Showing posts with label Daily News. Show all posts
Showing posts with label Daily News. Show all posts

Saturday, May 28, 2016

Hali ya Sukari Tanzania sasa Shwari!

 
 
 
HALI ya upatikanaji sukari nchini, imeanza kuwa kwenye mwelekeo mzuri, baada ya tani zaidi ya 10,000 kuingizwa kutoka nje. Nyingine 31,000 zinasubiriwa kuwasili huku viwanda vya bidhaa hiyo pia vikianza uzalishaji wiki hii.
 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alitoa taarifa hiyo jana bungeni wakati mjadala wa bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ukihitimishwa.
Akielezea sukari inayoingia kutoka nje, Mwijage aliwataka wafanyabiashara wote wanaojishughulisha na bidhaa hiyo, kujitambulisha kwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya ili wanayopewa Dar es Salaam, waifikishe kwa viongozi hao waione.
 
Kuhusu viwanda ambavyo awali vilitarajiwa kuanza uzalishaji Julai mwaka huu, Mwijage alisema, “Adha ya sukari iliyokuwepo, sasa inakwenda kuisha. Kuna sukari ya kutosha…kwani leo kiwanda cha Kagera Sugar kimeanza kuzalisha tani 250.”
 
Waziri Mwijage alisema pia Kiwanda cha Kilombero (K One), kimeanza kuzalisha na kitazalisha tani 600 kwa siku. Wakati matumizi ya nchi ni tani 1,200 za sukari kwa siku, Mwijage alisema tofauti iliyobaki ndiyo imeagizwa kutoka nje.
 
Aliwataka wabunge kutambua kuwa uamuzi uliochukuliwa na serikali, ulijenga imani na kuleta wawekezaji. Alisema hivi sasa, Kiwanda cha Sukari Kagera kinapanua eneo la Kitegule na kuzalisha tani nyingine 60,000 na pia kukiwa na mwekezaji kutoka Oman, ambaye ataongeza uzalishaji katika kiwanda hicho na kufikia tani 300,000.
 
Alisema adha ya sukari ambayo nchi inapitia sasa ni kwa ajili ya kudhibiti uingizaji sukari na kisha kuleta wawekezaji kwenye uzalishaji wa sukari. Mwijage alisema hali ya sukari ni ya kutosha na sasa wamechukua hatua ya kujenga kiwanda cha Kigoma Sugar katika eneo la hekta 47,000.
 
 Kutoka 

Sunday, June 21, 2015

Wapiga Picha wa Vyombo Vya Serikali Enzi Hizo!

 Nilifanya kazi nao wapiga picha nikiwa mwandishi wa habari Daily News miaka ya 1980's! Enzi zile tulikuwa wachache na wote tulijuana.  Mzee Makwaia alikuwa Mwalimu wetu TSJ. Alifariki tukiwa mwaka wa kwanza baada ya kugongwa na gari Morogoro Road.

 Kwa hisani ya Kaka Juma Dihule:

WAFAHAMU WAPIGAPICHA WA VYOMBO VYA SERIKALI ENZI HIZO.
Wapigapicha wa wakati huo ambapo vyombo vya habari vilimilikiwa na Serikali pamoja na chama tawala. Waliosimama nyuma toka kushoto marehemu Max Madebe (Mpigapicha Mkuu gazeti la Mfanyakazi, Marehemu Sam Mbando, mpigapicha mwandamizi Shirika la Habari Tanzania (SHIHATA), Marehemu Vincent Urio (Mpigapicha Mkuu magazeti ya Serikali ya Daily News & Sunday News, Marehemu John Makwaia ndiye aliyekuwa mwalimu wetu sisi wote na mpigapicha mkuu wa Serikali katika Idara ya Habari (MAELEZO), akifuatiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye pia ni marehemu, David Saileni ambaye wakati huo akiwa mpigapicha mwandamizi wa Sinema, upande wa Idara ya Habari, (Film Unit), Juma Dihule, Mpigapicha Mkuu SHIHATA, Marehemu Adnani Mihanji, Mpigapicha Mwaandamizi, SHIHATA na Moshy Kiyungi, Mpigapicha mwandamizi ( Idara ya Habari).
Walioketi toka kushoto, Steven Kasange, IKULU, Charles Kagonji , Mkutubi Mkuu wa maktaba ya picha MAELEZO na pia akiwa mpigapicha, Gaspar Msilo, Daily News, Mwanakombo Jumaa, MAELEZO, Hatib Ali Mpichapicha Mkuu (Uhuru na Mzalendo) Raphael Hokoro , ambaye hivi sasa ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO).

Sunday, March 01, 2015

Captain John Komba Obituary

Kutoka Daily News 

 Mbinga West MP Komba is No More

Published on Sunday, 01 March 2015

By DEOGRATIAS MUSHI 

The late Captain John Komba 

 Mbinga West Member of Parliament and Member of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) National Executive Committee (NEC) Captain John Damian Komba is no more. He died at TMJ hospital in Dar es Salaam Today, where he had been admitted few hours before he breathed his last.

The Tanzania One Theatre (TOT) Secretary General Mr. Gasper Tumaini said that medical reports show that Komba was suffering from Pressure and Diabetes. According to him, Captain Komba was admitted to Sanitas Medical Clinic in Dar es Salaam a week ago, and after two days his health improved and he was discharged. Secretary, Mr Nape Nnauye meanwhile, expressed shock and sadness over the sudden passing of Capt Komba saying that the void he has left behind would be difficult to fill.

Speaking at a press conference yesterday, Mr Nnauye said that the party’s National Chairman, President Jakaya Kikwete, had received the news with great shock. He said that the president has sent condolences to the late Capt Komba’s family and noted that he knew the deceased well because he had worked with him for many years. “Capt Komba was a veteran cadre, an artist, a music composer and he will be dearly missed.

He composed a song during the 38th anniversary of the party which touched many hearts, now it seems it was his way of saying goodbye,” he said. He said that he would forever be thankful to the late Komba because it was he who convinced his late father to enroll him into the party after completing national service and that the party sent heartfelt condolences to his family and friends.

 Captain Komba was born on March 18, 1954, then joined Lituhi primary school in 1963. After completing standard seven in 1970, he joined Songea boys secondary school where he completed in 1974, then joined Cleruu Teachers Training College where he attained teaching certificate in 1976. In 1978 he joined Monduli Military Cadet Training Unit in Arusha where he got a diploma, and then studied at Magdeburg Path in Germany where he got a diploma in politics. Captain Komba then joined Washington International University in 2006, where he was awarded BA in political science in 2008. During his life time, Captain Komba served Tanzania People's Defence Forces as Army Officer from 1978 to 1992.Before he had been employed by the Ministry of Education(1977 and 1978). Between 1992 and 2005 Captain Komba was TOT Executive Director, doubling also as CCM Chief Culture from 1992 to date. He served as Mbinga West member of Parliament from 2005, and also as member of CCM's National Executive Committee (NEC) from 1987 to date.

While in Parliament, Captain Komba once questioned why Tanzania did not unite with Burundi and DR Congo since the three governments of Rwanda, Uganda and Kenya had teamed up and set up an alliance within the community. He even threatened to embark on a rebellion if the Constituent Assembly (CA) could adopt a three-government system as it was proposed in the second draft constitution. He also questioned the rationale of Tanzania remaining in the EAC in light of actions which clearly sidelined it.

 He was once quoted saying he would be the last person to endorse the three-tier Union model and that he would defend the status quo at all costs. "Woe unto you if you will be persuaded to buy the idea of a three-government system. I will retreat into the forest to fight for the two-tier Union structure," he warned amid laughter. His body has been preserved at Lugalo hospital, pending funeral arrangements.

Friday, January 03, 2014

Tuesday, December 31, 2013

Msiba - Tony Barreto

 The late Anthony Edgar (Tony) Barreto gave me many words of wisdom when I worked at Daily News (Tanzania Standard Newspapers) . He could be very funny too. May he rest in eternal peace. Amen.

 Tony Barreto is dead

THE late Anthony Barreto.THE late Anthony Barreto.
A FORMER Advertising Manager with Tanzania Standard Newspapers Limited (TSN), Mr Anthony Barreto, is dead.
A brother-in-law to the late Barreto, Mr Diamond Carvalho, said in Dar es Salaam that the late Baretto died at his home in the city in the morning as he was preparing to go out.
He said the deceased’s body was sent to the Hindu Mandal Hospital for a postmortem and preservation, as the family is discussing the funeral arrangements.
Mr Carvalho told the ‘Daily News,’ where the late Barreto served for over a decade, that the burial will be held in the city either on Friday or Saturday depending on the arrival of the deceased’s relatives who are based abroad.
Prior to his death, Barreto owned a media consultancy and public relations firm in Dar es Salaam.
A close friend described ‘Tony’ as he was fondly called by friends as a ‘’cultured man who loved his roots’’. He was a stalwart at the Dar es Salaam Institute (Goan Club) in the city centre.
He leaves a widow, Pearl and two children, daughter Catherine-Rose and son John-Paul who are reportedly ‘’both enjoying success in their chosen fields.’’

Friday, June 08, 2012

TSN Haijamtelekeza Athumani Hamisi

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: TSN HAIJAMTELEKEZA ATHUMANI HAMISI

Athumani Hamisi Akiongea na Waandishi wa Habari jijin Dar juzi
Tarehe 5 Juni,2012, mfanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), ambaye amelemaa baada ya kupata ajali ya gari, Bwana Athumani Hamisi, aliitisha mkutano wa waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Maelezo, Dar es Salaam, na kutoa taarifa iliyojenga taswira kuwa ametelekezwa na TSN pamoja na Serikali.

TSN inapenda kufafanua kuwa Serikali na kampuni hii, ambayo ilimwajiri Athumani tarehe 1/09/2006 kama Mpiga picha Mwandamizi, wamemhudumia mfanyakazi huyo kikamilifu tangu alipopata ajali tarehe 12 Septemba, 2008 hadi sasa, na huduma hiyo inaendelea.

Baada ya kutokea ajali hiyo, TSN kama mwajiri ilisimamia matibabu yake ya awali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Kitengo cha Mifupa (MOI) mpaka Serikali, kwa kupitia Wizara ya Afya ilipomhamishia Netcare Rehabilitation Hospital nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.

Serikali ililipia gharama za matibabu yake yote akiwa Afrika Kusini kwa kipindi cha mwaka mmoja na miezi saba, ambayo yanazidi shilingi milioni mia moja. Gharama hizo ni pamoja na ununuzi wa kigari maalum ambacho Athumani anatumia sasa.

TSN kama mwajiri ililipa nauli ya ndege kwenda na kurudi pamoja na posho ya kujikimu ya mgonjwa pamoja na ndugu wasindikizaji ambao ni Bw. Hassan Hussein na Bi. Mirriam Malaquias.Posho ya kujikimu ilikuwa USD 6,210 sawa na Shilingi 9,315,000, na nauli kwa watu watatu ilikuwa ni Shilingi 3,535,869.92. Athumani aliendelea kupatiwa huduma akiwa huko Afrika Kusini kwa gharama za Serikali na TSN mpaka aliporejea nchini tarehe 08/05/2010. Gharama zilizolipwa na kampuni kwa mfanyakazi huyu hadi sasa ni takriban shilingi million 52.

Athumani aliporejea nchini alilakiwa na wafanyakazi na viongozi wa TSN na kupangiwa chumba hoteli ya Holiday Inn wakati utaratibu wa kumtafutia nyumba ya kupanga ukikamilishwa. Kampuni ilitumia kiasi cha Shilingi 1,756,979.50 kulipia hoteli. Baadaye alipelekwa kwenye nyumba ambayo alipangiwa na Kampuni katika eneo la Sinza Vatican ambapo ndipo bado anaishi hadi hivi sasa. Gharama ya nyumba kwa mwaka wa kwanza 2010 ilikuwa ni Shilingi 4,200,000 au Shilingi 350,000 kwa mwezi. Mwaka 201 mwenye nyumba alipandisha kodi hadi 400,000 kwa mwezi ambapo Kampuni ililipia Shilingi 4,800,000. Kodi hiyo imeishia Mei mwaka huu na kampuni imeshafanya mazungumzo na mwenye nyumba ili Athumani aendelee kuishi hapo kwa muda wakati mipango endelevu ya ustawi wake inafanywa kwa kuzingatia taratibu za ajira.

Mnamo tarehe 8/12/2010 Athumani alirudi tena Afrika Kusini kwa ajili ya uchunguzi wa maendeleo ya afya yake na matibabu yaligharimiwa na Serikali wakati TSN iligharamia nauli yake na ya muuguzi wake, pamoja na posho ya kujikimu Shilingi 6,300,000/-.

Pamoja na bwana Athumumai kulala kitandani kwa muda wote huo ameendelea kulipwa mshahara kamili bila kukatwa kama mfanyakazi wa kawaida ikiwa ni msaada wa kampuni kwa kuzingatia ulemavu alioupata.Mshahara aliolipwa kwa muda wote aliokuwa anaugua ni kiasi cha shilingi 26,773,000. Vile vile kampuni ilimlipa muuguzi toka Afrika Kusini ambaye alikuwa anamhudumiaa Athumani Rand 12,500 kama mshahara wake.

Kuanzia Januari 2011, mshahara wa Athumani umejumuisha asilimia 15 kama posho ya nyumba ambayo wafanyakazi wote wanalipwa. Aidha Athumani yupo kwenye mpango wa bima ya afya anayolipiwa na kampuni, ambayo inamwezesha yeye na familia yake kuweza kutibiwa katika hospitali yoyote hapa Tanzania. Kampuni inamlipia Shilingi 68,449.20 kila mwezi na bima hiyo ndiyo inayogharamia matibabu yake yote hapa nchini.

Bwana Athumani anapatiwa usafiri na TSN mara mbili kwa wiki kumtoa nyumbani hadi Muhimbili na kurudi kwa ajili ya mazoezi ya viungo.

Imetolewa na

OFISI YA MHARIRI MTENDAJI
08.6.2012

***********************************************************

Kusoma Story Aliyotoa Athumani Hamisi BONGO CELEBRITY , BOFYA HAPA

Thursday, February 18, 2010

Tanzia - Reginald Mhango (Reggie) Bosi wangu Daily News

Reggie na copy yake ya sinema Bongoland II. Sehemu ya hiyo sinema ilipigwa nyumbani kwa Reggie huko Magomeni Mikumi. Nilipomwomba kupiga sehemu ya sinema hapo allikubali bila kusita na pia alifurahi kuona jinsi wanavyotengeneza sinema. Alifurahi uchapa kazi wa crew waliotoka Marekani.
Mimi, Reggie Jr. (katikati) na Mzee Reggie Mhango. Picha hii tulipiga siku ya October 27, 2009 nyumbani kwa Reggie. Nilisikia kutoka kwa kaka Michuzi kuwa alipata stroke lakini hajambo. Nilimpigia Reggie simu kutoka Marekani mwezi wa saba na kumwaidi kuwa nitafika siku hiyo na nilifika. Alifurahi sana.
************************************
Wadau, nimepokea kwa majonzi habari ya kifo cha bosi wangu mpendwa nilipokuwa Daily News, Reginald Mhango (Reggie). Reggie alikuwa na utu, uvumilivu, na upendo kwa kila mtu. Nakumbuka nilikuwa napata shida nikiwa na mimba mwaka 1989. Tumbo ilianza kuwa kubwa na kutembea ilikuwa shida. Reggie aliniambia nikae nyumbani mpaka nijifungue na kumaliza maternity leave. Si hiyo tu lakini kwa kweli sikumbuki kumwona akiwa na hasira au akigombana na mtu. Alitufundisha sisi waandishi chipukizi uandishi wa habari hasa, na kutusaidia katika kuandika habari safi...to the point! Nje ya kazi, ilikuwa hata kama una shida binafsi alikuwa tayari kusikia na kutoa mawaidha.
Mnakumbuka ile kesi ya Mzee Athumani Ali Maumba. Yule babu wa Magomeni aliyekuwa analawiti watoto wa kike wa primary, Reggie alisaidia hizo habari zichapishwe. Hamwezi kuamini lakini mpaka hiyo kesi ya Maumba ilikuwa kama mwiko kuandika habari hizi. Hata waandishi wa habari wengine walikataa kuripoti. Mimi ndo nilikubali kwenda huko kwenye hiyo shule Kisutu na kuchunguza. Baada ya ripoti kukamilika wakuu walitaka kuzuia, Reggie aliongea. Kesho yake walitoa para mbili tena kwa kificho. Baada ya kuona si mwisho wa dunia, habari za Maumba zikawa front page. Msishangae na kusema najiona,lakini mkumbuke kuwa wakati huo kulikuwa na magazeti machache nchini. Daily News (serikali) Uhuru (Chama) na Mfanyakazi, Kiongozi (Wakatoliki). Redio ilikuwa RTD tu. TV ilikuja baadaye.
REST IN ETERNAL PEACE REGGIE. WE WILL MISS YOU DEARLY BUT YOU IMPARTED GREAT KNOWLEDGE AND WISDOM IN US AND WE WILL PASS IT ON!
Mnaweza kusoma habari zaidi kwa Kaka Michuzi.
Na pia someni Daily News:

Tuesday, January 13, 2009

Picha Blog

Mduara huko Mnazi Mmoja

Daily News/Habari Leo wana blogu ya picha:

Kuna picha nyingi za matukio ya hivi karibuni huko.

http://dailyhabari.wordpress.com/

Saturday, January 10, 2009

Msiba Daily News - Cassian Malima

Kutoka Lukwangule Blog:


ALIYEKUWA Mhariri wa 'HabariLeo', Cassian Kigeso Malima (44),pichani, amefariki dunia.
Taarifa iliyotolewa jana na Mhariri Mtendaji wa TSN Media Group, Issac Mruma, ilisema Malima alifariki dunia jana jioni katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam alikokuwa amelazwa tangu Jumamosi iliyopita.
Ilisema Malima ambaye hivi karibuni alipandishwa cheo kuwa Mhariri Msaidizi wa Magazeti ya Mwisho wa Wiki ya Kampuni ya TSN Media Group, alijiunga na kampuni hiyo Oktoba 10, 2004 akiwa Mwandishi Mkuu Daraja la Pili.


Baadaye alipanda cheo na kuwa Mhariri wa Habari wa Daily News na kuwa mmoja wa waanzilishi wa 'HabariLeo' baada ya kuteuliwa Agosti mosi 2006 kuongoza timu iliyoanzisha gazeti hili la Kiswahili linalomilikiwa na Serikali.


“Alitegemewa sana katika utendaji kazi, lakini pia alikuwa mcheshi na rafiki wa kila mtu … aliheshimu kila mtu,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Mruma katika taarifa yake alisema kampuni imepoteza si tu mfanyakazi, bali rafiki aliyekuwa tayari kubeba jukumu lolote alilopewa na alikuwa mtiifu kupindukia.

Mkewe Malima, Hellen Maro, ambaye walizaa binti, Elizabeth, alifariki dunia Mei 19, 2006.
Malima alizaliwa Mwanza Julai 14, 1965, alipata elimu yake ya msingi katika shule mbalimbali nchini, kati ya mwaka 1972 na 1979; elimu ya sekondari katika Sekondari ya Mwanza kati ya 1980 na 1983.
Alipata elimu ya sekondari ya juu katika Shule ya Sekondari ya Lake Mwanza kati ya 1984 na 1986 kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Rostav State cha Urusi kati ya mwaka 1988 na 1994 na kuhitimu Shahada ya Uzamili katika Uandishi wa Habari.
Katika uhai wake, Malima alifanya kazi katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (THA) kati ya 1987 na 1988; Mwandishi wa Habari Uhuru/Mzalendo tangu Mei 1988 hadi 1996 alipokuwa Mhariri.

Machi 1998 hadi Septemba 1999 alikuwa Mhariri wa Habari wa Gazeti la Mtanzania na kuwa Mhariri wa Mtanzania na Mtanzania Jumapili kati ya Septemba 1999 hadi Julai 2003 na kisha Mhariri wa Habari wa The African tangu Julai 2003 hadi Oktoba 2004 alipojiunga na TSN.
Aliwahi pia kuwa kiongozi katika vyama mbalimbali kitaaluma ndani na nje ya nchi ikiwa ni pamoja na kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Bunge Tanzania, mbali na kuhudhuria semina, makongamano, warsha na kampeni mbalimbali nje na ndani ya nchi. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

Mruma alisema mipango ya mazishi inafanywa na taarifa kamili itatolewa baadaye.

Monday, November 24, 2008

Mike Sikawa Laid to Rest


REST IN ETERNAL PEACE MIKE.

*********************************************************************

Kutoka Daily News:

Mike Sikawa laid to rest

CHARLES KIZIGHA in Arusha

Daily News; Monday, November 24, 2008

Former Prime Minister Edward Lowassa, accompanied by his wife Regina, yesterday led hundreds of mourners from all walks of life at the burial of veteran journalist Mike Sikawa at Mareu village in Arumeru district, Arusha region.

The well-attended burial service was preceded by paying last respects at the Mareu Rural Cooperative Society grounds, a stone’s throw away from his place of domicile. Mike was laid to rest at the family’s farm where his father and mother were buried.

Prior to paying last respects several speakers, including Mr Lowassa, described Mike as one of the outstanding journalists in the country and Africa at large. The same was echoed by the head of the BBC Kiswahili Service, Solomon Mugera who led a team of four BBC staff to represent the Broadcasting House.

“Although Mike had been sick for a long time, his colleagues did not know because he did not show any sign and continued working normally. This proved that Mike was a hard working journalist and was ready to go out for assignments without showing any hesitation much as he was sick,” said Mr Mogera.

The mourners, who included the clergymen from various churches, government leaders, representatives from AICC, Tanapa and Retired General Mirisho Sarakikya, said the only way to remember Mike is to continue practicing excellent journalism. Mike joined the 'Daily News' and 'Sunday News' in 1975 until 1994 when he joined the BBC. He begun battling with diabetes in 1978 and underwent several treatments inside and outside the country until November 18 when he lost the battle.

**********************************************

Navyokumbuka mimi aliondoka Daily News 1984. Na siyo 1994. Walibandika notice ubaoni newsroom kutujulisha.

Wednesday, November 19, 2008

Mike Sikawa wa BBC Afariki Dunia

(Mike Sikawa 1982 Dar es Salaam, Tanzania - Mike alinitumia hizi picha nikiwa denti Form Five, Tabora Girls. Mbona nilitamba nazo, kwanza zilikuwa za rangi, halafu pili alikuwa mwandishi wa habari maarufu sana hivyo kujuana naye ilikuwa fahari kweli. Miaka yote hii nimekaa nazo.)

*******************************************************************

Nimepokea habari za kusikitisha sana leo. Mwandishi wa Habari wa BBC, Mike Sikawa, amefariki dunia. Aliwahi kufanya kazi Daily News. Alikuwa na kipaji mkubwa wa kuandika habari mpaka Daily News walimpa 'special privileges'.

Nilikutana naye kwa mara ya kwanza nikiwa nasoma 'A' levels Tabora Girls. Nilikuwa likizo Dar na tuliktana kwenye party Chuo Kikuu cha DSM. Wakati huo Mike Sikawa alikuwa maarufu sana. Nilimwambia kuwa nataka kuwa mwandishi wa habari na yeye alisema kuwa huo kazi haufai mwanamke. Nikamwambia kuwa hata hivyo bado nataka kuwa mwandishi wa habari. Nilianza kazi Daily News Agosti 1984, na baada ya muda mfupi yeye alitoka na kwenda Uingereza. Nilikutana naye tena miaka ya 90 na Mike aliniambia kuwa alijua nitakuwa na mafanikio makubwa katika uandishi wa habari.

Nakumbuka huo ugonjwa wa kisukari ulianza kumsumbua wakati huo na ndo ulimaliza.

Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.

****************************************************
Kutoka Lukwangule Blog:

Mike Sikawa wa BBC afariki dunia

MTANGAZAJI wa idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Mike Sikawa (55) ,amefariki dunia jana mchana baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari.

Sikawa, ambaye pia aliwahi kufanya kazi katika Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayomiliki magazeti ya Daily News na HabariLeo, alifariki dunia juzi majira ya saa 8.47 mchana nyumbani kwake Njiro, nje kidogo ya mji wa Arusha.

Kwa mujibu wa mdogo wake marehemu, Mchungaji Charles Sikawa, ndugu yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu na kutokewa na kidonda mguuni.
Mchungaji huyo alisema ndugu yake alipata matibabu katika hospitali mbalimbali hapa nchini ikiwamo AICC, KCMC, St. Thomas na Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili iliyoko Dar es Salaam lakini hakupata nafuu yoyote.

Alisema ilifika wakati nusura akatwe mguu uliokuwa na kidonda lakini madaktari walifanikiwa kukwangua nyama ya mguu wa kidonda lakini haikuweza kusaidia.
Mchungaji huyo aliendelea kusema kuwa baada ya kuhangaika kwa muda mrefu katika hospitali mbalimbali hapa nchini na kushindwa kupata nafuu, Sikawa alikuwa akipata matibabu akiwa nyumbani kwake hadi alipofikwa na mauti.

Alizaliwa King’ori wilayani Arumeru mkoani Arusha na kusoma elimu ya msingi katika eneo hilo kabla ya kufaulu na kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Ilboru na Mzumbe ya mkoani Morogoro.

Katika miaka ya 1970, aliajiriwa katika kampuni ya TSN kama mwandishi wa kawaida na baadaye kujiunga na idhaa ya Kiswahili ya BBC kama mtangazaji. Ameacha mjane na watoto wawili ambao wako Amerika ya Kusini.

Mipango ya maziko inasubiri ndugu, jamaa na marafiki walioko nje ya mkoa wa Arusha na sehemu zote alizofanyia kazi.

Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro ametuma salamu za rambimbi kutokana na kifo cha mwandishi huyo na kuelezea jinsi alivyoguswa na msiba huo.

Dk. Migiro alisema alipoteuliwa kushika wadhifa huo katika UN, Sikawa alikuwa mwandishi wa kwanza kumtafuta kwa ajili ya kumhoji juu ya uteuzi huo.

Kwa habari zaidi soma:

http://dailynews.habarileo.co.tz/home/index.php?id=8536

Monday, September 29, 2008

Athumani Hamisi yuko South Africa kwa Matibabu



Kutoka Lukwangule Blog:

TAARIFA ambazo nimezipata leo mchana ni kuwa Athumani Hamisi ,pichani,ameshaanza kupata matibabu katika hospitali aliyofikishwa, nchini Afrika Kusini.

Matibabu hayo ni pamoja na vipimo vya muhimu kabla ya kumfanyika upasuaji.

Kwa mujibu wa mtu aliyekuwa ananipa habari hizi Athumani ameongezwa damu kwa siku ya leo kwa kuwa aliyokuwa nayo ilionyesha kuwa tatizo kwa madaktari wake.Vinginevyo wamesema hali ni shwari.Nitawapatia maelezo hali ya mpiganaji huyu kwa jinsi inavyowezekana lakini si mara zote.

************************

Wadau tuendelee kumwombea kaka Athumani apate nafuu na aweza kurudi kazini na kuendelea na maisha yake kama hapo awali.

Monday, July 21, 2008

Kwa nini sinema za Tanzania zilifanya vibaya ZIFF

Nimeona watu wanaulizia kwa nini sinema ya Bongoland II haikupata zawadi ZIFF, wala hata mention. Sina jibu. Sikuwepo huko ZIFF.

Ila nimeona hii story kwenye gazeti ya Daily News (TZ) leo iliyoandikwa na kaka Michuzi.

Naona Dr. Martin Mhando anasema kuwa ingawa Bongoland II, ilikuwa sinema pekee ya kiTanzania kwenye mashindano ya 'Feature' ina hadithi mbili, ya familia ya Juma na hadithi ya yeye kurudi Bongo. Alisema ni sinema nzuri kwa ujumla.

Haya, niwaulize wadau walioona sinema ya Bongoland II, mliionaje?

**************************************************************************
ZIFF wants more focus to develop film industry

MUHIDIN ISSA MICHUZI in Zanzibar
Daily News; Tuesday,July 22, 2008

The Zanzibar International Film Festival (ZIFF) believes that developing a funding structure to link up with creative capacity and a local distribution structure is the answer if Tanzania's infant film industry is to grow.

The Chief Executive Officer of ZIFF, Dr Martin Mhando, said this in an exclusive interview with the 'Daily News' here yesterday, adding that one of the key problems with African cinema depended entirely on distribution.

"ZIFF has undertaken research looking into distribution hence the Tanzania Film Chain Study Report that was presented at ZIFF 2008", he said, adding: "We hope we can have time to again discuss it at length with our filmmakers with the view of looking into how to link distribution to production", said Dr Mhando at the climax of the 11th edition of ZIFF on Saturday.

On the poor participation of Tanzanian films at the annual festival, the ZIFF CEO expressed deep concern, saying something should be done to reverse the situation as it makes them feel bad about it.

He said the ZIFF plans to begin serious discussions with local filmmakers so that production efforts on the ground were supported. He, however, pointed out that there a need to encourage local filmmakers to see the use of festivals in marketing or at least promoting their films.

"Festivals generally do not need to chase after filmmakers -- the opposite is the case. However ZIFF needs filmmakers just as filmmakers need ZIFF", he quipped. The ZIFF CEO emphasised that to learn how to distribute films internally was paramount to putting the industry on its feet.

Dr Mhando said until Tanzania reached the point that audiences who clamour for the local product are satisfied one can not say the country has an industry. "Therefore let us deal with what distribution structures exist in the country, know who our audiences are and how to reach them and then start making films for those audiences and their distribution structures" he stressed.

On Bongoland II, which was Tanzania's lone nominated entry in the ZIFF 2008, Dr Mhando said it is a good film but had its setbacks on its story board. He said while the juries did not discuss film by film but one of the things that have been said about Bongoland II is that it went well until it began the story of the family's intrigue.

"The family intrigue needed to be brought in earlier and better fused into the script for the film to work. "Currently it looks like there are two stories - about the young man's problems of resettlement and then the family's", he concluded.

Thursday, September 13, 2007

Hongera Mr. & Mrs. Mroki


Mpiga picha wa magazeti ya serikali Daily News na Habari Leo, Mroki Mroki aka Father Kidevu, amefunga pingu za maisha, na Bi Deborah Fute, wikiendi iliyopita.

Hongera Mr. & Mrs. Mroki. Nawatakia maisha mema. Zaeni matunda mema.

Monday, June 18, 2007

Waandishi wa Habari wa Daily News


(Kushoto, Dr. Mwamoyo Hamza, Kati, Lady Diana Kibodya, kulia, Chemi Che-Mponda)

Wikiendi hii tulisherekea 50th Birthday, ya Mama Diane Kibodya (Lady Diana), huko Springfield, Massachusetts. Ndugu na marafiki walitoka sehemu mbalimbali kusherekea.

Kwa bahati sisi watatu tuliowahi fanya kazi Daily News (TSN) na kusoma Tanzania School of Journalism (TSJ) (miaka mbalimbali) tulikutana na kupiga picha ya kumbukumbu. Mimi nilikuwa chipukizi kwa Dr. Mwamoyo na Lady Diana lakini walinifundisha mengi. Nawashukuru.

*******************************************************************

Kibodya Family watoa Shukurani

From an e-mail message 6/18/07

Dear Friends:

On behalf of Lady D, we the Kibodyas give many thanks to you and your family for coming to join us in Lady D 50Th Birthday Party. We could not do it alone, definitely your help has made this event "unique" in many ways. Thank you for your help, thanks for your time and resources. May The Almighty God reward you well.. Amen!

For some of you who could not attend because of other obligations, we know deeply in our hearts that you had good intentions and may The Almighty Lord reward you well.

All of you have a permanent place in our hearts for your kindly words, gifts, helping in cooking, taking pictures and video camera as well as for those tireless, the most talented DJ's who came all out to showcase their skills! (Paul Massudi, Samora and Rich Maka) Without forgetting our flamboyant outstanding MC "Mzee wa Ngwasuma!" Emmanuel Bandawe! What a talent!

I am sure you saw the dance! If you missed asked somebody! Our daughter Hawa and her 3 friends gave us an African "high energy" dance and we give special thanks our sisters and brothers from South Africa who did acapella songs and showed us how the banqanga dance is performed.

Thanks to all of you who travel from far and for those who live near and special thanks to "Father Chui" for your hospitality my family and I know we can count on you! This Email cannot be enough to thanks each and every individual but we chose to use as a mean of quicker communication and I have started to call each one of you to thank you personally!

Shukran!

Isaac A. Kibodya, Esq.,