao wengi wako Lushoto wanakusanyika tayari kwa safari ya Dar es salaam kesho kukamimlisha mipango yote.
Jah Kimbute, ambaye jina lake halisi alikuwa Samwel Mleteni, alitamba sana katika anga ya muziki na kuitwa Mfalme wa Reggae wa Tanzania miaka ya 80 akiwa na kundi lake la Roots and Culture lililokuwa na makaazi yake jijini Dar es salaam.

Sehemu ya marafiki wa karibu wa Jah Kimbute wakiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam Ijumaa jioni kuuaga mwili wa marehemu kabla ya kupelekwa Tanga kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika Jumamosi Septemba 22, 2018  (picha kwa hisani ya Michuzi blog)


Saturday, September 02, 2017

Burian Anatolia Nseka

BURIAN ANATOLIA NSEKA KAPUMZIKE KWA AMANI MAMA YETU
Mama Anatolia Nseka enzi za uhai wake

Saturday, July 22, 2017

Msiba wa Prof. Henslay Kabisama USA

WaTanzania nchini Marekani wanaomboleza msiba wa Profesa Henslay Kabisama aliyefariki huko California mwishoni mwa mwezi June
Mjane wa Marehemu pamoja na wadau kadhaa waliungana na Mubelwa Bandio katika kipindi cha NJE-NDANI kuongelea mipango ya mazishi ilipofikia sasa.
Unaweza kushiriki kusaidia gharama za kuusafirisha mwili kupitia akaunti HII ya GoFundME
Karibu uwasikilize

Wednesday, May 31, 2017

Mama Bishanga Amlilia Ivan X - Mume wa Zari

Pichani ni Mama Bishanga  aka Mrs. Marolen
MAMA BISHANGA AMLILIA IVAN X HUSBAND WA ZARI
Nimesikitishwa sana na kifo cha Ivan, ni mapema sana kwa yeye kuondoka duniani kuacha watoto wadogo sana, wanahitaji sana uwepo wa baba na mama, lakini Mungu ni Mwema amependezwa nae kuwa karibu yake mbinguni.
Zari binti yetu pole sana kwa pigo hili kubwa lisilozibika kwa wepesi, Mungu akutie nguvu. Wewe ni mmoja kati ya mabinti wachache walio na msimamo imara kimaisha, wasioyumba, wanaojitegemea zaidi kimaisha kwa kufanya biashara na shughuli mbalimbali kujipatia kipato, usieyumbishwa na mapito ya maisha ya dunia kirahisi. Naweza kusema nimekufahamu baada ya kuwa na mpenzi wako Diamond, umeonyesha msimamo na uimara wako ambao ni ushahidi mzuri kuwa utawatunza wanao watatu ambao sasa wako mikononi mwako forever. Usikate tamaa wengi tumepitia uliyopitia, kuvunjika kwa ndoa na kufiwa na wenzetu na kubakia na watoto, yalinikuta mimi binafsi hayo sikujua ada, nauli, kusomesha watoto  hadi mwenzangu alipofariki mwaka 1994 nikiwa Idara ya elimu ya juu na mshahara wa ualimu, na watoto kurudi kwangu, hapo ndio niliona jinsi Mungu huongeza baraka zake, na jinsi ukoo wa Kamota ulivyosimama nami kulea watoto. Nawewe daima muweke Mungu mbele mambo yatakuwa mazuri, hasa ukizingatia ulishajiimarisha na baba watoto wako amewaacha vizuri, Mungu atakuongezea na kukutia furaha ya maisha ya familia yako, na bila kusahau kuwa Diamond yuko pemebeni yako, tabasamu lake linatosha kukuongezea amani na nguvu ya maisha na kilo za uzito wa mwili confidence! Diamond amelelewa vizuri sana na mama yake na yuko wazi katika penzi lenu, sasa ni wakati wa kushikamana kikamilfu kupeana raha na amani na kuijenga familia yenu .
Kila la heri Zari, huenda tukaonana JHB maana sehemu ya maisha yangu ni JHB kwa mume wangu Orange Grove na Alexander township!
GOD BLESS YOU AND YOUR FAMILY ZARI
MAMA BISHANGA / MRS MAROLEN
CLEVELAND. OHIO

Saturday, September 17, 2016

Sala ya Kumuaga Marehemu Aisha Rupia Boston Leo

Sala ya kumuaga marehemu Aisha Rupia (39) itakuwa leo jumamosi 9/17/16 saa kumi jioni (4:00pm) huko Hurley Funeral Home, 134 Main St., Randolph, MA 02368.

Baada ya Sala, watu watajumika  kwenye Ukumbi wa VFW, saa kumi na mbili jioni (6:00PM). Anwani mi, Lt. John D. Crawford Veterans Asscociation, 10 Highland Avenue, Randolph, MA 02368.

Mwili wa marehemu Aisha utazikwa Louisiana wiki ijayo.

Wednesday, September 07, 2016

Mama Bishanga na Wadogo Zake Wafiwa na Mama Yao

MAMA BISHANGA NA WADOGO ZAKE WAFIWA NA MAMA YAO

         MWALIMU AGNES NDEMBO HATIA
Watoto wa marehemu mzee Isaya Innocent Hatia tumempoteza mpendwa mama
yetu mpendwa Mwalimu Agnes Ndembo Hatia kilichotokea hospitali ya Regency
 jana jumamamosi mchana. Mama yetu alikuwa nguzo pekee iliobakia nasi baada
ya kufariki baba yetu Mzee Isaya Innocent Hatia mwaka 2011. Tunamshukuru
Mungu sana kwa upendo wake kwa mama yetu aliempa nguvu ya kuishi miaka
tisini na sasa amempenda zaid mama yetu, bibi yetu na amempumzisha usingizi
wa milele na milele Ameni
Mwalimu Agnes Ndembo Hatia amefundisha watu wengi sana darasa la kwanza
tangia miaka ya hamsini hadi alipostaafu Tabora, Uhuru shule yamsingi.
Mama, ametuacha watoto wake Christina wa USA, Geofrey wa Namibia, Mwl
Mark Hatia wa Tambaza shule ya secondary, Bernadetta wa Dar, Isaya wa Finland,
Costancia wa Kibaha, na Oscar mdogo wetu wa mwisho. Ameacha wajukuu, na
vitukuu wengi ambao ni watoto na wajukuu zetu sisi watoto wake pamoja na dada
zetu marehemu Joyce Hatia na Mwalimu Cecilia Hatia. Picha zinaonyesha
mama Hatia mwaka 1966 akiwa na Constacia ambae picha yake pembeni ni Costancia
alivyo sasa, na zingine ni mama na wanae wajukuu na vitukuu
Kwa taarifa za maandalizi na ratiba piga simu zifuatazo. 0653 763 201 Kilian Kamota,
0755 333 948 Dick Hatia, 0788 627 430 Ibra Yunus, na 0763 833 893 Solmon.
 BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA. TUMSIFU YESU KRISTO: AMEN
 

Saturday, February 27, 2016

Taarifa Zaidi Kuhusu Msiba wa Dada Jessie Chiume USA

The Late Jessie Chiume (1960-2016)
Jumuiya ya Watanzania New York pamoja na familia ya Marehemu Mzee Kanyama Chiume inasikitika kuwataarifu Msiba wa Dada yetu mpenzi Jessie Wayasa Chiume (maarufu kama Da Mgeni) uliotokea ghafla asubuhi ya Jumatano February 24/2016 kwa ajali ya gari huko Mt. Vernon, NY. 


Jumuiya  ya Watanzania wa New York tunasisitiza ushirikiano katika kufanikisha Msiba huu mzito. Tuungane kuwafariji wanafamilia pamoja na kutoa rambirambi zitakazosaidia gharama za kumpumzisha Dada yetu kama ilivyo desturi yetu. 


Leo hii Ijumaa familia itaendelea kuwapo 44 Fleetwood Ave, Apt 3B, Mt Vernon NY 10552). Kuanzia kesho Jumamosi February 27 msiba utakwenda Poconos, PA nyumbani kwa Kaka mkubwa wa marehemu, Ndugu Michael Kwacha Chiume 
(Address : 359 Saunders Drive,Bushkill,
PA,18324) 
ambako ndipo pia alipo Mama Mzazi wa Marehemu hadi hapo taarifa zaidi za lini na wapi taratibu za mwisho zitakapoelekezwa.


Link ya kutoa rambirambi ni : 


Kwa taarifa zaidi wasiliana na:


Michael Chiume:#  646-662-6999
Chris Lutinwa :# 614-592-6231
Nathan Chiume:#  646-552-6347



Dada Jessie atakumbukwa na wengi kwa upole, ukarimu, ucheshi na mapenzi yake kwa Watanzania na wote waliobahatika kumjua. Da Jessie ametuachia pengo kubwa mno. Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema Peponi. AMEEN.
Mungu ametoa, Mungu ametwaa. 

R.I.P Jessica Chiume. We love you, we will miss you.

Saturday, October 24, 2015

2,177 Dead in Hajj Stampede including 20 Tanzanians

   DUBAI, United Arab Emirates (AP) - The crush and stampede that struck the hajj last month in Saudi Arabia killed at least 2,177 pilgrims, a new Associated Press tally showed Monday, after officials in the kingdom met to discuss the tragedy.

   The toll keeps rising from the Sept. 24 disaster outside Mecca as individual countries identify bodies and work to determine the whereabouts of hundreds of pilgrims still missing. The official Saudi toll of 769 people killed and 934 injured has not changed since Sept. 26, and officials have yet to address the discrepancy.

   Crown Prince Mohammed bin Naif bin Abdul Aziz, who is also the kingdom's interior minister, oversaw a meeting late Sunday about the disaster in Mina, according to the official Saudi Press Agency. The agency's report did not mention any official response to the rising death toll.

   "The crown prince was reassured on the progress of the investigations," the SPA report said. "He directed the committee's members to continue their efforts to find the causes of the accident, praying to Allah Almighty to accept the martyrs and wishing the injured a speedy recovery."

   King Salman ordered the investigation into the disaster, the deadliest in the history of the annual pilgrimage. It came after a crane collapse in Mecca earlier that month killed 111 worshippers, and the twin disasters marred the first hajj to be overseen by the king since he ascended to the throne at the start of this year.
Hajj Pilgrims

   The Saudi king holds the title of "Custodian of the Two Holy Mosques," and the monarchy's supervision of the hajj is a source of great prestige in the Muslim world. Riyadh has rejected a suggestion by Shiite power Iran, its main regional rival, to have an independent body take over planning and administering the five-day hajj pilgrimage, which is required of all able-bodied Muslims once in their lifetimes.

   Iran has repeatedly blamed the disaster on the Saudi royal family, accusing it of mismanagement and of covering up the real death toll, which Tehran says exceeds 4,700, without providing evidence.

   "The lying and hypercritical bodies, which claim to (be promoting) human rights, as well as the Western governments, which sometimes make great fuss over the death of a single person, remained dead silent in this incident in favor of their allied government," Iran's Supreme Leader Ayatollah Ali Khamenei said Monday, according to a transcript on his website.

Bodies of Hajj Stampede Victims
   "If they were sincere, these self-proclaimed advocates of human rights should have demanded accountability, compensation, guarantee for non-recurrence and punishment for the perpetrators of this catastrophe."

   Iran and Saudi Arabia are deeply divided on a host of regional issues and back opposite sides in the wars in Syria and Yemen, where a Saudi-led coalition has been at war with Iran-backed Shiite rebels, known as Houthis, since March.

   Saudi Arabia has meanwhile been targeted in gun and bomb attacks by an affiliate of the extremist Islamic State group, which holds a third of Iraq and Syria in its self-declared "caliphate." Like al-Qaida before it, the IS group views the Saudi royal family as illegitimate because of alleged corruption and its alliance with the United States.

   The AP count of the dead from the Mina crush and stampede comes from state media reports and officials' comments from 30 of the over 180 countries that sent citizens to the hajj.

   Iran leads all the affected countries, saying it had 465 pilgrims killed. Many of the dead also came from Africa. Mali said it lost 254 people, while Nigeria lost 199, Cameroon lost 76, Niger lost 72, Senegal lost 61, and Ivory Coast and Benin both lost 52.

   Others include Egypt with 182, Bangladesh with 137, Indonesia with 126, India with 116, Pakistan with 102, Ethiopia with 47, Chad with 43, Morocco with 36, Algeria with 33, Sudan with 30, Burkina Faso with 22, Tanzania with 20, Somalia with 10, Kenya with eight, Ghana and Turkey with seven, Myanmar and Libya with six, China with four, Afghanistan with two and Jordan and Malaysia with one.

   The previous deadliest-ever incident at hajj was a 1990 stampede that killed 1,426 people.

Friday, October 16, 2015

Tanzia - Mh. Deo Filikunjombe na Captain William Silaa


RIP Mbunge wetu wa Ludewa, Mh. Deo Filikunjombe. Doh! Nimepokea habari za msiba kwa masikitiko makubwa.  Poleni wanakunyumba.

Mwenyezi Mungu alaze roho za marehemu mahala pema mbinguni. Amen.

Wednesday, September 30, 2015

Tanzia - Mama Betisheba Ketangenyi

Bettisheba Pole Ketang'enyi enzi ya uhai wake

Tunasikitika kutangaza kifo cha mama Betisheba Ketangenyi, mama yake Yvonne Matinyi, Felicia Simms, Fredderek Ketangenyi pia ni Dada yake na Rossie Musika, Neema Musika, Daudi Musika, Sijaona Musika kilichotekea 9/30/15 katika hospitali ya NIH Maryland mipango ya kusafiri mwili wa marehemu inaendelea kwa mdogo wa marehemu Daudi Musika
3819 Gateway terrace Burtonsville MD 20866
Unaweza kuwasiliana
Rossie Musika 240 408 2693
Neema Musika 571 991 9819
Specioser Musika 571332 2215
Sijaona Musika 202 487 8412

Sunday, July 12, 2015

Mzee Ojwang Afariki Dunia!


The Late Benson Wanjau aka Mzee Ojwang
Muigizaji maarufu wa kipindi cha runinga cha "Vitimbi" Benson Wanjau aka
"Mzee Ojwang" ameaga dunia.
Mzee Ojwang ameaga dunia muda mchache uliopita katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta mjini Nairobi Kenya.

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Nairobi, Kenya: Kenyan actor Benson Wanjau alias Mzee Ojwang died Sunday evening at the Kenyatta National Hospital where he had been admitted.
Read more at: http://www.standardmedia.co.ke/article/2000168994/end-of-an-era-mzee-ojwang-passes-on
Nairobi, Kenya: Kenyan actor Benson Wanjau alias Mzee Ojwang died Sunday evening at the Kenyatta National Hospital where he had been admitted.
Read more at: http://www.standardmedia.co.ke/article/2000168994/end-of-an-era-mzee-ojwang-passes-on
Nairobi, Kenya: Kenyan actor Benson Wanjau alias Mzee Ojwang died Sunday evening at the Kenyatta National Hospital where he had been admitted.
Read more at: http://www.standardmedia.co.ke/article/2000168994/end-of-an-era-mzee-ojwang-passes-on

Saturday, June 20, 2015

Tanzia - Florence Dyauli, Mtangazaji wa TBC

 Nimesikitika sana kusika habari ya kifo cha Dada Florence Dyauli.  Nilifanya kazi naye nilipokuwa Practical Training RTD nikiwa mwanafunzi Tanzania School of Journalism. Pia tulikuwa pamoja kwenye shughuli za TAMWA.  Rest in peace Dada Florence.

*************************************************

KUTOKA LUKWANGULE BLOG:


The Late Florence Dyauli (1961-2015)

MWANDISHI wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwa upande wa Televisheni Florence Dyauli amefariki dunia usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Rabininsia memorial iliyopo jijini Dar es salaam alipokuwa amelazwa kutokana kusumbuliwa na maradhi ya Nimonia

Taarifa iliyotolewa jana na ofisi za TBC ilisema kuwa marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa Nimonia na alilazwa kwa ajili ya matibabu hadi jana usiku mauti ilipomfika.

Taratibu za mazishi zilikuwa bado hazijafanyika na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo ya Rabininsia ukisubiria taratibu za mazishi kutoka kwa ndugu wa familia.

Florence alizaliwa Julai 27, 1961 ambapo alipata elimu yake ya msingi kuanzia 1968 hadi mwaka 1975 katika shule ya Msingi Chang’ombe iliyopo jijini Dar es salaam.

Alifanikiwa kujiunga na elimu ya Sekondari katika shule ya Kisutu girls kati ya mwaka 1976 hadi 1979. Baadae alijiunga na chuo cha Tabora secretarial College kuanzia mwaka 1980 hadi 1981 na kujipatia mafunzo ya cheti cha ukarani.

Mnamo mwaka 1986 hadi 1988 alijiunga na chuo cha uandishi wa habari kwa ngazi ya stashahada ya uandishi wa habari.

Aliniajiriwa kama mwandishi wa habari msaidizi katika kituo cha Radio Tanzania Dar es salaam kuanzia 1982 hadi Novemba 1999.

Kisha mwaka 1994 hadi Novemba 1999 alikuwa Shift Editor .

Hadi mauti inamkuta, marehemu alikuwa mwandishi wa habari daraja la kwanza kwa upande wa Televisheni ya Taifa TBC.

Friday, April 24, 2015

Memorial Service for Dr. Aleck H. Che-Mponda - Sunday April 26, 2015 in Chelsea, MA

There will be a Memorial Service for my father, this Sunday at our Church in Chelsea. Please see below:

This is a friendly reminder about a memorial service for Dr. Aleck Che-Mponda . Service will be held at 3:00 p.m. Sunday, April 26 at the International Gospel Church located at 85 Crescent Avenue Chelsea, MA 02150.

************************************

Misa ya Kumbuka Dr. Aleck H. Che-Mponda itafanyika katika Kanisa la International Gospel Church siku ya jumapili, Aprili 26, 2015.  Misa itafanyika saa 9 mchana. Anwani ni  85 Crescent Avenue, Chelsea, MA, 02150.

The Late Dr. Aleck H. Che-Mponda 1935-2015