Showing posts with label Vitabu. Show all posts
Showing posts with label Vitabu. Show all posts
Thursday, April 05, 2012
Sandra Mushi Akusanya Vitabu Kwa Ajili ya Watoto Muhimbili
Muhimbili Hospital Childrens Book Collection
G’afternoon happy people!!
Thank you so so so so so so much for the books, toys, exercise books, colouring pencils. Crayons etc that we collected for MOI kids – and which I dropped today.
I am so proud and happy to say that we collected about 6 boxes. Thank you ever so much!
I have taken some pictures of what was collected ...
I was asked to go see the kids – and maybe take pictures of them too – but I didn’t have the heart to. So I am sorry that I didn’t take pictures of the kids.
Sarah Clittero and the Novel Idea team, thank you and God bless you! This should not be the end, but only the beginning – there is so much more that we can do and that is needed from us. Pamoja tunaweza na pamoja tutafika.
Thank you all!
Regards,
SANDRA MUSHI
Saturday, March 31, 2012
Walimu Zimbabwe Wauza Vitabu Viliyotolewa Kama Msaada
Umasakini jamani! Leo, kuna habari kuwa vitabu viliyotolewa na UNICEF kwa ajili ya watoto wa shule Zimbabwe, zimeuzwa badala ya kupewa wanafunzi. Aibu kweli!
****************************************************
HARARE, Zimbabwe (AP) - Zimbabwe's education ministry says it is investigating into how school text books donated by the U.N. children's agency wind up in the hands of bookstores and street vendors.
The United Nations Children's Fund has supplied 22 million books since late 2010 after a decade of economic meltdown that left many schools without teaching materials. In some schools, scores of pupils shared a single book.
Education Minister David Coltart said Friday culprits behind the theft of books - officially the property of government schools - will be prosecuted
The books, stamped and identifiable, sell for up to $10 on the street. A main teachers union says teachers may be stealing to make up for poor salaries.
****************************************************
HARARE, Zimbabwe (AP) - Zimbabwe's education ministry says it is investigating into how school text books donated by the U.N. children's agency wind up in the hands of bookstores and street vendors.
The United Nations Children's Fund has supplied 22 million books since late 2010 after a decade of economic meltdown that left many schools without teaching materials. In some schools, scores of pupils shared a single book.
Education Minister David Coltart said Friday culprits behind the theft of books - officially the property of government schools - will be prosecuted
The books, stamped and identifiable, sell for up to $10 on the street. A main teachers union says teachers may be stealing to make up for poor salaries.
Wednesday, October 07, 2009
Vitabu Kwa Ajili ya Shule za Afrika - Changamkeni!
Sent: Wednesday, October 7, 2009 2:04:29 AM
Subject: Anybody know of an African school that needs books: queryDate:
Tuesday, 6 October 2009From: Cynthia Brantley <http://us.mc397.mail.yahoo.com/mc/compose?to=clbrantley@ucdavis.edu> I am retiring and leaving my office by October 30. Does anyone know of an African school or university that needs books? I would be happy to learn of any.
Cynthia Brantley
**********************************************************************************
Subject: Anybody know of an African school that needs books: queryDate:
Tuesday, 6 October 2009
From: Richard Seltzer <http://us.mc397.mail.yahoo.com/mc/compose?to=seltzer@samizdat.com>
I have many collections of the classics http://samizdat.stores.yahoo.net/ and would like to donate some toAfrican schools that could make good use of them.
Best wishes.Richard
Subject: Anybody know of an African school that needs books: queryDate:
Tuesday, 6 October 2009From: Cynthia Brantley <http://us.mc397.mail.yahoo.com/mc/compose?to=clbrantley@ucdavis.edu> I am retiring and leaving my office by October 30. Does anyone know of an African school or university that needs books? I would be happy to learn of any.
Cynthia Brantley
**********************************************************************************
Subject: Anybody know of an African school that needs books: queryDate:
Tuesday, 6 October 2009
From: Richard Seltzer <http://us.mc397.mail.yahoo.com/mc/compose?to=seltzer@samizdat.com>
I have many collections of the classics http://samizdat.stores.yahoo.net/ and would like to donate some toAfrican schools that could make good use of them.
Best wishes.Richard
Wednesday, October 22, 2008
Ya Kale Dhahabu

Wadau, nilopokuwa nasoma Zanaki Girls 1977, amri ilitoka ya kuchoma vitabu vyote vilvyoachwa na Aga Khan Girls. Zanaki ilikuwa Aga Khan Girls kabla ya kutaifishwa. Vitabu vilikuwa vingi. Kulikuwa na vitabu vya hesabu, literature, Shakespeare, English na masomo mengi. Nilikuwa Form One na walikuwa wanavichoma kwa vile vilikuwa na kasumba! Tuliletewa vitabu vya Tanzania curriculum, hivyo literature badala ya Shakespeare na wengine tulisoma African writer's series. Ten a wakati tunachoma hivyo vitabu, kupata hata za kiswahili ilikuwa shida kidogo. Hizo zilizochomwa zingetusaidia anagalau.
Mnakumbuka enzi zile, eti ukiongea kiingereza unatukanwa eti una kasumba! Ilikuwa enzi za kukuza Kiswahili kuwa lugha ya taifa. Matokeo yake watu waliokuwa wanajua kiingereza walifanya kuwa hawajui! Matokeo yake wabongo wengi wanaongea kiingereza kibovu kwa vile walifundishwa na walimu wasioelewa lugha vizuri.
Dada Subi ameniletea habari za kusikitisha. Ni tukio uliotokea alipoenda kwao. Alikuta vitabu vya kiswahili vimechomwa! Khaa! Jamani, kwa nini vitabu vichomwe??? Si zina gharama. Yaani hazina faida tena? Hata hapa Marekani hawachomi vitabu vinapelekwa second hand store au zinasafirishwa nchi za nje.
*******************************************************************
Imeandikwa na Dada Subi:
Ya kale dhahabu!
Mimi nilipokuwa Tanzania majuzi niliwenda hadi shule yangu ya Msingi kumwomba Mwalimu Mkuu vitabu vya zamani, hadithi niliyopewa nilichoka. Ati Waalimu wakuu wa shule za msingi wote walipewa amri toka kwa Waziri wavichome vitabu vya zamani ili kutoa nafasi kwa vitabu vipya. Huyo waziri mbumbumbu sijui alitamka akiwa amelewa buza ama gongo gani. Kumbuka zile stoo za vitabu zilivyokuwa zimejaa vitabu, vyote vikapigwa kiberiti. Najiuliza, kwa nini hakuwepo mjanja mmoja akahifadhi nakala moja moja?
Nina imani atakuwepo mtu mmoja mmoja aliyeficha kimoja na mwingine kingine na siku moja tutaviona tena na vitauzwa kwa bei nzuri kweli. Nilipambana na maboksi ya vitabu vya Bibi na Mama kwa kuwa wao walikuwa Waalimu, wakanifahamisha kuwa sitafanikiwa kuvipata kwani wao walikuwa watiifu, hawakuchukua mali ya Shule/Serikali na kuihifadhi kama yao.
Kila mara huwa nakumbuka:
Juma na Roza. Someni kwa Furaha, hatua ya tatu.
Hadithi za Pazi na Jogoo alivyomning'iniza kichwa chini miguu juu, na ile hadithi ya Mwanamke aliyevalia hereni kubwa kisha akaenda sokoni kuuza bidhaa zake mara mbuzi wakapita wakarusha mguu ndani ya tundu la hereni nayo ikalikata sikio....
Unamkumbuka Kalumekenge alipokataa kwenda shule? Fimbo ikaambiwa imchape Kalumekenge ili Kalumekenge aende shule. Lakini fimbo ikakataa kumchapa Kalumekenge aliyekataa kwenda shule. Moto ukaambiwa uichome fimbo ili fimbo imchape Kalumekenge ili Kalumekenge aende shule. Lakini moto ukakataa kuichoma fimbo, iliyokataa kumchapa Kalumekenge, aliyekataa kwenda shule. Ndipo maji yakaambiwa yauzime moto, uliokataa kuichoma fimbo, iliyokataa kumchapa Kalumekenge, aliyekataa kwenda shule. Ndipo maji yaka kuuzima moto, moto ukaichoma fimbo, fimbo ikammchapa Kalumekenge, ndipo Kalumekenge akaenda shule.
Unawakumbuka Wagagagigikoko?
Unamkumbuka yule mtoto aliyetumwa kwenda kwa Bibi yake akacheza barabarani hadi simba akamla Bibi yake na kulala kitandani halafu yule mtoto alipofika akamwuliza, Bibi mbona masikio yako makubwa? Bibi akamjibu, ili niweze kukusikia vizuri. Akamwuliza tena, mbona macho yako makubwa? Akamjibu, ili niweze kukuona vizuri. Akamwuliza, mbona meno yako makubwa? Akamjibu, ili niweze kukutafuta vizuri. Ndipo akaiona miguu yake na simba akamrukia na kumla.....
Nikakumbuka na hadithi ya Usiku wa Mbalamwezi, na kabla ya hiyo ilikuwepo hadithi ya Muro na mifugo yake, halafu ilikuweko 'Leo ni Sikukuu' wachilia mbali ile hadithi ya mjukuu aliyekuwa anataka kushindana na babu yake kunywa chai lakini kumbe chai ni ya moto, basi babu yake akawa anatoa sababu ambazo zilikuwa zinaishia na neno 'fu' na kila aliposema 'fu' alipuliza chai 'fu fu fu'....
Mi nilikuwa nasoma na kurudia zile hadithi hadi nyumbani. Bibi kwa vile alikuwa Mwalimu, basi alikuwa akiazima kitabu kwa niaba yang nami nakisoma nyumbani na kukikabishgi ili kirudishwe kabla Ijumaa makusudi nisikose kuazimwa wiki inayofuata. Nilikuwa nasoma hadi mwisho na nyuma ya kitabu, jalada, kabisa nahakikisha nimesoma kujua kama kitabu kile kina chapa ya MTUU, TPS, Oxford, Longman ama Maximillian Publishing!
Unakumbuka hesabu zilivyokuwa zimepangika kwenye vitabu halafu pembeni zina picha zinazoendana na hisabu yenyewe?
Halafu somo la mwandiko nimemkumbuka mwalimu alikuwa anatufundisha kuumba herufi kwa wimbo, 'chirioooo cha, chirioooo cha....'
Eh jamani! Wametupa jongoo na mti wake! La haula la kwata!
Nasikitika sana mimi lakini najipa moyo kuwa ipo siku tutaviona tena vitabu vyenye hadithi na mafunzo murua...
Golden Days Are Gone? Aaaarrrrrrrgh!
Memories are made of this!
Subi
Mnakumbuka enzi zile, eti ukiongea kiingereza unatukanwa eti una kasumba! Ilikuwa enzi za kukuza Kiswahili kuwa lugha ya taifa. Matokeo yake watu waliokuwa wanajua kiingereza walifanya kuwa hawajui! Matokeo yake wabongo wengi wanaongea kiingereza kibovu kwa vile walifundishwa na walimu wasioelewa lugha vizuri.
Dada Subi ameniletea habari za kusikitisha. Ni tukio uliotokea alipoenda kwao. Alikuta vitabu vya kiswahili vimechomwa! Khaa! Jamani, kwa nini vitabu vichomwe??? Si zina gharama. Yaani hazina faida tena? Hata hapa Marekani hawachomi vitabu vinapelekwa second hand store au zinasafirishwa nchi za nje.
*******************************************************************
Imeandikwa na Dada Subi:
Ya kale dhahabu!
Mimi nilipokuwa Tanzania majuzi niliwenda hadi shule yangu ya Msingi kumwomba Mwalimu Mkuu vitabu vya zamani, hadithi niliyopewa nilichoka. Ati Waalimu wakuu wa shule za msingi wote walipewa amri toka kwa Waziri wavichome vitabu vya zamani ili kutoa nafasi kwa vitabu vipya. Huyo waziri mbumbumbu sijui alitamka akiwa amelewa buza ama gongo gani. Kumbuka zile stoo za vitabu zilivyokuwa zimejaa vitabu, vyote vikapigwa kiberiti. Najiuliza, kwa nini hakuwepo mjanja mmoja akahifadhi nakala moja moja?
Nina imani atakuwepo mtu mmoja mmoja aliyeficha kimoja na mwingine kingine na siku moja tutaviona tena na vitauzwa kwa bei nzuri kweli. Nilipambana na maboksi ya vitabu vya Bibi na Mama kwa kuwa wao walikuwa Waalimu, wakanifahamisha kuwa sitafanikiwa kuvipata kwani wao walikuwa watiifu, hawakuchukua mali ya Shule/Serikali na kuihifadhi kama yao.
Kila mara huwa nakumbuka:
Juma na Roza. Someni kwa Furaha, hatua ya tatu.
Hadithi za Pazi na Jogoo alivyomning'iniza kichwa chini miguu juu, na ile hadithi ya Mwanamke aliyevalia hereni kubwa kisha akaenda sokoni kuuza bidhaa zake mara mbuzi wakapita wakarusha mguu ndani ya tundu la hereni nayo ikalikata sikio....
Unamkumbuka Kalumekenge alipokataa kwenda shule? Fimbo ikaambiwa imchape Kalumekenge ili Kalumekenge aende shule. Lakini fimbo ikakataa kumchapa Kalumekenge aliyekataa kwenda shule. Moto ukaambiwa uichome fimbo ili fimbo imchape Kalumekenge ili Kalumekenge aende shule. Lakini moto ukakataa kuichoma fimbo, iliyokataa kumchapa Kalumekenge, aliyekataa kwenda shule. Ndipo maji yakaambiwa yauzime moto, uliokataa kuichoma fimbo, iliyokataa kumchapa Kalumekenge, aliyekataa kwenda shule. Ndipo maji yaka kuuzima moto, moto ukaichoma fimbo, fimbo ikammchapa Kalumekenge, ndipo Kalumekenge akaenda shule.
Unawakumbuka Wagagagigikoko?
Unamkumbuka yule mtoto aliyetumwa kwenda kwa Bibi yake akacheza barabarani hadi simba akamla Bibi yake na kulala kitandani halafu yule mtoto alipofika akamwuliza, Bibi mbona masikio yako makubwa? Bibi akamjibu, ili niweze kukusikia vizuri. Akamwuliza tena, mbona macho yako makubwa? Akamjibu, ili niweze kukuona vizuri. Akamwuliza, mbona meno yako makubwa? Akamjibu, ili niweze kukutafuta vizuri. Ndipo akaiona miguu yake na simba akamrukia na kumla.....
Nikakumbuka na hadithi ya Usiku wa Mbalamwezi, na kabla ya hiyo ilikuwepo hadithi ya Muro na mifugo yake, halafu ilikuweko 'Leo ni Sikukuu' wachilia mbali ile hadithi ya mjukuu aliyekuwa anataka kushindana na babu yake kunywa chai lakini kumbe chai ni ya moto, basi babu yake akawa anatoa sababu ambazo zilikuwa zinaishia na neno 'fu' na kila aliposema 'fu' alipuliza chai 'fu fu fu'....
Mi nilikuwa nasoma na kurudia zile hadithi hadi nyumbani. Bibi kwa vile alikuwa Mwalimu, basi alikuwa akiazima kitabu kwa niaba yang nami nakisoma nyumbani na kukikabishgi ili kirudishwe kabla Ijumaa makusudi nisikose kuazimwa wiki inayofuata. Nilikuwa nasoma hadi mwisho na nyuma ya kitabu, jalada, kabisa nahakikisha nimesoma kujua kama kitabu kile kina chapa ya MTUU, TPS, Oxford, Longman ama Maximillian Publishing!
Unakumbuka hesabu zilivyokuwa zimepangika kwenye vitabu halafu pembeni zina picha zinazoendana na hisabu yenyewe?
Halafu somo la mwandiko nimemkumbuka mwalimu alikuwa anatufundisha kuumba herufi kwa wimbo, 'chirioooo cha, chirioooo cha....'
Eh jamani! Wametupa jongoo na mti wake! La haula la kwata!
Nasikitika sana mimi lakini najipa moyo kuwa ipo siku tutaviona tena vitabu vyenye hadithi na mafunzo murua...
Golden Days Are Gone? Aaaarrrrrrrgh!
Memories are made of this!
Subi
Subscribe to:
Comments (Atom)





