Jamani, sasa hii kuita watu Celebrity sijui Supastaa huko Bongo Unawafanya wengine wawe na AKILI FINYU!
******************************************
KUTOKA FACEBOOK -
 |
| Ommy Dimpoz |
MAJANGA!!!!! --HUYU NDIYE OMMY DIMPOZ, MSANII WA BONGO ALIYEAMUA KUMTUKANA MAREHEMU MANGWEA!.
MATUSI : Sitaki kufa Masikini kama Mangwea!
NGWAIR,AMEKUFA AFRIKA KUSINI,HATA KUUSAFIRISHA MWILI KUULETA TANZANIA
IMEBIDI MPAKA WATU WACHANGIE,ILE NI AIBU SANA",alisema Ommy kwa dharau.
...
Vile vile Ommy baada ya kushinda tuzo ya video bora ya mwaka Ommy
alibwabwaja:"jamani tumechoka kuzika wasanii maskini wenye majina
makubwa",kama vile haitoshi Ommy alizidi kusisitiza kuwa HATAKI KUFA
MASKINI KAMA NGWAIR,
Nikitazama sura yako ya upole,vidimpozi vyako hivyo yaani hata huelekeani na shombo hili ulilojipaka,
Kwa kweli nimesikitika sana hasa msanii kama wewe Ommy Dimpoz umekuja
juzi tu umeshaanza kujikweza na dharau kiasi hiki?, ukweli nyimbo zako
binafsi nazipenda na una kipaji ila utumbo huu uliotoa utaumeza maana
Mungu hajaribiwi, hakuna mwenye mamlaka juu ya kifo,ni Msiba gani
hukuona mchango?,
je Umasikini wa Ngwair ni lini uliupima? uliwahi kusikia familia yake imelala njaa?, alishawahi kukupiga mizinga?,
Ninachojua mimi Marehemu(Dead Body) kamwe hapewi tuhuma kwa sababu
hayupo around kuji-defend,once ukiamua kushusha tuhuma dhidi ya dead
body jiandae kujibiwa na Mungu aliyemchukua.
Kama unahitaji
kuhamasiha utajiri kwa wasanii ni vema ukaandaa mikutano na Warsha na
walio hai,sasa wewe unamuita Marehemu Fukara????? this is Shit!!!, Babu
zako,wajomba zako,na woooooote wamekufa matajiri???, Once U talk
again,talk in decent way.
### Aisee hiki ni kituko,sijui fans wangu mnaonaje hili!!!
