Showing posts with label Dar es Salaam. Show all posts
Showing posts with label Dar es Salaam. Show all posts

Saturday, April 17, 2021

Buriani Prince Philip (1921-2021) - Mume wa Malkia wa Uingereza

 Leo  mume wa Malkia wa Uingereza, Prince Philip, amezikwa katika kanisa la Mt.George huko Windsor Castle, Uingereza.  Prince Philip alifaikri tarehe 9 Aprili akiwa na miaka 99.  Alikuwa mume wa Malkia Elizabteh kwa miaka 73. 

Niliwahi kuongea na Prince Philip. Mwaka 1979, nikiwa mwanafunzi wa  shule ya sekondari Zanaki,  tulikuwa Ikulu, kuwapokea.  Enzi zile, kama anakuja kiongozi wa nchi ya nje, wanafunzi walikuwa wanatumiwa kupanga  njia kumlaki   

Basi, malkia na familia yake walishuka kwenye gari, na walitembea kwa miguu kwenye  kapeti nyekundu kuingia Ikulu.  Prince Philip alisimama, na kutangalia sisi wanafunzi.  Akauliza,  nyie ni wanafunzi wa shule gani, kwa Kiingereza,  Wanafunzi waliokuwa karibu na mimi walikimibia.  Nikamjibu,  " We are students from Zanaki Girls Secondary School.  (sisi ni wanafunzi kutoka shule ya sokndari Zanaki".  Akauliza  shule ilikuwa inaitwa nini zamani, nikamwambia, Aga Khan Girls.  Alisema  asante, na kuendelea kuingia Ikulu.  Doh!  Niliongea na Royalty!  nilirudi yumbani kwa furaha na kuwasimulia wazazi wangu na marafaiki jinis nilivyoongea na Prince Philip.

Kwenye ziara ile ya mwaka 1979, Malikia alisali na sisi, katika Kanisa la Mt. Albano, Dar es Salaam.  

Mungu ailaze roho ya marehemu Prince Philip.  

Kuona video fupi ya ziara ya Malkia Elizabeth II na familia yake East Africa mwaka 1979  BOFYA HAPA:

 Wanafunzi na wakazi wa Dar es Salaam, wakiwashangalia Malkia Elizabeth na familia yake wakielekea Ikulu alipotembelea Tanzania mwaka 1979,


Malkia Elizabeth II na hayati Prince Philip wakiwapungia waTanzania baada ya ziara yao mwaka 1979.


Maisha ya Prince Philip

Saturday, March 18, 2017

Mbinu Hizi zitakusaidi Kukabiliana na Mvua Jijini Dar es Salaam

Na Jumia Travel Tanzania

Hivi kuna mkazi yeyote wa jiji la Dar es Salaam ambaye ni mgeni wa adha zitokanazo na mvua zinazonyesha? Sidhani kama kuna mtu yeyote hafahamu ya kwamba mvua ikinyesha kutakuwa na foleni zisizokwisha, barabara na mitaa tofauti jijini kujaa maji, mafuriko na matamko kadha wa kadha kutoka kwa viongozi wa serikali kuwataka wananchi wahame mabondeni.

Lakini ni wangapi wametafakari watawezaje kukabiliana na mvua zitakaponyesha? Zipo mbinu nyingi tu ambazo Jumia Travel inakushauri uzizingatie ili kipindi cha mvua nyingi za Dar es Salaam kwako kiwe ni cha kawaida katika mwaka. 


Amka mapema kukabiliana na foleni ili uwahi shughuli zako
Hakuna wakati ambao kunakuwa na foleni kubwa na zisizopungua kwa muda mrefu jijini Dar es Salaam kama kipindi cha mvua! Lakini jambo hili sio la kushangaza kwa sababu kila mwaka hali hii inajirudia. 

Na hiki ni kipindi ambacho mabosi wengi huchukia sana pengine kuliko vipindi vyote vya mwaka maana visingizio vya wafanyakazi wao kuchekelewa kazini kwa sababu ya mvua huwa haviishi. Kwa hiyo unakabiliana vipi na hali hiyo? 

Kwanza kabisa lazima uwe makini katika kuwahi kuamka mapema na pia njia ya usafiri utakayoitumia. Inakubidi kuwahi kuamka mapema sana kama unategemea usafiri wa umma au binafsi. Kwa sababu ukifanya hivyo kama kutakuwa na foleni barabarani basi utaziwahi ukilinganisha na ukichelewa kuingia barabarani. Lakini pia kama unategemea usafiri wa umma, mabasi ya mwendokasi ni mkombozi mkubwa kwenye kipindi hiki. Hivyo kwa maeneo ambayo usafiri huu unapatikana ni vema kuutumia ipasavyo kwa sababu yenyewe hayakai foleni kutokana na kuwa na njia zao pamoja na kupewa kipaumbele.    

Nunua vifaa vya kujikinga na mvua
Kutokana na jiji la Dar es Salaam kuwa na vipindi virefu vya jua na joto kali, imekuwa ni nadra sana kuwakuta wakazi wake wana vifaa vya kujikinga na mvua kama vile mwamvuli, koti, sweta au viatu vya mvua. Inashauriwa kuwa na vifaa hivi nyumbani kwako ili kujikinga ifikapo kipindi cha mvua na sio kuanza kufikiria kununua kwani inawezekana usiwe na bajeti hiyo pindi unapovihitaji. Vifaa hivyo ni muhimu kwani hukukinga na baridi, kutolawana, magonjwa na hata kutunza mavazi yako kutokana na maji ambayo huweza kusababisha kuharibika.
Umakini kwenye chombo chako cha usafiri 
Kwa wenye vyombo vya usafiri wanajua wenyewe ni kadhia gani wanayokumbana nayo ikifika kipindi cha mvua. Kipindi hiki ni jambo la kawaida kukuta magari kadhaa yamezimika au kukwama barabarani kutokana na sababu mbalimbali za kiufundi. Lakini pia barabara nyingi huharibika na kutopitika kabisa hivyo kulazimisha chombo chako kupita ni kujitafutia kuingia gharama zisizohitajika siku za usoni. Kama inawezekana tafuta njia mbadala ya usafiri katika kipindi hiki au pita kwenye njia ambazo una uhakika ni salama kwa chombo chako.

Kuwa makini na vifaa vyako vya umeme
Siyo vifaa vyote vya umeme vimetengenezwa vikiwa na uwezo wa kuzuia maji kutokuingia ndani yake. Licha ya makapuni mbalimbali kuja na teknolojia hiyo lakini unashauriwa kuwa makini sana aidha kwa kuvivika vifaa maalumu vya kuzuia maji au kuvikinga kabisa na maji. Kipindi hiki ndicho ambacho wengi hupatwa na majanga ya kuharibikiwa na simu, kompyuta, radio pamoja na luninga huko majumbani.

Kuwa makini na vyakula utakavyokula
Kama huwa unakuwa makini na aina ya vyakula unavyokula basi kipindi hiki inabidi uwe makini zaidi. Mvua zikinyesha jijini Dar es Salaam ndiyo kipindi ambacho pia kunakuwa na mlipuko wa magonjwa kadha wa kadha kama vile kipindupindu. Inashauriwa kula chakula sehemu ambayo unaiamini na inayozingatia usafi wa hali ya juu au kama inashindikana uwe unabeba chakula unachopika mwenyewe au kutokula kabisa.  

Tumia muda wako kusoma vitabu
Sio watu wote wana utaratibu wa kusoma vitabu kwenye siku zao za kawaida badala yake wanatazama filamu, kusikiliza muziki, kutoka wikendi au kupendelea kutembea. Lakini katika kipindi hiki ambacho mvua zinanyesha, barabara hazipitiki, hali ya hewa ni baridi na sehemu nyingi za starehe au kutembelea zinakosa watu ni vema ukajaribu kusoma vitabu. Amini usiamini kuwa hata kutazama filamu na kusikiliza muziki hufikia mahala vinachosha, hiki kinaweza kikawa ni kipindi kizuri cha kujaribu kitu tofauti, nunua vitabu na usome ili uongeze maarifa. 

Hivyo basi tusiifanye mvua ikawa ni kisingizio cha kutofanya shughuli zingine au majukumu mengine yanayotukabili. Kila kipindi huja na changamoto pamoja na fursa zake, ni vema kupambana nazo na kuzitumia ili kusonga mbele.

Saturday, December 17, 2016

Kongamano la Kumuenzi Fidel Castro


Nilibahatika kuhudhuria japo kwa muda mfupi Kongamano ya Kumuenzi Marahemu Rais Fidel Castor wa Cuba, iliyofanyika mjini Dar es Salaam, Tanzania, jumapili iliyopita December 11, 2016 kwenye hall ya Taasisi ya Watu Wazima. (Symposium to Honor the Legacy of Fidel Castro).  Waliongolea jinsi Castor alivyotoka kwenye familia ya matajiri lakini alipenda kusaidia na kunyanua maskini.  Pia jinsi Cuba ilivyosaidia Tanzania.


Jenerali Ulimwengu Akiongea
Audience Participants
The Symposium Leaders

Friday, October 21, 2016

Wananchi Waliobomolewa Nyumba Jijini Dar, Leo Kuitua Kwa Mkuu wa wilawa Kupeleka Kilio Chao

 Mkazi wa eneo hilo, Lukia Khalid (aliye kaa), akiwa amekaa nje na vyombo vyake baada ya kubolewa nyumba yake.
 Wananchi wa Tegeta A Kata ya Goba wakiwa wamesimama chini ya mti Dar es Salaam jana, baada ya nyumba zao kubomolewa na Kampuni ya Udalali ya Yono kwa madai ya kuvamia eneo hilo. Hata hivyo wamekanusha kuvamia eneo hilo. Zaidi ya nyumba 150 zilibomolewa. Wananchi hao leo wanaandamana kwenda kwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kupeleka malalamiko yao.
 Askari polisi wakiwa eneo hilo kuimarisha ulinzi.
 Watoto wakiangalia nyumba yao baada ya kubomolewa.
 Mkazi wa eneo hilo akiwa kando ya nyumba yake iliyobomolewa.
 Mkazi wa eneo hilo akiangalia nyumba yake baada ya kubomolewa.
Magodoro yakiwa yamefunikwa na paa la nyumba baada ya kubomolewa kwa nyumba hizo.

Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya Udali ya Yono Aution Mart imebomoa nyumba zaidi ya 150 za wakazi wa Tegeta A Kata ya Goba jijini Dar es Salaam kwa madai ya kujengwa eneo ambalo sio lao huku Kaya zaidi ya 450 zikikosa makazi ya kuishi.

Hata hivyo ubomojai huo umepingwa na wananchi hao wakidai eneo hilo ni lao na wapo kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Zoezi la ubomoaji wa nyumba hizo lililofanyika Dar es Salaam jana, ulisimamiwa na askari polisi waliokuwa na silaha za moto na mabomu ya machozi huku wakiwa katika magari yenye namba PT, 3475, 1986 na  3675 huko kukiwa na askari hao zaidi ya 15.

Mmoja wa wananchi hao, Macarios Turuka  akizungumza na Jambo Leo eneo la tukio alisema eneo hilo kwa kipindi kirefu lilikuwa halitumiki na lilikuwa ni vichaka vya wahalifu kwani wanawake walikuwa wakibakwa na kutumiwa na watu kwa uhalifu ndipo walipoingia na kujenga.

Aliongeza kuwa baada ya kuanza ujenzi ndipo alipo ibuka Benjamini Mutabagwa na kueleza kuwa ni lake ndipo walipofungua kesi mahakama ya Kimara ambapo alishindwa kupeleka vielelezo vya umiliki wa eneo hilo.

Mwanasheria anayewatetea wananchi hao, Moses Chunga alisema kitengo cha kubomoa nyumba hizo ni kukiuka sheria za mahakama kwani kuna kesi ya msingi namba 188/ 2016 waliyofungua mahakama kuu ya ardhi ambapo walitakiwa tarehe 31 mwezi huu kwenda kuisikiliza lakini wanashangaa kuona nyumba hizo zikibomolewa.

Alisema wananchi hao wanajipanga kudai fidia ya uhalibifu huo na kuwa kabla ya yote wanahitaji kumuona rais kuona wanapata haki yao.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart, Yono Kevela alisema kampuni ya ke imevunja nyumba hizo kwa amri ya mahakama na polisi walikuwepo kusimamia zoezi hilo.

"Mwenye eneo hilo ambaye ni Kanisa la Winers alishinda kesi mwaka mmoja uliopita na leo jana ulikuwa ni utekelezaji wa kuwaondoa wavamizi hao" alisema Kevela.

Mkazi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Hamisi alisema kitendo walichofanyiwa si cha uungwana hata kidogo kwani wao wapo katika eneo kwa siku nyingi mpaka wamefikia hatua ya kujenga nyumba hizo hizo mmiliki huyo alikuwa wapi kwa siku zote hizo.

"Kwa kweli hawa watu wanatufanya tusiipende serikali yetu tunaomuomba rais atusaidie katika jambo hili" alisema Hamisi.

Hamisi alisema kesho leo wanatarajia kwenda kwa mkuu wa wilaya ya Ubungo kupeleka kilio chao na kama akishindwa watakwenda kwa mkuu wa mkoa na kama napo hawatapata ufumbuzi watakwenda kumuona waziri Lukuvi na Rais.

Hawa Musa alisema baada ya kuvunjiwa nyumba zao wapo katika wakati mgumu na hawajui wataisheje na watoto wao.

Alisema wamepanga vitu vyao nje na mvua yote iliyonyesha jana imelowanisha vyombo vyao yakiwemo magodoro na hawajui huyo mtu anayedai ni eneo lake nyuma yake yupo nani.

Alisema nyumba yake iliyobomolewa ilikuwa inathamani ya sh. 700,000.

"Tangua tufungue kesi mahakama ya Kimara hakuwahi kufika kama yupo kweli kwanini anashindwa kuhudhuria mahakamani " alihoji Musa.

Musa aliongeza kuwa kabla ya kubomoa nyumba hizo walipaswa kutoa notsi lakini wao hawajafanya hivyo wamefika saa mbili asubuhi na kuanza kubomoa bila hata ya kuwa shirikisha vipongozi wa eneo hilo.

Mkazi mwingine wa eneo hilo Juma Abdallah amelalamikia jeshi la polisi kwa kuchukua TV, king'amuzi na sh. 80,000 zilizokuwepo ndani kabla ya nyumba yake kubomolewa.

"TV yangu na king'amuzi na sh.80,000 zimechukuliwa wakati wa zoezi hilo" alisema Abdallah.

 Katika hatua nyingine wananchi hao wamemtupia lawama Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Tegeta A  kuwa amekuwa akiwakumbatia watu wanaodai kuwa eneo hilo ni lao wakati anaelewa fika ukweli halisi wa eneo hilo.

Mwenyekiti huyo Marko Vaginga alipopigiwa simu ili kuzungumzia suala hilo hakuwa tayari kuzungumza chochote zaidi ya kumtaka mwandishi kwenda ofisini kwake kwa mazungumzo zaidi.

"Nakuomba uje ofisini tuzungumze kwa leo sipo tayari kuzungumza chochote" alisema Vaginga na kukata simu.

Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni alipopigiwa simu alisema polisi walikuwa eneo hilo kwa ajili ya kusimamia amri ya mahakama.


Saturday, June 11, 2016

Tukumbuke Askari Wetu Waliopigana kwa Niaba ya Mkoloni



Askari Monument in Dar es Salaam, Tanzania
 Leo nimekumbuka ule wimbo tuliokuwa tunaimba jeshini, JKT, inaenda hivi..... Askari Eh, Vitani yee mama......   

Wadau, mnajua ile sanamu pale City Center Dar. Inaitwa Askari Monument.  Ni kumbukumbu ya Askari waafrika waliopigana katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.  Waafrika walichukuliwa na Mkoloni kuwa Askari katika Majeshi yao, Walifanya kazi ngumu ya kupigana huko wazungu walikaa kwenye viti vyao wanapunga hewa!  Kwa maana hiyo Akari wa nchi fulani, walikuwa wanaua Askari wa nchi nyingine, Kama mchezo vile!  (Gameborad) Askari wengine walipelekwa Ulaya na hawakurudi kwa familia zao, wala familia zao hawajui waliishia wapi!

Nimekusanya picha ya Askari waliopigana katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, wakati huo Tanzania, inaiitwa Deustche Oost Afrika (German East Africa).

Na Mjerumani alikuwa ni msehenzi mkatiki kwa Waafrika..  Waafrika huko vijijini waliuawa wengi sana na Mjerumani eti wazaa au wagonjwa.

Kwa habari zaidi za Vita Kuu ya Kwanza na Dunia na Tanzania (German East Africa) BOFYA HAPA:

Askari Akiaaga Familia Yake kabla ya kwenda Vitani

Askari kwenye Gwaride Dar es Salaam

Askari kwenye Mafunzo 1918










Askari Monument Mwaka 1945

Monday, May 30, 2016

Miss Tanzania USA Atembelea Shule ya Kenton Dar

Miss Tanzania USA 2015-2016 Aeesha Kamara akiongea na wanafunzi wa Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam siku alipotembelea shuleni hapo katika moja ya majukumu yake ya kuhudumia jumuiya. Miss Kamara anadhamini wanafunzi wawili shuleni hapo
Miss Tanzania USA Pageant Aeesha Kamara akimkabidhi msaada mwalimu mipira siku alipotembela shule ya Kenton High School ya Tabata jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania USA Aesha Kamara akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wawili anaowadhamini kwa kuwasomesha shuleni hapo.
Picha ya pamoja

Saturday, August 22, 2015

Prof. Henry Kadete Thirty Year Wedding Anniversary!




It was 30 years ago tomorrow 8/24/85, that I said "I Do" to Prof. Henry Kadete, (pronounced KAH-DEH-TEH) in Dar es Salaam, Tanzania at St. Alban's Anglican Church. It was the wedding of the year in Dar. Both my grandfathers were in attendance (my grandmothers had both passed). My grandpa flew from USA to attend and always talked about it until his death. Sadly Prof. Kadete, was taken from us ten years later in 1995 leaving me with two beautiful children. May he continue to rest in eternal peace. Amen. Tanzania and the African continent lost a genius of Electrical Engineering. For those who don't know, Prof. Kadete did the groundwork for bringing LUKU (prepaid) Electricity to Tanzania. At the time of his death, he was the Head of the Electrical Engineering Department at the University of Dar es Salaam. Only God, knows why some die so young. Prof. Kadete may be gone, but he is not forgotten.

Saturday, July 25, 2015

Sherehe za Arobaini ya marehemu Baba Yangu Dr. Aleck Che-Mponda Yafanyika Dar Leo!

Wadau, leo sherehe za Arobaini ya marehemu baba yangu mzazi, Dr. Aleck. H. Che-Mponda, zilifanyika mjini Dar es Salaam, pale nyumbani Tenki Bovu, Mbezi Beach Juu. Nafurahi mwanangu, Camara aliweza kuhdhuria pamoja na mdogo wangu Jessica.

REST IN ETERNAL PEACE DR. ALECK H. CHE-MPONDA (1935-2015)

Mapadre wa Anglikana waliosimamia Misa
Wapwa wa Marehemu
Father Haule wa Kanisa Anglikana Kawe akiongea

Ndugu wa Marehemu



Ndugu wa Marehemi


Saturday, May 09, 2015

Mafuririko Dar es Salaam!

Jamani, jamani!  Watu wameambiwa wasijenge Jangwani! Lakini wapi, wanajenga.  Haya sasa ona matokeo! Picha Kutoka Facebook.



Fenecha ya mtu


Sebuleni hapo



Aerial View of Jangwani Dar es Salaam
Mliozoea kwenda shopping hapo, mlie tu!



Hapo Sinza