Showing posts with label Nauli. Show all posts
Showing posts with label Nauli. Show all posts

Wednesday, July 24, 2013

Pesa Ina Majina Mengi



PESA INA MAJINA MENGI. Ona;

Kwenye ibada inaitwa Sadaka au Zaka,

Msibani inaitwa Rambirambi,

Shuleni inaitwa Ada au Karo,

Kwenye Vyombo Vya Usafiri inaitwa Nauli,

Ukinunulia Haki inaitwa Rushwa,

Kumdhaminia Mtu Mahakamani inaitwa Dhamana,

Pesa ya uchumba inaitwa POSA,

Pesa ya itolewayo mtu akabidhiwe mke inaitwa MAHARI.

Je PESA inayohongwa kwa mpenzi inaitwaje?

 Jibu tafadhali.

Friday, August 01, 2008

Nauli Mpya Bongo

Nilipoanza Form One 1977, nauli ilikuwa sumni (senti hamsini) kwa mwanafunzi. Tena hata wikiendi na jioni uliweza kulipa sumni, mradi una kitambulisho. Mnakumbuka mabasi ya UDA? Basi kila mwezi tulikuwa tunaenda Kurasini Depot ya UDA kununua 'monthly pass' nadhani ilikuwa kama shilingi 20/-! Walifuta pass hizo 1979.

Nilivyomaliza mwaka 1980, nauli ilikuwa shilingi 1/-. 1984 nikiwa nafanya kazi Daily News mabasi binafsi yaliingia. Nauli ulikuwa shilingi 5/- (dala) Ndo jina daladala. Tuliona hiyo dala nyingi lakini ulikuwa usafiri mzuri kuliko wa UDA. Miaka imeenda na sasa nauli ni shs. 500/- (one way). )Of course miaka ya 70 hiyo dola ilikuwa eight shillings to the dollar. Kwa sasa ni 1 dollar -1,200/-.)

Sasa jamani, matatizo ni yale yale, Mtu unapata mshahara lakini haitoshi hizo bili za mwezi. Na siki hizi kila kitu ni kulipia, shule, hospitali. Watu wanakoma ingawa serikali ilipandisha kima cha chini mwaka jana. Mambo ni yale yale maana hata wakati ule mshahara ulikuwa hautoshi. Miradi ndo ziliokoa watu, kuku, ice cream.

Nimeona wanafunzi wamechachamaa huko Dar Leo. Lakini jamani, Bongo kuna mabadiliko. Enzi za Mwalimu mnadhani watu wangeweza kuandamana hivi hivi na mabango?! Watu fulani wangezolewa halafu ungewaona wanarudi 'kiiimya" hawana neno tena. Nyie wengine mngeshulikiwa vizuri na FFU. Ndo tulikuwa tunsema, "kamchape class".

Serikali itazame upya hi suala la nauli. Dar mji mkubwa, watu kutembea miendo si mchezo. Na familia enye watoto wengi wanaosoma si ni balaa kwao!

Miaka mingi tumekuwa tunasema 'Tunataka hali bora ya maisha kwa kila MTanzania'. Sijui hali itakuwa bora lini.


*******************************************************************************

Nauli Mpya ni Kilio

2008-08-01

Na Sharon Sauwa, Jijini

Hatimaye kile kiama cha nauli mpya kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kimeanza leo asubuhi na kuwatoa chozi abiria kibao hasa wale akina kwangu pakavu tia mchuzi.

Alasiri ilipovinjari maeneo kadhaa ya Jiji imeshuhudia abiria kadhaa wakiwalilia makonda wa mabasi kuwaruhusu japo kwa leo kulipa nauli ya zamani kwa kile walichodai kuwa hawakuwa na pesa zaidi.

``We vipi, mlishatangaziwa kwamba nauli mpya inaanza leo...kama huna mia nne yangu, anza...dereva ondoa gari, hakuna kichwa hapa`` konda mmoja wa basi la kutoka Mbezi-Mwenge alisikika akimwambia abiria aliyekuwa akimlilia apokee nauli ya zamani. Kutokana na kupanda kwa nauli, baadhi ya abiria walionekana wakitembea kwa mguu huku wengine wakitokwa na majasho kutokana na kupiga kwata umbali mrefu.

``Tangu saa 11:30, niko njiani. Mshahara wenyewe ndio huo...nikitoa kodi ya nyumba, chakula, ada ya watoto, umeme, nauli hii ya Sh. 600 kwa kila ruti nitaipata wapi? Nimeona nianze mapema kabisa kutembea,`` mwanamama mmoja aliyekuwa akitokea Boko kwenda Mwenge ameliambia Alasiri.

Kwa upande wa wanafunzi, wengi walionekana wakiwa wamejazana vituoni kutokana na makonda kuwazuia kupanda mabasi hadi waonyeshe nauli yao mpya. ``Tulidandia malori la sivyo tusingekwenda shule kabisa,`` denti mmoja kutoka Tabata anayesoma maeneo ya Mbezi amesema.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Usafiri, Nchi Kavu na Majini, SUMATRA, nauli mpya ilitakiwa kuanza kutumika leo ambapo watu wazima wanatakiwa kulipa Sh. 300 kwa safari fupi ambazo hazizidi kilomita kumi wakati wale wa umbali wa kilomita kumi na tano wanatakiwa kulipa nauli ya Sh. 400 na wale wa kilomita 25, nauli yao ni Sh. 500.

Kwa upande wa ruti za kulala usingizi, yaani zile za umbali wa kilomita 30, wanatakiwa kulipa nauli ya Sh. 600 wakati wanafunzi nauli yao imepanda kutoka Sh. 50 hadi Sh. 100. Habari zilizotufikia wakati tukienda mitamboni zinasema kuwa wanafunzi wa shule mbalimbali Jijijini Dar es Salaam wameitisha mgomo mkubwa kupinga nauli mpya za daladala.

Imedaiwa kuwa wametinga ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Kandoro kumweleza tatizo hilo.

Sunday, July 20, 2008

Mnao lilia kuja Dar Shauri Lenu! - Father Kidevu

Mnao lilia kuja Dar shauri lenu!

Kutoka Father Kidevu Blog

Na Father Kidevu

YALAAAH! Jamanai mjini sasa hapafai na chonde chonde mlio huko mashambani wala msililie kuja jijini Dar es Salaama maana kuna tabu na karaha siku hizi.Nimelia maana sasa ninaona tunakokwenda kwa hizi nauli za daladala na mabasi ya kwenda huko kwa babu na bibi ni hatari.

Wajameni mimi leo nalia na na nimeamua kuropoka niwezavyo juu ya upandaji huu wa nauli hapa mjini na za kwenda makwetu, walahi ni zambi kabisa. sababu naambiwa eti mafuta na gharama za uendeshaji zimepanda, Haya mi mnyonge sina la kusema pandisheni tu hata misosi nayo hivi sasa sii ipo juu kisa mafuta.

Juzi hapa muuza madafu na machungwa wananiambia sasa dafu ni 300 badala ya 250 kisa eti mafuta. Mafuta haya hadi lini? SUMU ya MATRA nayo hiyo imekubali kutuua kwa kupanda kwa mafuta. haya tuendelee.

Ndio! Hatari sana, eti SUMATRA imeridhia baadhi ya nauli za mikoani kupanda, awali nilipo sikia ni nilihisi sasa maskani huko kwa babu watanisahau zaidi maana huu mwaka wa nne sijatia tumu bado naichanga nauri na leo huyu Izraeli Mwakilasa wa hiyo Mammlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini ameongeza tena.Kha!

Nitaendaje kwetu Kigoma kwa basi maana bila ya kuwa na shilingi 200 elfu/= sijaenda na kurudi kwangu Vingunguti. Nauri tu ya kwenda ni sh 84,elfu nikichanganya na msosi inaweza fika 100 elfu na zaidi.Lakini usishtuke hiyo ni ya ndugu zangu walio soma na wakabahatika kufanya kazi BOT au katika mashirika na taasisi kubwa kama Mabenki na kule TRA ambao hupenda kupanda mabasi yaliyo na raha kamili.

Mimi na mwenzangu hapo ambao hufanya kazi katika NGOs za kuzoa taka hapa mjini na kuropoka ropoka kama huku nauri yetu leo imepanda kutoka sh 40,500 hadi 49,000 hadi huko Kigoma.Nauri hii jamani inatugombanisha na kututenganisha na familia zetu.

Akina Masawe, Mushi, Manka, Kekuu, Mboro, Lymo, Mgonja, Mbaga, Msuya, Nendiwe, Nakiete na hata wewe Naelijwa kwenda kwenu kama mpo hapa Disim mtalipa sh 31,000 kama mmesoma na mnamiliki maduka makubwa pale Kariakoo na mnamabucha ya kule Koregwe ya kuuza Astaghafilula.

Ofkozi nitatumia ka eropleni kwenda kwetu Kyaka na hata kwa my frendi Prof. Rwegoshora wa pale Chuo kikuu cha Univasiti, lakini siwezi lipa 75,000 hadi Bukoba.Kaka Kyaruzi, nawewe Rwebangira mmesoma au ndio akina mimi?

Haya wewe Bishanga hukusoma lipa 44,000 tu hadi kwenu Kanyigo.Hahahahaaa! Yeto Msangi, unastuka nini kwani nani kakuita kuja hapa mjini uache mikahawa yako na makilaume kule kwenu, Masawe unalia sana, kama pato lako la chini panda mabasi yale yaliyo na Chesisi za malori ambazo nauri zake sasa ni 18,000 badala ya 14,900.

Akina Lukwangule, Msimbe, Mloka, Malonga, Chamhene, Mwenda na wewe Chuma mnaotoka hapo Matombo, Mgeta, Mlali na kule Gairo hadi Ifakara nauri hadi pale Msavu kituo Kikubwa Mjomba sasa uwe na buku sita (6,000) na sio 5,000 ya zamani.Be Mwakitosi, Se-Fute, Mwatagalile, kule kwetu Lilinga ah! Iringa, sasa kwenda kusalimia home kupata Ulanzi kidogo na tule tumboga twetu tudogo ni sh 29,000 taslim kama unataka kuangalia na video kama hutaki panda Upendo ulipe 17,000.

Wewe nani anasema kwa Akina Somo kule Ntwara na Lindi ni Mbali? Acha habari hiyo kule ukipanda basi swafi Video na Maliwato humo humo utalipa 25,00 tu hadi Lindi na kama utashukia Ntwara lipa 29,000.Jamani wewe bado unataka kuja bandari ya Salama tu, kwa kazi gani kubwa unayotaka huku, kuuza maji au mambo flani…. Tulia huko huko unaweza kushindwa hjata kurudi bush bure maana wengine kwa kuja na malori ama mabehewa ya Ng’ombe na mbio zamwenge ndio wenyewe halafu kurudi soo.Kuna watu wanacheka hapa!

Eti aende huko sijui Kigoma,Moshi na Iringa kuna nini ilhali babu yake mwenyewe kazaliwa Taasisi ya Saratani Ocean Road, nauri ya kuja kutoka Mwenge au Kimara ni 300 mara mbili hapo 600 umeliwa.Kwataarifa yako sasa nauri zote za hapa town zimepanda. Tobah!

Ndio Sekilasa wa SUMATRA amesema hivi sasa ukitoka Mbezi mwisho hadi Kariakoo au Posta utalipa Sh 600, Mwenge Posta sasa utalipa 500 na nauri ya chini sasa ni 300 hakuna kulia lia.Hapo sasa utajiuliza kwa mshahara gani niupatao nauri 1200 kwa siku?

Ebwana ninawazo sasa akili zikiniruka tu nahamisha watz wote weupe pale NHC za Posta na Kariakoo wakaishi Kimara naTegeta halafu WaTz weusi tuhamie zile nyumba za mjini amabazo hata kodi yake ni nafuu.

Watahama tu wao si, wanavipato vikubwa unafikiri watashindwa kukaa nje ya mji na magari wanayo.Waajiri sasa muangalie upya sakata hili la nauri kupanda na gharama nyinge za maisha, muwahurumie hao wanao wazalishia kwa kuwapa nyongeza kama ya SUMATRA.-------------------------------------------------------------------------------------------------

Wasomaji wa gazeti tando hili kuanzia sasa nitakuwa naweka maneno kama haya hapa chini na yeyote mwenye maoni au ushauri aniandike mrokim@gmail.com au sms +255373999.