Showing posts with label Beauty Pageant. Show all posts
Showing posts with label Beauty Pageant. Show all posts

Saturday, December 24, 2016

Unyanyasaji wa Kijinsia: Mchango wa UMIss Tanzania Unaonekana?

Na Elias Muhongo

Tukiwa tunaangalia tangazo la biashara la ‘BIG BOSS’ nikashtukia mwanangu mmoja akilalamika: “Hapo si tunajinyanyasa kweli?”. Nikamuuliza ana maana gani? Akasema “ Baba angalia sana tangazo hilo. Huyu mama anamfahamu boyfriend wake lazima, ndiyo maana alikuwa hakupotea nyumba. Lakini kukutana na harufu ya manukato anayotumia boyfriend wake akaamua kuondoka na aliyejipaka (manukato hayo)? Ni unyanyasaji wa kijinsia na hapo tunajinyanyasa wenyewe”. Mjadala ulikuwa mkali lakini nikomee hapo na kuendeleza mawazo yangu kuhusu unyanyasaji wa kijinsia, hasa unyanyasaji wa wanawake.
Nimeangalia mijadala mingi kipindi hiki na kuilinganisha na kipindi fulani kilichopita. Wakati wa maandalizi ya mkutano wa Beijing 1990, nilishiriki sana maandalizi hayo hapa nchini. Nakumbuka akina mama kufikia hatua ya kuainisha aina mbali mbali za unyanyasaji unaowakabili wanawake. Kupigwa na waume zao. Kusafiri mbali kutafuta maji. Huduma duni za afya wakati wa uzazi na uzazi wa mpango, nakadhalika. Lakini pia walijiambia ukweli mwingine wasiojiambia siku hizi. Walijiambia jinsi inavyokuwa vigumu kukutana na mwanamke aliye madarakani. Jinsi ilivyo vigumu mwanamke kumpigia kura mwanamke mwenzake licha ya wingi wao.
Tulijadili na jinsi katika michezo kama dansi akina mama wanavuliwa nguo na kujianika huku wenzao (wanaume) wanacheza wamejivalia nguo.

Wagombea Miss Tanzania 2009

Ninaamini kuwa huenda baadhi ya manyanyaso yamepungua. Lakini ukichunguza sana utakuta yale wanayojinyanyasa yanaendelea na hayapigiwi kelele kama yale wanayonyanyaswa.
Tuangalie na huu unyanyasaji wa kijinsia kupitia ‘Miss Tanzania’. Nakumbuka katika historia ya Miss Tanzania tangu viruhusiwe baada ya utawala wa Mwalimu Nyerere, naweza kudhibitisha kuwa ni mwaka mmoja ambao Tanzania iliwahi kuwakilishwa na mtanzania halisi licha ya kupingwa na watanzania wengi. Ni mwaka Tanzania ilipowakilishwa na Mtanzania mwenye asili ya India. Huyo alionyesha asili yake na utanzania wake. Lafudhi yake ilikuwa ya mtanzania mwenye asili ya India. Myondoko yake ilikuwa ya Mtanzania mwenye asili ya India. Rangi ya ngozi yake iliwakilisha Mtanzania mwenye asili ya India. Nywele za kichwa chake ziliwakilisha mtanzania mwenye asili ya India.

Nani anitajie mwingine? Anitajie Mis Tanzania ambaye aliiwakilisha Tanzania nje ya Tanzania na waangalizi wakaiona Tanzania? Sitarajii. Maandalizi ya Miss Tanzania yanamuandaa mwakilishi wetu kuuondoa utanzania ndani mwake. Maandalizi huanzia Willayani. Yanapokamilika ngazi ya Taifa mshindi na washiriki wote wanakuwa wamekamuliwa utanzania ndipo (mshindi) anakabidhiwa bendera ya Tanzania kwenda kuwakilisha kitu kisichojulikana. Huwezi kuuona utanzania katika lafudhi yake. Huwezi kuuona utanzania katika myondoko yake (gait). Huwezi kuuona utanzania katika asili ya ngozi yake wala nywele zake. 

Lakini kila mashindano hayo na maandalizi yake yanapokuwepo hukosi kuhisi unyanyasaji wa wazi na wa siri. Mavazi wanayovaa ni unyanyasaji wa ajabu usioendana na Utanzania. Lakini wasikie waandaaji wakijitetea kuwa hakuna eushwa ya ngono zinazoendelea katika shughuli hiyo. Nani haoni kuwa hayo hayawezi kukosekana? Huu wote ni unyanyasaji wa kijinsia unaoendelea kwa hiyari ya wanyanyaswaji na wanaharakati usioweza kupigiwa kelele kwa sababu tu wafadhiri wa miradi ya uanaharakati ndio wadhamini wa unyanyasaji huo.

Kuna wakati niliwahi kufikiri badala ya mashindano ya Miss Tanzania kwa nini kusianzishwe mashindano ysa mapishi ya kitanzania. Inahitaji kuandaa vigezo vya kuamua namna ya kuamua kati ya chakula cha kihaya na kipare. Mpare atapika kande na mhaya ndizi zilizochanganywa magarage mabichi na nyama iliyokauka watu watakula na kuuona utanzania. Ikishindikana basi shindanisha wapishi mbali mbali wa chakula aina moja. Mapishi yetu hayawezi kuchakachuliwa kama ambavyo utamaduni wetu unachakachuliwa kupitia mashindano haya ya Miss Tanzania.

Elisa Muhingo

Saturday, August 20, 2016

Mashindano ya Miss Mwanza 2016

Usiku wa jana Ijumaa Agost 19,2016 kuamkia leo Jumamosi Agost 20,2016, kulikuwa na mtifuano mkali wa kumtafuta mlimbwende wa taji la MISS MWANZA 2016 ambapo warembo 16 kutoka wilaya mbalimbali mkoani Mwanza walijitosa kusaka taji hilo.

Ilikuwa ni furaha kubwa kwa mrembo, Mary Peter (katikati), pale alipotangazwa kuwa MISS MWANZA 2016. Pia mwendelezo wa furaha uliwaendea warembo, Victoria Boniphace (kushoto) aliyetangazwa Miss Mwanza nambari mbili na Winnie Shayo (kulia), aliyetangazwa Miss Mwanza nambari tatu.

Kinyang'anyiro cha Miss Mwanza 2016, kiliandaliwa na Kampuni ya "Big D Entertainment" na baada ya kinyang'anyiro hicho, unafuata mtifuano wa MISS LAKE ZONE 2016 utakaofanyika Septemba 10,2016 ambapo washiriki wa Miss Mwanza 2016 waliongia nafasi tano bora, wanashiriki moja kwa moja kwenye shindano hilo.
Na BMG
Miss Mwanza 2015, Donny Roberty (kushoto), akimkabidhi taji Miss Mwanza 2016, Mary Peter (kulia) baada ya kuibuka mshindi wa shindano hilo.
Washiriki wa Miss Mwanza, walioingia nafasi tano bora
Warembo walioshiriki Miss Mwanza 2016
Warembo walioshiriki Miss Mwanza 2016.
Warembo walioshiriki Miss Mwanza 2016
Majaji walikuwa na Kazi pevu kuchagua mshindi
Baadhi ya waliohudhuria kwenye tukio
Msanii Elizayo HB kutoka Jijini Mwanza akidondosha burudani kwenye Miss Mwanza 2016
Burudani za kiafrika pia zilikuwepo
Mkali wa Moyo Mashine, Ben Pol, alidondosha burudani poa sana
Ben Pol kazini
Kupitia BMG, Ben Pol, aliwashukuru wakazi wa Jiji la Mwanza kwa namna wanavyopenda kazi zake na kuahidi kufanya kazi nzuri zaidi.
Miss Mwanza 2016 aliiambia BMG kwamba, maandalizi yake mazuri ndiyo yaliyompa fursa ya kunyakua taji hilo na kwamba amejiandaa vyema kwa ajili ya taji la Miss Lake Zone 2016 na pia Miss Tanzania 2016.
Miss Mwanza 2016 nambari mbili akibonga na BMG. Anasema shauku yake ni kuongeza juhudi zaidi ili kunyakua taji la Miss Lake Zone 2016.

Thursday, May 29, 2014

Miss Tanzania USA Pageant 2014




Attention Young Ladies. Are you interested in participating in the MISS TANZANIA USA Pageant? It will be held in Washington, D.C. later this year. You need to be between ages 16 -27 and have at least one parent from Tanzania. Contact me at chemiche3@yahoo.com for details on how to apply.

Saturday, March 01, 2014

Mrembo Miss Kentucky 2010 Asema Yeye Ni Shoga!!!

Miss Kentucky 2010 Djuan Trent

 Wadau, huko Kentucky moto unawaka baada ya Mrembo, Miss Kentucky 2010, Djuan Trent (26) kujitokeza na kusema yeye ni shoga.   Ameamua kujitokeza kwa vile Mkoa wa Kentucky karibu wataruhusu ndoa za mashoga!  Midume mlie tu....huyo mrembo anapenda wanawake na si nyie wenye dhakhari.

 Mikoa ya kusini ya Marekani wan Siasa kali dhidi ya wasenge na mashoga.

******************************************************

KWA HABARI KAMILI BOFYA HAPA:

On Thursday, there was huge news that a Kentucky judge ruled that same-sex marriages performed in other states and countries must now be recognized by the state. Some more news came out on Friday, Feb. 28, 2014, as former Miss Kentucky Djuana Trent publicly revealed in her blog that she is gay, per WKYT.

She started her blog post by wrestling with herself as to whether or not she should keep writing and reveal her news or still keep it inside. With that being said, she wondered how she should reveal her news - special date? Mysteriously? Seriously?
Djuan Trent simply decided to make her announcement with just three words:
"I am queer."
Djuan Trent went on to be crowed Miss Kentucky in 2010 and finished in the top 15 of the 2011 Miss America pageant. She had traveled all around Kentucky during her reign and was a spokesperson for the Kentucky Department of Agriculture's "Kentucky Proud" slogan and initiative.
Trent wrestled with how to make the announcement:
"I could write about what it was like to come out to my mom for the third and final time at the age of 26 (the first time was when I was in the 4th grade and the second time was in college). I could write about the years I spent praying to a God whom I wanted so badly to serve with all of my heart, but couldn't understand why this God made me "wrong". I could write about all the times that people have asked me if I have a boyfriend and I've purposely chosen to just say "no" with no further explanation."

Tuesday, July 23, 2013

Cheki Hiyo Shepu!


Mwanamke mweusi hasa ana hips!  Naomba maoni yenu.

Nedra Phillips

Thursday, December 20, 2012

Miss Tanzania Vazi la Taifa Katika Mashindano ya Miss Universe 2012


Wadau, hebu cheki hii Vazi la Taifa aliyovaa Miss Tanzania 2012, Winifrida Dominic, katika Mashindano ya Miss Universe. Samahani lakini sioni UTanzania! 
Miss Tanzania Winfrida Dominic performs onstage at the 2012 Miss Universe National Costume Show at PH Live in Las Vegas, Nevada December 14, 2012. The 89 Miss Universe Contestants will compete for the Diamond Nexus Crown on December 19, 2012. REUTERS/Darren Decker/Miss Universe Organization/Handout



Miss Bostwana 2012
Miss Ethiopia 2012


Wednesday, August 22, 2012

Miss East Africa Belgium 2012

Miss East Africa Belgium 2012


Mwakilishi wa Tanzania kwenye fainali Miss East Africa Belgium yatakayofanyika tarehe 1 September 2012, Miss Juliana Pierre


Muunge mkono mwakilishi wetu huyu kwenye Fainali husika kwa kuongeza idadi ya kufahamika kwake.

Juliana anaomba uingie kwenye ukurasa wake wa (Face book) na kubonyeza kitufe cha “like” kwa anuani hii: https://www.facebook.com/JulianaPierreFinalisteMissEastAfricaBelgium2012

Tangaza Vipaji Vyetu,Tangaza Utalii Wetu, Tangaza Tanzania.