Showing posts with label Mafuriko. Show all posts
Showing posts with label Mafuriko. Show all posts

Saturday, September 16, 2023

Mji wa Derna, Libya Yaangamizwa na Mafuriko! Watu zaidi ya 20,000 wahofia kufa!

Ni Mambo ambayo tumesoma kwenye biblia...mji mzima kuangamizwa!   Wiki iliyopita huko Libya mashariki ulipita Kimbunga Daniel.  Mvua ulinyesha mwingi sana hadi bwawa mbili zilipasuka na kusababisha mji wa Derna kuteketezwa kwa maji!   Ajabu, Libya ni JANGWA! Crescent Nyekundu wa Libya wanasema watu karibu 20,000 wamehofia kufa!  Ila wataalamu wamiundo mbinu wanasema kuwa tangu Rais Ghadaffi auawawa hizo Bwawa hazikutunzwa ipasavyo ndo maana zika pasuka

KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA:

Saturday, March 18, 2017

Mbinu Hizi zitakusaidi Kukabiliana na Mvua Jijini Dar es Salaam

Na Jumia Travel Tanzania

Hivi kuna mkazi yeyote wa jiji la Dar es Salaam ambaye ni mgeni wa adha zitokanazo na mvua zinazonyesha? Sidhani kama kuna mtu yeyote hafahamu ya kwamba mvua ikinyesha kutakuwa na foleni zisizokwisha, barabara na mitaa tofauti jijini kujaa maji, mafuriko na matamko kadha wa kadha kutoka kwa viongozi wa serikali kuwataka wananchi wahame mabondeni.

Lakini ni wangapi wametafakari watawezaje kukabiliana na mvua zitakaponyesha? Zipo mbinu nyingi tu ambazo Jumia Travel inakushauri uzizingatie ili kipindi cha mvua nyingi za Dar es Salaam kwako kiwe ni cha kawaida katika mwaka. 


Amka mapema kukabiliana na foleni ili uwahi shughuli zako
Hakuna wakati ambao kunakuwa na foleni kubwa na zisizopungua kwa muda mrefu jijini Dar es Salaam kama kipindi cha mvua! Lakini jambo hili sio la kushangaza kwa sababu kila mwaka hali hii inajirudia. 

Na hiki ni kipindi ambacho mabosi wengi huchukia sana pengine kuliko vipindi vyote vya mwaka maana visingizio vya wafanyakazi wao kuchekelewa kazini kwa sababu ya mvua huwa haviishi. Kwa hiyo unakabiliana vipi na hali hiyo? 

Kwanza kabisa lazima uwe makini katika kuwahi kuamka mapema na pia njia ya usafiri utakayoitumia. Inakubidi kuwahi kuamka mapema sana kama unategemea usafiri wa umma au binafsi. Kwa sababu ukifanya hivyo kama kutakuwa na foleni barabarani basi utaziwahi ukilinganisha na ukichelewa kuingia barabarani. Lakini pia kama unategemea usafiri wa umma, mabasi ya mwendokasi ni mkombozi mkubwa kwenye kipindi hiki. Hivyo kwa maeneo ambayo usafiri huu unapatikana ni vema kuutumia ipasavyo kwa sababu yenyewe hayakai foleni kutokana na kuwa na njia zao pamoja na kupewa kipaumbele.    

Nunua vifaa vya kujikinga na mvua
Kutokana na jiji la Dar es Salaam kuwa na vipindi virefu vya jua na joto kali, imekuwa ni nadra sana kuwakuta wakazi wake wana vifaa vya kujikinga na mvua kama vile mwamvuli, koti, sweta au viatu vya mvua. Inashauriwa kuwa na vifaa hivi nyumbani kwako ili kujikinga ifikapo kipindi cha mvua na sio kuanza kufikiria kununua kwani inawezekana usiwe na bajeti hiyo pindi unapovihitaji. Vifaa hivyo ni muhimu kwani hukukinga na baridi, kutolawana, magonjwa na hata kutunza mavazi yako kutokana na maji ambayo huweza kusababisha kuharibika.
Umakini kwenye chombo chako cha usafiri 
Kwa wenye vyombo vya usafiri wanajua wenyewe ni kadhia gani wanayokumbana nayo ikifika kipindi cha mvua. Kipindi hiki ni jambo la kawaida kukuta magari kadhaa yamezimika au kukwama barabarani kutokana na sababu mbalimbali za kiufundi. Lakini pia barabara nyingi huharibika na kutopitika kabisa hivyo kulazimisha chombo chako kupita ni kujitafutia kuingia gharama zisizohitajika siku za usoni. Kama inawezekana tafuta njia mbadala ya usafiri katika kipindi hiki au pita kwenye njia ambazo una uhakika ni salama kwa chombo chako.

Kuwa makini na vifaa vyako vya umeme
Siyo vifaa vyote vya umeme vimetengenezwa vikiwa na uwezo wa kuzuia maji kutokuingia ndani yake. Licha ya makapuni mbalimbali kuja na teknolojia hiyo lakini unashauriwa kuwa makini sana aidha kwa kuvivika vifaa maalumu vya kuzuia maji au kuvikinga kabisa na maji. Kipindi hiki ndicho ambacho wengi hupatwa na majanga ya kuharibikiwa na simu, kompyuta, radio pamoja na luninga huko majumbani.

Kuwa makini na vyakula utakavyokula
Kama huwa unakuwa makini na aina ya vyakula unavyokula basi kipindi hiki inabidi uwe makini zaidi. Mvua zikinyesha jijini Dar es Salaam ndiyo kipindi ambacho pia kunakuwa na mlipuko wa magonjwa kadha wa kadha kama vile kipindupindu. Inashauriwa kula chakula sehemu ambayo unaiamini na inayozingatia usafi wa hali ya juu au kama inashindikana uwe unabeba chakula unachopika mwenyewe au kutokula kabisa.  

Tumia muda wako kusoma vitabu
Sio watu wote wana utaratibu wa kusoma vitabu kwenye siku zao za kawaida badala yake wanatazama filamu, kusikiliza muziki, kutoka wikendi au kupendelea kutembea. Lakini katika kipindi hiki ambacho mvua zinanyesha, barabara hazipitiki, hali ya hewa ni baridi na sehemu nyingi za starehe au kutembelea zinakosa watu ni vema ukajaribu kusoma vitabu. Amini usiamini kuwa hata kutazama filamu na kusikiliza muziki hufikia mahala vinachosha, hiki kinaweza kikawa ni kipindi kizuri cha kujaribu kitu tofauti, nunua vitabu na usome ili uongeze maarifa. 

Hivyo basi tusiifanye mvua ikawa ni kisingizio cha kutofanya shughuli zingine au majukumu mengine yanayotukabili. Kila kipindi huja na changamoto pamoja na fursa zake, ni vema kupambana nazo na kuzitumia ili kusonga mbele.

Saturday, May 09, 2015

Mafuririko Dar es Salaam!

Jamani, jamani!  Watu wameambiwa wasijenge Jangwani! Lakini wapi, wanajenga.  Haya sasa ona matokeo! Picha Kutoka Facebook.



Fenecha ya mtu


Sebuleni hapo



Aerial View of Jangwani Dar es Salaam
Mliozoea kwenda shopping hapo, mlie tu!



Hapo Sinza

Tuesday, January 29, 2013

Kimbunga Felleng Kutua Afrika Mashariki - Tropical Cyclone Felleng


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF TRANSPORT
TANZANIA METEOROLOGICAL AGENCY

Telegrams:"METEO"DAR ES SALAAM.
Telephone: 255 (0) 22 2460706-8
Telefax: 255 (0) 22 2460735 P.O. BOX 3056
E-mail: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM.
http//www.meteo.go.tz

Our ref: TMA/1622 29th January, 2013

Information to the Public: Heavy Rainfall expected

Information No. 20130129-02

Time of issue(Hour)
EAT 6:00pm

Category:

1:Information  2: Advisory 3:Alert   4:Warning:

Advisory Valid from: Date 30th January, 2013

Valid to:Date 1st February, 2013

Phenomena/Hazard/Disaster Heavy rainfall (above 50 mm in 24hrs)

Level of Confidence: Medium

Expected affected Areas :

Some areas of Rukwa, Iringa, Mbeya, Njombe, Ruvuma, Morogoro, Lindi, Pwani, Mtwara regions and neighboring areas.

Text:

Existence of Tropical cyclone “FELLENG” over the North-eastof Madagascar which pulls moisture-rich air from Congo through above mentioned areas.

Advisory:

Residents of high-risk areas, users of land and sea; and Disaster management institutions are advised to take necessary precaution

Remarks: Updates regarding the mentioned Tropical cyclone will be issued when necessary

ISSUED BY TANZANIA METEOROLOGICAL AGENCY   *****************************************

Taarifa kwa umma: Uwezekano wa matukio ya mvua kubwa

Taarifa Na. 20130129-02

Muda wa Kutolewa Saa za Afrika Mashariki Saa 12:00 Jioni

Daraja la Taarifa:

1:Taarifa 2:Ushauri 3:Tahadhari 4:Tahadhari Kubwa:

Ushauri

Kuanzia:

Tarehe 30 Januari, 2013 Mpaka: Tarehe  01 Februari, 2013

Aina ya Tukio Linalotarajiwa

Mvua kubwa (zaidi ya milimita 50 katika kipindi cha saa 24 kilasiku)

Kiwango cha uhakika: Wastani

Maeneo yatakayoathirika Baadhi ya maeneo ya mikoa ya Rukwa, Iringa, Mbeya, Njombe,Ruvuma, Morogoro, Lindi, Pwani, Mtwara na maeneo jirani na mikoa hiyo.

Maelezo:

Kuwepo kwa kimbunga “FELLENG” kaskazini-mashariki mwa,Madagascar ambacho kinavuta upepo wenye unyevunyevu.kutoka Congo kupitia maeneo tajwa hapo juu.

Angalizo:

Wakazi wa maeneo hatarishi, watumiaji wa Bahari na nchi kavuwanashauriwa kuchukua tahadhari. Aidha taasisi zinazohusika na Maafa zinashauriwa kuchukua hatua stahiki.

Maelezo ya Ziada

Mamlaka inaendelea kufuatilia mwenendo wa kimbunga hicho,na kutoa mrejeo (updates) kila itakapobidi.

IMETOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Saturday, February 25, 2012

Kuna GAS Pwani Ya Tanzania!!!

HOUSTON—Exxon Mobil Corp. and Norway's Statoil ASA said Friday a recent discovery off the coast of Tanzania has proved to hold large quantities of natural gas, further cementing the idea that East Africa could become an exporter of liquefied natural gas to Asian markets. 

Analysis of the Zafarani discovery in Block 2 offshore Tanzania showed it holds up to five trillion cubic feet of natural gas, the companies said in a press release. The gas find was announced a week ago.

The drilling success is good news for several East African countries, where offshore oil and gas exploration is picking up speed and prospecting results have been encouraging. Italy's Eni SpA and Anadarko Petroleum Corp. of the U.S. have made large discoveries in neighboring Mozambique. BG Group PLC last year also made a discovery in Tanzania. 

"This discovery is...an important event for the future development of the Tanzanian gas industry," Tim Dodson, Statoil's executive vice president for exploration, said in prepared remarks. Statoil is the operator of the block with a 65% interest, while Exxon Mobil has the remaining 35%.

The discovery was the second large gas find Exxon Mobil announced in recent days. On Wednesday, Exxon and its partners exploring for hydrocarbons in the Black Sea unveiled a potentially large natural gas discovery. The Domino-1 exploration well, located in the Neptun Block, encountered 70.7 meters of net gas, implying the field can hold between 1.5 trillion and three trillion cubic feet of natural gas. OMV Petrom SA, a subsidiary of the Austrian oil-and-gas company OMV AG, and Exxon Mobil each hold a 50% interest.
The discovery—the first one offshore Romania—is significant as it opens a new frontier. But production is still several years off, according to OMV Petrom. The field lies in an area awarded to Romania in 2009 by the International Court of Justice after a decades-old dispute with Ukraine.

—Katarina Gustafsson contributed to this article. 

Write to Isabel Ordonez at Isabel.ordonez@dowjones.com

Tuesday, January 03, 2012

Kuchangia Wahanga wa Mvua Dar

 Kuchangia Wahanga wa Mvua DSM

 +255786 806028 Kwa Airtel Money

 na


 +255767806028 kwa Mpesa

Wednesday, December 21, 2011

Mafuriko Dar - Hali Ni Mbaya!

Wadau, kutokana na mvua mwingi kumetokea mafuriko ya ajabu mjini Dar es Salaam! Nasikia kuna daraja moja tu, kwenda maeneo ya Mbezi Beach!  Katika mji wa Dar es Salaam hasa Idara ya Mipango Miji naona wamesahau mambo ya STORM DRAINAGE!!!  Hata hivyo kutokana na Ujenzi holela mambo yangekuwa bure!

Nasikia kuna vifo!  Je, RED CROSS/RED CRESCENT wataingia kusaidia waathirika?

Msamaria akimvusha kikongwe mkazi wa Jangwani baada ya makazi yake kuharibiwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia Desemba 20. (Picha na Fadhili Akida).

Jangwani nako  Balaa!

Old Bagamoyo Road baada ya Mafuriko. (Picha kwa hisani ya Michuzi Blog)

BALAA TENKI BOVU


Baada ya daraja kati ya Lugalo na Tenki Bovu (Mbezi Beach) kumegeka...Inabidi watu watembee kwa miguu kwenda upande wa pili wa daraja iliwapate usafiri  kumaliza safari zao.


*****************************
MJI wa Dar es Salaam Umekuwa Ziwa Dar es Salaam

(Picha Zifuatazo Kwa Hisani ya Tutoke Media Blog)



Tuesday, January 12, 2010

Kampeni ya Kitaifa ya Kuchangia Wahanga wa Mafuriko

Wazalendo Wanataaluma Wenzangu; Mtandao Wa Wanataaluma Tanzania (TPN) Kwa kushirikiana na Push Mobile na wadau wengine inaendesha kampeni ya kusaidia wahanga wa mafuriko yaliyoikumba Tanzania tangu wakati wa Siku Kuu ya Krismasi 2009 ambapo maelefu ya watu (hadi sasa zaidi ya 40,000), Familia zaidi ya 8,000 wameathirika kwa kukosa makazi, vyakula, na huduma za afya na kupoteza mali nyingi.

Hadi sasa idadi ya waliokufa inakadiriwa kuwa zaidi ya 14huku kukiwa na hofu ya mlipuko wa magonjwa yatokanayo na maji machafu kama Kipindupindu na Typhoid. Harambee hii inahusu kuwasaidia wananchi wenzetu ambao wako katika hali ngumu kutokana na athari za mvua kubwa na mafuriko. Mafuriko haya hadi hivi sasa yamegusa mikoa ya Morogoro, Dodoma, Shinyanga, Mwanza, Ruvuma, Arusha (Karatu); Rukwa; Tanga; Kilimanjaro n.k.. Na kwa vile mvua zinaendelea kunyesha kuna uwezekano wa maeneo mengi zaidi kuathirika. Uwezo wa Tanzania Red Cross kusaidia ni mdogo sana ukilinganisha na mahitaji.

TPN na wadau wake inaratibu harambee ya kuchangia wahanga wa mafuriko haya kwa kukusanya misaada ya vitu mbalimbali na pesa kwenda kwenye ofisi za Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania. Chama cha Msalaba Mwekundu ndio chombo ambacho kiko mstari wa mbele kuongoza juhudi za kusaidia walioathirika ikishirikiana na taasisi mbalimbali binafsi na vyombo vya serikali.

TPN inatoa wito kwa Wanachama wake, wapenzi na Watanzania kwa ujumla kuchangia kupitia makato ya kila siku ya muda wa maongezi wa simu za mkononi (Zantel; Tigo; Zain na Vodacom): “Changia Shs 150 kwa siku kwa waathirika wa mafuriko. Tuma SMS yenye neno TPN kwenda 15522. Utakatwa Shs 250 kujisajili. Kwa maelezo zaidi wasiliana na 0715 740 047”

Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Maafa cha Chama cha Msalaba Mwekundu Bw. Joseph Kimaryo ambaye TPN na wadau wake ilifanya naye mkutano mahitaji makubwa hivi sasa ni pamoja na Magodoro, Mahema, Vyandarua, Vyakula (visivyoharibika), Maji safi (masanduku ya chupa za maji), Madawa ya kuzuia maambukizi (ambayo hayajaharibika au kufunguliwa), Vifaa kwa ajili ya matumizi ya kina mama na watoto, Makaratasi ya kujipangusia (clean wipes), Fedha kwa ajili ya mahitaji Muhimu na kugharimia usafirishaji na ufikishaji misaaa kwa walengwa, n.k.

Misaada itakapokelewa katika makao makuu ya Msalaba Mwekundu Jijini Dar-es-Salaam Masaki; Mrokao Street/Coral Lane (Karibu na Kora Beach Hotel, barabara ya kwenda Chole) na katika matawi ya Red Cross mikoani pote. Hakuna msaada mdogo au usio na maana na Chama kitapokea misaada ya aina zote. Misaada ya fedha na vitu yaweza kupokelewa kwenye ofisi YOYOTE ya Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania. Au ofisi za Tanzania Professionals Network. Kwa wale watakopenda kutoa michango yao kupitia TPN. Misaada itolewe kwa njia zifuatazo:

1. Crossed Cheque written to: Tanzania Professionals Network

2. Bank Deposits or Transfers to: Account Name: Tanzania Professionals Network, Bank Name: CRDB Bank, Bank Branch: Lumumba Branch, City: Dar Es Salaam, Country: Tanzania, Swift Code: CORUTZ TZ, US $ A/C No: 02J1 007 608 900; TZS A/C No: 01J1 007 608 901

3. M-Pesa (Vodacom): 0768 777 888

4. Z-Pesa (Zantel): 0773 88 18 88

5. Zap (Zain) 0784 00 88 99

6. Western Union — Tuma kwa: Mr. Emmanuel Mmari; TPN Finance and Administrative Manager; Dar Es Salaam. Tuma nakala ya MTCN kwa president@tpn.co.tz

7. Fedha Taslimu: Ofisi za TPN — Barabara ya Nyerere; Jengo la TOHS (Dar Group); Ghorofa ya 1, karibu na Radio Tanzania.

8. Kuchangia kupitia makato ya kila siku ya muda wa maongezi: “Changia Shs 150 kwa siku kwa waathirika wa mafuriko. Tuma SMS yenye neno TPN kwenda 15522. Utakatwa Shs 250 kujisajili. Kwa maelezo zaidi wasiliana na 0715 740 047”

9. Kuchangia vitu mbalimbali: Leta ofisi za TPN — Barabara ya Nyerere; Jengo la TOHS (Dar Group); ghorofa ya 1 karibu na Radio Tanzania au piga simu namba: 0715 740 047 ili ofisa wa TPN avifuate (utalipia usafiri)

10. Kwa kutumia kadi za Kibenki kwa walio USA na sehemu nyingine ambazo kadi hizi hutumika (Visa, MasterCard, Discovery na America Express) kupitia mtandao wa www.mwanakijiji.com , upande wa kulia chini kuna mahali pana nembo yenye maneno “donate”.

Kwa kuanzia TPN imechangia TZS Million 1.0. na tunawaomba wote kila moja kwa nafasi yake kuchangia.

Pamoja Tunaweza! Amua sasa kuwasaidia Wahanga Wa Mafuriko. Kwa maelezo zaidi, tuandikie: president@tpn.co.tz

Tafadhali tuma ujumbe huu kwa wengine wengi.

Imetolewa na:

Sanctus Mtsimbe;

Rais; Mtandao Wa Wanataaluma Tanzania

Tel: 255 754 833 985