Showing posts with label Daraja. Show all posts
Showing posts with label Daraja. Show all posts

Wednesday, December 21, 2011

Mafuriko Dar - Hali Ni Mbaya!

Wadau, kutokana na mvua mwingi kumetokea mafuriko ya ajabu mjini Dar es Salaam! Nasikia kuna daraja moja tu, kwenda maeneo ya Mbezi Beach!  Katika mji wa Dar es Salaam hasa Idara ya Mipango Miji naona wamesahau mambo ya STORM DRAINAGE!!!  Hata hivyo kutokana na Ujenzi holela mambo yangekuwa bure!

Nasikia kuna vifo!  Je, RED CROSS/RED CRESCENT wataingia kusaidia waathirika?

Msamaria akimvusha kikongwe mkazi wa Jangwani baada ya makazi yake kuharibiwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia Desemba 20. (Picha na Fadhili Akida).

Jangwani nako  Balaa!

Old Bagamoyo Road baada ya Mafuriko. (Picha kwa hisani ya Michuzi Blog)

BALAA TENKI BOVU


Baada ya daraja kati ya Lugalo na Tenki Bovu (Mbezi Beach) kumegeka...Inabidi watu watembee kwa miguu kwenda upande wa pili wa daraja iliwapate usafiri  kumaliza safari zao.


*****************************
MJI wa Dar es Salaam Umekuwa Ziwa Dar es Salaam

(Picha Zifuatazo Kwa Hisani ya Tutoke Media Blog)



Wednesday, August 01, 2007

Poleni mlioko Minneapolis, Minnesota - Daraja laanguka





DOH! Kwa kweli ni makubwa! Sijui kama watasema ni terrorism au vipi.

Daraja kubwa limeanguka huko Minneapolis, Minnesota, tena saa ambazo ilikuwa imejaa magari na watu waliokuwa wantoka kazini. Hiyo daraja inavuka mto Mississippi. Taarifa za awali zinasema kuwa watu kadhaa wamekufa na wengi wamejeruhiwa. Pia kuna wazamaji (Divers) ambao wanacheki mtoni, kuona kma kuna watu kwenye aji. Wanasema magari zaidi ya hamsini yalianguka ndani ya maji.

Pia wanaomba watu watoe damu kwa ajiliya kusaidia waliojeruhiwa.

Mungu awape nguvu waliofiwa, walioumia ma watu wa Minnesota kwa ujumla. Poleni sana.


Kwa habari zaidi someni: