Wadau, ndo Uselebriti huo, Uzushi mwingi! Saida Karoli yu Hai! Mungu azidi kumbariki!
Hakuwemo kwenye boti iliyopata ajali, Ziwa Victoria!
*********************************************
Taarifa ya Neville Meena kuwa ingawa ni kweli kuna ajali ya
boti iliyotokea, mwanamuziki Saida Karoli hakuwa mmoja wa waliokuwemo
kwenye boti hiyo na yuko hai!Taarifa hiyo imetoa angalizo kutafuta uhakika kwani inasemekana kuwa
Saida Karoli ni mzima, yupo jijini Dar es Salaam: “Nimetafuta namba yake
ya simu sijaipata, ila taarifa kutoka Bukoba na ofisi ya Ofisa
Utamaduni Muleba zinasema siyo kweli…” ameandika Meena.
Kuhusiana na ajali ya boti, Meena amesema, “…ni kweli kwamba kuna boti
imezama katika Ziwa Victoria, na kulikuwa na uvumi mwingi mjini Bukoba
na Wilayani Muleba kuhusu
mwanamuziki huyo kufariki lakini baadaye ikathibitika kwamba hakuwa
mmoja wa abiria.”Nayo Upland FM
radio, Kwa kupitia Facebook page yake, imekanusha taarifa za kufariki
Saida kalori na kusema msanii huyo ni mzima wa Afya. “TAARIFA: Kumezuka
habari zisizo rasmi juu ya mwanamuziki SAIDA KALORI. Tunaomba
kuthibitisha kwa Mwanamuziku huyo ni MZIMA wa afya kabisa. Usidanganywe
na uzushi wowote. ASANTE.” imesema taarifa hiyo ya Upland FM
Showing posts with label Boat. Show all posts
Showing posts with label Boat. Show all posts
Tuesday, June 18, 2013
Tuesday, June 26, 2007
Safari ya Boti


Nimeona hii picha ippmedia.com leo. Caption ilisema kuwa ni wakazi wa Dar es Salaam wakienda kustarehe Bongoyo Island, kwenye boti iiliyotoka pale Slipway Dar.
Picha ni nzuri lakini iliniaacha na maswali. Mbona wazungu tu wamevaa lifejackets? (vifaa vya kuokoa maisha). Bila shaka hizo lifejackets ni zao binafsi. Na mawimbi hayo, duh! Ama kweli watu wameweka maisha ya mikononi mwa malaika. Lifejackets ni muhimu kama unasafiri kwenye boti na kwa bahati mbaya inapinduka au inazama. Maana unaweza kuelea kwenye maji kwa muda hata kama hujui kuogelea. Mara nyingi watu wanazama shauri ya uchovu kama hawajivaa.
Nakumbuka miaka ya nyuma Tanzania, maboti kadhaa yalipinduka na watu walikufa maji shauri ya kutokujua kuogelea na kuzama. Hata boti zilizama Lake Victoria na Lake Nyasa na watu kadha walipoteza maisha yao. Watu wangepona kama wangekuwa wamevaa lifejackets.
Na hata ukipanda kwenye ndege kitu cha kwanza wanakuambia hizo lifejackets ziko wapi kama kwa bahati mbaya ndege inaanguka kwenye maji.
Sidhani kama kuna sheria inayolazimisha hao wenye boti wawe na lifejackets za kutosha kwa ajili ya abiria yao. Na huenda ingekuwa ghali sana kwa hao wenye boti. WaBongo tuna maarifa lakini na hata dumu tupu inaweza kusaidia kuokoa maisha maana inalea kwenye maji.l
Lakini Mungu yupo na atatulinda. Ni kuomba kabla hujaingiwa kwenye boti.
Subscribe to:
Comments (Atom)



