Showing posts with label Vita Kuu ya Dunia. Show all posts
Showing posts with label Vita Kuu ya Dunia. Show all posts

Saturday, June 11, 2016

Tukumbuke Askari Wetu Waliopigana kwa Niaba ya Mkoloni



Askari Monument in Dar es Salaam, Tanzania
 Leo nimekumbuka ule wimbo tuliokuwa tunaimba jeshini, JKT, inaenda hivi..... Askari Eh, Vitani yee mama......   

Wadau, mnajua ile sanamu pale City Center Dar. Inaitwa Askari Monument.  Ni kumbukumbu ya Askari waafrika waliopigana katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.  Waafrika walichukuliwa na Mkoloni kuwa Askari katika Majeshi yao, Walifanya kazi ngumu ya kupigana huko wazungu walikaa kwenye viti vyao wanapunga hewa!  Kwa maana hiyo Akari wa nchi fulani, walikuwa wanaua Askari wa nchi nyingine, Kama mchezo vile!  (Gameborad) Askari wengine walipelekwa Ulaya na hawakurudi kwa familia zao, wala familia zao hawajui waliishia wapi!

Nimekusanya picha ya Askari waliopigana katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, wakati huo Tanzania, inaiitwa Deustche Oost Afrika (German East Africa).

Na Mjerumani alikuwa ni msehenzi mkatiki kwa Waafrika..  Waafrika huko vijijini waliuawa wengi sana na Mjerumani eti wazaa au wagonjwa.

Kwa habari zaidi za Vita Kuu ya Kwanza na Dunia na Tanzania (German East Africa) BOFYA HAPA:

Askari Akiaaga Familia Yake kabla ya kwenda Vitani

Askari kwenye Gwaride Dar es Salaam

Askari kwenye Mafunzo 1918










Askari Monument Mwaka 1945

Tuesday, March 01, 2011

Askari Wa Vita Vya Kwanza ya Dunia - German East Africa

Hii ni meli ya kivita Mjerumani SMS Konisberg ikiwa imita nanga bandarini Bagamoyo. Bagamoyo ilikuwa mji mkuu wa Tanganyika enzi za MJerumani
Askari kwenye foleni
Waliopitia JKT wataelewa hii...ROUTE MARCH!

Sijui ni Tanga au Bagamoyo hapo au Itakuwa kwenye Ziwa Victoria au Nyasa

Hao watakuwa wale Asakri wa kwanza kabisa. Hawana viatu!

Askari wakisfisha bunduki zao

Enzi za MJerumani walikuwa wanatumia Rupia siyo Shilingi


Bahati mbaya hatuna majina ya hao Askari pichani



The Force Publique in German East Africa during World War One

Monday, September 28, 2009

Askari Wakisoma Gazeti la Kiongozi 1916

Kumbe gazeti la 'Kiongozi' ilikuwepo tangu enzi za Mjerumani! Hao askari wa enzi za Mjerumani wanaburudika kwa kusoma gazeti la Kiongozi iliyoandikwa kwa lugha ya Kiswahili. Hii Picha ilipigwa wakati wa Vita Kuu ya Dunia ya Kwanza (World War I) na Walther Dobbertin.


Askari eh, Vitani eeh Mamaaa!