Showing posts with label Jason Hudson. Show all posts
Showing posts with label Jason Hudson. Show all posts

Saturday, October 25, 2008

Mama na Kaka wa Jennifer Hudson Wameuawa!

Jennifer Hudson ma Mama yake mzazi

Kuna habari za kusikitisha. Mama yake mzazi Jennifer Hudson, Darnell Donerson (57), na kaka yake Jason Hudson (29), walmeuawawa kikatili jana nyumbani kwao huko Chicago. Mpwa wake mwenye miaka 7 anatafutwa na polisi wametoa Amber Alert (tangazo maalum kwa ajili ya watoto waliohatarini). Polisi wanamshikilia William Balfour (27) ambaye ni mume kwa mdogo wake.

Jennifer Hudson alipata tuzo la Oscar mwaka jana kwa ajili ya sinema, Dreamgirls. Aliigiza kama Effie White ambaye alikuwa mwimbaji mkuu wa kikundi cha Dreamgirls kabla ya kupinduliwa na Deena Jones (Beyonce). Jennifer alipata umaarufu kwenye American Idol.

Wiki iliyopita sinema, The Secret Life of Bees, ilitoka. Jeenifer anaigiza mle na akina Queen Latifah, Alicia Keys na Sophie Okonedo. Hivi karibuni kachumbiwa na mwanasheria na mwigizaji, David Otunga.

Mungu awalaze roho za marehemu mahala pema mbinguni. Amen.

Watu wanauliza kwa nini Jennifer hawakuhamisha familia yake kutoka South side ambayo inajulikana kwa kuwa eneo hatari sana huko Chicago. Habari zinasema kuwa mama yake hakutaka kuhama maana alikaa pale maisha yake yote.

Kwa habari zaidi someni:

http://www.latimes.com/news/nationworld/nation/la-na-hudson25-2008oct25,0,4062243.story

http://hollywoodinsider.ew.com/2008/10/jennifer-hudson.html?iid=top25-20081025-Jennifer+Hudson

http://ap.google.com/article/ALeqM5iIqSbmp7cCrnSvw1FIMxIvjQa8AQD941DLG80