Showing posts with label Muhimbili. Show all posts
Showing posts with label Muhimbili. Show all posts

Saturday, July 22, 2017

SGA Security Comes to the Rescue of Abandoned Patients at MOI

In response to appeal in both mainstream and social media, the largest and oldest security company in the Tanzania, SGA Security, responded with donations. 

These were presented on 21st July 2017 to the management of Muhimbili Orthopaedic Institute(MOI) and received by the Director of Nursing – Ms. MF Kimaro. She expressed their gratitude to SGA for being the first to respond to the plight of the patients.  
 Security Group Africa Group (SGA),Managing Director, Eric Sambu (right) handing over donations worth 2.5m/- to the Nursing Director at the Bone Institute (Moi), Ms. Flora Kimaro during a special visit to patients.

The donations included foodstuff, sanitary items and wheel chairs, all valued at TZS.2.5 Million. The SGA Customer and Public Relations Manager, Ms. Aikande Makere, explained that it is their practice to support community initiatives, in line with their corporate social responsibility. 

SGA has health and safety core theme and that extends to the public. She explained that she heard the appeal and felt that they needed to chip in and called upon other institutions to follow suit. “The patients belong to all of us and we have to shoulder this responsibility, as a society, jointly”, she added.

Mr. Jumaa Tram Almasi, MOI’s Manager, Welfare& Public Relations Unit expressed gratitude to SGA Security for choosing their institution to make the donation. “As you might be aware, treatment of the destitute patients is costly and we cannot do it alone, that is, provision of both medical and social needs. 

We need support from Well-Wishers and Good Samaritans to support us”, he said. “Patients dumped by their relatives add a strain in the already overloaded health services. 

The support from SGA security is timely and a stitch in time. We kindly urge the rest to support us through their CSR Programs”, he added.


SGA Security Managing Director, Mr. Eric Sambu, explained that they have spent over TZS.55 million this year on CSR programs, with a few activities remaining before end of the year. He explained that being part of the society, they always decide on areas to provide support as a way of giving back to the public.

 He was there with the ambulance team and guards during the presentation. They visited the patients in wards to give them a word of encouragement.
Security Group Africa Group (SGA),Managing Director, Eric Sambu (right) handing over donations worth 2.5m/- to the Nursing Director at the Bone Institute (Moi), Ms. Flora Kimaro during a special visit to patients.

SGA Security was the first Private Security Company registered in Tanzania in 1984, as Group Four Security, following deregulation of the sector from Government control. Today, after more than 33 years of successful operations, SGA is the largest private security company in Tanzania, represented in every service area in the sector. Employing about 5,000 employees in Tanzania and over 18,500 in the region, SGA is one of the largest employers in the region.


Speaking during the presentation at MOI, the Managing Director, Mr. Eric Sambu, said that they aid to entrench corporate citizenship by playing bigger role in the society as they strive to continuously add value to their customers. 

SGA recently launched a new fleet of ultra-modern and fully-equipped armored vehicles to provide alarm response services and cash in transit services in the country. SGA provides a full spectrum of integrated security services, which ensures that its clients enjoy a cost-effective interfusion of manpower and technology, safeguarding their personal and business assets, wherever they may be located. “We are presently updating skillsets for all our employees to empower deliver our promises in line with our mission. 

The training cuts across all cadres and facilitators are from all sectors, including our disciplined forces.”, he added. In addition to donations like this, SGA conducts free awareness training to selected public to improves health and safety in the society. They recently completed such training to bodaboda riders that covered 230 riders. They also donated reflective jackets and helmets after the awareness training.
Mr. Sambu continued to explain that SGA is the largest provider of Cash in Transit and Cash Management services in Tanzania and the provider of choice for over 85 Banks and Financial Institutions in the East Africa region. Our large fleet of fully armoured CIT vehicles visit over 750 bank branches in Tanzania, safely moving tens of billions of shillings, millions of kilometres each year. 

All our Cash Management services are fully insured through reputable, internationally renowned insurers. Our expertise extends to the Diplomatic and NGO sectors with over 65 Embassies and Development Aid clients in the region. We understand the specific risk profile of these clients and have specifically trained staff for these.

Saturday, November 21, 2015

Fedha za Hafla ya Bunge Zinunue Vitanda Muhimbili: Rais Magufuli

Baada ya kulihutubia na kulizindua bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt JOHN POMBE MAGUFULI amehudhuria hafla fupi iliyoandaliwa kwa ajili ya wabunge katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma na kuagiza fedha zilizochangwa kwa ajili ya kugharamia hafla hiyo zipelekwe Katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kununulia vitanda vya wagonjwa.

Mheshimiwa Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa kuwa wadau mbalimbali wamechanga kiasi cha shilingi milioni 225 kwa ajili ya kugharamia hafla ya wabunge katika siku ya uzinduzi wa Bunge.

Dkt Magufuli amesema alipata taarifa za kuwepo kwa michango hiyo ya fedha na kutoa maelekezo kuwa zitumike kwa kiasi kidogo kwa ajili ya hafla hiyo na sehemu kubwa zipelekwe katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili zikatumike kununulia vitanda na hivyo kupunguza tatizo la wagongwa wanaolala chini kutokana na uhaba wa vitanda unaikabili hospitali hiyo.

“Nilipoambiwa kwamba zimechangwa shilingi milioni 225 zimekusanywa kwa ajili ya sherehe, nikasema fedha hizo zipelekwe katika hospitali ya Taifa Muhimbili zikasaidie kununua vitanda” alisema Dkt Magufuli na kusisitiza kuwa “kwa kufanya hivyo tutakua tumejinyima sisi wenyewe lakini tutakua tumewanufaisha wenzetu ambao wanamatatizo makubwa yanayoweza kutatuliwa kwa fedha hizo”.

Awali akitoa taarifa ya michango hiyo Ofisa wa Spika wa Bunge Bwana SAID YAKUBU amesema jumla michango iliyopatikana na shilingi milioni 225 na kwamba fedha zilizotumika katika hafla hiyo ni shilingi milioni 24 tu baada ya kuzingatia maagiza ya Rais Magufuli.

Katika Hafla hiyo Rais Magufuli amekabidhi vyeti vya kutambua mchango wa wadau waliochangia fedha wakiwemo Benki za NMB, CRDB na Benki ya Afrika pamoja na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PSPF na PPF.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano IKULU

November 20, 2015

Saturday, June 21, 2014

Tanzia - Deborah John Said (Muimbaji wa Nyimbo za Injili)

Nimepata taarifa  kwa Email:

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. AMEN.

The Late Deborah John Said


Taarifa zilizotufikia katika Chumba cha Habari muda huu zinasema kwamba , Muimbaji wa Nyimbo za Injili Deborah John Said Amefariki Dunia katika Hospitali ya Muhimbili. Endelea kufuatilia hapa kwa taarifa zaidi. Tunatoa pole kwa wote waliopatwa na Msiba huu Mkubwa.


********
IBADA YA KUMUAGA DADA YETU DEBORA SAID ITAFANYIKA JUMATATU SAA NNE ASUBUHI KATIKA KANISA LA MAISHA YA USHINDI MABIBO EXTERNAL NA BAADAYE SAA NANE MCHANA MAZISHI KATIKA MAKABURI YA MABIBO JESHINI

kwa habari zaidi tembelea www.johnshabani.blogspot.com
 

Sunday, June 01, 2014

Mtoto Nasra Afariki Dunia


Marehemu Mtoto Nasra

MTOTO Nasra aliyekuwa akiishi kwenye box kwa miaka minne ikidaiwa kuteswa na mamake mkubwa baada ya mama yake kufariki, huku akikosa uangalizi wa karibu, chakula, tiba na huduma nyingine muhimu AFARIKI DUNIA KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI usiku wa kuamkia leo majira ya saa saba, tatizo ni Nimonia (Pneumonia) na homa ilipanda sana.

 R.I.P NASRA wewe mbele sisi nyuma tutakufuata.Tulikupenda lakini Mungu amekupenda zaidi.


Kwa habari zaidi kuhusu Maisha ya Mtoto Nasra BOFYA HAPA:

Sunday, August 11, 2013

Sheikh Ponda Yuko Muhimbili Kwa Matibabu

Video Kwa Hisani ya Imma Mbuguni




Sheikh Ponda Akitibwa Jereha la Kupigwa Risasi Begani Muhimbili



Kutoka: MICHARAZO MITUPU BLOG

Sheikh Ponda Issa Ponda ameletwa Dar na kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu na tayari kuna habari kwamba Polisi wakiwa kwenye madifenda yao wameshatimba hospitalini hapo.

MICHARAZO inafuatilia taarifa hizo zilizopenyezwa hivi punde kujua ukweli na ikiwezekana kuwatupia na picha kama ni kweli Sheikh huyo machachari na kiongozi wa umma wa waislam walio wengi amepelekwa hospitalini hapo.
Pia taarifa rasmi kuhusu hali ya Sheikh Ponda inatarajiwa kutolewa Alasiri hii katika Msikiti wa Mtambani na Amir wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Mussa Kundecha baada ya kuwepo kwa mkanganyiko juu ya hali ya kiongozi huyo wa umma wa waislam Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda juu ya tukio la kujeruhiwa kwa risasi begani na Polisi wakati alipotaka kukamatwa, japo Polisi wanaendelea kukomaa kwamba hawajui lolote.

Picha Kutoka Daily Mirror

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Monday, June 10, 2013

Msanii Kashi Afariki Dunia

Wasanii wengi wa Tanzania wamefariki dunia katika kipindi kifupi.  Leo nimesikia kuwa msanaai Kashi ametuaga. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.

******************************

Kutoka Swahili World Planet Blog:

Habari zilizotufikia ni kuwa muigizaji wa filamu Jaji Hamisi maarufu kama Kashi amefariki dunia leo hii katika hospitali ya Muhimbili. bado hatujajua chanzo cha kifo chake lakini tutawaletea updates. Kashi alikuwa muigizaji mwenye kipaji cha hali ya juu katika filamu, pia aliwika na kundi la Shirikisho msanii Afrika lililokuwa linaonyesha michezo yake ITV.  Rest in peace Kashi

Msanii Kashi

The Late Kashi

Thursday, March 28, 2013

Mbunge Salim Hemed Khamis Akimbizwa Muhimbili

WADAU NINA SWALI.  Hivi huko Bungeni, hakuna Stretcher ya kubeba wagonjwa?  Je, hakuna watu wa First Aid?   Hii ni mwaka 2013, wanatakiwa wawe na wahudumu wa afya, ambulance, wahudumu onsite yaani pale pale kwenye ofisi za Bunge. Watu wawepo wanaoelewa jinsi ya kubeba wagonjwa. Na hasa huko Bungeni waBunge wengi wana umri mkubwa na matatatizo ya kiafya.  - Chemi

KUTOKA GAZETI LA NIPASHE



Mbunge wa Jimbo la Chambani, Salim Hemed Khamis (CUF), ameugua ghafla wakati akihudhuria kikao cha Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kukimbizwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).


Mbunge huyo alikutwa na masahibu hayo jana na alikimbizwa hospitalini kwa matibabu ambako alilazwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu (ICU).

Wajumbe wa kamati hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Edward Lowassa, na Makamu Mwenyekiti, Mussa Hassan Zungu na baadhi ya wajumbe walimtoa nje ya ukumbi na kumpepea kwa kutumia magazeti na majarida.

Hata hivyo, hali yake ilizidi kuwa mbaya huku akizungumza kwa tabu kuwa alikunywa dawa za shinikizo la damu (BP) kabla hajala chochote na hivyo kuzidiwa.

Wabunge hao na maofisa wa Bunge, waliendelea kumpepea ili apate ahueni, lakini hali ilizidi kuwa mbaya na kushindwa kuongea kila alipoulizwa jambo.

Walimbeba na baada ya muda waliomba msaada kwa wanahabari waliokuwapo eneo hilo huku wakiwazuia wasipige picha za tukio hilo kwa maelezo kuwa si kila kitu ni habari.

Waandishi watano walisaidiana na wabunge hao kumbeba kwa kupitia mlango wa dharura na alipakizwa kwenye gari la ofisi ya Bunge lenye namba za usajili STK 2178 likiongozwa na pikipiki ya polisi yenye namba za usajili PT 2591.

Gari iliyombeba Mbunge huyo iliondoka kwenye ofisi hizo saa 5:15 asubuhi na habari zilizopatikana baadaye zilieleza kuwa alipelekwa Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Baadhi ya wabunge walisema kuwa Khamis akiwa amekaa, ghafla alianza kutapika huku akilalamika kuwa hajisikii vizuri baada ya kunywa dawa za BP na hali yake kubadilika na walisaidiana kumtoa nje ya chumba cha mkutano.

Pamoja na wabunge hao pia, alikuwapo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi.

Waliomsindikiza hospitalini ni Mbunge wa Mpanda Mjini, Said Amour Arfi (Chadema) na Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa (CUF).

Aizungumza na waandishi wa habari baada ya kurejea kutoka Muhimbili, Khalifa alisema Khamis alipokewa na alikuwa anaendelea kupatiwa matibabu.

Khalifa alifafanua kuwa Khamis anasumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Edward Lowassa, alisema hali yake ilikuwa inaendelea vizuri na kuthibitisha kuwa amelazwa ICU. Lowassa alisema kuwa miezi mitatu iliyopita Khamis alikuwa India kwa matibabu. Ofisa Uhusiano wa Muhimbili, Aminiel Eligaesha, alipoulizwa kwa njia ya simu, alithibitisha kuwa mbunge huyo kupokewa hospitalini hapo na kuongeza kuwa alipatiwa matibabu na anaendelea vizuri. Hata hivyo, alisema taarifa kamili itatolewa na ofisi za Bunge.

Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel, alisema hadi jana jioni mbunge huyo alikuwa bado ICU chini ya uangalizi wa madaktari. “Bado yuko ICU. Wanamwangalia. Presure (shinikizo la damu) iko juu, tunampumzisha kidogo,” alisema Joel akijibu swali la NIPASHE kuhusu maendeleo ya afya ya mbunge huyo. Akijibu swali iwapo kuna mpango wowote wa kumpeleka mbunge huyo kupatiwa matibabu zaidi nje ya nchi, alisema: “Tunasubiri ushauri wa madaktari.”

CHANZO: Nipashe

Monday, July 02, 2012

Madaktari Muhimbili Warejea Kazini

Muhimbili National Hospital, Dar es Salaam, Tanzania

MADAKTARI HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI WAREJEA KAZINI

JULAI 2, 2012


Huduma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili zimerejea katika hali ya kawaida baada ya Madaktari kurejea kazini Jumatatu ya leo Julai 2, 2012.

Tathimini iliyofanyika kuanzia asubuhi saa mbili hadi saa 11 jioni inaonyesha kuwa katika Idara ya Tiba, Madaktari Bingwa 19 kati ya 21 wamefika kazini ambapo watatu wako likizo. Aidha Registrars wote 12 walikuja kazini. Kliniki zote za tiba zimefanyika kama kawaida.

Katika Idara ya watoto, yenye Madakatari Bingwa 16, kati yao 14 walikuja kazini wengine wawili wako likizo na Registrar watatu kati ya sita walikuja kazini ambapo watatu wako likizo

Upande wa OPD yenye Registrars saba, sita kati yao walikuja kazini na mmoja yuko likizo. Aidha Madaktari Bingwa wote walikuja kazini.

Idara ya Magonjwa ya Afya ya Akili yenye Madakatri Bingwa 10, tisa walikuja kazini na mmoja wao yuko masomoni.

Upande wa Emergency Medicine, Registrars wote 10 walikuja kazini.

Kuhusu huduma za upasuaji, wagonjwa wote waliolazwa wodini wameonwa, na baadhi ya kliniki za huduma ya upasuaji zilifanyika. Hata hivyo, upasuaji haukufanyika kwani hakukuwa na orodha ya wagonjwa waliopangwa kufanyiwa upasuaji..

KWA UJUMLA, MADAKTARI WAMEREJEA KAZINI.

Imetolewa na;

Aminiel Buberwa Aligaesha
Afisa Uhusiano Mwandamizi
Julai 1, 2012

Monday, April 09, 2012

Kanumba Alikufa Kwa Brain Concussion!

Duh! Kama kweli alipata concussion ina maana Steven Kanumba, alipigwa na kitu kizito kichwani au alianguka kweli.  Polisi wanasemaje?  Madakatari wanasema ubongo wake ulikuwa umevimba.

KUTOKA WEB MD

What is a concussion?
A concussion is a type of traumatic brain injury that is caused by a blow to the head or body, a fall, or another injury that jars or shakes the brain inside the skull. Although there may be cuts or bruises on the head or face, there may be no other visible signs of a brain injury.4


 
******************************************************************************
KUTOKA  GAZETI LA MWANANCHI:

NI BAADA YA JOPO LA MADAKTARI MUHIMBILI KUMFANYIA UCHUNGUZI, BABA YAKE AZUNGUMZA, WABUNGE WAANGUA KILIO

Florence Majani na Suzzy Butondo

MSANII nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitalaamu kama Brain Concussion, taarifa za kitabibu zimeeleza.


Taarifa hizo za ndani, zilizopatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu huyo, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa. Mmoja wa madaktari hao ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya saa mbili.

“Tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 6:45 mchana na tukagundua kuwa marehemu alifariki kutokana na mtikisiko wa ubongo kwa kitaalamu, Brain Concussion,” alisema daktari huyo. Alisema Kanumba alipata mtikisiko wa ubongo ambao husababisha kufeli kwa mfumo wa upumuaji (cardio-respiratory failure) “Kilichomuua hasa ni mtikisiko wa ubongo, ambao endapo unatokea katika sehemu ya nyuma ya ubongo (cerebrum), huua kwa haraka” alisema daktari huyo na kuongeza kuwa mtikisiko wa ubongo wa nyuma, husababisha matatizo ya mfumo wa upumuaji na hilo limeonekana katika mwili wake.

“Baada ya ubongo wake kutikiswa kwa nguvu, mfumo wa upumuaji ulifeli na ndiyo maana tumekuta kucha za Kanumba zikiwa na rangi ya bluu, huku mapafu yake yakiwa yamevilia damu na kubadilika kuwa kama maini, hizo ndizo dalili za kufeli kwa mfumo wa upumuaji.”

“Mtu aliyepata mtikisiko wa ubongo huweza kutokwa na mapovu mdomoni na hukoroma kabla ya kukata roho na ndivyo ilivyokuwa kwa Kanumba kabla hajafariki.”

Daktari mwingine aliyeshiriki katika uchunguzi huo ambaye pia aliomba jina lake lisitajwe alisema ubongo wa mwigizaji huyo ulikuwa umevimba na kushuka karibu na uti wa mgongo na hivyo kuathiri mfumo wa upumuaji.
Alisema sehemu ya maini na majimaji ya machoni ya marehemu, vimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini endapo kuna sumu au kitu kingine katika mwili huo.

Baba mzazi azungumza Baba mzazi wa mwigizaji huyo, Charles Musekwa Kanumba alisema kwamba alipata taarifa za kifo cha mwanawe Jumamosi saa 10:00 alfajiri baada ya kupigiwa simu na dada wa marehemu, Sara Kanumba. “Sara aliniuliza: ‘Una taarifa yoyote kuhusu mwanao Kanumba?’ Nikamjibu kuwa sina taarifa yoyote, ndipo aliponieleza habari za kifo hicho. Aliniambia Kanumba hatupo naye tena amefariki kwa kuanguka, amekorofishana na mpenzi wake.” alisema taarifa hizo zilimsababisha aishiwe nguvu kwa kuwa kilikuwa kifo cha ghafla… “Basi kuanzia hapo, nilianza kupigiwa simu za kupewa pole, ndipo nilipoamini kumbe mwanangu amefariki.”

Akizungumzia kuchelewa kufika msibani, alisema kumetokana na tatizo la mawasiliano. Awali, alikuwa amepanga mtoto wake Kanumba akazikiwe Mwanza kwa babu yake ndiyo maana hakufika mapema msibani. “Nilikuwa nimepanga apitishwe hapa kwangu Shinyanga aagwe, halafu tumpeleke Mwanza kwa babu yake kumzika huko lakini alipokuja mama yake alinishauri kuwa huko kutakuwa na nafasi ndogo kwa sababu watu ni wengi pia alikuwa na marafiki wengi, wengine wa kutoka nje ya nchi kwa hiyo alinishawishi na tukakubaliana kumzika Dar es Salaam,” alisema.

Pia alikanusha uvumi kuwa hajafika msibani kwa kuwa walikuwa na ugomvi na marehemu akisema walishamaliza tofauti zao. Alisema anatarajia kufika leo usiku tayari kushiriki mazishi hayo.

Wabunge kilio Jana, baadhi ya wabunge waliofika nyumbani kwa marehemu Kanumba waliangua vilio wakati walipotoa salamu zao za rambirambi.

Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata hakuzungumza na badala yake aliimba kipande cha wimbo uliozungumzia kifo na maneno ya wimbo huo yalionekana kuwagusa wafiwa na kusababisha vilio kuanza upya huku baadhi wakipoteza fahamu.
Mbunge mwingine, Neema Mwinyimgaya aliongeza majonzi masibani hapo alipounganisha msiba huo na wa mama yake… “Mama yangu amefariki miezi mitatu iliyopita, huko uliko mama, nakuomba umpokee kijana mwenzetu,” alisema mbunge huyo na kushindwa kuendelea.

Wabunge wengine waliohudhuria msiba huo ni Ismail Aden Rage (Tabora Mjini), Aboud Juma (Kibaha Vijijini), Mussa Azan Zungu (Ilala), Abbas Mtemvu (Temeke), Peter Serukamba (Kigoma Mjini) na Ritha Kabati (Viti Maalumu).
Kova na mchango wa Kanumba Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema anakumbuka mchango wa Kanumba katika kuzuia uhalifu jijini.

“Tulishirikiana naye pamoja na wasanii wengine kuandaa bonanza maalumu ambalo lilidhamiria kukabiliana na uhalifu hapa jijini na kwa kweli mchakato ule ulifanikiwa kwani uhalifu ulipungua kwa kiasi kikubwa” alisema Kova.
“Kifo chake kimekuwa cha ghafla mno na nafikiri kujiweka tayari (kiimani) ni jambo ambalo kila mmoja anatakiwa kuwa makini nalo katika maisha yake,” alisema Kova.

Ratiba ya mazishi
2:30 - Msafara kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia Barabara ya Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi hadi Viwanja vya Leaders Club.
3:30 - Misa ya kumuombea na salamu mbalimbali.
6:00 – Kuaga
9:00 - Kuelekea Makaburi ya Kinondoni kupitia Barabara ya Tunisia

SAHIHISHO
Rais Jakaya Kikwete jana alilazimika kubadili ratiba yake ya safari za ndani ya nchi ili kwenda kujumuika na waombolezaji wengine katika msiba wa msanii nguli, Steven Kanumba na hakuwa na safari nje ya nchi kama ilivyoripotiwa na gazeti hili jana. Mhariri.

SOMA HABARI ZAIDI HAPA:

Thursday, April 05, 2012

Sandra Mushi Akusanya Vitabu Kwa Ajili ya Watoto Muhimbili




Muhimbili Hospital Childrens Book Collection


G’afternoon happy people!!

Thank you so so so so so so much for the books, toys, exercise books, colouring pencils. Crayons etc that we collected for MOI kids – and which I dropped today.

I am so proud and happy to say that we collected about 6 boxes. Thank you ever so much!

I have taken some pictures of what was collected ...
I was asked to go see the kids – and maybe take pictures of them too – but I didn’t have the heart to. So I am sorry that I didn’t take pictures of the kids.

Sarah Clittero and the Novel Idea team, thank you and God bless you! This should not be the end, but only the beginning – there is so much more that we can do and that is needed from us. Pamoja tunaweza na pamoja tutafika.

Thank you all!
Regards,

SANDRA MUSHI

Thursday, February 09, 2012

Maazimio ya Kikao Kati ya Waziri Mkuu na Madaktati Leo CPL

Asante Da Subi kwa Kuleta Taarifa Hii:


Tamko la Kamati: MAAZIMIO YA KIKAO CHA WAZIRI MKUU; MADAKTARI

09/02/20120 Comments Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari inayoongoza mgomo wa Madaktari, Dkt. Stephen Ulimboka baada ya kuzungumza na madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es salaam, Februari 9, 2012. (Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu)
TAARIFA KWA UMMA NA MADAKTARI WOTE NCHINI JUU YA MAAMUZI YALIYOFIKIWA LEO FEBRUARY 9, 2012 KUFUATIA MKUTANO KATI YETU NA WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA KATIKA UKUMBI WA CPL, HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

Kamati ya muda ya kushughulikia madai ya madaktari nchini inapenda kuwajulisha madaktari wote pamoja na kada nyingine zote za afya nchini juu ya kile ambacho kimejiri katika siku ya leo ya tarehe 09.02.2012 ikiwa ni matokeo ya kikao wanataaluma wa kada za afya na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda na baadaye kufuatiwa na kikao kati ya madaktari na kada nyingine za afya.

Ifahamike kuwa kama Kamati tulipata mwaliko wa kushiriki katika Mkutano huo ambapo ilitarajiwa kuwa Mhe, Waziri mkuu atafika kwa nia ya kutoa mrejesho wa madai ya madaktari yaliyowasilishwa mezani kwake mnamo tarehe 23.01.2012. Madai yetu yalikuwa manane na Mh Wazizri mkuu aliweza kutoa maelezo ya dai moja baada ya lingine.

Miongoni mwa madai ambayo mpaka sasa yamepatiwa majibu ya kuridhisha ni pamoja na;

Kuwawajibisha watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, wakiwemo Katibu Mkuu Mama Blandina Nyoni , na Mganga Mkuu wa Serikali Dr. Deo Mtasiwa. Aidha Mh waziri mkuu alisema kuwa ameshalifikisha kwa Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania suala zima la kuwawajibisha watendaji wa wakuu wa kisiasa wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambao ni Waziri Mh Hadji Mponda na Naibu Waziri Mhe. Lucy Nkya.

Kama sehemu ya maridhiano, Mh Waziri Mkuu pia aliahidi mbele ya mkutano kuwa hakutawepo na unyanyasaji au vitisho vya aina yoyote ile kwa wale wote walioshiriki katika kushinikiza Serikali kutatua kero hizo. Aidha kama sehemu ya maridhiano, Mh waziri Mkuu pia alifuta zuio la madaktari kutokufanya mikutano. Lakini pia, Mh waziri Mkuu alisema kuwa Serikali haina kusudio la kumfukuza kazi mtumishi yeyote wa afya yule kazi aliyeshiriki katika mchakato huu wa kuishikiniza Serikali kutafuta ufumbuzi madai ya madaktari nchini.

Aidha, Mh waziri Mkuu amesema “Interns” wote waliokuwa wamehamishwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wamesharudishwa bila masharti katika hospitali hiyo ili kuendelea na program kama kawaida. Hili pia linaambatana na kulipwa na kupewa stahiki zao zote.

Pia suala la madaktari na familia zao kuwa na Kadi ya Bima ya Afya ya kijani( Green Card) limekubaliwa na kwa sasa tusubiri utekelezaji.

Pia ilikubaliwa kuwa madaktari watapata fursa ya kukopeshwa magari kama watumishi wengine wa umma.

Mbali na madai hayo, pia Mh. Waziri Mkuu alitoa ufafanuzi juu ya madai yanayuhusu maslahi ya watumishi wa afya ikiwa ni pamoja na Mishahara na Posho na stahiki mbalimbali. Lakini hata, Mh waziri Mkuu hakutoa majibu ya moja kwa moja ya kiwango gani kitakachoweza kulipwa na Serikali kama mishahara, posho na stahiki mbalimbali kwa minajili kwamba bado zinafanyiwa kazi na kamati ya wataalamu aliyoiunda ili waweze kumshauri. Aidha, Mh waziri Mkuu alisema kuwa kwa wakati huu inaweza kupandisha “on call allowances” za kada mbalimbali za afya kutoka shilingi 3,000 – 10,000/= na kufikia kati ya shilingi 5,000 hadi 25,000. Madaktari bado wanaona ongezeko hili halilingani na ukubwa wa kazi ifanywayo pindi mtumishi wa afya anapokuwa “on call” na hivyo basi kuendelea kupendekeza kuwa “on call” allowance iwe ni 10% ya mshahara wa mtumishi husika.

Pia Mhe, Waziri Mkuu hakuweza kueleza kinagaubaga mkakati kazi wa uboreshaji wa huduma za afya wapatayo wananchi wa Tanzania.

Baada ya tamko hilo la Serikali kumalizika, Mh Waziri Mkuu na ujumbe wake waliondoka, na Mkutano huo ukaendelea kwa Kamati kufanya Mkutano na madaktari wote, lengo ikiwa kujadili tamko hilo na kutoa maazimio.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu, madaktari walikubaliana kwamba; kwa kuwa Serikali imeanza kuonyesha nia ya kutatua tatizo hili kwa kutekeleza baadhi ya maazimio yetu, wajumbe kwa niaba ya madaktari wote nchi nzima tulikubaliana na kuazimia yafuatayo;

Kurudi kazini mara moja kuanzia kesho tarehe 10.02.2012 bila masharti yeyote.

Kamati ya jumuiya ya madaktari kama sehemu ya MAT kuendelea kukaa mezani ya majadiliano na Serikali ili kuanza kupitia madai hasa yale yanayohusu maslahi.

Kukutana tena tarehe 03.03.2012 ili kupata mrejesho wa kiwango cha utekelezaji wa madai hayo kwa mujibu wa vikao vya majadiliano na makubaliano na hatimae kuchukua hatua zaidi.

Kujadili utekelezaji juu ya Kuwawajibisha Waziri na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi na Jamii.

Mwisho kabisa Madaktari wote kwa ujumla wake walilaani na kukemea kitendo cha Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwahoji wanaharakati wa haki za kibinaadamu na mashirika ya kijamii wakiwemo Dr. Hellen Kijo-Bisimba na Mama Ananilea Nkya na wanaharakati wengine wote waliokumbwa na kamata kamata hiyo na hivyo basi tunalitaka jeshi hilo kuwaachilia huru mara moja bila masharti yeyoye.

Pamoja Tunaweza

Imetolewa na Kamati ya muda ya kushughulikia madai ya madaktari Tanzania

Dr, Ulimboka Stephen
Mwenyekiti.

Wednesday, September 14, 2011

Mgonjwa Muhimbili Anatafuta Ndugu Zake

PRESS RELEASE FROM MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL - DAR ES SALAAM, TANZANIA
(Unidentified Patient in ICU at Muhimbili Hospital in  Dar es Salaam)

Hospitali ya Taifa Muhimbili ilipokea mgonjwa toka Hospitali ya Mwananyamala tarehe 18/08/2011 akiwa mahututi na hajitambui. Inasemekana kuwa mgonjwa huyu aliokotwa na wasamaria wema barabarani akiwa amegonjwa na gari usiku wa kuamkia tarehe 18/08/2011 ambao walimpeleka Hospitali ya Mwananyamala. Kwakuwa alikuwa ameumia sana Hospitali ya Mwananyalama iliamua kumleta Hospitali ya Taifa Muhimbili ili aweze kupata huduma na uchunguzi mkubwa zaidi.


Mgonjwa huyu hajulikani jina lake kwani hawezi kuongea toka alipoletwa kutokea Mwananyamala. Mgonjwa huyu alifanikiwa kuonwa na madaktari bingwa siku hiyohiyo ya tarehe 18/08/2011 na kufanyiwa uchuguzi wa vipimo mbalimbali ikiwemo X-Ray ya tumbo, kichwa, kifua na kiuno. Matokeo ya vipimo hivyo yalionekana kuwa kichwani kulikuwa na damu kidogo iliyoganda kutokana na kuvujia kwa ndani, picha za kifua na kiuno zilionyesha kuwa hakuna tatizo.

Picha ya tumbo ilionyesha kuwa bandama lilipasuka hali iliyopelekea kufanyia upasuaji siku hiyohiyo ya tarehe 18/08/2011 ili kuondoa bandama. Baada ya upasuaji mgonjwa alipelekwa moja kwa moja chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) siku hiyo hiyo ya tarehe 18/08/2011.

HALI YAKE:

Tangu apelekwe ICU hali yake bado ni mbaya, hajitambui. Aidha tangu tarehe 18/08/2011 hakuna ndugu au jamaa aliyejitokeza kuulizia hali ya mgonjwa huyu.

Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili unaomba yeyote anayemfahamu mgonjwa huyu atoe taarifa kwa ndugu na jamaa zake ili waweze kuja kumtambua ndugu yao. Tunaendelea

Imetolewa na:


Aminiel Aligaesha,
Afisa Uhusiano,
Hospitali ya Taifa Muhimbili,
Septemba 2, 2011.

Friday, December 17, 2010

Muhimbili Moments

Baba akisoma nakala ya Daily News. Nilikuwa Cover story kwenye Woman section.
Baba akipelekwa Theatre kwa ajili ya Upasuaji.

Njia panda kwenda Block za Sewa Haji na Kibasila


Wagonjwa wakisubiri kuingia Muhimbili Orthopedic Institute

Father Fidelis wa R. C. akipita kusalimia wagonjwa


Roundabout

Magoroja yanjengwa Upanga!


Mafuriko Jangwani - View from Mwaisela Block


Kaka Michuzi na Mke wake nao walipita kutoa salamu za pole kwa Baba.

Mwaisela Block Muhimbili

Mwaisela Block Mwaisela Annex

Ward Number 8 Upande unaotazamana na Orthopedic Institute


Wheelchair Mbovu Ward 8, Watu wanaitumia kukalia tu

Mimi Mwaisela Ward 8

Kunguru

Mwaisela Annex


Mwaisela Ward 8 Emergency Exit


Mwaisela Ward 8 Emergency Exit -lakini mbona hutaweza kupita ikitokea kasheshe?

Panya aliyekamatwa Mwaisela Ward 8 na Mgonjwa

Mdudu aina ya Preying Mantis

Mwaisela Ward 8 upande uinaotazamana na Jangwani

Muhimbili Garden

Pale Garden Muhimbili unaweza kupata vinywaji kama chai, soda, juisi bia. Pia kuna chakula kizuri tu. Asubuhi unaweza kupata supu, maandazi, sambusa, egg chop, mayai etc. Mchana, pilau, wali, ndizi, etc. Bei siyo mbaya. Watu wanamimiminika pale kule. Unaweza kupata phone card pia.



Mwembe Mkubwa Pale Garden
Huo Mwembe una miaka mingapi?
Pilau Nyama Bei 1500/-, Juisi 500/-

Wednesday, December 15, 2010

Mifugo Wodini Mwaisela



Wadau, nilikuwa pale Mwaisela Ward namba 8, majuzi ghafla nikasikia watu wanapiga kelele kwenye wodi ya vitanda vitano (viko vitanda tisa). Halafu nikasikia wagonjwa wakisema kuwa kuna mifugo wodini. Kumbe walimwua panya!
Watu walienda kuangalia ni nini? Mgonjwa huyo alisema aliwua kwa kumpiga na kiatu. Manesi walisema kweli panaya wapo wanapanda kwenye mabomba ya vyoo.

Pichani ni mgonjwa aliyemwua huyo panya akienda kumtupa kwenye takataka za Biohazard.

Nimerudi Boston

Mashine ya Fluoroscopy juzi kabla haijatengenezwa na fundi.

Mimi na baba jana nyumbani mara kabla ya mimi kuondoka kurudi Boston.


Wadau, nimerejea Boston kutoka Dar leo.

Baba alifanyiwa X-ray aliyohitaji baada ya mashine ile ya Fluoroscopy kupona. Alikuwa discharged juzi, lakini tulimrudisha Muhimbili jana kwa ajili ya hiyo X-ray. Yuko nyumbani Tenki Bovu sasa anaendelea vizuri. Hiyo X-ray tulilipa 80,000/- wiki tatu zilizopita lakini ndo alipata jana. Nilikuwa nimeanza mpango wa kumpeleka private kwa ajili ya hiyo x-ray lakini nilipigiwa simu kuwa mashine imepona na angeweza kufanyiwa. Ingawa ilifanya kazi jana huenda mashine hiyo imekwishaharibika tena. Niliambiwa ilishawahi kufa kwa miezi mitatu! Sasa wale wagonjwa wasio na uwezo wa kwenda private walifanya nini?
Wanaofanya kazi pale wako frustrated kwa vile wanshindwa kufanya kazi yao vizuri kutokana na mashine mbovu. Ilivyoharibika, wafanayakazi waliondoka kwa vile hawakuwa na kazi ya kufanya. Ilikuwa kila nikienda kucheki kama mashine imepona, hakuna mtu! Wana frustration ya hali ya juu.

Kwa kweli lazima niseme huduma Muhimbili ilikuwa nzuri kwa ujumla. Siyo Best lakini nzuri, tofauti na miaka ya nyuma. Baba alikuwa Semi private Ward huko Mwaisela.

Ila jamani tulikuwa tunafika pale Muhimbili kila siku saa 12 asubuhi, halafu unasikia vilio, mtu kaja kamkuta mgonjwa wake ameaga dunia usiku.
Picha tele za Muhimbili zinakuja. Safari hii sijaweza kwenda popote maana kila siku ilikuwa safari ya hospitali.

Friday, December 10, 2010

Muhimbili Wanahitaji Fluoroscopy X-Ray Machine

Ofisi ya X-Ray Fluoroscopy huko Muhimbili National Hospital

Wadau, nimehangaika na baba yangu hapa Muhimbili siku kadhaa sasa ili afanyiwe Cystourethrography. Bado hajafanyikiwa, mashine inaharibika kila saa. Kuna backlog ya wagonjwa wanaohitaji kufayiwa x-ray na hiyo mashine lakini haijawezekana.

Jana ilikuwa sikukuu hivyo walikuwa wamefunga. Ile juzi tulimtoa baba wodini Mwaisela na kumpeleka kwenye X-ray. Kakaa masaa kadhaa ndo wakasema mashine imeharibika na fundi anitengeneza.

Alitokea Acting Head wa Idara, Dr. Flora Lwakatare, alisema kuwa wana mashine mbili za fluoroscopy. Moja ndo mbovu kabisa na nyingine ndo hiyo inayoleta matatizo mara kwa mara. Alisema wametarifu Waziri kuhusu tatizo lao lakini bado hawajapata mashine mpya.

Haya leo, tumemtoa baba wodini kumpeleka huko kwenye x-ray. Mashine ikaleta matatizo. hivi sasa wanasema fundi anakuja kutengeneza. Isipowekezekana leo basi mapaka juamatatu. Tunaomba mungu kuwa watafanikwa kutengeneza mshine na itaweza kufanya kazi.

Na si zaidi ya saa moja iliyopita, babu ambaye alitolewa wodi nyingine kwa ajili ya vipimo alizimia (fainting) na kuanguka hadi kwenye sakafu! Nesi aliyemsindikiza baba yangu kamhudumia yule mzee mara moja. Wamerudisha wodini. Inasikitisha kweli kuona wagonjwa wamelundikana pale x-ray.

Kwa kweli huduma hapa Muhimbili umekuwa mzuri, ila ndo tumekwama kwenye hiyo x-ray. Je, serikali inampano wa kuleta mashine hiyo, maana wagonjwa wanateseka.

Saturday, November 13, 2010

Diasaster Preparedness

DISASTER PREPAREDNESS

By Dr. Amur Abdullah Amur
Principal Specialist in Internal Medicine, Muhimbili National Hospital, Dar-Es-Salaam

The success of the plan of action to rescue miners in Chile reflects to well organized disaster preparedness activities by the Public Health Authorities. This rescue involved Chilean miners who had been trapped for almost 70 days some 600 meters underground after the mine they were working in collapsed around them 5th Aug.2010 , puzzled the attention of many.

The possibility of Public Health Emergencies concerns many people in the wake of frequent outbreaks of diseases and environmental mishap particularly in developing countries.

Many would agree with me that disaster preparedness helps people to deal with disasters of all sorts much more effectively when they do occur. Disaster preparedness is efficiently accomplished from family level to the national level. Charity starts at home! At a family level, keeping a three-day supply in the reserve and at least an additional four-day supply per person for use at home by each family is advisable. Public Health Disaster Preparedness teams are expected to provide operational requirements include tents and toilet facilities, contracted support for food, potable water, protective gears, transport , portable medical kits including oxygen cylinders, and biomedical waste disposal. Disaster Teams provide primary and acute care, initial resuscitation and stabilization, advanced life support and preparation of sick or injured for evacuation. Each team includes physicians, nurses, medical technicians, and supporting staff. The team is expected to sustain operations for 72 hours without external support.

Disasters disrupt hundreds of thousands of lives every year and have lasting effects, both to people and property. There is a need to establish tailor made Training Courses on Disaster Management that involve all walks of Life. During our school time, we used to have Scout Clubs that conduct elementary disaster preparedness programs. Such activities should be incorporated formally to an accredited level so as to produce cadres who can serve as Emergency Medical Responders, Paramedics and Members of Ambulance Teams. Institutes like Red Cross and Red Crescent play vital role in conducting short and long term First Aid Training. Provision of assistance consists of medical materiel, personnel, and technical assistance. These resources may provide response capability for the emergency response needs. Collab­oration in advance with rescue teams helps to promote alertness, disseminate health information, minimize confusion, and identify appropriate actions and responses.

Due to increasing vulnerability of developing countries to suffer various natural disaster in a form of outbreak of infectious diseases and environmental hazards, there is a need to establish Disaster Management Institute within the Public Health Program.

Lesson from Chile has proved that appropriate disaster preparedness reduces the devastating impact on human life, economy and environment . This is achieved through education, implementing warning strategies , toll free numbers, safety measures, users friendly infrastructures, developmental plans to provide coverage to such disasters ,provision of resources and rehabilitation as well as post-disaster reconstruction.

Disaster Management is multidisciplinary approach which involves nationwide participation, different professions and different scientific fields, and has become an important measure for human, society and nature sustainable development. Developing countries that lack the necessary facilities, planning, expertise and resources for

disaster preparedness arguably need them the most. The development of Disaster Preparedness within a Public Health Program should be seen as an important opportunity for the development within the nationwide health program.

The responsibility of Disaster Preparedness is to provide for a comprehensive Emergency Management Program that meets the emergency needs of those who either have been or might be affected by an emergency or major disaster for example cholera outbreak .

The population explosion and exposure to inadequate space, substandard sanitation, pollution, poor housing and lack of safety measures in poor resource countries have increased the frequency and severity of disasters. Surface decontamination remains an uphill task in case of chemical or biological pollution in developing countries. With the prevailing background of the high disease burden an environmental hazards present in many poor resource countries, the cost of running Disaster Management could be very high. In any public health program, a well-integrated Disaster Preparedness ultimately result in cost savings through early recognition and management of the disasters.

Some countries have units of Medical Response Cops(MRC) consist of organized medical and public health professionals who serve as volunteers to respond to natural disasters and emergencies. The MRC helps to engage medical and public health personnel in response to an emergency. MRC team is capable of providing primary and secondary medical care as well as to stabilize victims for transportation to hospital facilities .

Application of proper disaster management strategies involves formation of disaster management teams ,identifying phases of disaster preparedness, pre-disaster planning, resources preparedness, monitoring including relief management capability, prediction, early warning, damage assessment and relief management. Disaster Preparedness aims to save lives, prevent injuries, preserve the environment and protect property and the economy. Disaster management is comprised of four interdependent risk-based functions: prevention/mitigation, preparedness, response and recovery. Mitigation provides a critical foundation for disaster management.

The followings are the Phases of Disaster Preparedness:

1.Mitigation/Prevention -- A period of time during which activities are undertaken by individuals/institutes to improve their capabilities to respond to a potential emergency and fulfill their assigned responsibilities. Mitigation efforts attempt to prevent hazards from developing into disasters altogether, or to reduce the effects of disasters when they occur. The mitigation phase concentrates on short and long-term measures for reducing or eliminating risk. The implementation of mitigation strategies can be considered as a part of the recovery process if applied after a disaster occurs. The need of Establishment of Curriculum to train cadres of Disaster Management Team should be emphasized. Strategies of mitigation eliminate or reduce the impacts and risks of hazards through proactive measures taken before an emergency or disaster occurs.

2. Preparedness --

A period of time during which activities are undertaken by individuals and disaster teams to increase their alertness during periods of heightened risk. The emergency managers develop plans of action to manage and counter their risks and take action to build the necessary capabilities needed to implement such plans during this phase. Common preparedness measures include communication plans, emergency population alertness, evacuation, shelters, and provision of supplies. Public Health Program have the task to ensure first responders and emergency management personnel are well-prepared through education, support and exercises.

3. Response --

A period of time during which activities are undertaken by individuals and institutes to respond to an occurrence that threatens or harms human beings and environment. The response phase includes the mobilization of the necessary emergency service and members of disaster teams in the affected area. A well organized emergency plan activities developed as part of the preparedness phase enables efficient coordination in saving life ,prevention of injuries and protection of environment . The earlier response commences the better the outcome . Depending on impact of disaster sustained by the victims, virulence in case of infections, and access to health management, the vast majority of those affected by a disaster will die within 72 hours after impact. Regardless of the cause of the disaster, hygienic precautions such as hand washing ,wearing protective gears must be the rule of the game. Thorough hand-washing with antiseptics between examining victims and after contact with blood, body fluids, secretions, excretions, and equipment contaminated by them is an important component of infection control during disaster.

4. Recovery --

A period of time during which activities are undertaken by individuals and institutes to provide for the welfare of the people following a Disaster and/or emergency. Recovery efforts are primarily concerned with actions that involve counseling, crisis intervention, rehabilitation , moral support and rebuilding destroyed property. Efforts should be made to build user friendly structures taking safety measure techniques into account . This requires collective responsibilities and commitment of the community and the nation to develop and deliver disaster financial assistance, determining the amounts and types of assistance that will be provided to those who have experienced losses.

Thursday, October 08, 2009

Muhimbili Wapandisha Bei ya Huduma


Hizi bei ni chee ukilinganisha na hela tunaolipa hapa Marekani. Lakini kwa Bongo ni hela nyingi kweli. Kazi ipo!

************************************************************************
Kutoka ippmedia.com

Private patients seeking treatment at the Muhimbili National Hospital will have to pay more than double the amounts charged previously, The Guardian has learnt.

Fees which have gone up effective this month include those for laboratory, dental, blood, x-ray and ultra-sound services.

Also raised are charges for admission, consultancy, and surgery. A patient will now have to pay more than one million shillings for surgery, way above the previous charges.

A survey by this reporter, showed that charges for kidney, urethral and stomach x-ray has gone up from 9,000/- to 20,000/-.

Full body x-ray which previously cost 12,000/- has had its charges raised to 40,000/- Lumbar and back x-ray charges have now gone up to 51,000/- from the previous 18,000/-.

Ultrasound charges have gone up from 15,000/- to 35,000/-

Fluoroscopy charges have in some cases gone up from previous 20,000/- to 35,000/- those of x-ray of the throat have risen from 30,000/- to 40,000/-.

A few other charges such as those for CT Scan have not changed, while charges for others such as MRI plain have gone down to 350,000/- from 400,000/-.

An official of MNH, Aminiel Buberwa Aligaesha,

told this reporter that rising operational, equipment and patient overhead costs had forced the hospital to raise the charges.

The national referral hospital was also seeking to raise funds to finance its drive for better services, he said.


SOURCE: THE GUARDIAN