Showing posts with label Msaada. Show all posts
Showing posts with label Msaada. Show all posts

Thursday, December 22, 2016

Zanzibar ilitoa Msaada Kwa Uiingereza!!!!

Jamani tumezoea kuwa wapokea misaada. Lakini je, mlikuwa na habari kuwa wakati wa Vita Kuu ya pili vya dunia (World War 2) Zanzibar ilitoa msaada wa chakula Kwa waingereza wenye nja? Wakati Ile Zanzibar ni Sultanate.




Monday, November 16, 2015

Msaada wa Wasamaria Wema Unahitajika Kwa Ajili ya Matibabu

Ndugu Wasamaria wema
Napenda kutumia fursa hii kukushirikisha habari ya kusikitisha kuhusu dada Joyce Mwambepo (pichani akiwa na mwanaye, na migu yake iliyopooza) mkaazi wa Sinde jijini Mbeya. Dada huyu mwenye umri wa miaka 27 anaishi na bibi yake mwenye umri wa miaka 80 pamoja na mwanaye mwenye umri wa miaka 4.
Kwa bahati mbaya mwezi April mwaka jana dada huyu alipata ajali ya kugongwa na gari ambayo haikusimama kumsaidia. Ila kwa msaada wa wasamaria wema alipelekwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa  Mbeya ambako inasemekana alikaa kwa miezi mitatu bila kupata matibabu.
Katika uchunguzi wa awali ilibainika kuwa Joyce amevunjika miguu yote miwili,  hivyo akahamishiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili ambako pia baada ya kukaa kwa miezi kadhaa alirejeshwa Mbeya baada ya kukosa shilingi 550,000/- za vipimo na matibabu.
Hadi nakutana naye dada huyu alikuwa amelala nyumbani kwa bibi yake (pichani kushoto) ambaye ni mlezi wake tangu akiwa na miaka minne baada ya wazazi wote wawili kufariki dunia. 
Hawezi kukaa wala kusimama na anajisaidia hapo hapo kitandani kwa msaada wa mwanaye na bibi yake. Inasikitisha.
Hivyo nimejitahidi kufuatialia ili kujua mahitaji halisi lakini sikufanikiwa kumpata daktari bingwa wa mifupa . Ili kumsaidia Joyce inatakiwa aanze process upya za matibabu kuanzia hapa Mbeya referral Hospital  hadi Muhimbili jijini Dar es salaam.
Gharama za matibabu ni kama ifuatavyo:
1. shilingi 300,000/- za kupima CT-SCAN
2. Shilingi 250,000/- za MRI
3. Usafiri wa kutoka Mbeya-Dar kwa gari maalum la kukodi 700,000/-
4. Gharama za msaidizi ambaye ni rafiki yake 300,000/-
5. Chakula 450,000/- (Endapo watakaa hospitali mwezi mzima)
6. Gharama za matibabu (CT-SCAN&MRI ni vipimo tu) 500,000/-
7. Na mahitaji mengineyo wakiendelea kupata tiba 500,000/-

Hivyo kwa kuanzia kiasi cha shilingi 3,000,000/- (milioni tatu) kinahitajika kumpunguzia mateso dada yetu huyu. Asante sana kwa moyo wako wa kujitoa na Mungu atakubariki.

Deo Kakuru Msimu
Msamaria mwema
+255769 512 420

Wakati huo huo kwa niaba ya Michuzi Media Group, Ankal amejitolea kusaidia uratibu wa kufanikisha matibabu ya dada Joyce. Hivyo unaweza kuwasiliana naye kwa email issamichuzi@gmail.com ama whatsapp namba +255 754 271266 kwa jina la Ankal.

Sunday, May 25, 2014

Mh. Mohamed Dewji Atoa Misaada Jimboni Mwake

DSC_0025

Mbunge wa Singida Mjini, Mh. Mohammed Dewji (MO), akizungumza na viongozi wa Mahakama ya Qadhi wakati alipotembelea Mahakama hiyo kuona namna inavyohudumia waumini wa Dini ya Kiislamu katika kutatua migogoro ya ndoa.

DSC_0029

Sheikh wa Mahakama ya Qadhi, Ramadhani Kaoja akimweleza Mheshimiwa Mbunge shughuli za Mahakama hiyo pamoja na changamoto mbalimbali zinazowakabili, Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Singida Mjini , Hamis Nguli, wa pili kulia ni Katibu wa Mahakama ya Qadhi, Alhajj B. Mlau.

DSC_0133

Mbunge wa jimbo la Singida Mjini MO akisalimiana na waumini wa Msikiti wa Kata ya Mtipa wakati alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa Msikiti huo, ambapo mara baada ya kuona hatua zilizofikia za ujenzi huo aliahidi kutoa Mabati 50 pamoja na mifuko 50 ya Saraji kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo.

DSC_0171

MO akitoka kukagua ujenzi wa Msikiti wa kijiji cha Mangwanjuki kata ya Mtipa.

DSC_0237

Waumini wa Msikiti wa kijiji ch Mangwanjuki wakimsikiliza Mbunge wao Mheshimiwa MO.

DSC_0262

Baadhi ya wapiga kura wa kijiji cha Mangwanjuki wakipeana mikono ya Kheri na Mbunge wao.

DSC_0287

Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu wa Msikiti wa Mwankonko darajani wakimsikiliza Mbunge wao (hayupo pichani) wakati alipoendelea na zoezi la kutembelea nyumba za kuabudu zilizopo jimboni kwake.

DSC_0314

Jengo la wa Mwankonko darajani likiwa kwenye hatua Lenta, ambapo baada ya Mbunge kuona hatua hiyo ya nguvu za wananchi aliahidi Bati 50 na Mifuko ya Saruji 50.

DSC_0713

Mheshimiwa Mohammed Dewji na baaadhi ya viongozi wa Msikiti wa kijiji cha Kisasida.

DSC_0729

Mbunge MO akizungumza na waumini wa Msikiti wa Kisasida, ambapo ameahidi kutoa msaada wa Mabati 100 na Mbao 100 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Msikiti huo.

DSC_0738

MNEC wa Manispaa ya Singida, Hassan Mazala akitoa hamasa kwa wakazi wa Kisasida kushiriki Mkutano wa hadhara ambao umeitishwa kwa ajili ya Katibu Mkuu CCM Taifa, Abdulrahman Kinana wa kuongea na wakazi wa jimbo la Singida Mjini utakaofanyika viwanja vya People’s Club.

DSC_0750

Mheshimiwa Mohammed Dewji akielekea kukagua ujenzi wa Msikiti wa Minga mjini Singida.

DSC_0336

Watoto wa Madrasa ya Msikiti wa Mwankoko Darajani wakimpokea Mbunge wao kwa mabango yenye ujumbe mbalimbali wakati alipotembelea ujenzi wa Msikiti huo.

DSC_0343

Mheshimiwa Mohammed Dewji akifurahia jumbe zilizoandikwa na watoto wa Madrasa ya Mskiti wa Mwankoko Darajani.

Kwa picha zaidi bofya hapa

Monday, February 20, 2012

Mtoto wa Gaddafi Aomba Msaada!

Hao matapeli wanazidi kuchekesha!

**********************************************************
How is everything over there?

I know this letter will definitely come to you as a huge surprise, but I implore you to take the time to go through it carefully as the decision you make will go a very long way to determine my future and continued existence.

My name is Saadi Gaddafi, I am the son of the late Muammar al-Gaddafi and the National Security Adviser of Libya. I am at the moment very depressed as I write to you. I got your mail from search engine and I really think you can be of help to me. At the moment I have been banned from traveling and some of my assets have been frozen already and that of my late father (Muammar al-Gaddafi ) and families.

Due to the situation at hand, I do not possess the right to move about as I will be arrested and prosecuted in an international court of justice. In my possession right now is my internet connection, it is the only means I am able to make contact with the outside world. Also as another measure that has been taken by the international community, our asset i.e the assets of Muammar al-Gaddafi and family worldwide have been frozen due to the actions of my late father.

The above mentioned reasons are what have compelled me to write you this mail as I seek to partner with a trustworthy person who can assist me in transferring some of my monetary assets worth about 5,000,000 GBP (FIVE MILLION GREAT BRITISH POUNDS). This funds has been lodged in a bank account in the United Kingdom and as things are shaping now this money is likely to be discovered soon, all the legal documentation concerning the deposit are with me, I will only authorize the power of attorney and next of kin certificate making you the new beneficiary of the deposit so that the bank will transfer the funds into your account immediately, so I seek your assistance in helping me transfer this money into your account so that it is not discovered. I am ready to offer as much as 30% of this money to you if you render to assist in transferring this money and the money is transferred successfully,
Please i want this to be a confidential deal between both us and if you are not interested in this deal, kindly delete this message from your email box  without keeping any content of this message and never act like if you received any mail from me, because i will not be pleased to lose this money in any way.
This is my personal email saadi_gaddafi101@yahoo.com i created this email today just to have a confidential communication with you, if you know you can assist me out from my present pain and stress, you are free to contact me.

Please be honest and truthful because some of my assets have been frozen already, and i don't want to lose this money.

PLEASE LET ACT FAST AS A MATTER OF URGENT.

Thanks,
Saadi Gaddafi.

Saturday, July 02, 2011

OMBI KWA WAZEE WATARAJIWA WOTE - Tangazo

(Tandika Kilalakala - Wakina mama waliokusanyika sehemu moja kupata misaaada. wengi wao wana ulemavu wa kutembea, hawana kipato na mmoja ana wajukuu wawili walioachwa na wazazi wao)

( pichani - Magomeni Mzee Simba Maduwilo kwa sasa mlemavu wa miguu, na mkewe hali yake ya afya sio nzuri. Wanaishi kwa kumtegemea binti yao anaejishughulisha na mama lishe.)


Kwa mara nyingine tena TUSHIKAMANE PAMOJA FOUNDATION imetembelea wazee wanao ishi katika mazingira magumu na kutoa misaada mbali mbali.

TUSHIKAMANE PAMOJA FOUNDATION tunaomba watu watakaoguswa na watakaopenda kusaidia kikundi hiki kiendelee kutoa misaada kwa wa lengwa, tupigieni simu 0787 558550 au 0787 177077 au 0784 265560 au 0784 950250 Tunapokea nguo mitumba isiochakaa saaana, vifaa vya nyumbani, mashuka, vyakula vikavu, kama, unga, mchele, sukari, Mmaharagwe, majani ya chai n.k...

Bado wapo wazee wengi hatuja wafikia. Lengo letu ni kuwapa angalau vyakula kidogo mwezi mara moja.... TUSHIKAMANE PAMOJA TUFIKISHE MALENGO YETU.