Showing posts with label Khadija Kopa. Show all posts
Showing posts with label Khadija Kopa. Show all posts

Saturday, October 29, 2016

Khadija Omar Kopa Adunda Mjini Mwanza na Show Kabambe!

Malikia wa Taarabu Afrika Mashariki na Kati, Khadija Omar Kopa, akitoa burudani kwa wakazi wa Jiji la Mwanza usiku wa kuamkia leo ndani ya Villa Park Resort kwenye show ya Usiku wa Mshike Mshike iliyoandaliwa na 102.5 Lake Fm Mwanza.
Na BMG
Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.
Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.
Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.
Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.
Wananzengo wakifurahia burudani iliyotolewa kwenye Usiku wa Mshike Mshike na 102.5 Lake Fm
Timu ya Uongozi na Wafanyakazi wa 102.5 Lake Fm Mwanza pia ilitambulishwa kwa Wananzengo kwenye show hiyo
Timu ya Uongozi na Wafanyakazi wa 102.5 Lake Fm Mwanza pia ilitambulishwa kwa Wananzengo kwenye show hiyo
Wananzengo kutoka 102.5 Lake Fm Mwanza
Timu ya Uongozi na Wafanyakazi wa 102.5 Lake Fm Mwanza pia ikijitambulisha kwa Wananzengo kwenye show hiyo
Madjz wa 102.5 Lake Fm, Dj Hcue (katikati), Dj KFlip (kushoto) na Dj Dhifa (kulia)
Dj Dhifa
Dj KFlip (kushoto) na Dj Hcue
Khadija Omar Kopa akihojiwa na wanahabari baada ya show
Hakika 102.5 Lake Fm Mwanza ni Raha ya Rock City na ni Redio ya Wananzengo. Kaa tayari kwa show ijayo.
Bonyeza HAPA Kwa Taarifa Zaidi

Saturday, February 28, 2015

Historia Fupi ya Marehemu Captain Komba!

 Mbunge wa Mbinga na Msanii maarufu, Captain John Komba, alifariki dunia leo katika hospitali ya TMJ mjini Dar es Salaam, kutokana na athari za ugonjwa wa kisukari. Mwenyezi mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.
The late Captain John Komba


Historia Fupi ya Marehemu John Komba
Marehemu Kaptain Komba alizaliwa Marchi 18 mwaka 1954 alipata elimu ya msingi huko nchini Tanzania katika shule ya Lituhi baadae elimu ya sekondari katika shule ya sekondari ya Songea iliyopo kusini mwa Tanzania kuanzia 1971 hadi mwaka 1974.

Mwaka 1975 hadi mwaka 1976 Marehemu John Komba alijiunga na chuo cha ualimu kilichopo Kleruu Iringa, Kusini Magharibi mwa Tanzania ambapo alihitimu cheti cha ualimu.

Marehemu John Komba ni mwanajeshi ambaye alipata mafunzo ya uafisa wa Jeshi katika chuo cha Maafisa wa Jeshi kilichopo Monduli kaskazini mwa Tanzania mwaka 1977 hadi mwaka 1978.

Keptain John Komba pia alipata mafunzo mengine ya siasa kutoka chuo Kikuu cha Washngton International ambapo alitunukiwa shahada ya siasa mwaka 2006 hadi mwaka 2008.


**********************************************************************

Waziri wa Ardhi,William Lukuvi (wa kwanza kushoto) akimfariji mke wa marehemu, Salome Komba

Khadija Kopa akilia kwa Uchungu nyumbani kwa Komba.
 

Thursday, June 06, 2013

Khadija Kopa Yu Hoi Kwa Majonzi - Msiba wa Mume Wake Jaffari Ally

Yaani namwonea huruma Dada Khadija, alikuwa safarini hakupata nafasi ya kumwaga mume wake,  mume wake amefariki ghafla yaani. Mimi mwenyewe kama mjane mara mbili ninaelewa uchungu wake. Sasa hebu cheki hiyo picha ya chini. Huyo jamaa anayecheka anastahili kuzabwa kibao!  Hata haya hana!

Picha hizi ni kwa Hisani ya Ofisi wa Makamu wa Rais


 Mkuu wa mkoa Rukwa Eng. Stella Manyanya kushoto akimfariji msanii na taarab na malkia wa mipasho Tanzania Khadija omar Kopa alipokua kwenye chumba maalum cha kupumzikia wageni kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leoa alfajiri kutokana na ugonjwa. Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani kitaifa yaliyoadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana (Picha na ofisi ya Makamu wa Rais).


Picha juu na chini ni Baadhi ya viongozi na wananchi wa mkoa wa Rukwa na Mpanda wakimsindikiza kupanda ndege msanii wa taarab na malkia wa mipasho Tanzania Khadija Omar kopa kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf.


Siku ya Harusi ya Dada Khadija Kopa na Jaffari Ally Mwaka 2008 (picha za harusi kwa hisani ya Michuzi Blog)

*****************************************
Kutoka Tanzania Daima

Mume wa Khadija Kopa afariki


\na Andrew Chale, Bagamoyo

DIWANI wa Kata ya Magomeni mjini hapa, ambaye alikuwa mume wa Malkia Mipasho nchini, Khadija Kopa, Jaffar Ali Yusuf amefaiki usiku wa kuamkia jana katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Tanzania Daima mjini hapa jana, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi, alisema msiba huo umepokelewa kwa masikitiko makubwa.

“Msiba tumeupokea kwa masikitiko makubwa na shughuli za mazishi zinaendelea, ambapo marehemu anatarajiwa kuzikwa, kesho...” alisema Kipozi.

Baadhi ya watu wa karibu wa marehemu, walibainisha kuwa alikuwa akiumwa muda mrefu bila kutaja ugonjwa uliokuwa ukimsibu.

Kwa upande wake, Katibu wa Tanzania One Theater (TOT), Gasper Tumaini, alithibitisha kupokea msiba huo na kubainisha kuwa malaria kali ndiyo iliyosababisha kifo hicho.

Marehemu alinyakua kiti hicho cha udiwani wa Magomeni miezi michache iliyopita baada ya diwani wa awali aliyekuwa anaongoza kata hiyo, Abdalah Mshindo kufariki mwaka jana.


Khadija Kopa Afiwa na Mume Wake!

Nimepata taarifa kuwa mume wa malkia ya mipasho, Khadija Kopa,  Mr. Jaffari Ally amefariki dunia saa 9 usiku wa kuamkia leo. Nitabandika updates nikipata. 

Pole sana Dada Khadija Kopa.   Mungu akutie nguvu katika kipind hiki kigumu.  Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi. Amin.

Naona salamu za pole zinamiminika kwenye Facebook page yake: https://www.facebook.com/MalkiaKhadijaKopa?fref=ts 
  
Jafari na Khadija Kopa, walifunga ndoa mwaka 2008.
 
 Wakati kifo hicho kinatokea mke wake hakuwepo jijini Dar, kwani alikuwa safarini Rukwa alikokwenda na kundi zima la TOT kwa ajili ya kusherehesha Sherehe za Siku ya Mazingira Duniani zilizofanyika Kitaifa mkoani humo, ambapo leo anatarajia kuwasili jijini. 

Ratiba kamili ya msiba huo bado hadi sasa haijafahamika lakini inadhaniwa huenda msiba huo ukawa  maeneo ya Chaline au Lugoba ambako ni nyumbani kwa wazazi wa Marehemu.
***********************************************
Khadija Kopa (kulia) mume wake na watoto wao mwaka jana kwenye tuzo.

Khadija Kopa akiwa na mumewe kabla ya kupanda jukwaani kutoa burudani  (picha ilipigwa 2012)


MUME WA KHADIJA OMARY KOPA"MALKIA WA MIPASHO TANZANIA"AMEFARIKI USIKU HUU MIDA YA SAA TISA USIKU POLEE SANA KHADIJA KOPA NDUGU JAMAA NA MARAFIKI

BWANA AMETOA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE!
"AMEN"

Wednesday, September 03, 2008

Bibi Arusi ni....Khadija Kopa! Anameremeta!




Malkia wa mipasho, Khadija Kopa ameolewa!
Hebu wapashe dada! Ulipendeza sana siku ya arusi.
Picha kutoka Michuzi Blog.