Tumwombee uzima Rais wetu Mpendwa, Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete. Amen, Amin.
****************************
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete alfajiri ya jana, Jumamosi, Novemba 8, 2014, alifanyiwa
upasuaji wa tezi dume (prostrate) katika Hospitali ya Johns Hopkins
iliyoko Baltimore, Jimbo la Maryland, Marekani.
Rais Kikwete amefanyiwa upasuaji huo baada ya madaktari waliomfanyia
uchunguzi wa afya yake kujiridhisha kuwa Rais alikuwa anahitaji
matibabu ya aina hiyo.
Upasuaji huo uliofanyika alfajiri na kuchukua kiasi cha saa moja
unusu, umefanyika salama na kwa mafanikio makubwa. Hali ya Mheshimiwa
Rais Kikwete inaendelea vizuri, bado yuko wodini akiendelea kuwa chini
ya uangalizi wa madaktari na kupatiwa tiba.
Wananchi wataendelea kupewa taarifa sahihi kuhusu hali ya Rais Kikwete
kwa kadri zitakavyokuwa zinapatikana.
Imetolewa na
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS, IKULU
DAR ES SALAAM,
NOVEMBA 9, 2014
Showing posts with label Abdul Thecla Mjatta. Show all posts
Showing posts with label Abdul Thecla Mjatta. Show all posts
Sunday, November 09, 2014
Friday, July 27, 2007
Picha zaidi za Bongoland II Film Shoot Dar es Salaam
Cameraman and Cinematographer Sam Fischer, akifanya vitu vyake mitaani Dar es Salaam.
Moja wa Interns kutoka kampuni ya Sofia Records akirekodi somo kuhusu film editing kwenye shoot ya Magomeni.
Mama Thecla Mjatta akisome script kabla ya scene huko Tanki Bovu.
Gayle alikuwa in charge kwenye msawala ya chakula. Hapa yuko Manzese.
Bwana Kibira alimdraftio baba yangu kuwa extra kwenye scene. Nyuma ni Mzee Olutu na Mama Thecla Mjatta .
Mbele ni mcheza sinema maarufu wa Bongo, Shafii. anaposi na interns wa UCLA, baba yangu na Peter Omari.
Mama Mjatta na Mzee Olotu wakipata maelezo kutoka kwa Mwuongoza sinema, Josiah Kibira kabla ya kufanya scene Manzese.Kwa kweli nashukuru kuwa nilipata nafasi ya kushiriki katika sinema ya Bongoland II. Ninamshukuru hasa Bwana Josiah Kibira, kwa kuandika script nyingine safi na kufanikisha kutengeneza kwenye sehemu halisi (authentic location) Dar es Salaam. Kwa kweli safari ilikuwa ndefu mpaka kukamilisha lakini yeye na timu yake walikamilisha.
Natumaini sinema ya Bongoland II ikitoka mtaifurahia mno.
Hizi ni picha zaidi na bado sijasafisha mikanda mingine.
Kwa habari zaidi za Bongoland II someni:
Natumaini sinema ya Bongoland II ikitoka mtaifurahia mno.
Hizi ni picha zaidi na bado sijasafisha mikanda mingine.
Kwa habari zaidi za Bongoland II someni:
Labels:
Abdul Thecla Mjatta,
Bongoland II,
Josiah Kibira,
Manzese,
Mzee Olotu,
Peter Omari,
Shaffii
Subscribe to:
Comments (Atom)






