Showing posts with label Kevin James. Show all posts
Showing posts with label Kevin James. Show all posts

Tuesday, January 22, 2013

Mimi Katika Sinema Here Comes the Boom

Haya wadau, katika sinema, Here Comes the Boom, niliigiza kama moja wa wanafunzi wa darasa la watu wazima wanaotafuta uraia wa Marekani. Darasa ilikuwa inafundishwa na Mr. Voss (Kevin James) ambaye anatafuta hela zaidi ya mshahara wake kwa ajili ya kusaidia wanafunzi wa muziki katika shule ya sekondari anayofundisha.  Mimi nilikuwa background actor, hivyo siongei. Nimefananikiwa kupata picha za scenes zangu.








Sunday, October 14, 2012

Niko katika Sinema - Here Comes the Boom

Wadau, nafurahi kuwatangazia kuwa niko katika sinema mpya, Here Comes the Boom.  Stelingi wake ni mwigizaji maarufu Kevin James.  Mtaniona katika scenes za  darasa la Uraia. Niligiza kama moja wa wanafunzi watu wazima wanaotafuta uraia wa Marekeni. Wanasoma kwa ajili ya mthiani wa uraia.

Katika sinema hii, Kevin James anaigiza kama Mwalimu Voss ambaye anakuwa mpiganiaji wa MMA (Mixed Martial Arts) ili kutafuta hela ya kuokoa somo la muziki katika shule yake. Kwa vile bajeti ya shule inapungukiwa Mwalimu mkuu anaamua kufuta somo la muziki. Kwa maana hiyo hata mwalimu wa muziki ambaye ni rafiki yake, atakosa kazi.

Nilienda kuiangalia jana na nilifurahi sana kujiona.  Yaani nimeigiza katika sinema nyingi za Hollywood na mara nyingi scene inakatwa, au unaniona sekunde! Lakini hii nimeonekana vizuri tu. 

Tuesday, April 29, 2008

Sinema - Paul Blart:Mall Cop

Mimi na Mcheza sinema, Jamal Mixon kwenye set ya Mall Cop
Mimi na Mcheza sinema, Jerod Mixon


Mcheza sinema, Kevin James
Mcheza sinema, Jayma Mays
Segway

Wadau, jana nilikuwa extra kwenye sinema, Paul Blart:Mall Cop ambayo itakuwa sinema ya vichekesho (Comedy). Nilishinda kwenye seti huko Burlington Mall siku nzima. Kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi saa nne usiku (8:30am -10:00PM). Tulifanya kwanza scene ya arusi. Bwana arusi ni Kevin James na Bibi Arusi ni Jayma Mays. Kevin ndo mhusika mkuu wa hi sinema, yeye ndiye Paul Blart:Mall Cop.

Kwanza tulipiga scene tumekaa kwenye meza kama wageni waalikwa. Food Court ulikuwa umepambwa kama ukumbi wa arusi. Halafu walipiga scene kadhaa, wanafungishwa ndoa, busu, Bibi harusi kutupa bouquet, wahusika wakuu wengine wa sinema waki-react kwenye arusi. Halalfu walipiga scene za Bibi na Bwana arusi kuondoka wakiwa kwenye segways. Halafu tuliambiwa tucheze densi. Wimbo ulikuwa, 'Ain't No Mountain High Enough' ulikuwa unaimbwa na kaka yake Kevin James.

Mwisho walicheza densi wakiwa kwenye segways ndani ya gazebo. Hapo tuliambiwa tuzunguke gazebo. Ilitokea kichekesho wakati titi la Jayma ilitoka nje ya gauni la arusi. Watu walichecka walisema kumbe ana matiti feki. Yaani unaona kabisa ni mpira wa kupachikwa.
Basi, kuna kipindi tulikuwa tunapumzika. Akatokea mcheza sinema, Shirley Knight, ambaye anacheza kama mama yake Jayma Mays. Alikuja mezani kwetu alichukua kisu na kasema, "Naomba mtu anichome kisu!" Heh! Tulipigwa butwaa na kubakia midomo wazi. Alichukua kisu na kuanza kujichoma maeneo ya tumbo. Tukadhania huyo mama ni mwendazimu. Basi aliishia kucheka na kusema kavaa mapedi kusudi aonekana ni mnene maana siyo mnene hivyo. Hapo na sisi tulianza kucheka. Lakini kwa kweli tulishikwa na woga.

Kwenye scene ya mwisho ya arusi, mimi na mama mwingine mweusi tuliambiwa tusimame na Jamal Mixon. Nilifurahi kweli maana hapo chensi ya kuonekana vizuri kwenye sinema inakuwa kubwa kama uko na moja na wahusika wakuu wa sinema. Jamal utamkumbuka kwenye sinema kama, The Nutty Professor na Gridiron Gang.

Baada ya kumaliza scene ya arusi, tuliambiwa tubadilishe nguo. Halafu tulipiga scene ambayo tunakimbia. Jamaa anafoka, "Kuna mtu mwenye bastola!" Basi ndo tunakimbia kutoka nje ya mall. Karibu tukanyagane utadhani mtu alikuwa na bastola kweli.

Wakati tunasubiri kupiga hizo scene niliongea na Jamal na kaka yake Jerod Mixon. Kwa kweli ni vijana poa sana. Tuliongea kuhusu sinema za Hollywood na jinsi roles kwa ajili ya weusi ambazo ni za maana ni chache. Jamal alisema kuwa anatunga screenplays sasa akiwa hayuko kwenye sinema.

Kuona scene kutoka The Nutty Professor Bofya linki chini ni sinema ya kwanza ambayo Jamal alifanya wakati huyo ana miaka 14:

Tuesday, March 25, 2008

Sinema ya Mall Cop

Hapa niko Holding Area nangojea kuitwa kwenye seti. Kwa nyuma kabisa ndo walikuwa wanapaka watu make-up na kutengeneza nywele na sehemu ya kubadilisha nguo. Holding ilikuwa kwenye tent iliyowekwa kwenye parking lot ya Mall.
Mimi na Mwanangu


Wadau, hamkujua kuwa nilifungua miezi mitatu iliyopita! Jina la mwanangu ni Prop.

Ukweli huyo ni mdoli. Jana, nilikuwa extra kwenye sinema 'Mall Cop aka. Untitled Kevin James Project.' Hatujui itaitwa nini ikitoka mwakani.

Kulikuwa na hizi baby strollers kama 5 zenye midoli halafu Prop Master (anayegawa vifaa), alikuwa anachagua watu wa kuwa Moms. Ukichaguliwa unapewa stroller. Wengine walipewa shopping bags zilizojaa vitu kama makaratasi na chupa tupu. Sasa sinema ikitoka utaona huyo mtoto anasukumwa na watu mbalimbali, lakini kwa asiyejua wanavyotengeneza sinema utadhani kila mtu ana mtoto wake. Partner wangu kwenye set alikuwa mwanaume wa kizungu anaitwa Steve.

Tulikuwa extras zaidi ya 250 ilikuwa shuti kubwa Burlington, Mall, huko Burlington, Massachusetts. Tulifika kwenye set saa 11:30 (5:30am) na kuruhusiwa kuondoka saa 1 jioni (7:00PM). Siku ilikuwa ndefu. Na miguu wa watu iliuma maana kazi yetu ilikuwa kutembea mle kwenye seti na kujifanya ni shoppers.

Tulikuwa na yule Kevin James, wa ile show, The King of Queens. Yeye ndo stelingi. Nilipita nyuma yake. Sijui kama nitaingia kwenye final cut yaani picha ambao watu wataiona kwenye sinema.