Showing posts with label Habari Leo. Show all posts
Showing posts with label Habari Leo. Show all posts

Saturday, May 28, 2016

Hali ya Sukari Tanzania sasa Shwari!

 
 
 
HALI ya upatikanaji sukari nchini, imeanza kuwa kwenye mwelekeo mzuri, baada ya tani zaidi ya 10,000 kuingizwa kutoka nje. Nyingine 31,000 zinasubiriwa kuwasili huku viwanda vya bidhaa hiyo pia vikianza uzalishaji wiki hii.
 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alitoa taarifa hiyo jana bungeni wakati mjadala wa bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ukihitimishwa.
Akielezea sukari inayoingia kutoka nje, Mwijage aliwataka wafanyabiashara wote wanaojishughulisha na bidhaa hiyo, kujitambulisha kwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya ili wanayopewa Dar es Salaam, waifikishe kwa viongozi hao waione.
 
Kuhusu viwanda ambavyo awali vilitarajiwa kuanza uzalishaji Julai mwaka huu, Mwijage alisema, “Adha ya sukari iliyokuwepo, sasa inakwenda kuisha. Kuna sukari ya kutosha…kwani leo kiwanda cha Kagera Sugar kimeanza kuzalisha tani 250.”
 
Waziri Mwijage alisema pia Kiwanda cha Kilombero (K One), kimeanza kuzalisha na kitazalisha tani 600 kwa siku. Wakati matumizi ya nchi ni tani 1,200 za sukari kwa siku, Mwijage alisema tofauti iliyobaki ndiyo imeagizwa kutoka nje.
 
Aliwataka wabunge kutambua kuwa uamuzi uliochukuliwa na serikali, ulijenga imani na kuleta wawekezaji. Alisema hivi sasa, Kiwanda cha Sukari Kagera kinapanua eneo la Kitegule na kuzalisha tani nyingine 60,000 na pia kukiwa na mwekezaji kutoka Oman, ambaye ataongeza uzalishaji katika kiwanda hicho na kufikia tani 300,000.
 
Alisema adha ya sukari ambayo nchi inapitia sasa ni kwa ajili ya kudhibiti uingizaji sukari na kisha kuleta wawekezaji kwenye uzalishaji wa sukari. Mwijage alisema hali ya sukari ni ya kutosha na sasa wamechukua hatua ya kujenga kiwanda cha Kigoma Sugar katika eneo la hekta 47,000.
 
 Kutoka 

Tuesday, January 13, 2009

Picha Blog

Mduara huko Mnazi Mmoja

Daily News/Habari Leo wana blogu ya picha:

Kuna picha nyingi za matukio ya hivi karibuni huko.

http://dailyhabari.wordpress.com/

Saturday, January 10, 2009

Msiba Daily News - Cassian Malima

Kutoka Lukwangule Blog:


ALIYEKUWA Mhariri wa 'HabariLeo', Cassian Kigeso Malima (44),pichani, amefariki dunia.
Taarifa iliyotolewa jana na Mhariri Mtendaji wa TSN Media Group, Issac Mruma, ilisema Malima alifariki dunia jana jioni katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam alikokuwa amelazwa tangu Jumamosi iliyopita.
Ilisema Malima ambaye hivi karibuni alipandishwa cheo kuwa Mhariri Msaidizi wa Magazeti ya Mwisho wa Wiki ya Kampuni ya TSN Media Group, alijiunga na kampuni hiyo Oktoba 10, 2004 akiwa Mwandishi Mkuu Daraja la Pili.


Baadaye alipanda cheo na kuwa Mhariri wa Habari wa Daily News na kuwa mmoja wa waanzilishi wa 'HabariLeo' baada ya kuteuliwa Agosti mosi 2006 kuongoza timu iliyoanzisha gazeti hili la Kiswahili linalomilikiwa na Serikali.


“Alitegemewa sana katika utendaji kazi, lakini pia alikuwa mcheshi na rafiki wa kila mtu … aliheshimu kila mtu,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Mruma katika taarifa yake alisema kampuni imepoteza si tu mfanyakazi, bali rafiki aliyekuwa tayari kubeba jukumu lolote alilopewa na alikuwa mtiifu kupindukia.

Mkewe Malima, Hellen Maro, ambaye walizaa binti, Elizabeth, alifariki dunia Mei 19, 2006.
Malima alizaliwa Mwanza Julai 14, 1965, alipata elimu yake ya msingi katika shule mbalimbali nchini, kati ya mwaka 1972 na 1979; elimu ya sekondari katika Sekondari ya Mwanza kati ya 1980 na 1983.
Alipata elimu ya sekondari ya juu katika Shule ya Sekondari ya Lake Mwanza kati ya 1984 na 1986 kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Rostav State cha Urusi kati ya mwaka 1988 na 1994 na kuhitimu Shahada ya Uzamili katika Uandishi wa Habari.
Katika uhai wake, Malima alifanya kazi katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (THA) kati ya 1987 na 1988; Mwandishi wa Habari Uhuru/Mzalendo tangu Mei 1988 hadi 1996 alipokuwa Mhariri.

Machi 1998 hadi Septemba 1999 alikuwa Mhariri wa Habari wa Gazeti la Mtanzania na kuwa Mhariri wa Mtanzania na Mtanzania Jumapili kati ya Septemba 1999 hadi Julai 2003 na kisha Mhariri wa Habari wa The African tangu Julai 2003 hadi Oktoba 2004 alipojiunga na TSN.
Aliwahi pia kuwa kiongozi katika vyama mbalimbali kitaaluma ndani na nje ya nchi ikiwa ni pamoja na kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Bunge Tanzania, mbali na kuhudhuria semina, makongamano, warsha na kampeni mbalimbali nje na ndani ya nchi. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

Mruma alisema mipango ya mazishi inafanywa na taarifa kamili itatolewa baadaye.

Monday, September 29, 2008

Athumani Hamisi yuko South Africa kwa Matibabu



Kutoka Lukwangule Blog:

TAARIFA ambazo nimezipata leo mchana ni kuwa Athumani Hamisi ,pichani,ameshaanza kupata matibabu katika hospitali aliyofikishwa, nchini Afrika Kusini.

Matibabu hayo ni pamoja na vipimo vya muhimu kabla ya kumfanyika upasuaji.

Kwa mujibu wa mtu aliyekuwa ananipa habari hizi Athumani ameongezwa damu kwa siku ya leo kwa kuwa aliyokuwa nayo ilionyesha kuwa tatizo kwa madaktari wake.Vinginevyo wamesema hali ni shwari.Nitawapatia maelezo hali ya mpiganaji huyu kwa jinsi inavyowezekana lakini si mara zote.

************************

Wadau tuendelee kumwombea kaka Athumani apate nafuu na aweza kurudi kazini na kuendelea na maisha yake kama hapo awali.