Showing posts with label Fatma Alloo. Show all posts
Showing posts with label Fatma Alloo. Show all posts

Monday, October 03, 2011

Sinema 'Historia ya Khanga" Cheki Mimi na Kaka Michuzi!

MaStaa wa Bongowood 1991 Michuzi & Chemi


Kabla ya Kanumba na Ray kulikuwa na Chemi na Michuzi!

Wadau, kwenye mwaka 1992 nilishiriki katika sinema ya TAMWA, "The History of Khanga".  Hebu itizame, Utaniona mimi na Kaka Michuzi, "Tunajiandaa kulala"

Mwongozaji alikuwa Dada Fatma Alloo. Pia kuna mahojiano na marehemu Bibi Titi Mohamed.

Sinema sasa iko YOU TUBE kwa hisana ya Dada Fatma na Kaka Michuzi:

http://www.youtube.com/watch?v=jAuhAB0HeeA&feature=player_embedded

Wednesday, June 22, 2011

Society for International Development - Tanzania Chapter Election Results
















Society for International Development, Tanzania Chapter Elects New Office Bearers

The Society for International Development (SID) Tanzania Chapter on Saturday 18th June 2011 elected new office bearers for its chapter.

Mahmoud Thabit Kombo (pichani) has been appointed chapter’s President while Richard Kasesela will serve as Vice-President. June Warioba becomes the chapter’s Secretary General, Muhidin Issa Michuzi, Programs Officer and Yasmin Said Chali is Treasurer.

The following were elected members of the Executive Council: Ally Masoud (Kipanya), John Ulanga, Fatma Alloo, Salma Moulid and Chambi Chachage.

SID Tanzania is one of chapters of SID International and acts as an independent platform organisation, bringing together policy makers, academics, NGOs, the private sector, journalists and others to drive forward the development debate in Tanzania, and subsequently influencing the policy discussion.

Ambassador Juma Mwapachu, Vice President of SID’s Global Governing Council, said: "We are thrilled to have such thoughtful and knowledgeable members to lead SID Tanzania during this challenging period."

“We need to provide a forum for individuals and institutions that are seeking long-term solutions to issues such as good governance, food security and agriculture and gender in development to name a few” he added.

On his appointment, the in-coming President thanked members for the honor to serve SID Tanzania. “More than ever, we need the kind of forum that SID provides for enhanced collaboration, informed debate, and a steady focus on learning and innovation. I look forward to working in these areas with other members.”

“My colleagues and I are committed to broadening the dialogue on crucial development issues and promoting effective economic growth for our people” said Kombo.

Mr. Kombo succeeds His Lordship Chief Justice, Mohammed Chande Othman.

Founded in 1957, SID is an international association of individuals and organizations concerned with sustainable economic, social and political development. SID has over 3,000 individual and institutional members in 125 countries and over 65 local chapters worldwide, including in Tanzania.

For more information on SID Tanzania, contact:
June Warioba,
Tel: 0782/0655 004436
Email: sidtanzania@gmail.com
sidtanzania@yahoo.com

Thursday, July 08, 2010

Sauti ya Siti - Gazeti la TAMWA

Mwezi Machi, 1988 TAMWA ilizindua gazeti 'Sauti ya Siti'. Mimi ni mmoja wa waanzilishi wa TAMWA. Nakumbuka siku tulipotaarifiwa kuwa serikali imekubali kusajiliwa kwa TAMWA, na siku tuliporuhusiwa kuchapisha Sauti ya Siti. Ilikuwa jambo kubwa mno maana wanaume walitupinga kweli hata baadhi ya wanawake. Walisema TAMWA ni chama cha mashoga. Cha ajabu hao hao waliokuwa wanatusema walikuja kujiunga na TAMWA baada ya kuona mafanikio yetu.

Gazeti ya Sauti ya Siti ilikuwa na nia ya kuelezea habari za akina mama ambazo zilikuwa haziingii katika magazeti ya kawaida. Kumbuka wakati ule magazeti yalikuwa machache, Daily News, Uhuru, Mfanyakazi, Kiongozi. Redio ilikuwa Radio Tanzania tu!

Mzee Ali Hassan Mwinyi (Mzee Ruksa) ndiye alikuwa Rais. Mke wake alikuwa anaitwa Siti. Basi watu walisema eti sisi wanaTAMWA tuliamua kuita gazeti Sauti ya Siti ili kumpendeza Rais. Jamani!

Watu walikuwa wamesahau kuwa kulikuwa na Siti Binti Saad. Nia ya TAMWA ilikuwa kukumbusha watu juu ya mchango wa Bibi Siti katika muziki na pia hasa kuwa Siti ndiye alikuwa mwanamke wa kwanza wenye uwezo wa kufikisha ujumbe kwa Umati. Taarab aliyokuwa anaimba ilikuwa na ujumbe za kisiasa pamoja na mapenzi. Wangapi wanajua kuwaa Bibi Siti ndiye alihamisha watu kufanya mgomo huko Zanzibar miaka ya 1930's? Wanasema Siti alitunga zaidi ya nyimbo 600! Bahati mbaya nyingi zimepotea maana hazikuwa Recorded.

Nitafanya jitihada hivi karibuni za kufufua ile website niliyokuwa nayo iliyokuwa inaelezea mengi kuhusu maisha ya Siti Binti Saad.

Leo tunakukumbuka Bibi Siti Binti Saad.

Thursday, August 09, 2007

Viongozi wa TAMWA

Hapa niko na Dada yangu mpendwa, Bi Evodia Ndonde, ambaye aliwahi kufanya kazi Tanzania Film Company. Sasa ana kampuni yake ya video production. Naye ni mwanachama wa TAMWA miaka mingi.
Mwandishi wa Habari wa The Guardian, Lucas Lukumbo alipita kusalimia wana TAMWA. Kulia ni mwenyekiti wa TAMWA, Bi Ananilea Nkya.

Hapa niko na Dada Edda Sanga ambaye amestaafu kutoka Radio Tanzania hivi karibuni. Dada Edda aliwahi kuwa Mwenyekiti wa TAMWA.

TAMWA wanapokea interna kutoka nchi mbalimbali kila mwaka. Huyo dada yuko TAMWA kwa kipindi cha mwaka moja, anatoka Norway. Pia kulikuwa na akina dada kutoka Zambia, Ethiopia na Canada.
Hapa nipo na Dada Fatma Alloo, aliyekuwa Mwenyekiti wa TAMWA miaka mingi. Alitufundisha mengi kuhusu uongozi katika zile siku za mwanzo wa TAMWA.
Mwenyekiti wa TAMWA kwa sasa, Bi Ananilea Nkya, Mimi, Dada Evodia Ndonde na Edda Sanga. Dada Ndonde ana kampuni ya video production, na mimi niliwahi kuwa Publicity Secratary wa TAMWA na kwenye Executive Board.