Showing posts with label University of Dar es Salaam. Show all posts
Showing posts with label University of Dar es Salaam. Show all posts

Thursday, January 01, 2015

Kwa Nini Levina Alijiua ? The Case of Levina Mukasa - UDSM

Wadau niliandika habari hii nikiwa mwandishi wa habari Daily News mwaka 1991.  Kesi hii ilikuwa chanzo cha ile Movement ya Kumpambana na Unyanyasaji wa Kijinsia wa Akina Mama Tanzania (Sexual Harassment).  TAMWA iliongoza movement hiyo. Nasikia mmoja waliyomnyanyasa Levina, Omari Saloti ni marehemu. Sijui huyo Mark Victgor yuko wapi, lakini ana damu mikononi mwake.

******************************************************************************
The Late Levina Mukasa
Na Chemi Che-Mponda

 Tarehe kama ya leo mwaka 1990 wakati mwanafunzi wa kike wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alipojiua, watu wengi walifikiri kuwa alifanya hivyo kwa sababu alikuwa na matatizo kwao na kuwa masomo yalikuwa yanamshinda. Hata hivyo, waliposikia kwamba alifanya hivyo kutokana na unyanyawaji wa kijinsia uliofanywa na wanafunzi wawili wa Kitivo cha Uhandisi pamoja na kikundi kilichojukana kama “Punch”, baadhi walikasirika wakati wengine walicheka tu.

Marehemu Levina Mukasa, alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza aliyekuwa akisomea shahada ya ualimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kulingana na maelezo ya waliokuwa wakimfahamu wanasema alikuwa mkimya mwenye msaada na ambaye wakati wote alikuwa tayari kutumia vitu vyake na wenzake. Kila aliposoma wakati wote alishika nafasi ya juu darasani.

Mnamo tarehe 7 Februari 1990, Levina alikatisha maisha yake kwa kumeza vidonge vingi vya klorokwini (vinavyotumika kutibu Malaria). Swali linabaki, “kwa nini alifanya hivyo?” Karibu kila mwanafunzi wa kike aliyesoma katika kampasi kuu ya Chuo Kikuu (inayojulikana sana kama Mlimani) atakuwa amenyanyaswa kijinsia katika kipindi cha Miongo miwili iliyopita. Wamekuwa wakidhihakiwa, kutishiwa kijinsia au kuvamiwa papo kwa hapo na kubakwa.

PUNCH

Pamoja na hayo lipo kundi la kisirisiri hapo mlimani linajukana sana kama PUNCH, linafikia hata kiwango cha kuchapisha maandishi na michoro michafu kuhusu habari za kimapenzi za sasa au za zamani za Mhasirika wao. Madhumuni hasa ya PUNCH ni kuwaweka wanawake chini ya wanaume, kuwafanya wanafunzi bora wa kike washindwe masomo yao na hata kulazimika kukatisha masomo. Inatumiwa pia kuwatishia wasichana wakubali kufanya mapenzi na watu wanaowataka ambao wako katika kundi la PUNCH. Kumkataa mtu aliyeko kwenye kundi la PUNCH kunamfanya mhusika“apanchiwe”.

Bahati mbaya, wanawake walio katika kampasi wanaiogopa PUNCH. Wanafungwa na sheria zake kama vile kutokunywa chai ya saa 10.00 katika mgahawa, kutokukaa kwenye high table, kutokuvaa khanga Mgahawani n.k. Wengine wanafurahia hata kumwona mwanamke mwenzao akipanchiwa. Kutokana na maelezo ya shangazi wa marehemu, Dkt. V.K. Masanja, ambaye ni mhadhiri wa hapo Mlimani, matatizo ya Levina yalianza wakati wa dansi ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza iliyofanyika kwenye hoteli ya Silversands ambapo alikataa kwenda na mwanafunzi wa mwaka wa nne wa Kitivo cha Uhandisi aitwaye Mark Victor.

FUJO

Levina alienda dansi hiyo na rafiki zake. Victor alipomuona alimtaka warejee pamoja na akalalamika kwa nini alidhubutu kwenda kwenye dansi na watu wengine wakati alikataa kwenda naye. Levina alikataa kuondoka naye na Victor akamvuta gauni, rafiki zake walijaribu kumtetea na papo hapo ugomvi ukaanza. Baadhi ya marafiki wa Victor wanaojita “Engineers” [Wahandisi] [kundi linalofahamika sana kati ya wanafunzi] walimsaidia Victor. Kundi jingine lijulikanalokama “insiders” walimsaidia Levina. Hatimae, baada ya kushindwa Wahandisi waliondoka kwenye dansi, lakini huo haukuwa mwisho wa matatizo ya Levina.

Waliporejea kwenye dansi mgogoro mwingine ulizuka kati ya Victor na kundi lake na Levina na rafiki zake. Walipofika kwenye mabweni yao, Victor alikuwa akimsubiri ndipo ikawa usiku mzima kutupiana matusi. Asubuhi na mapema Levina alipeleka malalamiko MUWATA [Serikali ya wanafunzi] uongozi ambao ulisulihisha tatizo hilo. Victor aliomba radhi na akadai kuwa alikuwa amelewa.

Siku iliyofuatia, tukio la Silversands lilipanchiwa. Michoro ya Punch haikumwonyesha jina lake lakini kwa kutoa namba yake yakusajiliwa ilidhihirisha kuwa michoro inayofuatia angekuwemo. Baadhi ya wanafunzi wa kiume walimwendea Levina na kumwambia kuwa walikuwa kwenye kundi la PUNCH. Walimtishia kumpanchi iwapo angekataa kufanya nao mapenzi. Aliwakatalia na akakosa raha sana. Mmojawapo wa wanafunzi hawa alikuwa Omari Saloti, mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Uhandisi.

Dkt. Masanja alisema kuwa yeye (Levina) ndiye alimweleza yaliyotokea. Dkt. Masanja alisema kuwa alimweleza Levina kuhusu uzoefu wake na mambo ya PUNCH alipokuwa mwanafunzi na jinsi alivyoweza kuyapuuza. Alisema kuwa Levina alionyesha kupata ujasiri na akafikiria kuwa mambo yamekwisha. Marafiki wa Levina waliambiwa kuwa wangepanchiwa iwapo wangeonekana wakiandamana naye. Alitengwa. Maelezo machafu yalitolewa na maandishi yaliandikwa dhidi ya jina lake katika kila orodha ya majina ambamo majina yake yalikuwemo.

Usiku wa tarehe 3 Februari mwaka huu kiasi cha saa 7.30 wakati Levina alipokuwa kitandani akijisomea alisikia mlango ukigongwa. Kabla hajajibu, mlango ulifunguliwa na Omari Saloti aliingia kwa nguvu chumbani. Walipigana. Levina alimng’ata mkono naye alimpiga ngumi za mashavuni na kwenye matiti. Levina alikimbia akiwa amevaa gauni ya kulalia tu na akajificha kwenye kichaka kilichoko nje ya bweni wakati Saloti akiwa bado anamnyemelea. Aligonga nyumbani kwa mlinzi, ambaye alimsindikiza hadi chumbani kwake na akasubiri kwa muda nje.

Madhumuni hasa ya PUNCH ni kuwadhalilisha wanawake

Inasemekana kuwa Saloti alitaka kumbaka, wakati wengine wanasema alimbaka. Wanasema Levina alikataa tu kusema. Hata hivyo Saloti alikuwa amemtishia Levina kuwa angembaka na kumwibia vitu vyake. Asubuhi iliyofuatia, mlinzi alisema kuwa alizungumza na saloti na akasema alikuwa “Amelewa” wakati huo. Levina pia aliwona meneja wa bweni, ambaye alizungumza na Saloti. Alisema kuwa Saloti alimwambia kuwa alifunguliwa mlango na Modesta mwenzake Levina ambaye walikuwa wakiishi naye chumba kimoja. Modesta, alikanusha madai hayo kwani yeye ameoloewa na kila mwisho wa juma huwa nyumbani na familia yake.

Dkt. Masanja alisema alimpa barua Levina na kumwelekeza kwa Mshauri wa wanafunzi, Dkt. Biswalo ambaye alikuwa akienda kwenye Mkutano wa Baraza hivyo naye alimelekeza kwa Mama Rajabu. Waliitisha jalada la Meneja wa bweni/Mlinzi lakini halikuwa na chochote. Levina alifariki jioni ya tarehe 7, Februari 1990. Inaonekana kuwa kundi la Punch ni mabingwa wa vita vya kisaikolojia na wamefanikiwa lengo lao kinyume cha matarajio yao kwa kumkatisha tamaa Levina mpaka akaona kuwa maisha yake hayana maana tena. Zaidi ya hayo utu wake ulikuwa umedhalilishwa na jitihada za Saloti za kutaka kumbaka [Maana katika jamii ya Kitanzania inaaminika kuwa mwanamke akibakwa amependa mwenyewe].

Kutokana na Punch kuwalazimisha marafiki wa Levina wamtenge, kumdhihaki mbele ya kadamnasi, kumdhalilisha na kumuonea, kutokana na malalamiko yake kutoshughulikiwa na MUWATA kwa kumwambia kuwa hakuna awezaye kushindana na Punch, wakati wengine walikuwa wakimcheka tuu anavyolalamika na rafiki zake wakimuepuka, yote haya yamemfanya alazimike kukata maisha yake kwani aliamini jamii nzima ilikuwa dhidi yake.

Punch ilifanikiwa kuondoa umoja kati ya wanawake. Saloti alifanikiwa kumkosanisha Levina na Modesta, mtu pekee ambaye ndiye alikuwa akimwamini, kwa kudai kuwa yeye ndiye alimpa ufunguo. Ukweli ni kwamba funguo zote za Hall 7 [alimokuwa akiishi Levina] ziliweza kufungua angalau milango mitano, wakati katika Hall 3 bweni lingine la wanawake ufunguo mmoja unafungua milango yote ya gorofa hiyo. Walimfuatafuata na kumgongea mlango usiku wa manane, walimtupia maneno machafu na kumtishia mlangoni pake, walifanya aonekane kama ‘mwenda wazimu’ na asiyefaa.

Mkutano wa dharura wa wanafunzi wa kike wa Chuo Kikuu, wahadhiri, wafanyakazi na wakazi wengine kwenye kampasi uliotishwa tarehe 9 Februari ulikubaliana kuwa wanawake walilaumu uongozi kwa kukataa kuchukua hatua za kinidhamu wakati mambo kama hayo yalipotokea. Wanasema iliendelea hivyo hadi kufikia hatua ya kuwakatisha tamaa wahasirika wasichukue hatua za kisherina kushindwa kutoa ushauri unaofaa kwa wanafunzi.

Levina Shujaa

Walisema kuwa Serikali ya wanafunzi [MUWATA] imekuwa kimya ikiangalia tu na mara nyingine ilishirikiana na waovu hao. Walisema kuwa wanafunzi wa kike ambao walijaribu kupata msaada kutoka MUWATA walijikuta katika matatizo makubwa zaidi, maana walihubiriwa kuhusu ukubwa na uwezo wa Punch.

Zaidi ya hayo wakina mama walisema kuwa jumuiya ya wanafunzi wanaichukulia Michoro ya matusi ya Punch kama burudani muhimu na wanafunzi wanaonewa wametumbukia kutokana na mgawanyo na mbinu za utawala za Punch, wakati wasomi na uongozi wamekaa kimya wakihofia visasi kutoka kwa Punch ambayo ilikuwa, inatikisa jamii nzima. Wakina mama walikubiana kuwa, Levina “asipotee hivi hivi, sisi tumtangaze shujaa ambaye hatimae ameikomesha Punch”.

Hata hivyo wanaume wanaposikia haya wanacheka. Wanauliza, “kwa nini mmuite Levina shujaa? Alikuwa malaya! Alikula pesa za watu! Mlitaka ale tu halafu asilipe? Kwani yeye ni wa kwanza kujiua! Ni m.p.u.m.b.a.v.u. Alikuwa mdhaifu. Alikuwa mjamzito! Unyanyaswaji wa kijinsia ni jambo la kawaida, wanawake pia wanayanyasa kijinsia. Mwanafunzi mmoja alirukwa na akili kwa sababu alikataliwa na msichana.” hayo ni baadhi ya maelezo yanayotolewa na wanaume wetu ndani na je ya kampasi.

Hati zenye kuonyesha uso wa levina zilikuwa zimebandikwa fuvu la Punch. Aliyekuwa Waziri wa nchi asiye na Wizara Maalum, Mheshimiwa Getrude Mongella, alipozungumza kwenye mgahawa baada ya kunywa chai katika ‘high table’ alilaani unyanywasaji wa kijinsia huko Mlimani na kusema ni sawa na kitu kilichokuwa kinachemka na sasa kimepasuka baada yua kufikia kikomo. Mapambano ndiyo kwanza yameanza. Walakini mapambano hayo lazima yaenezwe katika asasi kwanza yameanza. Walakini mapambano hayo lazima yaenezwe katika asasi zote za elimu ya juu na sehemu za kazi. Lazima kuwepo na mapambano ya kitaifa dhidi ya uovu huu!

Makala hii iliandikwa na Chemi Che-Mponda.

Saturday, November 01, 2014

Mzee Richard Mabala Amefiwa na Mke Wake

Kutoka Facebook

Mke wangu mpenzi, Etinisimbo (Manka) amefariki dunia leo baada ya kuugua muda mrefu. Mungu amempumzisha maana magonjwa yalikuwa yanamtesa sana. Naomba sala zenu.

My beloved wide Etinisimbo (Manka) passed away today after months of fighting sickness. She has suffered so much. May God grant her peace now and all of us.

Monday, February 03, 2014

Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam ni kati ya Vyuo Vikuu Bora Africa!

 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni namba 12!!!!!  Miaka ya 1970's nadhani ilikuwa namba 2 nyuma ya Makerere.

*******************************************

University of Dar es Salaam Tops East Africa Top Web Rankings

By Kamau Mbote, 3 February 2014

Tanzania's university of Dar es |Salaam is the top ranked East African University at position 12 in the continent according to the 2014 university web rankings list released by 4icu.org that shows popularity of higher institutions online.

The university which is based at the port city of Dar es Salaam beat other regional heavy weights including Kenya's University of Nairobi at position 17 and Makerere university in Uganda while Rwanda's College of Arts and Social Sciences, university of Rwanda was at position 39.

Kenya however managed to sneak in the highest number of institutions on the top 100 list with five universities as compared to Tanzania's two, Uganda one and Rwanda's one.

4icu says it considers various variables while putting up the web ranking including: the Google Page Rank, Alexa Traffic Rank, Majestic Seo Referring Domains, Majestic Seo Citation Flow and the Majestic Seo Trust Flow. According to 4icu there were a number of universities without websites including two universities from Uganda namely Fairland University and the Uganda Pentecostal University, Rwanda's Kavumu College of Education, Rukara College of Education, while Katavi University of Agriculture in Tanzania also does not have web presence. Apart from web ranking 4icu also recognized universities official social media accounts.

4icu says the aim of its website is to provide an insight into the popularity of university websites especially to international students and academic staff to help them understand how popular a specific University/College is in a foreign country.


Saturday, June 22, 2013

Mwanafunzi wa UDSM Auwawa na Majambazi



Mwanafunzi mmoja kati ya wanafunzi wanne wa mwaka wa IV wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kampasi ya Mlimani wamevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo katika eneo la Yombo la Chuoni hapo. 
 
Inataarifiwa kuwa waanafunzi hao walikuwa wanajisomea na kuandaa “dissertation” zao kwa mwaka wao wa mwisho wa masomo, na ghafla wakavamiwa na watu waliowaamuru watoe kompyuta zao na pochi za fedha. Wanafunzi hao walikubali shuruti hiyo lakini mmoja wa wanafunzi alipoomba walao wachukue nakala ya documents zao kutoka kwenye computer hizo, ndipo mmoja wa majambazi hayo alipomoiga risasi ya tumbo mwanafunzi huyo, ambaye alianguka chini.

Imeelezwa kuwa wanafunzi wengine kuona hivyo waliwasiliana na uongozi wa Chuo kuomba gari la kumwahisha mwenzao Hospitalini.
Taarifa zaidi za hali ya majeruhi huyo bado hazijawekwa bayana.

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na matukio ya kuwavamia wanafunzi vyuoni kwa nia ya kuwapora ama kuwabaka, jambo ambalo limewaacha wengi wakiwa na hofu juu ya usalama wao, baada ya wenzao kupoteza vifaa vyao ama kujeruhiwa na wengine wakipoteza uhai.

Baadhi ya matukio haya yameripotiwa na wanafunzi kuandamana katika vyuo vya St John's Dodoma, IFM Dar, Uhasibu Arusha na sasa Mlimani, Dar.

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2WrTyqTKa

Thursday, April 04, 2013

Msiba - Prof. Michael Wambali (UDSM - Sheria)

Dear All,


Information from the Tanganyika Law Society regrets to announce the untimely death of Prof. Michael Wambali of the School of Law(Formerly Faculty of Law)

Prof. Wambali has passed on a few minutes ago at Muhimbili National Hospital.

Those who knew him have lost a teacher and a friend. The nation has, without doubt lost a legal luminary.

May his soul rest in eternal peace.

MJL

Wednesday, January 04, 2012

Salamu Kutoka Bongo!


Nimetumiwa kwa email:

Imeadikwa na Prof. Akwanza

Pokeni salamu kutoka Tanzania. Najua LGF alishawapelekea picha  ikinionyesha nikishuhulikiwa na joto la Dar.

Nataka kuwaarifu kuwa niweza kusalimika hapa Bongo kwa zaidi ya mwezi sasa.

There is a story I read (I do not remember where) some time ago. In  summary it went like this: One experimentalist took a frog and  put it in a  cooking pot with cold water. The frog was comfortable there.

Slowly the water temperature was raised and the frog kept on adjusting to the new environment. It continued like this up to when the water reached boiling  point and the frog was turned to a frog-stew. On the second
experiment the  water was first brought to boiling point and then the frog was dropped in.

It immediately jumped out and it survived though with some injuries.

Why am I telling this story? Many of those I know from before are at times > at a loss when I lament at the situation I see. Wanasema macho  yatazoea tu  na nitaona kila kitu sawa. Yaani nitakuwa frog-stew.

My arrival in TZ after about 5-years of absence was like that frog that was dropped in boiling water. I wanted to jump from every situation I  found myself. These include

 1. To be told to teach a class of 208 students in a room with only 98 chairs (A108 for those familiar with FoE now CoET). Wengine  wanachungulia> dirishani. I am told this is quit common in some classes.

 2. Really run down of the University of Dar-es-Salaam.  For example: my  favorite walkway "Havard" cafeteria through Hall 2 to my Hall 5 residence (ili ukutane na Warembo wa Hall 3) is barely passable.

 3. The traffic mess all over Dar. BTW I am NOT PROUD of what I have  become, i.e. driving in Dar like the rest of them.

4. The change in the people's values, very materialistic, selfish,  uncaring. This is my conclusion based on how people drive, the way they built security walls without taking into consideration those down stream they need a road too, Furthermore, the lack of care for the environment (mabonde yote yamejengwa) no wonder few hours of rain pour as we had the last two days there are no wetlands to slow down the waters and many many more.

 IMPORTANT

On the other hand there are some real improvements:1. Since my arrival I have no real memorable power outage yet.

 Though nlishakatikiwa maji halfway by shower thus end-up finishing the operation with a small Kilimanjaro water I had in the house.

 2. LGF amenisahau kabisa, baada ya kupata safari ya hafla siku ambayo tulikuwa tukutane ( touge-in-chic. the HAVES have to  working overtime to maintain their position at the top.

 3. Lot of new constructions, thou I do not like the structural  system they are using: heavy concrete frame with solid block for partitioning walls. Two things: either we need to stop paying Architects by the  parcentage of  the cost of the building or file mulpractice to structural engineers or both.

 BOTHERING DEVELOPMENTS

 1. In my opinion, some people have more money than the  government, thus  they can literally do what they want, including things such as to  pay to have a road closed at peak-hour to off-load your truck. I  witnessed this with my own eyes.

2. The widening gap between the HAVES and the HAVE-NOTS is a ticking bomb.

3. The weak goverment is making it possible for the HAVES to  accelerate 2) above.

Concerning the "mafuriko" you heard in the news, If you believe those who  say that it was heavy rains that caused the flooding you can well start raising funds for I have a bridge I will like to sell to  you. The  operative phrase should be "Environmental Degradation Caused Flooding and Loss of Bridges " With the wetlands all dessimeted there is no where for the water to be held and percolated slowlly throughout the  catchment area  and thus have river floww throughout the year and thus no excuse for
 TANESCO to cry falling Dam levels.

Allow me to stop my rambling here. I am going to try to locate the missing LGF. Kama ukimwona mwambie namtafuta !!!!!!!!!!!!.

 Akwanza

 On Sabbatical at UDSM