Showing posts with label Urembo. Show all posts
Showing posts with label Urembo. Show all posts

Saturday, December 24, 2016

Unyanyasaji wa Kijinsia: Mchango wa UMIss Tanzania Unaonekana?

Na Elias Muhongo

Tukiwa tunaangalia tangazo la biashara la ‘BIG BOSS’ nikashtukia mwanangu mmoja akilalamika: “Hapo si tunajinyanyasa kweli?”. Nikamuuliza ana maana gani? Akasema “ Baba angalia sana tangazo hilo. Huyu mama anamfahamu boyfriend wake lazima, ndiyo maana alikuwa hakupotea nyumba. Lakini kukutana na harufu ya manukato anayotumia boyfriend wake akaamua kuondoka na aliyejipaka (manukato hayo)? Ni unyanyasaji wa kijinsia na hapo tunajinyanyasa wenyewe”. Mjadala ulikuwa mkali lakini nikomee hapo na kuendeleza mawazo yangu kuhusu unyanyasaji wa kijinsia, hasa unyanyasaji wa wanawake.
Nimeangalia mijadala mingi kipindi hiki na kuilinganisha na kipindi fulani kilichopita. Wakati wa maandalizi ya mkutano wa Beijing 1990, nilishiriki sana maandalizi hayo hapa nchini. Nakumbuka akina mama kufikia hatua ya kuainisha aina mbali mbali za unyanyasaji unaowakabili wanawake. Kupigwa na waume zao. Kusafiri mbali kutafuta maji. Huduma duni za afya wakati wa uzazi na uzazi wa mpango, nakadhalika. Lakini pia walijiambia ukweli mwingine wasiojiambia siku hizi. Walijiambia jinsi inavyokuwa vigumu kukutana na mwanamke aliye madarakani. Jinsi ilivyo vigumu mwanamke kumpigia kura mwanamke mwenzake licha ya wingi wao.
Tulijadili na jinsi katika michezo kama dansi akina mama wanavuliwa nguo na kujianika huku wenzao (wanaume) wanacheza wamejivalia nguo.

Wagombea Miss Tanzania 2009

Ninaamini kuwa huenda baadhi ya manyanyaso yamepungua. Lakini ukichunguza sana utakuta yale wanayojinyanyasa yanaendelea na hayapigiwi kelele kama yale wanayonyanyaswa.
Tuangalie na huu unyanyasaji wa kijinsia kupitia ‘Miss Tanzania’. Nakumbuka katika historia ya Miss Tanzania tangu viruhusiwe baada ya utawala wa Mwalimu Nyerere, naweza kudhibitisha kuwa ni mwaka mmoja ambao Tanzania iliwahi kuwakilishwa na mtanzania halisi licha ya kupingwa na watanzania wengi. Ni mwaka Tanzania ilipowakilishwa na Mtanzania mwenye asili ya India. Huyo alionyesha asili yake na utanzania wake. Lafudhi yake ilikuwa ya mtanzania mwenye asili ya India. Myondoko yake ilikuwa ya Mtanzania mwenye asili ya India. Rangi ya ngozi yake iliwakilisha Mtanzania mwenye asili ya India. Nywele za kichwa chake ziliwakilisha mtanzania mwenye asili ya India.

Nani anitajie mwingine? Anitajie Mis Tanzania ambaye aliiwakilisha Tanzania nje ya Tanzania na waangalizi wakaiona Tanzania? Sitarajii. Maandalizi ya Miss Tanzania yanamuandaa mwakilishi wetu kuuondoa utanzania ndani mwake. Maandalizi huanzia Willayani. Yanapokamilika ngazi ya Taifa mshindi na washiriki wote wanakuwa wamekamuliwa utanzania ndipo (mshindi) anakabidhiwa bendera ya Tanzania kwenda kuwakilisha kitu kisichojulikana. Huwezi kuuona utanzania katika lafudhi yake. Huwezi kuuona utanzania katika myondoko yake (gait). Huwezi kuuona utanzania katika asili ya ngozi yake wala nywele zake. 

Lakini kila mashindano hayo na maandalizi yake yanapokuwepo hukosi kuhisi unyanyasaji wa wazi na wa siri. Mavazi wanayovaa ni unyanyasaji wa ajabu usioendana na Utanzania. Lakini wasikie waandaaji wakijitetea kuwa hakuna eushwa ya ngono zinazoendelea katika shughuli hiyo. Nani haoni kuwa hayo hayawezi kukosekana? Huu wote ni unyanyasaji wa kijinsia unaoendelea kwa hiyari ya wanyanyaswaji na wanaharakati usioweza kupigiwa kelele kwa sababu tu wafadhiri wa miradi ya uanaharakati ndio wadhamini wa unyanyasaji huo.

Kuna wakati niliwahi kufikiri badala ya mashindano ya Miss Tanzania kwa nini kusianzishwe mashindano ysa mapishi ya kitanzania. Inahitaji kuandaa vigezo vya kuamua namna ya kuamua kati ya chakula cha kihaya na kipare. Mpare atapika kande na mhaya ndizi zilizochanganywa magarage mabichi na nyama iliyokauka watu watakula na kuuona utanzania. Ikishindikana basi shindanisha wapishi mbali mbali wa chakula aina moja. Mapishi yetu hayawezi kuchakachuliwa kama ambavyo utamaduni wetu unachakachuliwa kupitia mashindano haya ya Miss Tanzania.

Elisa Muhingo

Tuesday, July 23, 2013

Cheki Hiyo Shepu!


Mwanamke mweusi hasa ana hips!  Naomba maoni yenu.

Nedra Phillips

Thursday, December 20, 2012

Miss Tanzania Vazi la Taifa Katika Mashindano ya Miss Universe 2012


Wadau, hebu cheki hii Vazi la Taifa aliyovaa Miss Tanzania 2012, Winifrida Dominic, katika Mashindano ya Miss Universe. Samahani lakini sioni UTanzania! 
Miss Tanzania Winfrida Dominic performs onstage at the 2012 Miss Universe National Costume Show at PH Live in Las Vegas, Nevada December 14, 2012. The 89 Miss Universe Contestants will compete for the Diamond Nexus Crown on December 19, 2012. REUTERS/Darren Decker/Miss Universe Organization/Handout



Miss Bostwana 2012
Miss Ethiopia 2012


Wednesday, August 22, 2012

Miss East Africa Belgium 2012

Miss East Africa Belgium 2012


Mwakilishi wa Tanzania kwenye fainali Miss East Africa Belgium yatakayofanyika tarehe 1 September 2012, Miss Juliana Pierre


Muunge mkono mwakilishi wetu huyu kwenye Fainali husika kwa kuongeza idadi ya kufahamika kwake.

Juliana anaomba uingie kwenye ukurasa wake wa (Face book) na kubonyeza kitufe cha “like” kwa anuani hii: https://www.facebook.com/JulianaPierreFinalisteMissEastAfricaBelgium2012

Tangaza Vipaji Vyetu,Tangaza Utalii Wetu, Tangaza Tanzania.

Thursday, August 21, 2008

Ukweli kuhusu Mamodo (Models)



Nilishasema hao warembo tunawaona ni feki wamevaa masks usoni. Ona huyo mpaka walimrefusha shingo kwa photoshop! Nawaona kwenye seti za sinema, wanapambwa kwa masaa mawili kabla ya kutoka kwenye trailer!

Saturday, February 09, 2008

Marudio - Tupende Urembo Asili




Baada ya kuandika kuhusu matako makubwa, na kusoma feedback yenu, nimeona niongee kuhusu mashindano ya urembo. Asante kaka Ndesanjo kwa kunichokoza!

Hivi karibuni Miss Tanzania 2005, Bi Nancy Sumary alienda kwenye mashindano ya Miss World na kafanikiwa kutwaa taji la Miss Africa. Kwa kweli lazima nimpongeze maana toka mashindano ya Miss Tanzania ifufuliwe miaka ya 90, hakuna Mtanzania aliyefanikiwa kuingia katika raundi za fainali na hata kutwaa taji lolote.

Kwa kweli Tanzania imepata sifa kubwa katika dunia ya mashindano ya U-Miss. Pia Tanzania imepata sifa kuwa ina wanawake wazuri, lakini nauliza ni uzuri wa aina gani? Maana sioni kama ni uzuri unayafuata maadili ya kiafrika bali ni uzuri wa kizungu!Nikitazama picha na kanda za video za Miss Ilala, Miss Kinondoni, Miss Utalii, na mashindano mbalimbali za u-Miss huko Tanzania nashangaa nachoona. Kwa kweli naona wasichana weusi wakijaribu kuiga wazungu!

Wengine wanapaka make-ups usoni ambazo zimetengezwa kwa ajili ya wazungu wakati make-up za weusi zipo. Yaani ni vichekesho mpaka wengine wanaonekana vituko. Najua hapo niatambiwa nawaonea wivu lakini si kweli na naomba mnisikilize kabla ya kunipa hukumu.

Kwanza tutazame hao wanaopelekwa na nchi zao katika mashindano hayo. Ukiangalia walio kwenye Miss World na Miss Universe, washindi wote wana hulka (characteristics) za kizungu. Tutazame waafrika wanaoenda, cheki nywele zao, zinafanana na wazungu, yaani zimenyoka kabisa. Na kama tunavyojua, sisi wenye asili ya Afrika nywele zetu ni za kipilipili. Hawa wanaweka dawa au weave! Wanaficha nywele zao za asili, sijui wanazionea haya.

Je, wanaona haya kusuka nywele zao au kuonyesha mtindo wa nywele enye asili ya Afrika?Haya, tutazame shepu zao, wote ni wembamba, hakuna mnene, hata hips za maana hawana. Na kama ana matako ni kiasi, sio ile boxi, wowowo, yokohama inayopendwa Africa. Yaani wanafanya mazeoezi eti kusudi wapunguze matako yao.

Na hao weusi kutoka Marekani na Ulaya wanafanya liposuction na surgery kupunguza matako yao asili, eti iwe ya kizungu fleti. Huko Afrika tunasema mtu mwembamba ana shida, hana raha, mgonjwa, lakini mzungu anasema ni uzuri. Na sisi tunaiga! Basi unakuta akina dada hata Tanzania, “Oh nafanya diet!” Kheh! Kisa anataka kufanana na mtu amliyemwona kwenye gazeti.

Hawajui kuwa hizo picha zinafanyiwa editing na air brushing. Kwa hiyo dada zetu wanashinda njaa kusudi wawe wembamba! Hawajui kuwa hao wanaofanikiwa kwenda kwenye u-Miss, wanajitapisha, na kujinyima chakula kusudi wasinenepe, na ukweli hawana raha.

Haya tuangalie wanavyotembea na kuongea…wanaongea na kutembea kizungu! Jamani na hata macho hawasahau, maana wanatia contact lenses zenye rangi ya bluu na kijani kusudi wawe na macho ya kizungu! Doh! Matokeo ni kuwa hao siyo watu tena bali na madoli.

Na kuhusu rangi ya ngozi, ni lazima niulize, je, umewahi kuona mshindi mweusi tii? Hao weusi wanaofanikiwa wengi ni weupe. Basi hao dada zetu wanajichibua na madawa ya ajabu. Ubaya ni kuwa usoni wanaonekana weupe lakini miili yao bado rangi yao ya asili. Mwisho wanakuwa na rangi mbili. Halafu wengine baadaye wanajikuta wana kansa ya ngozi shauri ya dawa hizo za kujichibua.Ubaya ni kuwa kama nchi ya kiafrika inataka kushinda mashindano kama Miss World, Miss Universe ni lazima mtu wao awe Mdoli wa kizungu.

Mfano, miaka mingi Nigeria walikuwa wanapeleka mrembo wao ambaye alikuwa mrembo Nigeria lakini mbaya kwa wazungu. Mwaka 2001, waliamua kumpeleka Mdoli wa kizungu, yaani dada fulani, mwembamba, futi sita na kashinda. Na tazama kesi ya aliyeshinda Miss Universe 1996, Miss Venezuela, Bi Alicia Machado…baada ya kashinda, alinenepa kweli! Yaani aliongezeka kama kilo 20! Basi majaji wakasema watamvua taji lake kama hatapungua! Dada wa watu alilia na kusema kachoka kashinda njaa!

Na tuanganlie hatima ya hao wanaoabudu hiyo standard ya kizungu na kuwa wembamba. Wanapambana na magonjwa kama Osteoperosis, yaani ugonjwa wa mifupa kuvunjika kwa urahisi, utapialmlo, na magonjwa wa akili. Ndiyo, mtu ambaye kila saa anawaza kujikondesha na kuwa hatapendwa kama si mwembamba ana ugonjwa wa akili.

Je, madaktari huko Tanzania wako tayari kutibu hayo magonjwa wa kisasa?Mashindano ya U-Miss yataendelea kuwepo, na dada zetu wataendelea kutaka kushindana na kufanana na madoli wa kizungu. Bahati mbaya ndo dunia ya leo. Lakini napendekeza tuwe na mashindano ya Miss Bantu, Miss Tanzania asili pia. Mashindano hayo yawe na nia ya kusifia uzuri asili wa mwanamke wa kiafrika. Tusisahau tulikotoka. Na hao wazungu wakiona tunajipenda basi wao wataanza kuheshimu maadili zetu.

UPDATE - Flaviana Matata aliwakilisha Tanzania kwenye Mashindano ya Miss Universe 2007 na kufika kwenye Top 10. Bado wanamzunguzia.