Showing posts with label Magauni. Show all posts
Showing posts with label Magauni. Show all posts

Saturday, February 28, 2015

Gauni ya Lupita Nyong'o Iliyoibiwa Hollywood Imepatikana - Ina thamani ya dola $150,000!


Mcheza sinema Lupita Nyong'o

Wadau, jumapili iliyopita, mceheza sinema na mrembo, Lupita Nyong'o,  alivaa gauni enye thamani ya dola za kiMarekani $150,000 kwenye Oscars.  Hiyo gaumi imepambwa na lulu 6,000 (ameivaa pichani) na imeshonwa na mwanafesheni maarufu, Calvin Klein.  Baada ya Oscars Lupita aliiacha kwenye chumba chake kwenye hoteli ya kifahari The London West Hollywood na alitoka.  Alivyorudi alikuta gauni imeibiwa.

Sasa indaiwa kuwa aliyeiiba, kariudisha baada ya kugundua kuwa hizo lulu ni feki.  Mwizi alinyofoa lulu mbili na kuzipeleka kwenda kuuza kwa sonara, ndo kaambiwa ni feki.
 
Lupita Nyong'o ni mcheza sinema kutoka Kenya aliyepata umaarufu baada ya kushinda Oscar mwaka jana, Aliigiza kama mtumwa katika sinema,  12 Years a Slave.  Pia, alipendwa kwa urembo wake hasa baada ya wanafesheni kugundua kuwa anaweza kuvaa nguo vizuri  na kupendeza kuliko Model!

Kwa habari kamili BOFYA HAPA.

Monday, May 18, 2009

Picha za Prom

Wadau, hapa Marekani watoto wakimaliza Form 4, wanafanya sherehe kubwa ambayo inaitwa PROM. Wanavyojiandaa kwa mavazi, usafiri wa limo, hoteli, utadhani ni arusi. Nimetumiwa hizi picha za nguo vijana waliovaa kwenye Prom mji fulani hapa USA. Nimetafsiri captions.


Tukae kimya dakika moja tuombee hao ndege.Doh! Mnaweza kuona chupi!
Hivi ilikuwa lazima ageueke? Na huko nyuma ni madudu gani tena?Huyo dada anaenda Prom au Beach?

Njemba kalazimishwa kwenda na huyo dada!
Nywele ya Maiti

Hajawahi kusikia habari ya deo za Invisible Solid?

Hata Mbwa kapakwa rangi!

Hao wamevaa nguo za kulala?

Huyo naye denti?
Yaani huyo bado anasoma Sekondari?

Njemba atahitaji 'counselling'!