Showing posts with label Mazishi. Show all posts
Showing posts with label Mazishi. Show all posts

Saturday, September 14, 2019

Funeral Services for Late Zimbabwe President Robert Mugabe Today

 

Late President Robert Mugabe Coffin Today

HARARE, Zimbabwe (AP) - African heads of state joined thousands of Zimbabweans at a state funeral Saturday for Zimbabwe's founding president, Robert Mugabe , whose burial has been delayed for at least a month until a special mausoleum can be built for his remains.

   More than 10 African leaders and several former presidents attended the service and viewing of the body of Mugabe, who died last week in Singapore at age 95, at the National Sports Stadium in the capital, Harare. The crowd filling about 30% of the 60,000 capacity of the Chinese-built stadium. Most of those attending were supporters of Zimbabwe's ruling ZANU-PF party.

   South African president Cyril Ramaphosa drew boos from the crowd, as a result of the recent attacks in Johannesburg on foreigners, including Zimbabweans. An official pleaded with the stadium crowd to let him speak. Ramaphosa apologized for the attacks.

   Kenyan President Uhuru Kenyatta described Mugabe as "a great icon of African liberation" and "a visionary leader and relentless champion of African dignity."

   The announcement Friday evening that that burial will be postponed until the building of a new resting place at the national Heroes' Acre Monument is the latest turn in a dramatic wrangle between Mugabe's family and President Emmerson Mnangagwa, a once-trusted deputy who helped oust Mugabe from power.

   Mnangagwa presided over Saturday's ceremony, attended by Mugabe's widow Grace, who wore a black veil.

   "A giant tree of Africa has fallen," said Mnangagwa, who hailed Mugabe as "a bold, steadfast revolutionary."

   He praised Mugabe for seizing land from white farmers. "To him, this was the grievance of all grievances of our people," Mnangagwa said. "The land has now been reunited with the people and the people have been reunited with the land." He also called on Western countries to remove sanctions imposed during Mugabe's era.

   "Go Well Our Revolutionary Icon" and "Farewell Gallant Son of the Soil" were among the banners praising Mugabe, who led the bitter guerrilla war to end white-minority rule in the country then known as Rhodesia. Mugabe was Zimbabwe's first leader and ruled the country from 1980 for 37 years, from years of prosperity to economic ruin and repression.

   He was deposed in 2017 by the military and Mnangagwa in a bloodless coup that was marked by more than 100,000 people demonstrating in Harare's streets to demand that he step down. Following Mugabe's resignation, Mnangagwa took power and won elections the next year on campaign promises he would improve the collapsed economy and create jobs. But Zimbabwe's economy has lurched from crunch to crisis and some in the crowd expressed the view that life was better under Mugabe's rule.

   "Bread was less than a dollar when we marched against him (Mugabe). It is now $9," said Munashe Gudyanga, 18. "I am just here to say `Sorry, President Mugabe, we didn't know things will be worse."'

   Some in the stadium sang an impromptu farewell to Mugabe, "When you left bread was a dollar," lyrics that implicitly criticized Mnangagwa, whose nearly two-year rule has been marked by rising prices, with inflation currently more than 175%.

   The visiting leaders viewed Mugabe's the partially open casket, followed by a 21-gun salute, a flypast by Zimbabwean air force jets and the release of 95 doves, to mark Mugabe's 95 years.

   Mugabe's body is to be viewed in his birthplace, Zvimba, on Sunday and then will be held in preservation until the new mausoleum is ready.

   In downtown Harare, many Zimbabweans were busy with their weekend errands, and expressed little interest in the funeral, which was open to the public.

   "What will I get if I go there? What will Mugabe do for me now that he failed to do when he was alive?" said Amelia Tukande, who was selling cellphone chargers along Harare's Samora Machel Avenue that leads to the stadium. "It is a waste of time. I have to work for my family."

   Others said they would have wanted to attend the funeral but cannot afford transport fares.

   "I didn't like him, but I still wanted to attend just to see for myself that he is gone ... but kombis (minivan taxis) want $3.50 just to get to the stadium," said Amos Siduna, waiting in line at a bank to get cash, which is in short supply. "That's too much money for me just to go and say `bye bye' to a corpse. Mugabe's corpse. No."

   The mourning period for Mugabe's death has been marked by the ongoing drama over where, when and how the ex-strongman will be buried. The new resting place will be built near the stadium at Heroes' Acre, a national burial site for top officials of Zimbabwe's ruling ZANU-PF party who contributed to ending white colonial rule

   The mausoleum will be at an elevated site above the other graves, according to Mnangagwa and a Mugabe family spokesman.

   Grace had previously insisting on a private burial rather than the state funeral and burial in a simple plot alongside other national heroes planned by the government.

   "We are building a mausoleum for our founding father at the top of the hill at Heroes' Acre," Mnangagwa said on state television Friday night, consenting to the Mugabe family's wishes.

   ---
The Late President of Zimbabwe Robert Mugabe

Saturday, April 13, 2019

Wehu Wavunja Kaburi ya Marehemu na Kubaka Maiti!

Imani ya Ushirikina (Uchawi) umezidi Tanzania!  Watu wanafukua maiti halafu wanaibaka!  Wana uchu ya pesa na mengine kuweza kufanya hivyo au ni wagonjwa wa akili?  Upumbavu! Mary Mkwaya Malamo alikuwa miaka 35. Alifariki mwanzoni mwa wiki.

*********************************************************************
The Late Mary Mkwaya Malamo

Mwili wa aliyekuwa Afisa wa Wizara ya Nishati Mery Mkwaya Maramo aliyefariki mwanzoni mwa wiki hii na kuzikwa jana katika Makaburi ya Pugu Mwakanga jijini Dar es Salaam, Usiku wa kuamkia leo (Ijumaa) watu wasiojulikana wameufukua na kuutoa nje ya jeneza kisha kuuvua nguo .
Kaka wa Marehemu Mary, Deogratius Maramo amesema inasemekana mwili wa marehemu uliingiliwa kimwili lakini bado wanasubiri ripoti ya Polisi ili wajue kilichomtokea ndugu yao.

Kaka huyo wa marehemu amesema kuwa hakuna kitu chochote kilichoibiwa kaburini humo.!


Kaburi la Marehemu Mary Mkwaya Malamo baada ya kuvunjwa na wachawi


Mnaweza kuangalia Video HAPA:

Maelezo ya Fundi aliyegundua Kaburi Imevunjwa. HAPA

Saturday, November 26, 2016

Aliyekuwa Rais wa Cuba , Fidel Castro Afariki Dunia

Rais Castro na Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1977
Aliyekuwa Rais wa Cuba, Fidel Castro, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90.  Castro alifariki usiku wa kuamkia leo.  Mdogo wake, Rais Raoul Castro aliwatangazia waCuba kuwa Castro amefariki saa nne na nusu usiku.  Alisema kuwa maiti ya kaka yake itachomwa moto leo (cremation) huko Cuba. Kutakuwa na Misa ya kumkumbuka  Taifa la Cuba itakuwa na siku kadhaa za kuomboleza.
Rais Raoul Castro alivyowantangazia wananchi:
The commander in chief of the Cuban revolution died at 22:29 hours this evening (03:29 GMT Saturday)," he said. "Towards victory, always!" he added, using a revolutionary slogan.
Marehemu Castro anakumbukwa kwa kuwa Dikteta. Alipindua serikali ya Cuba mwaka 1959, na hakutoka madarakani hadi mwaka 2006.  Alimwachia madaraka mdoo wake Raoul.  Castro alifanya mengi kusaidi nchi za Afrika ikiwemo Tanzania. Nchi ya Marekani waliweka vizuizi vingi juu ya Cuba ili kujaribu kumkomesha Castro lakini walishindwa.
Video ya Ziara ya Rais Castro nchini Tanzania kwa hisani ya AP



Sunday, November 13, 2016

Mazishi ya Marehemu Mzee Richard Binagi Yafanyika Jijini Dar es Salaam

Mazishi ya Mzee Richard Binagi (88) aliyefariki dunia Jumanne Novemba 08,2016 Jijini Dar es salaam baada ya kuugua, yamefanyika jana Jumamosi Novemba 12,2016 nyumbani kwake Kipunguni Jijini Dar es salaam. Alikuwa askari mstaafu wa JWTZ.
Na BMG
Taratibu za kuuaga mwili wa Mzee Binagi zikifanyika
Askari wa JWTZ wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Mzee Richard Binagi
Askari wa JWTZ wakiusindikiza malaloni mwili wa Mzee Richard Binagi
Gwaride la heshima
Gwaride la heshima
Askari wa JWTZ wakitoa heshima zao 
Wanafamilia (Profesa Lloyd Binagi na mkewe) wakiweka shada la maua
Wanafamilia (Mzee Chacha Binagi na mkewe) wakiweka shada la maua
Wanafamilia (Mama Binagi) akiweka shada la maua
Wanafamilia (Zakari Binagi na mkewe) wakiweka shada la maua
Wanafamilia wakiweka shada la maua
Wanafamilia wakiweka shada la maua
Wanafamilia wakiweka shada la maua
Wanafamilia
Wanafamilia
Wanafamilia
Ndugu, jamaa na marafiki
Bonyeza HAPA Kuhusu Msiba

Sunday, August 14, 2016

Tanzia - Mh. Mzee Aboud Jumbe

Rest in peace Mh. Mzee Aboud Jumbe. (1920 - 2016)

Sunday, May 15, 2016

Shukurani Kutoka Kwa Familia ya Michuzi - Msiba wa Maggid Muhidin

Familia ya Ankal Muhidin Issa Michuzi inapenda kutoa shukrani nyingi sana sana kwa ndugu, jamaa, majirani, marafiki na wafanyakazi wenzie kwa kujitoa kwa hali na mali katika wakati huu mgumu wa msiba wa mawanae Maggid (pichani) aliyefariki huko Durban, Afrika Kusini Jumapili ya wiki iliyopita na kuzikwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam juzi Jumamosi.
Ni vigumu mno kumshukuru mtu mmoja mmoja kutokana na wingi wenu na kwa jinsi kila mmoja wenu alivyojitoa na kuonesha upendo wa dhati kabla na baada ya mazishi. Tunaweza kujaza kurasa 200 kama hizi na tusiwe tumehitimisha robo tu ya shukrani zetu kwa kila mmoja wenu. Hivyo tunaomba radhi kwa yoyote ambaye hatutomtaja, kwani wafadhili wetu nyie mko wengi mno.
Pamoja na hayo shukrani za kipekee ziwaendee Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Mama Janeth Magufuli na familia yao yote, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete na familia yao yote, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na familia yake yote, Rais Mstafu wa awamu ya Tatu Mzee Benjamin William Mkapa na Mama Anna Mkapa na familia yao yote, Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba na Familia yake yote, Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Allan Kijazi, Katibu Mkuu Ikulu Mhe. Peter Ilomo, Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Mhe. Ombeni Sefue pamoja na wafanyakazi wenzie wote wa baba mfiwa kwa kuwa karibu naye katika wakati wote, na kuhakikisha kuwa kila kitu katika msiba huu kinaenda sawasawa. TUNAWAOMBEA KWA MOLA AWAPE BARAKA ZAKE ZOTE...

Salamu zingine za kipekee ziwaendee watumishi wote wa Ubalozi wetu Afrika kusini mjini Pretoria ambao wakiwa chini ya Brigedia Jenerali Kimaryo na Afisa wa Ubalozi kaka Awesi walisimamia maswala yote ya kuusafirisha mwili kutoka Durban kuja Dar es salaam. MOLA AWAONGEZEE PALE MTAPOPUNGUKIWA...

Vile vile shukrani za kipeke ziwaendee Viongozi na wanachama wa Jumuiya ya Watanzania waishio Durban pamoja na Muslim Burial Society ya hapo hapo Durban ambao walihakikisha mwili wa marehemu unahifadhiwa, unakafiniwa na unasafirishwa kwa heshima zote. ALLAH AWAJAALIE KATIKA KILA JAMBO...

Kwa Uongozi wa msikiti wa Maamur uliopo Upanga Dar es salaam pia familia inatoa shukurani za kipekee kwa yote mliotutendea ikiwa ni pamoja na mwongozo wa kidini katika wakati wote wa msiba na mazishi.
Tutakuwa watovu wa fadhila endapo kama hatutatoa shukurani za kipekee kwa magrupu ya WhatsApp yote ambayo baba mfiwa Ankal ni mwanachama. Shukurani hizi maalum ziwaendee Ma-Admin na wanachama wa Kariakoo Family Group (KFG), Dar es salaam Old Friends (DOF), Ma Best Group (MBG), Wanahabari, Tasnia ya Habari, Uongozi, Siasa na Matukio Mix, The New Team, TSJ Alumni, Zama Zile, The Brain Team, Jazz Fans, The Kop in Tanzania, LFC Bongo, Uswazi Academia, Tanzania Bloggers Network (TBN), The Legends Family, SID Tanzania Chapter, Mawasiliano, Team Michuzi, Amani Kwanza Group, Photojournalists TZ, PPAT Members, P Mamas, RUBY 15, Warembo wa KA, Mambachoz Group, Ndanshau Group, Empress Group kwa Fundi Mussa na wengi wengine wote katika Social media wakiongozwa na Jamii Forum na VIJIMAMBO BLOG ya Marekani. TUMEHEMEWA MNO NA KUFARIJIKA SANA KWA MICHANGO YENU YA HALI NA MALI. WE ARE HUMBLED. MBARIKIWE SANA, SANA, SANA...
Mwisho, lakini sio kwa umuhimu bali kwa nafasi na mpangilio, tunatoa shukrani za kipekee kwa shirikia la ndege la Emirates kwa kufanikisha usafiri wa mwili wa marehemu, hali kadhalika kampuni mahiri ya SWISSPORT kwa kusaidia logostics zote katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es salaam.

HATUNA CHA KUWALIPA ZAIDI YA KUTOA SHUKURANI NA KUSEMA ASANTE SANA NA KUWAOMBEA KWA MOLA KILA MMOJA WENU AWABARIKI KATIKA SHUGHULI ZENU ZOTE...

Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un

AMIN!




Saturday, May 14, 2016

Mazishi ya Maggid Muhidin Leo

CODES:
Mwili wa marehemu ukiingizwa katika msikiti wa Maamur Upanga jijini Dar es salaam leo tayari kwa kuswaliwa kabla ya mazishi.
Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete (kushoto) akimfariji baba wa marehemu Ankal Issa Michuzi.
Mama wa marehemu (aliyevaa nguo nyeupe) akiwa na ndugu wa karibu wakiomboleza.
Baba wa marehemu akiwa na viongozi wa dini wakiombea mwili wa marehemu dua.
Mke wa Rais mama Janeth Magufuli (kulia) akiwa na ndugu wa marehemu.
Baba wa marehemu Ankal Issa Michuzi akipata chakula.
Mke wa Rais mama Janeth Magufuli (kulia) akiwasili msibani Wazo hill akiwa na baba wa marehemu Ankal Issa Michuzi.
Baba wa marehemu akiwa na Balozi Cisco Mtiro na baadhi ya waombolezaji.
Baba wa marehemu (mwenye kofia), Ankal Issa Michuzi akipewa pole na baadhi ya waombolezaji mara baada ya maziko ya mtoto wake Maggid Muhidin Michuzi (18)yaliyofanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba akimpa pole Issa Michuzi.
Rais Mstaa mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete akimfariji Ankal Issa Michuzi.
Issa Michuzi (mwenye kofia) akifuatiwa na Rais mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, kulia kwake ni Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba na Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Mhe Ombeni Sefue. Kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi, Katibu Mkuu Ikulu Mhe. Peter Ilomo wakati maziko.
Waumini wakiomba dua.
Baba wa marehemu Issa Michuzi (katikati) akiwa na huzuni akiwa na Rais mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, kulia kwake ni Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde
Baba mkubwa wa marehemu, Ismail Issa Michuzi akitoa shukrani kwa walioshiriki mazishi ya mtoto wao.
Mroki Mroki ambaye aliyekuwa MC akitoa ya muongozo wakati wa mazishi.
Waombolezaji wakiweka udongo kwenye kaburi la marehemu.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Mhandisi John Kijazi akiweka udongo.
Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba akiweka udongo kaburini.
Rais mstaafu Jakaya Kikwete akiweka udongo kaburini.
Baba wa marehemu Ankal Issa Michuzi akiweka udongo kaburini.
Mwili wa marehemu ukiwekwa kaburini.
Mwili ukiwasili makaburini.

Rais mstaafu Jakaya Kikwete akimpa pole baba wa marehemu, Ankal Issa Michuzi. Kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi. Picha zote na Francis Dande