Showing posts with label Miss Uganda. Show all posts
Showing posts with label Miss Uganda. Show all posts

Thursday, February 23, 2012

Producer wa Amazing Race Afariki Uganda

Wadau, kama mtakumbuka kama miaka mitatu iliyopita TV Show Amazing Race, walipitia Tanzania.  Katika Amzaing race timu zinasafiri katika nchi kadhaa za dunia, timu ya kwanza kufika katika sehemu mjia kadhaa inashinda siku hiyo.  Zanzibar ilipata umaarufu walipopitia hapo.

Leo kuna habri kuwa moja wa maproducer, Jeff Rice, amefariki dunia mjini Kampala.  Alikuwa anafuatilia habari tofauati lakini.  Polisi wa Uganda wanasema kuwa kafa kwa cocaine overdose.  Jamani,  kama kweli kafa kwa cocaine overdose itakuwa si mara ya kwanza mzungu/mtalii kufa kwa overdose barani Afrika.  Wakati nafanya kazi Daily News kuna mwarabu kutoka Royal Family alikufa kwa overdose Embassy Hotel lakini tulizuiliwa kuchapisha hiyo habari.

Kuna watalii ambao kazi yao ni kwenda nchi zingine kutumia madawa ya kulevya na kufanya ngono ya ajabu kwa vile wakifanya hapa Marekani sifa zao zinaharibika na wanaweza kufungwa.

Lakini familia ya marehemu, Jeff Rice, wanadai kuwa huenda alipewa sumu kwa vile alikuwa anafanya uchunguzi sijui kuhusu nini.  Ukweli utajulikana.

REST IN PEACE JEFF RICE.


***************************



Production facilitator Jeff Rice, who worked for reality shows including the current season of 'The Amazing Race,' was found dead after a suspected poisoning.
'Amazing Race' Producer's Death: Police Await Assistant's Recovery to Gain More Info


By BAZI KANANI and KEVIN DOLAK
Good Morning America –

....Investigators and family of the former "Amazing Race" producer Jeff Rice, who was found dead in a Uganda hotel room last Friday, are waiting to learn more about what might have killed him -- a cocaine overdose or suspected poisoning -- from his assistant, who remains in critical condition in a Kampala hospital.

Rice's body was found at the luxury Serena hotel in the capital city of Kampala. His assistant, Katheryne Fuller, was found unconscious.

"Ms. Fuller is slowly recovering, and when she is recovered enough we will be able to talk to her and find out more about what happened," Uganda Police Force spokesman Asuman Mugenyi said. "She is not able to speak. Although she is responding to the treatment, she is not yet available to explain what transpired."

Police say hotel staff noticed a man hanging on a balcony last Friday, and when they went to the room they found the 39-year-old's body on the balcony and Fuller unconscious in the room. Staff called police and rushed the two to a hospital, where Rice was declared dead, police said.

Investigators initially believed Rice and Fuller may have been sickened by some type of food poisoning. Later Mugenyi denied reports that Rice had been poisoned after he rebuffed a shakedown attempt from local "thugs," although friends remain skeptical.

"I was shocked. Jeff was someone who was terrific at his job," Josh Gates, a friend of Rice's told ABC News. "I don't know exactly what to think about what happened to Jeff. I hear conflicting reports coming out of the region."

Ugandan police said they have now ruled out poisoning and said further testing found high-levels of cocaine in Rice's system. Sources said Rice and Fuller were working on an investigative documentary, and many fear they might have been targeted by locals.

"For him to pass away so young so suddenly is alarming, obviously, but also is surprising because he was someone who was really able to take care of himself in the field. He was excellent at what he did," Gates added.

Rice was a veteran producer who worked on the latest season of the hit reality series "The Amazing Race" and the Emmy-nominated Animal Planet series "Whale Wars." In addition to raising two young kids, Rice and his wife, Sally Blackman, operated a television and film production company called SB Productions in Durban, South Africa.

Katheryne Fuller's father Stuart Fuller confirmed Rice were shooting a documentary, and other crew members who were with them should know more about what sickened them. Stuart Fuller said he is now with his daughter at the hospital in Kampala.

"She is OK. We are trying to get her back to South Africa. She needs medical attention that they can't do here," he said.

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:

Wednesday, October 26, 2011

Gaddafi Aliwatendea WaTanzania Mabaya - Vita Vya Kagera


Inaelekea waTanzania wengi wamesahau historia kati ya Libya na Tanzania. Marehemu Gaddafi alikuwa rafiki yake mpenzi nduli mshenzi Dikteta Idi Amin Dada wa Uganda!  Gaddafi alitaka Amin amwoe binti yake! Gaddafi alituma wanajeshi kutoka Libya kuwasaidia Uganda katika vita vya Kagera mwaka 1978-79.  Sisi wazee tunaukumbuka huo vita na miezi kumi na nane (miaka 18) ya shida iliyofuata!  Maoni chini yameandikwa na mwanachama la kundi - Wanabidii
Gaddafi alipotembela Uganda mwaka 1973
 ...Wanabidii!


Binafsi nachukia sana kuandika bila ya ushahidi! Na zaidi sipendi kuandika "propaganda" na taarifa za uzushi; isipokuwa napenda kuandika taarifa zilizotafitiwa kwa kuandikwa na mtafiti mwenyewe (na au mwandishi aliyeandika matokeo ya utafiti au kufanya upembuzi wa utafiti husika). Takriban wiki moja sasa (tangu Alkhamis ya tarehe 20 Oktoba, 2011) uwanja wa "Wanabidii" na majukwaa mengine ya kijamii yamekuwa yakijadili "Kuuawa kwa Kanali Muammar Gaddafi" kulikofanywa na wale wanaoitwa waasi (wa NTC) wakisaidiwa na NATO wakiongozwa na Uingereza, Marekani, Ufaranza na washirika pamoja na Waarabu (Saudia na Qatar). Gaddafi ameuawa; kwa jinsi gani, kila mmoja amesoma, ameona (kwenye picha za mnato) na au kwenye picha za video!

Ninachotaka kuandika na pengine kuanzisha "mjadala" wa kiakili ni juu ya "GADDAFI KUMSAIDIA IDI AMIN DADA KWENYE VITA VYA KAGERA [UGANDA DHIDI YA TANZANIA MWAKA 1978 HADI 1979]". Napenda niweke wazi kwamba, "historia haisomwi ili kufufa 'chuki' bali husomwa kujua yaliyopita, kuyasanifu yaliyopo na kupanga mipango kwa yajayo!". Hivi ndivyo tunavyosoma historia iwe yenye kuhuzunisha au kufurahisha! Tanzania ilipigana vita na Uganda, vita iliyoitwa VITA YA KAGERA (japokuwa ilipiganwa hata ndani ya Uganda na Idi Amini Dada kufurushwa na kuikimbia Ugnda!).

Kwa ujumla, tangu pale kifo cha Muammar Gaddafi kilipotangazwa kwa mara ya kwanza na kituo cha runinga cha Al-Jazeera na kukaririwa na vituo vingine na mashirika ya habari ya kimataifa kama BBC, CNN, Reuters, Xinhua, AFP, AP na IRNA (Press Tv) kumekuwa na mchanganyiko wa "mawazo" kwa wananchi wa Tanzania juu ya "hali" ya Gaddafi kisiasa katika mtazamo wa kifalsafa...hususan wengi wa wachangiaji kwenye mijadala hiyo wanamuona Muammar Gaddafi kama "shujaa" na "mwanamapinduzi" na "kiongozi mtukuka" na "aliyejitolea kuunganisha Afrika" na hata wengine kufikia kiasi cha kuonyesha kwamba hajawahi kutokea kama Muammar Gaddafi na hata kumpa "daraja" ya kuwa "Baba wa Afrika" na mshumaa uliyozimika! Hata hivyo wengi wamesahau kamba ni Muammar Gaddafi ndiye aliyemsaidia Idi Amin Dada kwenye Vita vya Kagera! Naomba sasa tuangalie nini alifanya Gaddafi wakati wa vita vile.

Vita vinahitaji rasilimali watu (askari na wataalamu wa kijeshi), fedha za kuendeshea vita na zana (za kivita na za mawasiliano ya kivita). Kwa mujibu wa taarifa rasmi na zinazothibitishwa na taarifa rasmi za kihistoria Muammar Gadafi alimpa Idi Amin Dada usaidizi ufuatao:

1. WANAJESHI (WAPIGANAJI) 3,000 (Elfu tatu kutoka Libya na nchi zilizokuwa na mahusiano na Libya ambazo Gaddafi likuwa anazisaida na zenye uzowefu wa mazingira ya vita [military knowhow and skills on interlocustrine terrain]);

2. ZANA KAMA VIFARU AINA YA T-54, T-55, BTR, APCs, BM-21, Katyusha MRLs;

3. MIZINGA; na

4. NDEGE ZA KIJESHI AINA YA MiG-21s na Tu-22 Bomber.

Wanajeshi wa Libya waliyotumwa Uganda walikuwa katika makundi yafuatayo: ASKARI WA KAWAIDA; WANAMGAMBO; NA ASKARI WA VITA VYA MSITUNI (WENYE UZOWEFU WA VITA VYA KIENYEKI KUTOKA JANGWA LA SAHARA [MAARUFU KAMA WATUAREG KUTOKA TCHAD, NIGER, ALJERIA NA DARFUR]). Hata hivyo, shukrani za pekee kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (TPDF) waliyefanyakazi ya ziada ya kujitoa mhanga kupigana "kiume" na hatimaye kuyashinda majeshi ya Idi Amin Dada akisaidiwa na Muammar Gaddafi. Hata ilipofika mwezi wa Aprili, 1979 na Idi Amin Dada alipopoteza udhibiti wa nchi ya Uganda aliamua "kuikimbia" Uganda na kituo chake cha kwanza kilikuwa Libya (kwa Muamar Gaddafi) na alipewa "hifadhi" ya muda na baadaye kwenda "uhamishoni" nchini Saudi Arabia (alikoishi hadi kufa kwake akiwa Jeddah).

Kwa wasomaji na "wanabidii" na wengine wanaomtazama Muammar Gaddafi kwa kusahau "aliyoyafanya" dhidi ya kumsaidia Idi Amin Dada kuendesha vita na Tanzania nadhani wana wajibu wa kujiuliza masuala haya (hii ni pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inawajibu wa kusema ukweli):

1. Wamesahau "hadithi" hii ya Vita vya Kagera? Au, vita hivi vilikuwa "propaganda" ya kisiasa?

2. Gaddafi alidhamiria nini kumsaidia Idi Amin Dada aliyeapa kuisambaratisha nchi (Tanzania) na kwa kuanzia aliteka Kagera na kuifanya sehemu ya Uganda?

3. Kama Idi Amin Dada wa Uganda alitangazwa "dikteta", "bundi", "joka", "fisi mla watu", na masimulizi mengine ya kutisha (hata ya kula nyama za watu); mtu aliyekuwa akimsaidia mtu wa aina hiyo (kama Gaddafi) anaitwaje?

4. Je, historia ya Vita vya Kagera iliandikwa kwa wino "gani" hadi leo imesahaulika?

5. Au, wote wanaodhani kwamba Muammar Gaddafi ni "shujaa" wa Afrika wamezaliwa miaka ya 1980? Na kwa jinsi hiyo hawajui kilichotokea kati ya miaka ya 1978 na 1979?

Mwisho, siandiki haya katika kuwakumbusha "majonzi" wananchi wa Kagera waliyeuawa kikatili na Idi Amin Dada; siwakumbushi machungu ya kutiwa vilema vya maisha; siwakumbushi madhila ya "kubakwa" wanawake kulikofanywa na askari wa Idi Amin Dada; na wala siwakumbushi jinsi mali zao (mashamba na nyumba) zilizvyoharibiwa na "ushenzi" wa Idi Amin Dada! Nataka niwakumbushe kwamba, "hatuwezi kurudisha nyuma historia; lakini ni wajibu kuisoma ili vizazi vijavyo vipate kumbukizi yenye kujenga mujtamaa wao." Gaddafi alikuwa "rafiki" na wakati huohuo alikuwa "adui" kwa vile alikuwa na "sura mbili ndani ya moja".

Na kwa serikali (iliyoonekana kumuunga mkono); hii ni dhana (binafsi) inawezekana Muammar Gaddafi alilipa sehemu ya "maumivu" ya vita alivyomsaidia rafiki yake mpenzi Idi Amin Dada...kama ndivyo, basi ni vema watuambie! Hatuwezi kusomeshwa historia ya "uongo" juu ya Muammar Gaddafi kumbe "mtu" huyu (yaani Gaddafi) alikuwa "mtu mwema" na kiongozi "mzuri" kuliko hata Mzee Mandela na Mwalimu Nyerere...naomba tuwe "wakweli" na kwa kusisitiza: UKWELI UTATUWEKA HURU; KAMA GADDAFI ALIKUWA RAFIKI WA AFRIKA KWA NINI ALIMSAIDIA IDI AMIN DADA KUTUPIGA? TAFAKARI SEMA UKWELI JAPOKUWA UKWELI WENYEWE NI DHIDI YA NAFSI YAKO!

Bakari M Mohamed, BBA[PLM], CPSP[T], MSc (PSCM)

Tuesday, February 08, 2011

Lazima Uchanjwe Dhidi ya Ugonjwa wa Manjano Zanzibar

Kama unataka kusafiri kwenda Zanzibar ni lazima upate chanjo dhidi ya ugonjwa wa manjano (yellow fever). Miaka mingi ulikuwa huihitaji lakini baada ya kuibuka upya huko Uganda wasafiri wanalazimika kuchanjwa! Ugonjwa na manjano unasambazwa na mbu kama malaria. Ukipiupata si rahisi kupona. Je, Tanzania Bara watalazimisha wasafiri kuchanjwa?
***************************************************************************
Yellow fever vaccination needed for Zanzibar

1st February 2011

Those travelling to Zanzibar, will now require a yellow fever vaccination, after an outbreak of the disease has caused 53 deaths in northern Uganda

So far around 226 cases of yellow fever have been reported in northern Uganda, including 53 deaths. The Zanzibar Ministry of Health is now warning all tour operators and airlines, both national and international, that visitors will require a yellow fever vaccination certificate in order to enter the country.

Before the outbreak, travellers needed to have the yellow fever jab if they were travelling to Zanzibar from a yellow fever endemic zone, now however the Zanzibar Ministry of Health have announced all visitors entering Zanzibar will need to have the yellow fever vaccination and a certificate to prove it.

Chris McIntyre of Expert Africa explained, "We've usually recommended to clients that they have the Yellow Fever vaccination if going to Zanzibar, but now they are insisting on it, wherever you are coming from.

"There have been reports of people being taken off the plane, being given the jab, and being made to pay for it. We strongly advise you to have your jab before you go."

Yellow fever is a very serious viral disease with a high rate of fatalities. It is transmitted by the day-active, stripy-legged mosquitoes called Aaedes. The disease is preventable with a yellow fever vaccine.

Dr. Jane Wilson-Howarth emphasises that is is good sense to be protected from Yellow Fever, "Those contracting the disease have about a 50:50 chance of survival. It becomes effective 10 days after the vaccine has been given and so the certificate is valid from 10 days and for 10 years.

"If you do end up getting compulsory immunisation in country (and this certainly happens on occasion in South America) you cannot know about the quality of the vaccine nor the sterility of the needles. There also may not be medical back-up in case of an allergic or other vaccine reaction."

http://www.wanderlust.co.uk/magazine/news/yellow-fever-vaccination-needed-for-zanzibar

Wednesday, October 07, 2009

SweetEazy Ijumaa

Food from Uganda - Music from Uganda – Hosts from Uganda. Rest from Sweet Eazy.

Join the Uganda Independence Day Celebrations - this Saturday, from 8pm.
Tubaniliza!

Saturday, May 16, 2009

WaGanda Kutulipa Fidia Kwa Kumfukuza Idi Amin


Kutoka Bongo Pix Blog:


The government of Uganda is planning to pay a compensation fee to the government of Tanzania for the help offered Uganda in the 1979 liberation war that overthrew the government of self proclaimed Uganda life President Idd Amin Dada.

The Minister of East African Affairs, Eriya Kategaya says that the two government are still in discussions over the amount of compensation.He says that was it not for the support of Tanzania troops in 1979, Uganda would still be backward and probably still under the rule of Idd Amin.
Kategaya told Parliament today that Tanzania spent a lot of money to fight Amin, lost many soldiers in the war that overthrew the government of Amin, and therefore deserve to be compensated.He says the compensation is a sign of appreciation on the part of Uganda for the help Tanzania gave to Uganda at the time of need.

Many Ugandans who had been exiled mainly in Tanzania and Kenya appealed for regional support in overthrowing Amin, considered by many as a tyrannical dictator. The Tanzania government then under President Julius Kambarage Nyerere (RIP) sent its troops who fought alongside Ugandan guerilla forces to overthrow Amin.

Friday, December 05, 2008

Miss Uganda

(Pichani ni Miss Uganda 2008)

Wadau, hivi kwenye mashindano ya Miss Tanzania kuna kigezo cha Urefu? Katika Miss Uganda kuna kigezo kuwa mshiriki ni lazima awe na urefu wa futi 5'7" na zaidi.

http://missugandapageant.com/