Showing posts with label Elimu. Show all posts
Showing posts with label Elimu. Show all posts

Saturday, November 02, 2019

Leah Mwamoto Awaonya Wazazi wa Kilolo Wanaokatisha Masomo ya Wanafunzi

Mjumbe wa halmashauri Kuu (CCM) Mkoa wa Iringa, Leah Mwamoto akiongea na wazazi wa shule ya sekondari ya Mlafu iliyopo katika wilaya ya Kilolo mkoani Iringa
 Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mlafu iliyopo katika wilaya ya Kilolo mkoani Iringa wakicheza nyimbo mbele ya mgeni Rasmi

NA FREDY MGUNDA,KILOLO

Mjumbe wa halmashauri Kuu (CCM) Mkoa wa Iringa, Leah Mwamoto amewaonya wazazi wanaokatisha masomo watoto kuwa serikali itawachukulia hatua kali pindi watakapobainika kufanya kosa hilo.

Mwamoto ameongea hayo katika mahafali ya kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Mlafu iliyopo katika kijiji cha Mlafu wilayani Kilolo alipomuwakilisha mbunge wa jimbo la Kilolo Venance Mwamoto.

Akiwaonya wazazi katika mahafali hayo Mwamoto amewaeleza wazazi juu ya mazingira mabaya wanayoyakuta watoto wanaokwenda kufanya kazi za ndani katika miji mikubwa.

Hata hivyo amewaomba watendaji wa kata kuendelea kuwafutilia watoto ili kuwaepusha kujiingiza katika mazingira hatarishi yatakayoharibu ndoto zao.

Aidha Mwamoto amepongeza uongozi wa shule ya sekondari Mlafu kwa matokeo mazuri pamoja na mbunge wa jimbo la Kilolo, Mhe Venance Mwamoto kuchangia bati 180 na mifuko 100 ya saruji kwa ujenzi wa zahanati kijiji cha Mlafu.

Awali akisoma taarifa fupi ya shule mwalimu mkuu wa shule hiyo Emmanuel Mbangwa ameomba wadau kujitokeza kuboresha mazingira katika shule hiyo hususani kujenga nyumba za walimu na mabweni.

Nae diwani Mlafu Isidory Kiyenge amewataka wazazi wa kata hiyo pamoja na wadau kuwa tayari kuchangia katika sekta ya elimu ili kuongeza mazingira ya ufaulu.

Kayenge amewataka wanafunzi kujiandaa kwa mitihani ya kidato cha nne huku alito ahadi ya kuwaandalia chakula wakati wa mitihani.

Saturday, January 13, 2018

Serikali Yazipiga Marufuku Shule Binafsi Kukaririsha au Kufukuza Wanafunzi Walioshindwa Kufaulu

Serikali imezuia shule binafsi kumrudisha darasa, kufukuza mwanafunzi aliyefaulu mtihani darasa la 4, kidato cha 2 kwa kutofikia ufaulu wa shule husika.

Waraka wa Elimu Namba 7 wa Mwaka 2004 umepiga marufuku utaratibu wa shule zisizo za serikali kukaririsha Darasa, kufukuza au kuhamisha mwanafunzi aliyefaulu Mtihani wa Darasa la Nne, Kidato cha pili kwa kigezo cha wanafunzi hao kutofikia wastani wa ufaulu wa shule husika.




Saturday, November 12, 2016

Miss Tanzania 2010, Genevieve Mpangala Kusaidia Kurejesha Heshima ya Elimu Tabora

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010 Genevieve Mpangala amejitosa kusaidia kurejesha heshima ya mkoa wa Tabora katika elimu hasa kwa wasichana ambao ndio nguzo kubwa kwa familia na maendeleo ya taifa.

Mrembo huyo ameamua kufanya hivyo kwa kutembelea shule mbili za Tabora Girls na Isevya kuongea na wanafunzi, kuwapa moyo na kuangalia matatizo yanayowasumbua katika kujipatia elimu.

Akizungumza na Moblog amesema kwamba amekuwa na masikitiko makubwa na matokeo ya mitihani ya kitaifa ya sekondari kwa miaka mitatu ilhali simulizi za Tabora miaka iliyopita ni za kufurahisha sana uikionesha kwamba mkoa huo ndio kitovu hasa cha elimu.

Anasema ukisoma nyaraka mbalimbali unaona jinsi Tabora ilivyokuwa ngome ya elimu huku watanzania wengi wakifika hapo pia kupata elimu ya sekondari.

Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010, Genevieve Mpangala akizungumza wa shule ya sekondari Tabora Girls hivi karibuni.

“Kwa kweli pamoja na masimulizi mazuri kuhusu elimu Tabora miaka ya 80 na 90 ,nilichagua Tabora girls kwa sababu ni shule aliyosoma mama yangu mzazi form 1 mwaka 1977 mpaka 1980 mpaka na aliisifia sana shule yake hiyo na nikapenda niweze kuwa karibu nao kuhakikisha wanafunzi wote wanamaliza,na Isevya ilikua chaguo la pili kwasababu ilikua ni shule ya kutwa (day) na nilipendelea kuongea na wanafunzi hao” alisema Genevieve.

Mkoa wa Tabora ambao unapatikana kati ya Magharibi ya Tanzania kwenye uwanda wa latitudo 40-70 Kusini na longitudo 310 - 340 mashariki ukipakana na mikoa ya Shinyanga, Katavi, Singida, Kigoma na Dodoma ni mji ulioanzishwa na wafanyabiashara wa Kiarabu kwenye miaka ya 1850 ukijulikana kama Kazeh .

Kihistoria Kazeh ambayo ilikuwa kitovu cha biashara ya utumwa, mwaka 1871 robo ya mji ilichomwa moto na kuvurugwa na mtawala wa wanyamwezi Mirambo .

Ingawa mwaka 1885 hadi 1891 wajerumani walijaribu kutawala, historia zinasema kwamba mji huo ulikuwa na vurugu kubwa lakini baadae ukatawaliwa na wajerumani wakafanya mji wa utawala kabla ya vita kuu ya kwanza kuingia na wao kung’olewa.
Mrembo wa taji la Miss Tanzania 2010 Genevieve Mpangala akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi na mwalimu wao alipofanya ziara shuleni hapo.

Pamoja na historia yenye misukosuko ya Mkoa wa Tabora ambao ni moja ya mikoa yenye eneo kubwa unategemea sana kilimo kufanikisha maisha lakini kwa miaka mingi mkoa umekuwa ukididimia kimaendeleo na kijamii.

Mkoa wa Tabora ambao umekua wa mwisho kwa miaka mitatu mfululizo mwaka 2013,2014 na 2015 unahitaji nguvu kubwa ya kujiondoa katika shida ya kuporomoka katika elimu

Mrembo Genevieve anasema ziara yake katika shule hizo imemfumbua macho na kuona haja kubwa ya kuendelea na programu za kufufua matumaini.

Pamoja na kuwashukuru walimu kwa ushirikiano waliompa aliwataka wanafunzi kuweka mkazo katika imani, matumaini na kutekeleza ndoto zao katika uwanda mkubwa zaidi.
Aidha pamoja na kuzungumza "HAVE FAITH,HOPE FOR MORE AND DREAM EVEN BIGGER", pia aliwaasa kuwa elimu ni msingi mzuri wa maisha na kuwa wasiharakishe na kupotoshwa na mambo ya kidunia kwani haya maisha yapo.

Akiwa na wasichana wa shule ya Tabora Girls walimweleza changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni pamoja na kutokuwepo na uzio kwenye shule yao hiyo, uhaba wa vitabu, upungufu wa walimu, uhaba wa upatikanaji wa habari mubashara, kwa wanafunzi kwamba hawana king'amuzi,kwa wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi wanauhitaji wa msaada wa kofia pamoja na mafuta ya kuwakinga na jua.

Matatizo hayo yanatokana zaidi na kwamba wengi wao wanatoka kwenye mazingira duni. Changamoto nyingine ni pamoja na kuwa na zahanati ambayo ina uhaba wa vifaa mfano:vyandarua vya kutosha pamoja na vitanda,pia kwa wanafunzi ambao wanaulemavu wa macho ambao ni hafifu na vipofu kabisa hivyo kuna uhaba wa brail paper.

Ziara fupi ya Mrembo wa Tanzania 2010 Genevieve Mpangala kwa shule mbili za jijini Tabora za Isevya Secondary School na shule ya vipaji maalum ya wanawake Tabora girls.

Amesema katika mazungumzo yake na wanafunzi hao amebaini pia kwamba kutofanya vyema kwa wanafunzi pia kunasababishwa na wanafunzi hao kutumia madawa ya kulevya, utoro, mimba za shuleni na wazazi kuozesha mabinti katika umri mdogo kabla ya wao kumaliza shule.

Saturday, September 10, 2016

UNESCO Yazindua Ripoti ya Ufuatliaji wa Elimu Duniani (GEM) 2016

 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez akimkabidhi mgeni rasmi, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta, sanduku la Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM).
 Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya siku ya kisomo, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta akigawa Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani 2016 (GEM) kwa baadhi ya wafanyakazi wa wizara yake.


Na Mwandishi wetu
Katika kutambua umuhimu wa kusoma na kuandika Tanzania na mataifa mengine duniani zimeungana kwa pamoja kuadhimisha siku ya Kisomo Duniani ambayo huadhimishwa kila Septemba, 8 ya kila mwaka ambapo pamoja na maadhimisho hayo pia iliambatana na Uzinduzi wa Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani (GEM).

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Zulmira Rodriguez alisema kuwa dhumuni la UNESCO kuweka siku hii ya Septemba 8 kila mwaka kuwa siku ya kisomo kimataifa ili kuziunganisha jamii zote za kimataifa duniani kuweka na kuendeleza nguvu na juhudi kwa watu kujua kusoma na kuandika ili kuleta maendeleo katika jamii mbalimbali.

“Kauli mbiu hii inatufungulia milango ya uelewa juu ya malengo na mafanikio ya miongo mitano iliyopita ambayo yaliwekwa ya kutaka kila mtu anajua kusoma,” alisema Bi. Rodrieguez na kuongeza.

“Tunataka kujua ni changamoto gani zinazoikabili sekta ya elimu katika kusoma na kuandika na tunataka kufahamu namna ya kukabiliana na changamoto hizo ili kufikia malengo ambayo UNESCO iliyakusudia kufikiwa ya kila mmoja awe anajua kusoma.”

Kwa upande wa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Kaimu Kamishna wa Elimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bw. Nicholaus Bureta ambaye alimuwakilisha Mgeni Rasmi, Katibu Mkuu wa wizara hiyo alisema serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imejizatiti kuondoa tabaka la wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa vijana na watu wazima kwa kujenga uwiano sawa wa utoaji wa elimu kwa watu wote.

“Wizara imejipanga vizuri, na lengo kubwa la wizara ni kuhakikisha tunakuwa na mtanzania aliye elimika na aliye na stadi, maarifa na uwezo wa kutumia elimu aliyoipata,” alifafanua Bureta.

Vile vile Bw. Bureta amesema kwa sasa wizara ipo kwenye mpango wa kukuza stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) ambao unaanzia chini kwa wanafunzi wa awali mpaka shule za msingi.

Katika mpango huo walimu wamekuwa wakipata mafunzo mbalimbali ya namna ya kumuwezesha mwanafunzi kujua Kusoma Kuandika na Kuhesabu katika ngazi ya elimu ya awali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi, Basilina Levira amesema kwamba kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012, asilimia 78 ya vijana na watu wazima ndio waliokuwa wakijua kusoma na kuandika.

Akaongeza kuwa mwaka 2015 idadi hiyo ya wanaojua kusoma na kuandika ilishuka na kufikia asilimia 77 ambapo ilipelekea wizara hiyo kutoka na mikakati inayokusudia kuondoa kabisa tabaka la watu wasiojua kusoma na kuandika nchini.

Aidha, Basilina amesema kuwa Serikali ilipitisha sheria ya vyumba vya madarasa ya shule zote nchini kutumika kufundishia vijana na watu wazima ambao hawajui kusoma na kuandika muda wa jioni baada ya wanafunzi wa kawaida wanapomaliza masomo yao.

Amefafanua kwa kusema kuwa, wizara imeandaa programu ambayo iko kwenye mfumo wa Televisheni na picha za video (DVD) yenye masomo 65 ya kujifunza kusoma, kuandika na kuhesabu, ambapo kwa kutumia programu hiyo mwanafunzi anaweza kujua kusoma, kuandika na kuhesabu kwa muda wa miezi 4 mpaka 6.
Mafunzo hayo kwa njia ya Televisheni na Picha za Video tayari yameanza kutumika kwa wilaya za Ilemela, Dodoma Manispaa, Songea Manispaa, Bagamoyo, Mkuranga, Temeke, Ilala na Kinondoni, ambapo asilimia 65 ya vijana na watu wazima wasiojua kusoma na kuandika wamejitokeza kujiunga na Elimu hiyo huku idadi kubwa ikiwa ni ya wanawake.

Siku ya Kisomo Duniani huadhimishwa Duniani kote kila ifikapo Septemba, 8 ya kila ya mwaka, ambapo mwaka huu 2016 maadhimisho hayo yametimiza miaka 50 tangu yalipoanza kuadhimishwa mwaka 1966.

Kauli mbiu ya siku ya kisomo duniani kwa mwaka huu ni ‘Tunasoma yaliyopita, Tunaandika yajayo, Elimu endelevu’ ambayo kwa lugha ya kiingereza ni ‘Reading the future, Writing the past’.

Saturday, March 19, 2016

Uamuzi wa Kutoa Elimu Bure Utachochea Usawa wa Kijinsia

Hayo yalisemwa na Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb.)wakati akitoa taarifa ya nchi katika Mkutano wa 60 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hali ya Wanawake Duniani (CSW).

Mhe Ummy alieleza kuwa Adhma ya Mheshimiwa Dkt John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kutoa Elimu bure kwa shule za Msingi na Sekondari itakuwa na matokeo makubwa ya kuongeza udahili wa wanafunzi katika Elimu ya msingi, Sekondari na Elimu ya juu.

Akaongeza kwamba uimarishwaji wa upatikananaji wa elimu kwa wanawake ni msingi mkubwa wa kuwezesha wanawake kiuchumi, kwakuwa elimu hutoa ujuzi, maarifa na hali ya kujiamini kwa wanawake kuendea fursa za kiuchumi.

Ummy Mwalimu -CSW

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ( Mb) akizungumza wakati wa majadiliano kuhusu dhima ya uwezeshwaji wa wanawake na uhusiano wake na utekelezaji wa Agenda 2030. katika mchango wake Waziri anayeongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Wanawake amesema Serikali inatambua umuhimu wa mwanamke katika utekelezaji wa ajenda mpya ya maendeleo endelevu ( Agenda 2030) na kwamba itaendelea kumwezesha.

Katika Taarifa hiyo, Mheshimiwa Waziri, alieleza kuwa Serikali ya Tanzania inatambua kuwa uwezeshaji wa wanawake na Usawa wa jinsia unachangia kwa kiasi kikubwa kufikiwa kwa wepesi kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu ( Sustainable Development Goals). Kwa kutambua hilo Tanzania imejipanga kuhuisha Ajenda 2030 katika Sera, Sheria na Mipango ya nchi kwa kuhakikisha kunakuwa wa sheria zinazolenga kuleta Usawa wa Jinsia na uwezeshaji wa wanawake, ambapo pamoja na mambo mengine utekelezaji wa Mikakati, Sera na Sheria utaendelea kuzingatia haki ya kielimu kwa Wanawake na Wasichana.

Mheshimiwa Ummy, aliongelea pia umuhimu wa Afya kwa wanawake na Wasichana (ikiwa ni pamoja kupunguza vifo vya wajawazito na watoto) kama njia ya kumuwezesha mwanamke kushiriki kikamilifu katika uzalishaji mali.

Mkutano huo wa wiki mbili unafanyika NewYork, Marekani kuanzia tarehe 14-24 Machi 2016, ukihusisha wawakilishi kutoka serikali mbalimbali duniani na Asasi za Kiraia ambapo hujadiliana na kubadilishana uzoefu na kuelimishana kuhusu hatua mbalimbali ambazo Serikali zao zinachukua katika kuboresha maisha ya mwanamke na mtoto wa kike.

Ummy Mwalimu - CSW

Mheshimiwa Ummy Mwalimu akiwa pamoja na Mhe. Balozi Tuvako Manongi na Mhe Peter Serukamba (Mb.), mara baada ya kuwasilisha taarifa ya Tanzania kuhusu Masuala ya Maendeleo ya Wanawake.

Saturday, June 28, 2014

TAMWA kutoa Elimu Kupambana na Ulevi Kupindukia

TAMWA kutoa elimu kupambana na ulevi Kupindukia
Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Valerie Msoka akisisitiza jambo katika mkutano na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo.
KITUO cha Usuluhishi (CRC) kinachofanya kazi chini ya Chama cha Wanahabari Wanawakecha (TAMWA) kimejipanga kutoa elimu kwa jamii kuhakikisha kinapambana na matumizi ya pombe kupindukia kwa jamii suala ambalo limezidisha vitendo vya ukatili wa jinsia unaofanywa na watumiaji pombe kupindukia.

Akizungumza na wahariri wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Valerie Msoka alisema utafiti uliofanywa na Shirika la IOGT International unaonesha kuwa kiwango cha unywaji pombe jijini Dar es Salaam ni asilimia 47.6 kwa wanaume na asilimia 29 kwa wanawake huku ikibainika kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya vitendo vya ukatili na matumizi ya pombe kupita kiasi. 

Bi. Soka alisema takwimu zinaonesha kuwa wanawake ambao waume zao wanalewa mara kwa mara wengi wao wanakumbana na ukatili unaohusisha vipigo, kuumizwa na ukatili wa kingono kwa asilimia 77, huku kiwango cha ukatili kwa wanawake ambao waume ama wenzi wao hawanywi pombe ni asilimia 33.

"...Utafiti uliofanywa na shirika la IOGT International unaonyesha kwamba kiwango cha unywaji pombe katika jiji la Dar es Salaam ni asilimia 47.6 kwa wanaume na asilimia 29 kwa wanawake...lakini takwimu kutokana na utafiti wa Demographia na Afya Tanzania (TDHS) 2010...unaonesha wanawake ambao waume zao wanalewa mara kwa mara wengi wao wanakumbana na ukatili unaohusisha kipigo/kuumizwa na ukatili wa kingono kwa asilimia 77," alisema.

Aidha aliviomba vyombo vya habari kushirikiana na TAMWA kutoa elimu kwa jamii kupunguza matumizi ya pombe kupindukia kwani licha ya ukatili huo familia pia zimekuwa zikiathirika kiuchumi juu ya matumizi ya pombe huku baadhi ya watoto wakikosa huduma za msingi kutoka kwa baadhi ya wazazi ambao ni walevi kupindukia.

Alisema TAMWA inatekeleza mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na wasichana unaosababishwa na pombe huku lengo kuu ikiwa ni kuhakikisha maisha ya wanawake na watoto yanaboreshwa kwa kuimarisha sheria na kupunguza ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe kupindukia.

Hata hivyo alisema tayari chama hicho kimeanza kufanya utafiti mwingine katika Wilaya ya Kinondoni kuangalia madhara yanayotokana na unywaji wa pombe kupindukia ili kuangalia hali halisi ya matumizi ya pombe eneo hilo na madhara ambayo yamekuwa yakitokana na matumizi hayo.

Alisema malengo mengine ya mradi ni pamoja na kuboresha maisha ya wanawake na watoto kwa kuimarisha sheria na kupunguza ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe katika wilaya ya Kinondoni na pia kujenga uelewa miongoni mwa jamii juu ya madhara yatokanayo na unywaji wa pombe kupindukia. 

Mkurugenzi huyo Mtendaji wa TAMWA aliongeza kuwa mapambano hayo pia yatasaidia, kukabiliana na matumizi ya pombe na kutoa taarifa kwa vyombo husika kuhusu ukatili dhidi ya wanawake unaotokana na matumizi ya pombe, ikiwa ni pamoja na kujenga uwezo wa jamii kukabiliana na ukatili unaosababishwa na unywaji wa pombe dhidi ya wanawake na watoto.

Saturday, February 01, 2014

Tanzania Iko Nyuma Kwenye UPE (Universal Primary Education) - United Nations


Overcrowded Tanzanian Primary School Classroom

UNITED NATIONS (AP) - At least 250 million of the world's 650 million primary school age children are unable to read, write or do basic mathematics, according to a report Wednesday commissioned by the U.N. education agency.

   The report found that 130 million are in primary school but have not achieved the minimum benchmarks for learning, and almost 120 million have spent little or no time in a classroom including 57 million youngsters who are not attending school.

   The independent research team that wrote the report for UNESCO, the U.N. Educational, Scientific and Cultural Organization, calculated that the cost of 250 million children around the world not learning translates to a loss for governments of around $129 billion annually.

   UNESCO's U.N. representative Vibeke Jensen said this global "learning crisis" is mainly caused by a lack of well-trained teachers, especially in impoverished areas.

   "While more children are in school, it's been at the cost of quality," she said at a news conference launching the report. "The issue now is to put the focus on quality."

   In a third of countries analyzed by the team, less than 75 percent of the primary school teachers had been trained to meet national standards.

   "Teachers have the future of this generation in their hands," UNESCO's Director-General Irina Bokova said in a statement. "We need 5.2 million teachers to be recruited by 2015, and we need to work harder to support them in providing children with their right to a universal, free and quality education."

   The report said that ensuring an equal, quality education can increase a country's gross domestic product per capita by 23 percent over 40 years.

   But according to the report, almost half the children out of school globally are expected never to make it into a classroom - and that includes almost two-thirds of girls in Arab states and sub-Saharan Africa.

   The research team reported that almost half the world's out-of-school population of 57 million live in conflict-affected areas, up from 42 percent in 2008.

   It estimated that 14 countries had more than one million children out of school in 2011 including Afghanistan, China, Congo, Somalia, Sudan before its break-up, and Tanzania.

   On the plus side, it said three countries reduced their out-of-school populations by at least 85 percent in the last five years - Laos, Rwanda and Vietnam.

   World leaders set a goal in 2000 of giving every child a primary school education by 2015 but the report said it is "likely to be missed by a wide margin."

   Sub-Saharan Africa is the region lagging farthest behind.

   The researchers forecast that if recent trends in the region continue, the richest boys will achieve the goal of completing primary education in 2021 but the poorest girls will not catch up until 2086.

Thursday, October 11, 2012

Wasichana Wanaosaidiwa na Flaviana Matata Foundation



Leo ni sikukuu ya Kimataifa ya Msichana.  Flaviana Matata Foundation imetoa picha hii ili kuweza kuwatambulisha wasichana wanao wasaidia katika elimu. 
Hongera kwa Kazi nzuri Flaviana Matata Foundation.

Monday, April 23, 2012

Kiingereza ni Kasumba!


Kufundishia Kiingereza nchini: Ni Kasumba tu Inayodumaza Elimu!

• Angalia Saa yako, unahesabu Saa kwa Kiswahili, lakini lazima utakuwa umeirekebisha isomeke kwa Kiingereza!

Na Saidi Nguba

Rais wa Kwanza wa Afrika Kusini huru, Nelson R. Mandela, aliwahi kusema katika nukuu zake nyingi za busara, kwa Kiingereza:“If you talk to a man in a language he understands, that goes to his head. If you talk to him in his language, that goes to his heart.” Kwa tafsiri yangu, ya Kiswahili: “Ukizungumza na mtu neno katika lugha anayoielewa, linamuingia kichwani. Lakini ukizungumza naye katika lugha yake, linamuingia moyoni mwake”.

Mbunge, Profesa Kulikoyela Kanalwanda Kahigi, ambaye ni mtaalamu wa lugha, akizungumza katika mjadala wa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, bungeni mjini Dodoma Agosti mwaka 2011 alisema: “Lugha ni nguzo ya msingi ya kujenga uzalendo.

Vinginevyo utajengaje uzalendo kwa kutumia lugha ya kukopa ya kigeni?”.

Profesa Kahigi aliongeza: “Tunawafundishia vijana wetu kwa Kiingereza.

Je, tunawapa maarifa vijana wetu au tunawafurahisha mabwana zetu?”.

Hii ndiyo hali ilivyo nchini Tanzania, tuna kasumba ya Kiingereza, lugha ya kigeni na lugha ya kikoloni. Mpaka sasa, miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara, uamuzi haujafanywa wa kuitumia Lugha hii adhimu ya Kiswahili kufundishia nchini katika ngazi zote, pamoja na kuwa lugha hiyo ina vigezo vyote vya kukidhi kazi hiyo. Hii haina maana kukipuuza Kiingereza, ambacho watu wengine hapa nchini wanakiita kuwa ni “Kiswahili cha Dunia”. Ni vizuri Kiswahili kifundishwe vizuri, kitumike kufundishia na Kiingereza pia kifundishwe vizuri kama lugha na liwe ni somo la lazima kwa kila mwanafunzi kuanzia darasa la kwanza, hadi Sekondari, ili wanafunzi wote, wakifika kidato cha nne, kwa mfano, wazungumze na kuandika lugha hiyo kwa ufasaha mkubwa.

Kasumba imefikia kuona jambo hili kuwa ni kitu cha kawaida. Kwa mfano, ukimuuliza mtumiaji wa Kiswahili, je, sasa saa ngapi? Atakujibu, sasa ni saa 6. Lakini mwambie aangalie alivyorekebisha saa yake. Utaona mshale, badala ya kuwa katika sita, uko kwenye namba 12, kama vile walivyozoea Waingereza, kwa mfumo wao wa kujua wakati. Saa 6 ya mchana, kwa Kiswahili, Kiingereza siyo “Six o’clock” ni “Twelve o’clock”!

Kiingereza ni Lugha siyo Elimu

Swali la kujiuliza: Je ni kwa nini basi tunaendelea na kasumba hii ya kukipa kipaumbele Kiingereza na kupata kigugumizi cha kukitumia Kiswahili kufundishia katika ngazi zote?

Ubishi unaoenea kwa kasi ni kuwa Kiingereza ni “Lugha ya Kimataifa” na kwamba kwa kufundishia, vijana wetu watakuwa na elimu inayolingana kimataifa. Pili, kwa vile hakuna vitabu vya kutosha vya Kiswahili, ukilinganisha na vya Kiingereza, kufundishia Kiswahili, ni tatizo.

Sababu zote hizi zinamfurahisha zaidi Mwingereza tu.

Ukweli ni kwamba Kiingereza ni lugha tu na mtu anaweza akajifunza, na kwa utaalamu wa kisasa wa kufundisha lugha na nyenzo zilizopo, hata kwa miezi mitatu mtu anaweza akakielewa na kuzungumza. Lugha siyo elimu, isipokuwa ni chombo cha kusaidia kutolea elimu. Elimu ni uwezo mkubwa wa kuelewa na kugundua mambo, ili hayo unayoyaelewa na kuyagundua yatakusaidia kuleta mageuzi katika maisha yako na ya binadamu wengine, kutoka kiwango fulani na kwenda kiwango cha juu zaidi chenye kuleta manufaa na tija. Ili elimu nayo itolewe kwa vizuri zaidi ni lazima lugha ya kufundishia iwe ile ambayo anayefundisha na anayefundishwa wote wanaifahamu vizuri. Pili, hakuna vitabu vya Kiswahili nchini kwa sababu havina soko. Mara uamuzi wa kufundishia Kiswahili utakapochukuliwa, basi vitabu vya Kiswahili vitakuwa biashara kubwa na vitaanzishwa hata “viwanda” vya kufyatua vitabu vya elimu mbalimbali kutoka lugha za kigeni na kuwa vya Kiswahili.

Wataalamu Wamekwishathibitisha

Uwezo wa Kiswahili kufundishia ili hatimaye elimu ikue kwa kiwango kikubwa nchini na kujenga taifa la kujitegemea badala ya kuendelea kuwategemea wengine kwa kila kitu, siyo mahitaji ya kisiasa, bali ni jambo linalowezekana na lililothibitishwa na wanataaluma wa elimu na wa lugha pia.

Profesa John Kiango, Mkurugenzi wa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wakati anamkaribisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuzindua Taasisi mpya ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Julai 26, 2009, alisema: “Nikiwa mtaalamu wa lugha, napenda nichukue nafasi hii, kukuhakikishia kuwa Kiswahili kinaweza, na kikipewa nafasi kitaleta mageuzi ya kitaalamu na kiugunduzi nchini.”

Anaongeza:“Tafiti zimebaini kuwa nchi zote zilizo na ugunduzi asilia ambao siyo ule wa kuiga ni zile zinazotumia lugha zao. Nchi zinazotumia lugha za kigeni katika kutolea elimu zimebaki kuwa watumiaji wa teknolojia zilizogunduliwa mahali pengine, teknolojia ambazo tunauziwa kwa bei mbaya sana.”

Hatutaki tu kuuona ukweli. Kwa mfano, ukimuandaa mtaalamu wa Kilimo hadi anapata shahada, akija kuwa Bwana shamba kijijini, je elimu yake atawapatia wale wakulima kule vijijini kwa lugha gani? Kiingereza, alichojifundishia au kwa lugha ambayo walengwa wanaielewa? Kwa vile madhumuni ya elimu ni kwa watakaobahatika kuipata wawagawie maarifa na huduma wengine, kwa nini sasa tunalazimika hapa hapa nchini ambako tuna lugha yetu, kuifundisha elimu hiyo kwa lugha ya kigeni na ya kikoloni? Kama elimu utaipata kutoka China, ni dhahiri lazima kujifunza kwa Kichina.

Katika kitabu “Focus on fresh data on the Language of Instruction debate in Tanzania and South Africa” kilichoandikwa na Brigit Brock- Utne, Zubeida Desai na Martha Qorro, mwaka 2006, ikiwa ni sehemu ya matokeo ya tafiti za LOITASA (Language of Instruction in Tanzania and South Africa) ambayo ni Mradi wa NUFU (The Norwegian Programme for Development Research and Education) ulioanza mwaka 2001 na unaomalizika mwishoni mwa mwaka 2011, imebainishwa jinsi lugha ya Kiingereza ilivyokuwa tatizo katika ufundishaji kwenye shule za Sekondari nchini Tanzania.

Utafiti wa LOITASA ulifanywa katika shule mbili za Sekondari kwa kutumia utaratibu wa kufundishia somo la Baiolojia – darasa moja kwa Kiingereza na darasa jingine kwa Kiswahili. Kwa mujibu wa kitabu hicho, katika darasa lililokuwa linafundishiwa Kiingereza, wanafunzi walionekana kutochangamka na hawakuelewa kilichokuwa kinaendelea, wakati lile la Kiswahili, wanafunzi walikuwa wanachangia kwa uelewa wa hali ya juu na ukawepo mjadala wenye tija baina ya mwalimu na wanafunzi.

Tume ya Rais ya Elimu, iliyojulikana kuwa Tume ya Makweta (mwanasiasa na mwanataluma mashuhuri nchini) ilitoa mapendekezo ya kutaka Kiswahili kitumike katika ngazi zote, hatua kwa hatua, kuanzia kidato cha kwanza mwaka 1985 na Chuo Kikuu kuanzia mwaka 1992. Mapendekezo hayo mpaka sasa hayajatekelezwa.

Mapema tangu mwaka 1953, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), lilitoa azimio lililosema, pamoja na mambo mengine, ni vema hasa kwa elimu ya msingi kwa watoto wadogo, kuwafundisha kwa lugha wanazozielewa vizuri na hasa lugha za mama zao.

Sasa, kama wataalamu wamekwishamaliza kazi yao na kuthibitisha kuwa Kiswahili ni lugha inayojitosheleza kwa msamiati karibu katika kila fani, mbona Kiswahili hakitumiki nchini katika kufundishia, hasa elimu ya juu? Kwa nini?

Jibu la uhakika ni kwanza, matokeo na athari ya kutawaliwa na Waingereza na hivyo kupandikiza ndani ya akili zetu hali ya kutojiamini wenyewe, kuanzia katika lugha na hata katika maeneo mengine. Kazi yetu ni kuwategemea wengine, wa nje tu. Pili, kasumba tu ya kawaida kwamba Kiingereza ndiyo elimu na tatu ni kusita kuchukua uamuzi.

Sera; Dira, Hazitekelezwi

Sera ya Elimu ya Mwaka 1995 nchini inasema kuwa Lugha ya Kufundishia ni Kiswahili na Kiingereza. Sera hiyo inafanyiwa mapitio, lakini katika maandiko ya awali ya marekebisho yanayopendekezwa, haionekani kwamba uamuzi unafanywa wa kukitumia Kiswahili katika ngazi zote.

Kwa mfumo wa sasa nchini, kuanzia shule ya awali hadi darasa la saba, lugha ya kufundishia ni Kiswahili, lakini kuanzia kidato cha kwanza hadi kwenye vyuo, lugha ni Kiingereza. Ingawa ukweli ni kwamba hata kwenye vyuo, mwalimu akiona haeleweki kwenye ukumbi wa mhadhara, huwa anabadilisha lugha na anatumia Kiswahili na mara mambo yanabadilika na kwenda vizuri.

Katika Sera imetamkwa rasmi kuwa: “Serikali itakuza elimu ya awali ya watoto wenye umri wa miaka 0-6. Elimu hii itahakikisha kudumishwa kwa maadili yetu kiutamaduni”. Lakini hali halisi ya sasa, ni tofauti na tamko la Sera. Siku hizi kuna shule za binafsi nyingi zilizochipukia zinazofundisha kwa Kiingereza, ziitwazo kwa Kiingereza “English-Medium Schools”, hata kwa zile za elimu ya awali, tena nyingine ada ni lazima kulipwa kwa fedha za kigeni, hasa za Kimarekani, Dola! Kwa msingi huo, haitawezekana kuwa elimu hiyo “itahakikisha kudumishwa kwa maadili yetu ya kitamaduni”, kama yenyewe inatolewa kwa lugha ya kigeni ya kikoloni na kulipiwa kwa fedha za kigeni!.

Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, sehemu yake inasema: “Tanzania haina budi ijijengee misingi ya kujitegemea inayotokana na mazingira ya ukombozi wa kisakolojia, kifikra na kuweza kujiamini ili jamii iweze kuamua kuliongoza gurudumu lake la maendeleo kwa lengo la kutosheleza mahitaji ya msingi ya watu wote, wanaume, wanawake na watoto”. Je, tutaliweza hilo kwa kufundishia lugha ya kigeni, ya kikoloni?

Ni Siasa, Uchumi na Utamaduni

Karibu nchi zote duniani, zinatumia lugha zao kufundishia. Lakini katika Afrika karibu nchi zote (isipokuwa Ethiopia, inayotumia lugha yake ya Amharic na maandishi yake, pamoja na nchi za Kaskazini mwa Afrika zinazotumia Kiarabu na maandishi yake) zinatumia lugha za kigeni za Kiingereza, Kifaransa au Kireno, zilizorithiwa kutoka kwa Wakoloni hao. Haishangazi basi kuwa miaka 50 sasa tangu ukoloni uondoke, bado tunakuwa tegemezi kutoka kwa wakoloni hao.

Msomi B.F.P. Masele, katika makala yake yenye kichwa cha habari:

“Kiswahili au Kiingereza? Siasa na lugha muafaka ya kufundishiaTanzania,” alikariri “janga” lilioikuta nchi ya Afrika ya Madagaska iliyoamua mwaka 1975 kutumia lugha yake ya asili ya Kimalagasi, inayofahamika na kutumika kwa ufasaha zaidi nchini humo, katika nyanja zote za maisha ya watu, ikiwa ni pamoja na kufundishia elimu ya awali hadi vyuo vikuu.

Kwa mujibu wa Masele, baada ya Madagaska kukumbwa na hali mbaya ya kiuchumi, nchi ya Ufaransa, iliyokuwa ikiitawala zamani, ilishinikiza kuwa Kimalagasi kifutwe kama lugha ya kufundishia au kutumika katika shughuli nyingine rasmi kitaifa. Serikali, ikalazimika kukirudisha Kifaransa kuwa lugha kuu Madagaska baada ya kupewa ahadi ya fedha kutoka Ufaransa ili itatue matatizo yake ya kiuchumi. “Hili ni somo muhimu sana kwa Tanzania na nchi zote zinazofanana nayo”, anasema Masele.

Masele anaongeza: “Utekelezaji wa maamuzi ya matumizi ya Kiswahili kufundishia katika ngazi zote za elimu umekuwa mgumu ingawa jambo lenyewe liko wazi kiutafiti, kitaaluma, kipedagogia na kimantiki tangu zamani. Ugumu unatokana na ukweli kwamba, ingawa Kiswahili ni suala linalohusu lugha, mizizi yake ya fitina imejikita katika uwanja nyeti wa siasa, huku siasa hii ikifungamana na masuala ya uchumi na utamaduni. Bila ya kuichokonoa mizizi hii kutoka katika siasa, uchumi na utamaduni ilikojificha, si tu itakuwa vigumu, bali haitawezekana kukithamini Kiswahili”.

“Waafrika,” Masele katika makala hiyo amemnukuu mtaalamu mwingine nchini, M.M. Mulokozi akisema: “ni watu wa pekee duniani waishio kwa vitu vya kuazima; utamaduni wa kuazima, dini za kuazima, lugha za kuazima, majina ya kuazima, teknolojia ya kuazima, fasihi/fani za fasihi za kuazima, nywele na rangi za ngozi za kuazima, sanaa za kuazima, mavazi ya kuazima, vyakula vya kuazima…vitu ambavyo wengi wetu vinatufanya tuwe viumbe bandia, vichekesho vya dunia.”

Hivyo basi ni maoni yangu kuwa, kwa vile miaka 50 imekwishapita tangu uhuru bila ya kukifanya Kiswahili kiwe lugha ya kufundishia nchini katika ngazi zote, maandalizi yaanze sasa kwa kufundishia Kiswahili Sekondari na baadaye Chuo Kikuu. Kwa namna hii, utamaduni wetu utaendelezwa, vijana wetu wanaopata elimu watajijua vizuri wanatoka wapi na wanakwenda wapi na watakuwa na kitu cha kujitambulisha kama taifa. Isitoshe elimu itapanuka mno na taifa litapata wataalamu wanaoweza kujitegemea na wazalendo na hivyo utajengeka utamaduni wa kuwaamini wataalamu wetu na siyo wa nje. Ikifikia hapo, kasi ya maendeleo nchini itakuwa kubwa mno, kwa muda mfupi sana, kiajabu.

(mwisho)

• Saidi Nguba aliwahi kuwa Mhariri Mtendaji wa Magazeti

yanayochapishwa kwa Kiswahili ya UHURU (2000 – 2004) na Mwananchi

(2004 – 2005). Hivi sasa ni Mwandishi wa Habari wa Waziri Mkuu. Haya ni maoni na mawazo yake binafsi.

Simu: 0754 -388418, Barua-Pepe: sanguba@gmail.com

Wednesday, November 30, 2011

Ph.D Opportunities for Tanzanian Women

If you want to start doing a Ph.D, here is your chance:

 Deadline for submission of application is 31 December.

http://www.itc.nl/Pub/research_programme/Research_opportunities.html

Saturday, October 08, 2011

Futeni Tuition!

Hii imeandikwa na Mdau SK. Hata mimi naona siku hizi tuition imeua maana ya kusoma shule ya msingi, sekondari za serikali.
***************************************
Tuition Imeua Vipaji Vya Wanafunzi
Jamani kama kuna shimo la kufukia vipaji, na uwezo wa kufikiri kwa wanafunzi wetu ni TUITION. Sijui wazo hili lilitoka kwa nani. Tution ilizaliwa miaka ya 1990s na mbaya zaidi baada ya mwaka 2000. 
Tuition inafanya wanafunzi wasijiamini kabisa. Wanaona mwalimu wake darasani hawezi kumfundisha hadi aelewe na ndio maana anamtafuta mwalimu mwingine huku akijua msemo wa kiswahili usemao, wapishi wengi huharibu mchuzi.
Wanafunzi wa siku hizi hawapewi tena HOME WORK,  badala yake akitoka shule akienda nyumbani anamkuta mwalimu mwingine akimngojea. Wanafunzi wetu hawajui kujisomea wenyewe au kutumia maktaba, hata kufungua vitabu na kutafuta mada anayokusudia hawajui, maana muda mwingi wanazunguka na vipeperushi vilivyochakachuliwa na waalimu wa Tuition. Vitabu vya literature ambavyo enzi za 1980s tulivisoma vizima kama vile MINE BOY, THINGS FALL APART, THE RIVER BETWEEN, nk siku hizi wanafunzi hawavijui hata sura yake kwani wanasoma vipeperushi tu. Uwezo wa watoto wetu umewekwa kapuni.
Enzi zangu nikitoka shule nikenda nyumbani nilikabidhiwa jembe kulima ili kuchangia ada. Siku hizi wanafunzi wetu hawana nafasi ya kazi za mikono maana wamezungukwa na waalimu pande zote. Wamezoea kulishwa tu, SPOON FEEDING. Tunakwenda wapi?
Zamani tulifundishwa na kuzoeshwa kuwa ili ufaulu 60% ni juhudi ya mwanafunzi mwenyewe na 40% ni msaada wa mwalimu. Siku hizi wanafunzi wetu wamegeuzwa, wanajitegemea 20% na 80% ni kutegemea mwalimu. Wanafunzi hata wenye uwezo hawajiamini kufaulu bila dudu hili TUITION. 
Ninaomba serikali ifute mchezo huu mchafu wa TUITION kwani HUUWA VIPAJI NA UWEZO WA WANAFUNZI WETU KUFIKIRI. Serikali ilipe waalimu vizuri ili nao wafundishe vya kutosha na si ovyo ovyo kama ilivyo sasa na hatamae wanawaelekeza wanafunzi kuwa ukitaka kujua zaidi njoo jioni. Hii njoo jioni mabinti zetu hugeuzwa kuwa wake za waalimu. Mnafahamu hilo 
Mwasemaje?

Saturday, June 18, 2011

Msomi Afanya Fuja Kwenye Treni New York



Cheki huyo dada mwenye asili ya kihindi anayodai ni msomi kondakta wa treni alivyomwomba aache kutumia lugha ya matusi akiwa kwenye simu yake ya mkononi! Watu wanauliza kama huyo kondakta angekuwa mzungu anejibiwa hivyo. Mwisho watu wanakubai kuwa pamoja na usomi wa huyo dada hana akili za kuwa na watu hadaharani.

Monday, September 06, 2010

MFUMO WETU WA ELIMU NA CHANGAMOTO ZAKE!

Ubungo mwaka 1980. Mwanafunzi wa Chuo Kikuu alienda kunywa pombe kwenye baa fulani. Wakati ule wanafunzi wa UDSM walikuwa na hela shauri ya posho zao kutoka serikalini. Jamaa alilewa. Akaanza kuongea kimombo/kiingereza. Alipigwa na wananchi wenye hasira kwa vile jamaa eti alikuwa na KASUMBA!

Wadau waliosoma Tanzania tangu miaka ya sabini katikati waliposema kuwa eti Shule za msingi zifundishwe kwa kiswahili halafu sekondari na kuendelea ziwe English wtakubaliana na mada huu.

Na mimi siku zote nasema maana ya shule ya msingi ni nini? Si ndo msingi? Sasa kama huna msingi mzuri si utapata shida baadaye. Katika jumuiya ya Afrika Mashariki sisi waTanzania ndo tuna matatizo ya kuongea na kuandika kiingereza shauri ya kukosa msingi mzuri wa Kiingereza shuleni.

Fikiria watoto wanafundishwa kiingerea na watu ambao hawana msingi wa lugha, yaani lugha yao ni broken. Kuna dada moja ambaye nilisoma naye Tabora Girls alikuwa ancheka akisema, "Chemi, si unakumbuka English ilivyokuwa taabu kwangu, basi mimi ndio mwalimu wa English katika shule ya sekondari fulani! Si maajabu hayo" Maajabu ndo yeye eti alijua kiingerza kuliko wengine.

Hata hapa USA unakuta mTanzania ana Masters/Ph.D lakikni anakosa kazi ya maana kwa vile hajui kuongea kiingereza vizuri. WaKenya na WaGanda hawana shida hiyo. Naukumbuka miaka ya 90 mwanzo nilienda kwenye kijiji fulani huko Uganda. Wau masjini watoto wamevaa nguo zilizochanika hlafu mavumbi matupu lakini walikuwa wanajua kiingereza kizuri.

Nashukuru kuwa sasa Tanzania wameruhusu shule za msingi za kiingereza kwa muda, lakini ni za kulipia (private). Lakini ni wakina nana wanafaidi? Ndo matokeo ya KASUMBA.

Mwaka 1993 (?)...mara baada ya kuruhusu vyama vingi, Chifu Abdallah Fundikira alihubiria umati mkubwa wa wananchi huko Jangwani. Chama chake ilikuwa UMD. Alisema, "Mwalimu Nyerere alikuwa anaongea Kiingera kizuri sana...The Queen's English, halafui alitaka nyie msiongee!" (Nilikuwa mwandishi wa habari Daily News wakati huu, na iliandika hiyo kwatika original copy, lakini ilifutwa kabla ya kuchapishwa!)



***********************************************************************



Imeandikwa na Malkiory William Matiya

Waswahili walisema, mkunje samaki angali mbichi. Wataalamu na watafiti katika fani mbali mbali wanatuambia kuwa hali/tabia ya mtu mzima kwa kiwango kikubwa ni matokeo ya mazingira ya makuzi/malezi yake ya utotoni. Mfano tabia kama vile ukatili, ukimya, woga, wasiwasi, hasira, okorofi, furaha, upendo, kujiamini n.k. ukubwani ni baadhi tu ya matokeo hayo.

Kama hivyo ndivyo basi, nadhani utakubaliana nami kuwa tunahitaji mfumo dhabiti na bora wa kujifunza/ufundishaji katika ngazi ya elimu ya awali/kindergarten na msingi. Ni dhahiri kuwa tendo la kijifunza linakuwa limekamilika pale ambapo mabadiliko ya kudumu ya kitabia yanapoanza kujitokeza kwa walengwa ambao ni wanafunzi. Hivyo basi, inatubidi tukubali ukweli kuwa mabadiliko chanya ya kitabia yatatokana na ufundishaji/uelimishaji chanya pia.

Mtoto wa kitanzania anapoanza elimu ya msingi hufundishwa masomo yote kwa lugha ya kiswahili isipokuwa somo moja tu la kiingereza kwa miaka yote saba ya elimu yake ya msingi. Baada ya hapo mambo hubadilika ghafla pale mwanafunzi anapoanza elimu ya sekondari, kwani masomo yote huwafundishwa kwa kiengereza isipokuwa somo la kiswahili.

Tatizo hili huchangia kwa kiwango kikubwa kupunguza kasi, ari na uwezo wa mwanafunzi kujifunza, kwasababu mwanafunzi hujifunza mambo mageni kwa lugha ya kigeni kwa maana ya kiingereza. Hali hii kwa mtizamo wangu inachangia kuzorotesha na kupunguza ufanisi wa wanafunzi wetu kilugha katika ngazi zote.

Zaidi ya yote, mfumo wetu wa elimu katika ngazi zote haujaandaliwa katika misingi ya kumwezesha mwanafunzi kujifunza kwa vitendo. Pamoja na shule zetu kuwa na ukosefu wa vifaa vya kufundishia kwa vitendo, lakini pia ubunifu miongoni mwa walimu ni jambo jingine.

Mfano, wakati wa kufundisha somo la umeme kwa wanafunzi washule ya msingi, hapa si lazima kuwa na umeme, maana shule nyingi za vijijini hazina umeme, badala yake walimu wanaweza kutumia betri ya gari kuzalisha umeme na mwanga.


Madhalani, wakati wa kufundisha somo la uzazi wa mimea, hapa walimu wanapaswa kuandaa bustani ya majaribio, ambapo wanafunzi watapata fursa ya kuona jinsi mimea inavyoweza kuzaliana kwa vitendo.

Na kama kama ni wakati wa kufundisha somo linalohusiana na mifumo mbali mbali kama vile mfumo wa chakula, mfumo wa hewa, mfumo wa uzazi, mfumo wa neva, mfumo wa fahamu n.k hapa walimu wahusika wanaweza kumchinja chura au panya ili waweza kuonyesha kwa vitendo.

Ili kukabiliana na changomoto hizi ningependa kuishauri serikali kupitia wizara ya elimu na mafunzo kama ifutatavyo. Kwanza, kubadili mfumo wa mitaala yetu ambayo tumeirithi toka enzi za mkoloni. Jambo la msingi hapa ni kubadilisha lugha ya ufundishaji toka ngazi ya chini ya elimu hadi elimu ya juu, yaani kutoka shule ya vidudu hadi chuo kikuu.

Kama ni kiswahili basi iwe ni kiswahili toka mwanzo hadi mwisho na kama ni kiingereza basi iwe ni kiingereza toka mwanzo mpaka mwisho. Pili mitaala ibuniwe kwa lengo la kumwezesha mwanafunzi kujifunza kwa vitendo zaidi tofauti na hali ya ufundishaji wa sasa uliojikita zaidi kwenye nadharia.

Hakika kama serikali inakusudia kuwekeza kwenye ubora wa elimu basi ni lazima walimu wa stashahada/diploma na wale wa shahada/degree nao wapewe jukumu la kufundisha katika shule za msingi.

Jambo hili linaweza kuwa na ugumu wake katika utekelezaji endapo mazingira ya kufanyia kazi kwa walimu hayataboreshwa, hii ikiwa ni pamoja nyumba nzuri za kuishi walimu, huduma kama vile umeme, maji, internet, minara ya simu na TV. Upatikanaji wa huduma hizi unaweza kuwafanya walimu kudumu katika mazingira yao ya kufanyia kazi.

Iwapo jambo hili litazingatiwa basi ubora wa elimu yetu utaongezeka, na hata uwezekano wa kubadili mitaala yetu kuwa katika lugha ya kiingereza toka shule ya vidudu/ kindergarten hadi chuo kikuu utafanikiwa.

Mwisho, tukumbuke kwamba uimara wa nyumba kwa kiasi kubwa hutegemea MSINGI! Bila kusahau usemi kuwa, utavuna ulichopanda.


--
Malkiory William Matiya

Mnaweza kutembelea blogu yake: http://www.malkiory-matiya.blogspot.com/