Showing posts with label Dar es Saalam. Show all posts
Showing posts with label Dar es Saalam. Show all posts

Saturday, June 24, 2017

Wanawake wa Kanisa La Pentekoste Tanzania Wafanya Kongamano Jijini Dar es Salaam

 Askofu Saldonie Simon Sinde akiwasalimia Wakina mama katika Kongamano la Tatu la Wanawake wa Muungano wa Makani ya Pentekoste Tanzania (UW-MMPT), lililoanza Katika Kanisa hilo Sinza Afrika Sana Dar es Salaam jana. Askofu Sinde pia alivitambulisha vitabu vyake viwili alivyoviandika.

Saturday, October 22, 2016

Pikipiki Mzimu Jijini Dar Yazua Hofu!

 Mwananchi akipita kwa kuikwepa pikipiki yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika Kituo cha waendesha bodaboda cha Maganga Veterinary Dar es Salaam.
 Mwonekano wa pikipiki hiyo kwa nyuma.
Pikipiki hiyo ikiwa katika kijiwe hicho cha  Veterinary Maganga Temeke jijini Dar es Salaam.

Na Dotto Mwaibale

PIKIPIKI yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika kituo cha waendesha bodaboda cha Maganga Veterinary Temeke jijini Dar es Salaam inazua hofu kwa wananchi na hata kwa askari polisi ambao wameshindwa kuipeleka kituoni.

Imeelezwa kwamba pikipiki hiyo iliegeshwa katika eneo hilo na mtu mmoja ambaye alifika nayo akiwa akiiendesha mwishoni mwa mwaka jana.

Akizungumza jana na mtandao wa www. habari za jamii.com mmoja wa waendesha bodaboda wa kituo hicho ambaye hakupenda kujitambulisha jina lake alisema pikipiki hiyo inawapa hofu wananchi wa eneo hilo na hata waendesha bodaboda.

"Hata sisi wenyewe tuna hofu na pikipiki hii ndio maana tunaegesha mbalimbali na pikipiki zetu na ndio maana sitaki kutaja jina langu" alisema mwendesha bodaboda huyo.

Aliongeza kuwa awali baada ya pikipiki hiyo kutelekezwa katika kituo hicho mtu yeyote alipokuwa akiisogelea au kuigusa ilikuwa ikijiwasha yenyewe lakini baada ya kupita mwezi mmoja iliacha kujiwasha jambo ambalo limeongeza hofu kwa wananchi.

Mkazi mwingine wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Ismail alisema hata walipotoa taarifa kituo cha polisi cha Maganga walishindwa kuichukua pikipiki hiyo kutokana na tabia ya kujiwasha.

Alisema aaskari wa kituo hicho ambacho kipo mita 10 na eneo ambalo ipo pikipiki hiyo walitoa taarifa kwa wenzao wa kituo cha Chang'ombe ambao nao wameshindwa kuichukua na kwenda nayo kituoni kwa ajili ya kumtambua mmiliki wa pikipiki hiyo kupitia namba zake za usajili.

Ismail alisema inawezekana pikipiki hiyo ilifungwa kifaa maalumu cha utambuzi iwapo kama imeibiwa na ndio maana ilipokuwa ikiguswa au kusogelewa inajiwasha yenyewe licha ya baadhi ya watu wanahusisha kujiwasha kwake na imani za ushirikina.

Imeelezwa kuwa pikipiki hiyo wakati inatelekezwa ilikuwa katika hali ya upya lakini hivi sasa imeanza kupoteza upya wake kwa kukosa huduma ya matunzo.

Jitihada za mtandao huu kumpata Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa huo wa Maganga ili kuzungumzia suala hilo zimeshindika baada ya kuelekezwa alikuwa Manispaa ya Temeke kwenye mkutano.


Thursday, May 15, 2014

Dengue Fever Awareness

DENGUE FEVER AWARENESS
Dengue is a viral infection spread by mosquitoes.  It is widespread in tropical and sub-tropical regions. In the month of February 2014, the Dar es Salaam Public Health Officials confirmed a new wave of dengue fever cropped up in the most parts of Dar es Salaam and is still continuing.

The first ever recorded fever in Dar es Salaam was recorded in 2010 and in July last year. The Ministry reaffirmed that there were no confirmed death in either two past breakouts.(Tambwe M., Daily Newspaper, 8.2.2014)

Although dengue symptoms, when mild, can seem flulike, there is no vaccine or treatment for the infection other than staying hydrated and taking acetaminophen to manage the pain, other pain killers of the NSAID group like Ibuprofen & Diclofenac are not recommended as they can increase bleeding due to low platelet count (blood clotting cells). Those flulike symptoms also hamper public health officials’ ability to track the disease, because official surveillance of occurrences is based on medical reports and patients may not seek care for what they assume is a bout of flu. An estimated 50 million to 100 million dengue infections occur worldwide yearly, and severe forms of the disease can be fatal, especially among children. Beyond dengue’s death toll, its impact is largely felt in economic terms because sickened people cannot work or attend school.

Many people, especially children and teens, may experience no signs or symptoms during a mild case of dengue fever. When symptoms do occur, they usually begin four to 10 days after the person is bitten by an infected mosquito.

SYMPTOMS
The principal symptoms of dengue fever are listed below. Generally, younger children and those with their first dengue infection have a milder illness than older children and adults.
  • High Fever, up to 41ÂșC
  • Severe Headaches
  • Muscle, bone and joint pain
  • Pain behind your eye
Patient might also experience:
  • Widespread rash
  • Nausea and vomiting
  • Minor bleeding from your gums or nose
Most people recover within a week or so. In some cases, however, symptoms worsen and can become life-threatening. Blood vessels often become damaged and leaky, and the number of clot-forming cells in your bloodstream falls. This can cause:
  • Bleeding from the nose and mouth
  • Severe abdominal pain
  • Persistent vomiting
  • Bleeding under the skin, which may look like bruising
  • Problems with your lungs, liver and heart
  • Red spots or patches on the skin
  • Black, tarry stools (faeces, excrement)
  • Drowsiness or irritability
  • Pale, cold, or clammy skin
  • Difficulty breathing
PREVENTION
There is no vaccine for preventing dengue.
The best preventive measure for residents living in areas infested with Ae. aegypti is to eliminate the places where the mosquito lays her eggs, primarily areas that hold standing water to stop mosquitoes from multiplying
  • Items that collect rainwater or to store water (for example, garbage cans, house gutters, buckets, pool covers, coolers, toys, flower pots, plastic containers, drums, buckets, any other containers, pet's water bowls, or used automobile tires) should be covered or properly discarded.
  • Protect boats and vehicles from rain with traps that don’t accumulate water.
  • Maintain swimming pools in good condition and appropriately chlorinated. Empty plastic swimming pools when not in use.
  • Clothing: Wear shoes, socks, and long pants and long-sleeves. This type of protection may be necessary for people who must work in areas where mosquitoes are present.
  • Apply mosquito repellent containing DEET
  • Use mosquito netting to protect children younger than 2 months old.
  • Cover doors and windows with screens to keep mosquitoes out of your house
  • Repair broken screening on windows, doors, porches, and patios.
  • Using air conditioning or window and door screens reduces the risk of mosquitoes coming indoors.
  • Proper application of mosquito repellents.
  • Mosquito Control: Use screens on doors and windows; use patio insecticides such as Permethrin (pesticide and repellent) and Allethrin (candles and lanterns. Wear long sleeve shirts, long pants, socks and closed shoes to avoid mosquito bites at dusk and dawn especial.
  • Use repellents containing DEET (N, N-diethyl-m-toluamide) or Picaridin on your clothing and exposed skin. Follow manufacturer’s instructions and CDC recommendations. (www.cdc.gov)
 TREATMENT
There is no specific medication for treatment of a dengue infection. Persons who think they have dengue should use pain relievers such as acetaminophen, other pain killers of the NSAID group like Ibuprofen & Diclofenac are not recommended as they can increase bleeding due to low platelet count (blood clotting cells). They should also;
  • Rest,
  • Drink plenty of fluids to prevent dehydration,
  • Avoid mosquito bites while febrile and
  • Consult a physician.
You should see your GP if you develop a fever or flu-like symptoms within two weeks of returning from an area where the dengue virus is common. If a clinical diagnosis is made early, a health care provider can effectively treat you. Kindly VISIT your nearest Health centre for advice and to test and confirm diagnosis of Dengue fever.

Credit: KSIJ Central Board of Education

Thursday, March 14, 2013

Tanzia - Mrs. Suzan Mgwassa

MSIBA DAR: MAMA MGWASSA KATUTOKA

Marehemu Mrs. Suzan Mgwassa

FAMILIA YA MAREHEMU MZEE DAVID ELIYA MGWASSA INASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MPENDWA MAMA YAO, MAMA SUZAN MGWASSA, KILICHOTOKEA TAREHE 13/03/2013 KATIKA HOSPITALI YA AGAKHAN DAR ES SALAAM.

MSIBA UPO NYUMBANI KWAKE MAREHEMU KIJITONYAMA NYUMA YA KAMPUNI MPYA YA VING'AMUZI YA DIGITEK, AMA USONI PA KIJITONYAMA MAGHOROFANI.

SISI TULIMPENDA, BWANA ALIMPENDA ZAIDI NA KUMTWAA. MOLA AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI.

AMINA

Saturday, September 08, 2012

Wazazi Wangu Washerekea Miaka Hamsini ya Ndoa

Wadau, napenda kuwafahamisha kuwa wazazi wangu, Dr. Aleck na Mrs. Rita Che-Mponda wamesherekea miaka hamsini ya ndoa wiki iliyopita mjini Dar es Salaam. Ndoa yao ilibarikiwa katka kanisa la Anglikana St. Albans, Dar es Salaam. Walifunga ndoa mwaka 1961, baba akiwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Howard. Mama alikuwa amemaliza masomo yake ya unesi.

Mungu azidi kuwabariki.

Dr. & Mrs. Aleck Che-Mponda 
Misa ya Kuwabarika St. Albsans




Wazee wakiwa na baadhi ya ndugu


Friday, February 24, 2012

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Uwepo wa Dawa Bandia Kutiba Malaria

TAARIFA KUHUSU UWEPO WA DAWA BANDIA YA KUTIBU UGONJWA WA MALARIA IITWAYO ELOQUINE
 
TAARIFA KWA UMMA
TAARIFA KUHUSU UWEPO WA DAWA BANDIA YA KUTIBU UGONJWA WA MALARIA IITWAYO ELOQUINE (Quinine Sulphate 300mg USP)

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ni wakala wa Serikali iliyo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yenye jukumu la kudhibiti ubora, ufanisi na usalama wa vyakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba ili kulinda afya ya jamii.

TFDA inapenda kuutaarifu umma kuwa imebaini kuwepo kwa dawa bandia ya kutibu ugonjwa wa Malaria katika soko. Dawa hiyo inaitwa Eloquine (Quinine Sulphate 300mg U.S.P) na ipo katika makopo ya vidonge 1000 (elfu moja) kila moja. Maelezo yaliyopo katika lebo yanaonesha kuwa dawa hiyo imetengenezwa na kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd cha nchini Kenya.

Hata hivyo, TFDA imebaini kuwa kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd hakitengenezi dawa yenye jina la biashara la ‘ELOQUINE’. Kiwanda hicho kimesajili Tanzania Quinine Sulphate 300mg B.P isiyo na jina la kibiashara. Aidha, kiwanda cha Elys Chemical Industries Ltd kimebainisha tofauti mbalimbali zilizopo katika lebo ya dawa bandia ikilinganishwa na dawa halisi inayotengenezwa na kiwanda hicho iliyosajiliwa na TFDA na hivyo kuthibitisha kuwa kiwanda hicho hakitengenezi dawa hiyo.

Katika kudhibiti usambazaji wa dawa hiyo hapa nchini, hadi sasa TFDA imekamata jumla ya makopo 155 ya dawa hiyo bandia ya Eloquine jijini Dar Es Salaam yaliyokuwa yakisubiri kusambazwa. Aidha, kopo moja lenye vidonge 115 limekamatwa Moshi, Kilimanjaro. Tayari mtuhumiwa mmoja amekwishafikishwa mahakamani na upelelezi wa chanzo na wasambazaji wa dawa hii unaendelea kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Uchunguzi wa dawa bandia katika maabara umebaini kuwa vidonge hivyo havina kiambato hai (active ingredient) cha Quinine Sulphate kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa Malaria na hivyo matumizi yake ni hatari kwa afya ya binadamu.

Maelezo ya kina yanayotofautisha dawa halisi iliyosajiliwa na dawa bandia ni kama yalivyoainishwa katika jedwali hapa chini.

Dawa halisi iliyosajiliwa
Maelezo ya dawa bandia

· Jina la dawa: Quinine Sulphate 300mg B.P

· Jina la biashara: Haina jina la biashara

· Mtengenezaji: Elys Chemical Industries Ltd, Road B, Off Enterprise Road, P.O Box 40411, 00100 Nairobi, Kenya

· Rangi ya Lebo: Nyeupe na kahawia (Brown)

· Namba ya toleo: Huanzia na namba na siyo herufi. Kwa mfano: 2167E

· Muda wa matumizi (Shelf life): Miaka 4

· Jina la dawa: Quinine Sulphate 300mg U.S.P

· Jina la biashara: ELOQUINE

· Mtengenezaji: Elys Chemical Industries Ltd, Road B, Off Enterpises Road, P.O Box 4011 00100 Nairobi, Kenya

· Rangi la Lebo: Njano na Nyekundu

· Namba ya toleo: GE410

· Tarehe ya kutengenezwa: 04/2009

· Tarehe ya mwisho wa matumizi: 4/2014 (Miaka 5)

Wafanyabiashara wote wa dawa na wananchi wanatahadharishwa kutozitumia dawa hizi na wale wote waliouziwa dawa hizi wanaelekezwa kuzirudisha dawa hizo katika ofisi za TFDA, vituo vya afya vya Serikali au vituo vya polisi vilivyo jirani nao.

TFDA inapenda pia kuwakumbusha wafanyabiashara wa dawa, wasafirishaji wa vifurushi na wananchi kutoa taarifa haraka iwezekanavyo pale wanapohisi kuuziwa dawa duni, bandia au zilizoisha muda wa matumizi. Taarifa zitolewe ofisi za TFDA makao makuu zilizopo Barabara ya Mandela, EPI Mabibo External, Dar es Salaam na Ofisi za Kanda zilizopo mtaa wa Nkurumah, Mwanza, Mtaa wa Sakina – Arusha, Hosptali ya mkoa ya Dodoma na Jengo la Ofisi ya Mifugo Mkoa wa Mbeya.

Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na:-

MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA
EPI MABIBO EXTERNAL,
S.L.P 77150, DAR ES SALAAM
Simu: + 255 222 450512/450751/452108
Nukushi: + 255 222 450793
Barua pepe: info@tfda.or.tz
Tovuti: www.tfda.or.tz

Wednesday, December 21, 2011

Mafuriko Dar - Hali Ni Mbaya!

Wadau, kutokana na mvua mwingi kumetokea mafuriko ya ajabu mjini Dar es Salaam! Nasikia kuna daraja moja tu, kwenda maeneo ya Mbezi Beach!  Katika mji wa Dar es Salaam hasa Idara ya Mipango Miji naona wamesahau mambo ya STORM DRAINAGE!!!  Hata hivyo kutokana na Ujenzi holela mambo yangekuwa bure!

Nasikia kuna vifo!  Je, RED CROSS/RED CRESCENT wataingia kusaidia waathirika?

Msamaria akimvusha kikongwe mkazi wa Jangwani baada ya makazi yake kuharibiwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia Desemba 20. (Picha na Fadhili Akida).

Jangwani nako  Balaa!

Old Bagamoyo Road baada ya Mafuriko. (Picha kwa hisani ya Michuzi Blog)

BALAA TENKI BOVU


Baada ya daraja kati ya Lugalo na Tenki Bovu (Mbezi Beach) kumegeka...Inabidi watu watembee kwa miguu kwenda upande wa pili wa daraja iliwapate usafiri  kumaliza safari zao.


*****************************
MJI wa Dar es Salaam Umekuwa Ziwa Dar es Salaam

(Picha Zifuatazo Kwa Hisani ya Tutoke Media Blog)



Mafuriko Yaua Dar

Kutoka Afriquejet.com

Dar es Salaam, Tanzania - With at least four people reported killed in flash floods, Tanzania's meteorological agency is asking resident's of the country's Indian Ocean coastal areas to brace up for more downpours and flooding. The flash floods followed a heavy rain that hit this commercial capital of the East African country since early Tuesday. Meanwhile, floods have left trails of destroyed properties in slum areas of the city and cut off road links in many suburbs, causing traffic jams throughout the day.

According to Tanzania Meteorological Agency (TMA) Director General Agnes Kijazi, the downpour, which still pounded the coastal belt Wednesday, was due to a pressure build-up over the Indian Ocean.

The rain started with a very strong wind and thunderbolts that blew up some electricity transformers, leaving parts of the city without electricity.

“The situation is likely to last for at least two days,” said Kijazi.

The Police Force and the Tanzania People’s Defence Forces have joined hands, using helicopters in a search and rescue exercise within Dar es Salaam and surrounding areas.

Government officials blame some of the victims in low-lying areas for inviting the disaster after being warned several times to move to higher level ground.

“We have announced many times that people should not construct houses or stay in valleys, but most of them ignored the directive and this is the result,” said Dar es Salaam Regional Commissioner Said Mecky Sadick.

December is usually part of the dry season that runs through to March, when the long rainy season sets in.

http://www.afriquejet.com/tanzania-downpour-floods-dar-es-salaam-claims-four-lives-2011122130103.html

Kwa habari zaidi someni:

http://www.ippmedia.com/frontend/index.php?l=36630

http://thecitizen.co.tz/component/content/article/37-tanzania-top-news-story/18142-disaster-as-floods-kill-4.html

Saturday, December 10, 2011

New Africa Hotel 1936

New Africa Hotel, Dar es Salaam,Tanganyika
Wadau hebu cheki New Africa Hotel ilivyokuwa mwaka 1936 enzi za Ukoloni!