Showing posts with label Wezi. Show all posts
Showing posts with label Wezi. Show all posts

Wednesday, May 29, 2013

Mwanamke Auawa na Majambazi Dar

Hii ilitokea Mei 5, 2013 Mjini Dar es Salaam
 
 
 
 
Majambazi yamempora mama mmoja kiasi cha shilingi milioni kumi na kutokomea kusikojulikana....

Tukio hilo limetokea leo saa 5:16 jioni na inavyosemekana ni kuwa mwanamke huyo alikuwa akitoka benki ya CRDB tawi la Uhuru ambapo majambazi yakiwa na pikipiki yalikuwa yakimfuatilia..

Alipotoka ,majambazi hayo yalimfuata na kuligonga gari lake makusudi na ndipo dada huyo aliposimama ili angaalie nani kagonga gari yake ambapo jambazi mmoja alishuka na kumpiga risasi ya kifuani na kutokomea na kiasi hicho cha pesa. ..

Monday, January 03, 2011

Mashine Inayokamata Wezi




A Machine That Catches
Thieves ......

In the U.S. they invented a machine that catches thieves; they took it out to different countries for a test.

In the U.S.A, in 30 minutes, it caught 20 thieves;

UK, in 30 minutes it caught 500 thieves;

Spain, in 20 minutes it caught 25 thieves;

Ghana, in 10 minutes it caught 6,000 thieves;

Nigeria in 5 minutes it caught 9,000 thieves

Tanzania, hata dakika tatu hazikupita wajanja waliishaidaka!

Sunday, September 12, 2010

Vibaka Ubungo Dar es Salaam

Kuna Mdau H. S. ameleta taarifa hii:

Leo nimeibiwa pale ubungo mataa, gari langu limengolewa side mirror katika hali ya ajabu na wepesi hata nilipojaribu kujihami lau kwa kumpiga kibaka mmoja na Lungu niliyokuwa nayo bado sikumpata uzuri ameenda na side Mirror zangu!!!

Imeniuma sana lakini napanga kufanya operation kwenye hilo eneo lau nipate kibaka mmoja wa kutolea mfano...hili ni eneo ambalo kwa makusudi linageuka taratibu kuwa jehenamu kwa kila kitu ulichonacho, anzia sim,begi, saa, laptop, pochi na hata heleni za akina mama.

AJABU unapoibiwakama hivo walikua wa 4 na magari yalikua yapo sikupata msaada hata kwa mtu mmoja nilihangaika peke yangu huku watanzania wenzangu wanaangalia hilo LIMENISHANGAZA SANA,,,

Nchi hii sasa ina poteza usalama kiasi kile na kwa kweli watu wa mji huu wa Dar sijui ni uoga ama vipi!!! naamininingekua sehem nyingine kama mbeya wale vibaka wangekiona leo....natoa wito kwa wote kuweni makini na Ubungo mataa,keko,Fire,jangwani,buguruni haya maeneo yanatakiwa kusafishwa!